Infantry Soldier
JF-Expert Member
- Feb 18, 2012
- 15,892
- 16,476
- Thread starter
-
- #201
Hakika una moyo kama wa mwanajeshiUhai ulikuwepo kabla ya binadamu kugundua pesa na nyumba,Mimi nitauza kila kitu kupigania uhai was mmpendwa wangu!
Haya mavitu niyakutafuta Ila uhai haununuliwi haijalishi nitabaki kwenye wakati gani nitanyanyuka na kupambana tena
Well saidHalafu wanahangaika tu na dunia hii jambo ambalo ni dhambi sana mbele za Mungu...
HakikaHakunaga umuhimu kabisa kwa watu wanaotoka katika familia ya kipato duni/cha chini...
Sio sahihi hata kidogo mkuunyumba imeuzwa wanaoishi ndani wakapatwa na mshtuko wa moyo au presha wakafariki na wao ,badala ya mtu mmoja wanafariki watu wawili au watatu..je ni sahihi.?.
AyaLicha ya udogo wako Soja unaandikaga mada za maana sana. Kudos Soja wangu.
Kuna kisa kimoja cha shangazi yangu mwalimu mstaafu nitakuja kukiandika hapa ngoja kidogo kwa maana nipo safarini.
Doctor mbaya sana huyo aisee...Wengine tumeshapita huko, na shida ilikuwa maDr walikuwa wanadanganya kuwa mzee ana tatizo flani linalotibika lakini kwa pembeni wanawaambia watu baki kwamba huyu mzee hana muda mrefu, kansa imesambaa kila mahali.
Umefafanua vema sana mkuuHii Mada yako iko sawa; Labda ila nadhani inategemeana na Potential ya Mtu; Mfano mtu alikuwa ni mpambanaji (potential) hili lazima liangaliwe kwanza kupambana kuhakikisha anatoboa,
Sasa unakuta watu wanapambana na Mtu wa 90, of which kama Busara alishawaachia wenye umri mdogo, lakini hela inatumika nyingi sana tena kwa kuchangishana binafsi sionagi umuhimu wake.
Kama Hela ya Matibabu ya muda mrefu ipo na si tatizo miongoni mwa wanafamilia, then atibiwe tu mpaka umauti utakapomfiika.
Umenena vema hapaKuna kipindi ni muhimu kukubali kwamba kifo kwa ujuzi wetu wa sasa hakiepukiki, na kuna watu wataendelea kuishi baada ya mtu kufariki, hivyo, inaweza kuwa busara kuweka mbele interests za watakaobaki.
Hususan kama mgonjwa anaumwa ugonjwa chronic na kashakuwa mtu mzima.
Mimi siwezi kubariki wazo la kuuza nyumba zangu nilizohangaikia maisha yangu yote, zije kuwa nguzo ya kusaidia uchumi wa kizazi changu na ndugu zangu wa karibu, ili tu niongeze miaka michache katika maisha yangu.
Kitu cha muhimu kabisa ni kujiweka katika mazingira ambayo hatuhitaji kuchagua kimoja kati ya mawili haya, na tunaweza kufanya yote. Kujihudumia matibabu bila kufikia hatua ya kufanya kitu kama kuuza nyumba.
Umenena vema sana mkuu...
Pole sana mkuuWengine tumeshapita huko, na shida ilikuwa maDr walikuwa wanadanganya kuwa mzee ana tatizo flani linalotibika lakini kwa pembeni wanawaambia watu baki kwamba huyu mzee hana muda mrefu, kansa imesambaa kila mahali. Kukawa na plan ya kwenda India, wakataka vipimo flani ambavyo ilibidi kwenda Muhimbili baada ya kama wiki nikawa na wasiwasi na hali ya mgonjwa maana alikuwa katika hali ambayo hawezi safiri mwenyewe, kumbana Dr mmoja akawa mkweli akasema huyu mzee ana prostate cancer na imeshakula organs zote na cha kufanya sasa nawapa dawa za kupunguza maumivu mrudisheni nyumbani akapumzike. Hakumaliza week 2 mzee akapumzika.
Mimi sio kiranga ndugu yanguHivi kiranga watu wakupinga pinga wanapinga hili pia!?
OkayUmenena vema hapa