Kuna kitu hakipo sawa makanisani, ni muda wa wakristo kuamka na kuhoji

Kuna kitu hakipo sawa makanisani, ni muda wa wakristo kuamka na kuhoji

Mimi ni Mjinga Namba moja,kwa Mambo yahusuyo MUNGU,acha Mimi niitwe Mjinga au vyovyote vile ili mradi wewe umerizika kuwa umenitukana, Kiufupi Tukana hadi roho yako ijisikie vizuri.
Mbona mnapenda kumsingizia Mungu kwenye ulafi wenu?

Mungu hausiki katika hili, huu ni UAMSHO wa kukataa kutumia jina la mungu kubariki unyang'anyi na mbaya zaidi wahanga ni watu maskini ambao tegemeo lao pekee ni life after death, maisha ya duniani wameshapigwa tatu bila
 
Unachanganya mafile, halafu mimi sitaki kumkashifu mtu ila ujuwe mwezi wa Ramadhani wafanyabiashara wa kiti moto, bar na guest house wanalalamika biashara ni ngumu, sijafanya research ni kwa nini kila kipindi cha Ramadhani biashara hizo zinakuwa tete.
🤣🤣🤣
 
Hiyo sio njia sahihi ya kushughulikia migogoro baina yako na jirani yako.Yesu alitoa muongozo wa namna ya kushughulikia migogoro hiyo ktk Mt.18:15-17, imeandikwa hivi.[emoji116][emoji116][emoji116]


Mathayo 18:15 Na ndugu yako akikukosa, enenda ukamwonye, wewe na yeye peke yenu; akikusikia, umempata nduguyo.
Mathayo 18:16 La, kama hasikii, chukua pamoja nawe tena mtu mmoja au wawili, ili kwa vinywa vya mashahidi wawili au watatu kila neno lithibitike.
Mathayo 18:17 Na asipowasikiliza wao, liambie kanisa; na asipolisikiliza kanisa pia, na awe kwako kama mtu wa mataifa na mtoza ushuru.


Kwa hiyo,usiache kwenda kusali jumuiya au Kanisani kwa visingizio vya kitoto vya eti fulani amenikwaza au fulani na fulani hatuelewani.Huu ni ushauri tu.
Ni kwa nini unachaguwa verse unazozipenda wewe tu?

Tukumwagie verse za Biblia hapa kama haujakimbia kuhusu watu wanafki kama wewe? Hata shetani anayajuwa maandiko na alimjaribu Yesu kwa kutumia maandiko.
 
Hakuna anaelia kutoa sadaka ndg katekista, ninachopinga ni michango yenye uelekeo wa anasa na kuwaumiza bure waamini.

Nimekupa mfano wa parokia yangu Kinyerezi, nyumba ya mapadre ipo tulionunua sh 400M haina miaka 10.
Sasa wamekuja upya na mchango wa kujenga nyumba ya ghorofa eti ile haina hadhi.
Wewe unaona ni sahihi? Hao waumini wanaishi nyumba za namna gani?
Umeshawahi kuwauliza Viongozi wako wa Parokia Kwanini wamechukua Maamuzi ya kujenga ghorofa badala ya nyumba mliyokuwa mmeinunua??. Inawezekana mahitaji ni makubwa kiasi Cha kudai ghorofa ijengwe.
 
Huku uchaggani picha linaanza kwanza Padri anaheshimika Kama mungu.

Yaani mtu anaweza kuitwa kwenda kea Mtendaji wa Kijiji au Police aisende lakini akiitwa kwa Padre. Kwanza anapata hofu kubwa kuwa tatizo ni nini[emoji1787]

Na ukifiwa Padre akija ile sadaka ya ibada ya mazishi anabeba anaondoka nayo. Na kwako ni masikini hata ibada ya mazishi hamalizi, anafanya nusu akimaliza naaepa anawaachia waumini waendelee.

Ila binafsi naona utamaduni wa uchaggani ndio umepelekea tatizo kuwa kubwa sana. Maana huku ukipata MSIBA usitegemee kabisa ushirikiano kutoka kwa watu.

Hata Kulia Wala maombolezo Wala huzuni. Kwahiyo kinachofanyika ukipata MSIBA, inabidi uwe na pesa ukodi VITI, MAHEMA, POMBE, NYAMA na MUZIKI.

Muziki ndio utaomboleza pamoja na watu wa kukodiwa ( TARUMBETA).

Bila kufanya hivi Hakuna mtu atajua kwako Kuna msiba. Na kibaya zaidi na kanisani ukiwa umetengwa, utazikwa Kama mzoga was mbwa Koko.

Hii ndio hali HALISI.
Kila nikisoma comments humu ndani nazidi kupata ufumbuzi kuhusu wakristo wanavotapeliwa
 
Ukishaingia mfumo wa jumuia lazima utowe pesa ya kuwa mkatoliki kila mwezi.

Pili harambee za kipuuzi na sadaka nyingi kwenye ibada inaondoa system ya kikatoliki ambayo tulizoea ibada ya misa ya jumapili ni lisaa limoja na nusu tu na ikizidi kwa special case ni masaa mawili tu, sasa kwa huu upumbavu ulioanza ibada inakwenda mpaka masaa matatu, misa ya kwanza mnaingia saa 12 asubuhi mnatoka saa mbili na kitu.

Samahani, naomba nifahamishe, uendeshaji wa ibada au misa kikatoliki una basis 'mapokeo - maandiko' "kwamba: jinsi viongozi wanavyofanya ndivyo Yesu alivyokuwa akifanya au alivyofundisha kimatamshi na kimatendo?"

Zingatia: Utoaji sadaka ni moja ya kitendo
 
Oh!!!,swali zuri sana Mkuu.Ktk Kanisa Katoliki Kuna muongozo wa Ibada ya mazishi uliotokana na Sheria ya Kanisa;Ambapo Marehemu yeyote ambaye aliishi ktk ushirika na Kanisa na MUNGU anapaswa kupewa Heshima ya kuzikwa kwa Misa Takatifu itakayoongozwa na padre au Askofu,lkn ktk mazingira ambayo padre au Askofu hayupo karibu basi Katekista anaweza kumzika mtu huyo kwa ibada maalumu ya mazishi ambayo itazingatia vipengele vyote muhimu vya Ibada ya mazishi ya Mkristo aliyeshirikiana vema na Kanisa.Sasa unawezaje kutofautisha Ibada iliyoongozwa na Katekista kwa Marehemu aliyekuwa mshirika mzuri wa Kanisa na yule ambaye hakuwa mshirika mzuri wa Kanisa??,Jibu ni fupi,yule aliyekuwa mshirika mzuri wa Kanisa ibada itafuata vipengele vyote muhimu, wakati yule ambaye hakuwa mshirika mzuri ibada itakuwa fupi sana,inaweza kusaliwa sala chache tu na Kisha kumzika,na hapa huwa inaangaliwa pia juu ya ndugu za Marehemu kwa nia ya kuwafariji na kuwaasa wasiwe km ndugu yao, Ndio maana km Marehemu hakushiriki ktk Mambo ya Kanisa na ndugu zake pia,uwezekano wa kukosa kabisa mazishi ni mkubwa, anaweza kuzikwa tu km mbwa au mzoga na Serikali au jamii yake.


Kimsingi Kanisa Katoliki halimtengi mtu,Bali mtu mwenyewe kwa akili zake timamu ndio anajitenga na Kanisa (Excommunication).

Muda si mrefu nitaweka hapa muongozo wa mazishi ktk Kanisa Katoliki.Kaa mkao wa kula.

Kwa hiyo ibada inayoongozwa na Padri/Askofu na Katekesta kwa upande mwingine zinautofauti kwa sheria za Kanisa..

Kama kwa sheria ya Kanisa kuna utofauti kwa maana ya hadhi, vipi kwa upande wa imani huyo marehemu aliyeombewa na Padri /Askofu na Katekesta hadhi zao zinakuwa sawa mbele za Mungu.?
 
Huna lolote ulijuwalo, wakati Galileo anasema dunia ni duara nyinyi wahafidhina wa Vaticano si ndio mlimbishia na kusema dumia ni bapa huyu anakufuru?

Kiko wapi sasa Vaticano inakuja kumuomba radhi mtu ameshafariki miaka kibao baada ya kuijuwa kweli na kuishi kumpa heshima ya maktaba Vaticano ya Galileo Archives?

Wewe hakuna unalolijuwa katika kanisa hili kaa kimya.

Hivi Unajuwa baada ya recession iliyotekea miaka hiyo Vaticano ikaanzisha dhua na kutunga cheti cha maondoleo ya dhambi ambacho kilikuwa kinanunuliwa kwa pesa nyingi leo ndio mnadanganywa kwamba ni kitubio? Unayajuwa haya?
Mzee Matola,wewe Unaumwa ugonjwa wa Sonona,mada iliyopo mbele yetu ni juu ya Sadaka na Michango mbalimbali, Sehemu uliyoiquote ni jibu langu kwa muuliza swali kuhusu Taratibu za mazishi,sasa hbr ya Akina Galileo Galilei imekujaje hapa?,Oh!!,mara wewe Hujui kitu,kipi nisichojua kuhusu Kanisa langu Katoliki??, Sasa km kwa upeo wako umeona sijui Kwanini unaniquote na kutoa comment yako??.Anyway Jitahidi kupunguza mawazo ya chuki za kidini utaishi kwa furaha sana.
 
Ni kwa nini unachaguwa verse unazozipenda wewe tu?

Tukumwagie verse za Biblia hapa kama haujakimbia kuhusu watu wanafki kama wewe? Hata shetani anayajuwa maandiko na alimjaribu Yesu kwa kutumia maandiko.
"Kuwa kichaa sio lazima uokote makopo,hata kwenda nje ya utaratibu ni ukichaa pia".-
 
Kuna Parokia zingine Paroko anatembelea waumini majumbani mwao "kubariki" jumuia moja hadi nyingine then unampa the so called SHUKURANI.(kiwango chochote)

Ikitokea ukatoa kiasi ambacho kwa utashi wake Paroko akaona ni kidogo kutokana na hali yako ya maisha aliyoiona hapo kwako,anakataa mnaanza kupandishiana dau kama mnada wa Majembe Auction Mart.😁.

NB:Anaingia hadi ndani na ukizubaa hadi vyumbani!
 
Shida yote ya nini ndugu zangu si bora mje upande wetu waislam
Labda huko unakoishi wewe...

Huku kwetu Ni Yale Yale .. pesa za misaada..za yatima..za sadaka ..zinapigwa vibaya na ugomvi usiokwisha wa kugombea uongozi wa misikiti .. ..

Binadam ndiye bilisi...wa mwanzo...
 
Mbona mnapenda kumsingizia Mungu kwenye ulafi wenu?

Mungu hausiki katika hili, huu ni UAMSHO wa kukataa kutumia jina la mungu kubariki unyang'anyi na mbaya zaidi wahanga ni watu maskini ambao tegemeo lao pekee ni life after death, maisha ya duniani wameshapigwa tatu bila
Endelea kujiamsha wewe uliyelala na akili zako za kuazima.
 
Leo ni Jumapili ya matawi Yesu anaingia Jerusalem, lakini nikitafakari imani yangu ya ufuasi wa kristu napata mashaka makubwa sana.

To declare interest mimi nimezaliwa nimejikuta tu ni mkatoliki kwahiyo nipo hivyo mpaka leo, mahusiano yangu na Mungu naamini ni mazuri kiroho lakini mahudhurio yangu kanisani kwa miaka ya karibuni si mazuri huwa nakwenda na kuacha kwenda.

Basi mambo yasiwe mengi last Sunday nikatimba church kwenye parokia yetu mambo niliyokutana nayo huko ni ya kusikitisha na nathubutu kuita kile alichokikemea mwokozi wetu Yesu kristu kwamba wasigeuze nyumba ya baba yake kuwa pango la walanguzi, kwa hakika hicho ndicho kinachoendelea parokiani kwetu si kanisa tena bali ni pango la walanguzi.

Sisi Wakatoliki huko nyuma tulikuwa tukiwacheka Lutheran kwa utaratibu wa sadaka nyingi na bahasha nyingi kumbe sasa utaratibu huo umeingia kwa speed kubwa kwenye kanisa katoliki ibada ya misa moja sadaka mnatowa mara saba, sina hakika na parokia zingine hali ikoje.

Sasa kila mwanaparokia unapewa kadi ya kuchanga pesa ya kuwa mkatoliki mume na mke 10,000)= kwa mwezi na watoto buku mbilimbili kila mwezi hii ni nje ya sadaka harambee na michango mingine, tunakwenda wapi?

Najuwa wapo watetezi waliolewa mvinyo wa dini watatetea uharamia huu kwa utetezi ni lazima tuchangie ujenzi wa kanisa, hakuna anayekataa hilo na tumekuwa tukijitolea miaka yote kwa kiasi, lakini naamini mtu ambaye yuko free minded hawezi kutetea uharamia huu kugeuza kanisa kuwa pango la walanguzi, na wasiokuwa na pesa za kuamka kwenye mabenchi mara saba kutowa hizo sadaka hawatojisikia vizuri na wataacha kuja kanisani kwa kuteswa kihisa kila watu wakiinuliwa kwenye mabenchi wao hawana kitu.

Hiyo sasa tisa kumi ni hawa jamaa zetu born again, nipo hapa nyumbani namsikiliza mtumishi wa Mungu akitangaza viwango vya sadaka ya kugombowa uzao wa kwanza ni laki mbili, uzao wa pili laki na na nusu, uzao wa tatu laki.

Kutokana na uharamia huu na unyang'anyi unaoendelea kupitia mwamvuli wa dini serikali haiwezi kusaidia lolote katika hili kwa sababu ni partners muhimu in crime.

Kwakuwa waislamu wanajitambuwa sana katika hili ni wakati sasa kwa wakristu wote kuamka na kupinga dhulma hii ambayo cha kusikitisha sasa imeingia radmi kanisa katoliki na hakuna hata mkatoliki mmoja aliwahi kuhoji miradi yote ya kanisa hadi mkombozi bank ipo kwa faida ya nani na inalisaidia vipi kanisa?

Tumsifu Yesu kristu.
Naunga mkono hoja. Hata Yes hapendi kinachoendelea Sasa kwa kutumia jina lake. Yes alikuja kuonyesha njia ya wanadamu kuishi kwa upendo ili siku moja tuwe wote mbinguni. Kuishi kwa kutokumtendea mwenzako kill ambacho hupendi yeye akutendee. Hi haihitaji pesa Wala sadaka. Sadaka mpelekee mhitaji. Mtu mwenye shida. Taasisi za kikristu yaani dini zimeanzishwa na watu wajanja kwa maslahi yao. Hao achana nao. Wewe kazania amri kuu ya Mungu UPENDO. Mpende Mungu kwa moyo wako wote na kwa akili yako yote na jirani yako kama unavyojipenda wewe. Japo Kuna watu wengine hawajipendi
 
Mimi angalau Paroko wetu wa zamani nilimkubari sana maana alikuwa na utaratibu wa kuja vijiwe vyetu mtaani kututembelea kwenye mapub ajuwe tunaishi vipi kondoo wake na anazungusha round mpaka anaondoka hataki mumpe yeye offer anasema yeye ndio amewafuata mtaani ana ela yake.

Kiukweli nilimkubali sana paroko huyu kwa sasa amehamishiwa parokia nyingine miongoni mwa parokia zetu.
Unapenda sana slope.
 
Back
Top Bottom