Kuna hatua ugonjwa ukifika ni lazima busara itumike. Mnauza mali zote kulipia matibabu, ndugu anakufa kisha familia inabaki na umasikini wa kutupwa

Kuna hatua ugonjwa ukifika ni lazima busara itumike. Mnauza mali zote kulipia matibabu, ndugu anakufa kisha familia inabaki na umasikini wa kutupwa

Kwenye kuuguza msikilize Daktari kwa makini hapo utafanya maamuzi sahihi. Hakuna Daktari mwenye hekima na busara atakuambia huyu mgonjwa wako hatibiki tena Bali atakupa ishara utumie akili zako.

Kwa mfano unaambiwa hii cancer ni stage four tumaini la kupona dogo sana lakini mnaweza kwenda kujaribu India, kama pesa ipo ya kutosha beba mgonjwa nenda India lakini kama ni kuuza nyumba ambayo ni hifadhi ya familia achana na hiyo safari.

Rafiki yangu mmoja alikuwa diagnosed obstructive azoospermia(at the of 32years) ili apate mtoto anatakiwa afanye IVF,at that time jamaa alikuwa ana fight kuanzisha company ili awe na economic freedom. Mkewe akawa ana force watumie pesa ya mtaji kufanya IVF,for three wanashindana mwisho ndoa ikavunjika jamaa akatafuta single mother mwenye mtoto wa 1year akamuoa na kumu adopt mtoto. Daima hisia zisiongeze uhalisia.
Sure
 
Mada nzuri but kibinadam ni ngumu sana kumsusa mpendwa ndio maana familia hujitoa kwa kila hali, hitimisho lako lilipaswa kuihamasisha jamii iwe na utamaduni wa kuchangia matibabu kama wafanyavyo kwenye masherehe na misiba na sio busara za kususa.
 
Kwenye kuuguza msikilize Daktari kwa makini hapo utafanya maamuzi sahihi. Hakuna Daktari mwenye hekima na busara atakuambia huyu mgonjwa wako hatibiki tena Bali atakupa ishara utumie akili zako.

Kwa mfano unaambiwa hii cancer ni stage four tumaini la kupona dogo sana lakini mnaweza kwenda kujaribu India, kama pesa ipo ya kutosha beba mgonjwa nenda India lakini kama ni kuuza nyumba ambayo ni hifadhi ya familia achana na hiyo safari.

Rafiki yangu mmoja alikuwa diagnosed obstructive azoospermia(at the of 32years) ili apate mtoto anatakiwa afanye IVF,at that time jamaa alikuwa ana fight kuanzisha company ili awe na economic freedom. Mkewe akawa ana force watumie pesa ya mtaji kufanya IVF,for three wanashindana mwisho ndoa ikavunjika jamaa akatafuta single mother mwenye mtoto wa 1year akamuoa na kumu adopt mtoto. Daima hisia zisiongeze uhalisia.
Mfano wako sio LIFE & DEATH

Hujafikiwa kukaribia kuwapoteza watu wa muhimu Mama/Baba/Mtoto wako

Ndo Utajua kuwa mbele ya hizo unaita "hisia" nyumba na Mali zote sio kitu. And u would give anything to have them, hata kuwaongezea muda kidogo tu. Hata Daktari akwambie ni stage 11

Mali zinatafutwa, hasara roho
 
Mtu chake mali kazitafuta yeye zitumike tu kumtibia alizitafuta zimfae akifa waliobaki watatafuta zao kama yeye alivyotafuta

Mleta mada una roho ya kivivu nyie ndio hutolea mimacho wagonjwa wenye mali wafe mgombanie kurithi chake

Wewe waonyesha wazi una roho ya kiuaji waweza ua hata mzazi wako ukiona anaumwa sana na gharama za kutibu kubwa ili mchukue chake
Una pepo mchafu
 
Ndiyo maana wachina viumbe dhaifu wanachoma tu sindano ya sumu na kuvipumzisha kwa amani.
 
Ingekuwa jamii yetu ni yenye kujitegemea, kuwa Mzee kachuma na kuwekeza, na Vijana wake nao wameanza kuchuma na kujitegemea na kutafuta mali zao, ningesema Mzee amestahili alichochuma. Kwamba kwa kujenga nyumba, hiyo ilikuwa ndio bima yake, ama akiba yake ya uzeeni. Sijui kama angepona kungekuwa na pesa za ziada kutoka kwenye mauzo ya nyumba, ambazo zingemsukuma mpaka kifo chake, ila hayo hayakutokea.

Jamii zetu zinabweteka, alichochuma baba, hata mjukuu atataka ajibane hapo hapo, badala ya kila mtu kutafuta chake.
 
Habari za wakati huu kaka na dada zangu wa humu jamiiforums.

Ndugu zangu watanzania;

Kuna stage ugonjwa ukifika ni lazima busara itumike. Mnauza mali zote kulipia matibabu, ndugu anakufa kisha familia inabaki na umasikini wa kutupwa.

Ninaandika haya nikijua fika ya kwamba hakuna idadi ya mali au pesa kinachoweza kulingana na uhai wa mwanadamu. Unakumbuka ajali ya MV Bukoba wewe? Unakumbuka ajali ya MV Spice kule Zanzibar?

Ni watanzania wangapi walikufa katika ajali zile? Hivi wakati wa majanga yale uliwahi kusikia hata siku moja watanzania wanalalamika kuhusiana na thamani ya zile meli?

Unajua gharama ya vyombo vile ni mamilioni ya pesa ngapi za kitanzania? Licha ya kuwa ni pesa nyingi sana zilitumika katika kununua/kuunda vyombo vile watanzania bado wakawa wanalilia roho za binadamu wenzao kwa maana kwamba hakuna cha kufananisha na uhai wa mwanadamu.

Hiyo ndio asili ya huruma ambayo Mungu ametupa sisi wanandamu. Familia zetu hizi masikini, mali tunazipata kwa tabu sana, ujenzi wa kuungaunga nyumba moja unajenga kwa kudunduliza miaka zaidi ya 9.

Baada ya ujenzi kukamilika, mnaishi miaka yenu 3, alafu ghafla mnasikia baba yenu mzazi anasumbuliwa na ugonjwa wa kansa ya ini au vigo zote zimefeli anapaswa kupelekwa India kwa matibabu zaidi.

Ndugu wanajitahidi kuchangisha kwa jamaa na rafiki zao hapa na pale kiasi hakifikii pesa sahihi inajohitajika kuweza kukidhi gharama za matibabu hivyo wanaamua kuuza mali zao za thamani walizonazo kumpeleka baba yao nje ya nchi (India) kwa matibabu zaidi.

Matokeo yake baba anakufa, mzee wa miaka 69, na mali zote mmeuza. Unaikuta familia iliyotoka kupanga chumba na sembule kisha wakajikwamua kujenga wanarudi tena katika nyumba za kupanga na maisha ya kuomba omba.

Nimemua kuleta mada hii hapa baada ya kukutana na kijana mmoja jina lake ni ****** ambaye nilikuwa ninakaa nao Keko Juu mwaka 2011 ambaye baba yao alifariki mwaka 2014 kwa ugonjwa wa saratani ya kibofu cha mkojo.

Inasemekana kwamba mzee yule wa miaka 66 hakuwa na matumaini ya kupona, kulingana na taarifa ambazo mmoja wa ndugu yao wa karibu (baba mdogo) alipewa na daktari katika hospitali moja maarufu tu hapa Dar.

Kwa kuwa familia bado ilikuwa inampenda na kumthamini mzee wao wakaona ni bora wauze hata nyumba waliokuwa wanajenga huko Toa Ngoma njia ya Kongowe ili wampeleke baba yao huko India. Matokeo yake ndio kama haya. Wamepoteza nyote, baba pamoja na nyumba.

Mama ndio hivyo tena biashara za kuungaunga za akina mama lishe, dada zake wawili walizaa tu hapo nyumbani yaaani nilipoonana na huyu kijana (ni agemate na mimi) machozi yalitaka kunitoka.

Basi tu kwa kuwa na mimi mwenyewe ni Taxi Driver mlala hoi sina cha kumpa zaidi ya kusimuliana story za zamani tulipokuwa tunacheza mpira (cha ndimu) wote na kwenda kuogelea baharini kule Kurasini tulikuwa tunapaita ZAMCARGO au SAVA.

Ndugu zangu, kuna stage ugonjwa ukifika ni lazima busara itumike tusizidishe umasikini katika familia.

USISAHAU: ENDELEA KUWA MZALENDO IPENDE TANZANIA. USICHAFUE TASWIRA NJEMA YA TAIFA LAKO. USTAWI WA NCHI YETU UNAANZA NA WEWE. TIMIZA WAJIBU WAKO IPASAVYO.
VIP tangazo letu LA vitabu vya kijerumani silioni siku hizi
 
Kifo kipo kila binadamu ataonja umauti kwa wakati wake, unaweza ukaondoka wewe mzima ukamuacha mgonjwa na ugonjwa.

Tunachowapambania wapendwa wetu ni maumivu makali wanayopitia, hata kama atakufa unasema tumpunguzie maumivu anayopitia kwa Hali na Mali.

Subiri uuguze utaelewa kwa Nini wañauza Mali.
 
Mfano wako sio LIFE & DEATH

Hujafikiwa kukaribia kuwapoteza watu wa muhimu Mama/Baba/Mtoto wako

Ndo Utajua kuwa mbele ya hizo unaita "hisia" nyumba na Mali zote sio kitu. And u would give anything to have them, hata kuwaongezea muda kidogo tu. Hata Daktari akwambie ni stage 11

Mali zinatafutwa,hasara roho

Unajua maana ya cancer stage four?
 
Habari za wakati huu kaka na dada zangu wa humu jamiiforums.

Ndugu zangu watanzania;

Kuna stage ugonjwa ukifika ni lazima busara itumike. Mnauza mali zote kulipia matibabu, ndugu anakufa kisha familia inabaki na umasikini wa kutupwa.

Ninaandika haya nikijua fika ya kwamba hakuna idadi ya mali au pesa kinachoweza kulingana na uhai wa mwanadamu. Unakumbuka ajali ya MV Bukoba wewe? Unakumbuka ajali ya MV Spice kule Zanzibar?

Ni watanzania wangapi walikufa katika ajali zile? Hivi wakati wa majanga yale uliwahi kusikia hata siku moja watanzania wanalalamika kuhusiana na thamani ya zile meli?

Unajua gharama ya vyombo vile ni mamilioni ya pesa ngapi za kitanzania? Licha ya kuwa ni pesa nyingi sana zilitumika katika kununua/kuunda vyombo vile watanzania bado wakawa wanalilia roho za binadamu wenzao kwa maana kwamba hakuna cha kufananisha na uhai wa mwanadamu.

Hiyo ndio asili ya huruma ambayo Mungu ametupa sisi wanandamu. Familia zetu hizi masikini, mali tunazipata kwa tabu sana, ujenzi wa kuungaunga nyumba moja unajenga kwa kudunduliza miaka zaidi ya 9.

Baada ya ujenzi kukamilika, mnaishi miaka yenu 3, alafu ghafla mnasikia baba yenu mzazi anasumbuliwa na ugonjwa wa kansa ya ini au vigo zote zimefeli anapaswa kupelekwa India kwa matibabu zaidi.

Ndugu wanajitahidi kuchangisha kwa jamaa na rafiki zao hapa na pale kiasi hakifikii pesa sahihi inajohitajika kuweza kukidhi gharama za matibabu hivyo wanaamua kuuza mali zao za thamani walizonazo kumpeleka baba yao nje ya nchi (India) kwa matibabu zaidi.

Matokeo yake baba anakufa, mzee wa miaka 69, na mali zote mmeuza. Unaikuta familia iliyotoka kupanga chumba na sembule kisha wakajikwamua kujenga wanarudi tena katika nyumba za kupanga na maisha ya kuomba omba.

Nimemua kuleta mada hii hapa baada ya kukutana na kijana mmoja jina lake ni ****** ambaye nilikuwa ninakaa nao Keko Juu mwaka 2011 ambaye baba yao alifariki mwaka 2014 kwa ugonjwa wa saratani ya kibofu cha mkojo.

Inasemekana kwamba mzee yule wa miaka 66 hakuwa na matumaini ya kupona, kulingana na taarifa ambazo mmoja wa ndugu yao wa karibu (baba mdogo) alipewa na daktari katika hospitali moja maarufu tu hapa Dar.

Kwa kuwa familia bado ilikuwa inampenda na kumthamini mzee wao wakaona ni bora wauze hata nyumba waliokuwa wanajenga huko Toa Ngoma njia ya Kongowe ili wampeleke baba yao huko India. Matokeo yake ndio kama haya. Wamepoteza nyote, baba pamoja na nyumba.

Mama ndio hivyo tena biashara za kuungaunga za akina mama lishe, dada zake wawili walizaa tu hapo nyumbani yaaani nilipoonana na huyu kijana (ni agemate na mimi) machozi yalitaka kunitoka.

Basi tu kwa kuwa na mimi mwenyewe ni Taxi Driver mlala hoi sina cha kumpa zaidi ya kusimuliana story za zamani tulipokuwa tunacheza mpira (cha ndimu) wote na kwenda kuogelea baharini kule Kurasini tulikuwa tunapaita ZAMCARGO au SAVA.

Ndugu zangu, kuna stage ugonjwa ukifika ni lazima busara itumike tusizidishe umasikini katika familia.

USISAHAU: ENDELEA KUWA MZALENDO IPENDE TANZANIA. USICHAFUE TASWIRA NJEMA YA TAIFA LAKO. USTAWI WA NCHI YETU UNAANZA NA WEWE. TIMIZA WAJIBU WAKO IPASAVYO.
Uhai ni bora kuliko mali.
 
Hahahaha ndo maana nikakwambia hata "Stage 11" kama unajua kuchambua ungejua nimekutajia sarcastically, na ungeng'amua kama najua/sijui ngazi zake mpaka Terminal stage

Anyway tukubaliane kutokubaliana

Nini tofauti ya terminal stage and stage four?
 
Hakuna palliative care, ni sawa na tunavyotunza wazee wetu ni jukumu la familia zaidi...ni kama utamaduni hatuwezi kufanya vitu nje ya tulivyovizoea....kikwetu kisaikolojia tunaenda hospitali tutibiwe na kama ikitokea tukipewa majibu tofauti tutafuta na kutafuta hospitali nyingine ambazo tuna perceive kuwa better, kumbe ugonjwa hautibiki...
 
Mtu chake mali kazitafuta yeye zitumike tu kumtibia alizitafuta zimfae akifa waliobaki watatafuta zao kama yeye alivyotafuta

Mleta mada una roho ya kivivu nyie ndio hutolea mimacho wagonjwa wenye mali wafe mgombanie kurithi chake

Wewe waonyesha wazi una roho ya kiuaji waweza ua hata mzazi wako ukiona anaumwa sana na gharama za kutibu kubwa ili mchukue chake
Una pepo mchafu
Kwa bahati nzuri tangia ulivyonitukana katik ile mada ya vodacom ya kutuma na ada ya kutolea, nilishakuweka katika IGNORE LIST yangu. Sijui kwanini nime-click kusoma comment yako.
 
Mkuu acha tu, mimi nimepambana mpaka mama yangu mzazi kafariki, kungekuwa na rufaaa hata ya kwenda wapi ningeuza kila kitu nibaki na nguo nilizovaa Ili mradi apone.

Sio rahisi kama unavyodhani, ni ngumu sanaa kusema tusiuze Mali kisa atakufa. Jibu ni hapana lazima tupambane mpaka mwisho tubaki kulia kuwa Mungu kampenda zaidi na sio tumeshindwa kumuokoa
 
Back
Top Bottom