Kuna kitu hakipo sawa makanisani, ni muda wa wakristo kuamka na kuhoji

Kuna kitu hakipo sawa makanisani, ni muda wa wakristo kuamka na kuhoji

Mkuu unaweza nisaidia sadaka hizi tisa zilikua zipi na mlitoa kwa wakati gani?. Ili ni muhimu usiache kujibu.

Mimi kwangu ilishabaki na sali sala binafsi nyumba. Ikiwa tofauti mara moja moja naenda kanisani nasali na kuondoka. Ukweli michango imekua mingi imefika hatua hadi kanisa wanajisajili kulipa kwa mpesa au tigo pesa. Huwa siaangaiki ata na mchango mmoja. Utasikia kanisa halijaisha, shule ya chekechekea, nyumba ya sisters.

Swala la zaka sijawai toa na sitarajii kama ntakuja kutoa. Ile asilimia 10 ya kipato cha mtu inatofauti gani kodi wanayotoza TRA katika kila faida anayopata mtu. Ni onyonyaji.

Nafikiri hofu ya wengi huwa wana hofu padri hasipokuja siku ya maziko yako. Kwangu ili si hofu maana ntakua mfu sitojua walinitupa au walinivisha nguo gani. Nani alikuja msibani nani hakuja

Hapa ndio naona dini wakati mwingine ni mchongo. Haiwezekani wao wakitaka gari aua nyumba tuwachangie. Ila sisi wauumini tukitaja gari au nyumba tupige magoti tuombe sana.
Suala la sadaka na zaka kwa karne hii naona inamantiki Sana kama utaitumia sadaka yako na zaka yako kusaidia wahitaji na wasiojiweza kuliko kutoa kwenye makanisa ambayo Sasa yamegeuka biashara. There are a lot of needy people out there wanahitaji msaada.
 
Leo ni Jumapili ya matawi Yesu anaingia Jerusalem, lakini nikitafakari imani yangu ya ufuasi wa kristu napata mashaka makubwa sana.

To declare interest mimi nimezaliwa nimejikuta tu ni mkatoliki kwahiyo nipo hivyo mpaka leo, mahusiano yangu na Mungu naamini ni mazuri kiroho lakini mahudhurio yangu kanisani kwa miaka ya karibuni si mazuri huwa nakwenda na kuacha kwenda.

Basi mambo yasiwe mengi last Sunday nikatimba church kwenye parokia yetu mambo niliyokutana nayo huko ni ya kusikitisha na nathubutu kuita kile alichokikemea mwokozi wetu Yesu kristu kwamba wasigeuze nyumba ya baba yake kuwa pango la walanguzi, kwa hakika hicho ndicho kinachoendelea parokiani kwetu si kanisa tena bali ni pango la walanguzi.

Sisi Wakatoliki huko nyuma tulikuwa tukiwacheka Lutheran kwa utaratibu wa sadaka nyingi na bahasha nyingi kumbe sasa utaratibu huo umeingia kwa speed kubwa kwenye kanisa katoliki ibada ya misa moja sadaka mnatowa mara saba, sina hakika na parokia zingine hali ikoje.

Sasa kila mwanaparokia unapewa kadi ya kuchanga pesa ya kuwa mkatoliki mume na mke 10,000)= kwa mwezi na watoto buku mbilimbili kila mwezi hii ni nje ya sadaka harambee na michango mingine, tunakwenda wapi?

Najuwa wapo watetezi waliolewa mvinyo wa dini watatetea uharamia huu kwa utetezi ni lazima tuchangie ujenzi wa kanisa, hakuna anayekataa hilo na tumekuwa tukijitolea miaka yote kwa kiasi, lakini naamini mtu ambaye yuko free minded hawezi kutetea uharamia huu kugeuza kanisa kuwa pango la walanguzi, na wasiokuwa na pesa za kuamka kwenye mabenchi mara saba kutowa hizo sadaka hawatojisikia vizuri na wataacha kuja kanisani kwa kuteswa kihisa kila watu wakiinuliwa kwenye mabenchi wao hawana kitu.

Hiyo sasa tisa kumi ni hawa jamaa zetu born again, nipo hapa nyumbani namsikiliza mtumishi wa Mungu akitangaza viwango vya sadaka ya kugombowa uzao wa kwanza ni laki mbili, uzao wa pili laki na na nusu, uzao wa tatu laki.

Kutokana na uharamia huu na unyang'anyi unaoendelea kupitia mwamvuli wa dini serikali haiwezi kusaidia lolote katika hili kwa sababu ni partners muhimu in crime.

Kwakuwa waislamu wanajitambuwa sana katika hili ni wakati sasa kwa wakristu wote kuamka na kupinga dhulma hii ambayo cha kusikitisha sasa imeingia radmi kanisa katoliki na hakuna hata mkatoliki mmoja aliwahi kuhoji miradi yote ya kanisa hadi mkombozi bank ipo kwa faida ya nani na inalisaidia vipi kanisa?

Tumsifu Yesu kristu.
Ajabu Sasa ya wakristo, ulieleta hii mada Ni muumini mwenzao, lakini utashangaa wataanza kushambulia Waislamu na uislamu, jamaa Ni mazuzu!!
 
Labda huko unakoishi wewe...

Huku kwetu Ni Yale Yale .. pesa za misaada..za yatima..za sadaka ..zinapigwa vibaya na ugomvi usiokwisha wa kugombea uongozi wa misikiti .. ..

Binadam ndiye bilisi...wa mwanzo...
Sawa ila hatujafiki kutozika mtu kisa hakuwa mchangiaji sadaka msikitini au huko unapokaa wewe imetokea
 
Umeshawahi kuwauliza Viongozi wako wa Parokia Kwanini wamechukua Maamuzi ya kujenga ghorofa badala ya nyumba mliyokuwa mmeinunua??. Inawezekana mahitaji ni ma
Umeshawahi kuwauliza Viongozi wako wa Parokia Kwanini wamechukua Maamuzi ya kujenga ghorofa badala ya nyumba mliyokuwa mmeinunua??. Inawezekana mahitaji ni makubwa kiasi Cha kudai ghorofa ijengwe.
Ukisema kiongozi wa Parokia kwamba anaweza kunipa majibu unakosea.
Unafahamu fika kwamba mambo ya kanisa ni up - bottom
Hiyo halmashauri walei inapokea maelekezo toka kwa paroko, wajibu wao ni kugawana majukumu ya utekekelezaji.

Halafu sina haja ya kumuuliza kiongozi au paroko kwasababu ilitangazwa kanisani sababu ni haina hadhi. Kwahiyo suala ni status sio uhitaji.
 
Utaratibu ambao sikubaliani nao ni huu wa usipotoa, basi hupewi huduma kama ubatizo na ndoa. Hili jambo kipindi cha nyuma halikuepo, sijui nani alianzisha. Sikuhizi kutoa sio moyo, ni kulazimisha.
 
Shukurani kwa ufafanuzi.....Ni Marehemu wa aina gani anastahili kuongozwa na Padri ama Askofu, na huyu anaeongozwa na Katekesta sifa zake ni zipi.?
Huduma ya Mazishi/Kuzika (kwa Wakatoliki) inaweza kuongozwa na MTU YEYOTE MKRISTU MKATOLIKI aliyepata kibali /idhinishwa kutoka kwa uongozi Mahalia kuendesha shughuli hiyo.. Lakini Huduma hiyo inapohusisha kuwepo kwa Misa Takatifu ni LAZIMA awe ni Padre au Askofu kwa kuzingatia Uzito/Sensitivity ya Shughuli yenyewe. e.g. Tukio limegusa vipi Jamii husika mathalan akifariki kiongozi mtu maarufu/Mwenye Heshima ya kipekee kiimani, Mzee, Mtu mzima mwenye familia n.k.n.k
Kama shughuli yenyewe itahusu Ibada tu ya Mazishi hiyo inaweza/ itaendeshwa na Katekista au Mtu aliyeidhinishwa na Uongozi Mahalia.
Kama hakuna Katekista, Uongozi (Padre kiongozi) Mahalia humwidhinisha mtu wa kusimamia na kuongoza shughuli hiyo kwa kuzingatia Uadilifu wake, Mcha Mungu (Bidii katika mambo ya Sala/ Kanisa) na anao Uwezo au Uzoefu katika shughuli hiyo.
Naomba kusahihishwa au marekebisho
 
Utaratibu ambao sikubaliani nao ni huu wa usipotoa, basi hupewi huduma kama ubatizo na ndoa. Hili jambo kipindi cha nyuma halikuepo, sijui nani alianzisha. Sikuhizi kutoa sio moyo, ni kulazimisha.
Hama Kanisa.
 
Ukisema kiongozi wa Parokia kwamba anaweza kunipa majibu unakosea.
Unafahamu fika kwamba mambo ya kanisa ni up - bottom
Hiyo halmashauri walei inapokea maelekezo toka kwa paroko, wajibu wao ni kugawana majukumu ya utekekelezaji.

Halafu sina haja ya kumuuliza kiongozi au paroko kwasababu ilitangazwa kanisani sababu ni haina hadhi. Kwahiyo suala ni status sio uhitaji.
Basi km huoni haja acha kulalamika sasa.
 
Hiyo sio njia sahihi ya kushughulikia migogoro baina yako na jirani yako.Yesu alitoa muongozo wa namna ya kushughulikia migogoro hiyo ktk Mt.18:15-17, imeandikwa hivi.[emoji116][emoji116][emoji116]


Mathayo 18:15 Na ndugu yako akikukosa, enenda ukamwonye, wewe na yeye peke yenu; akikusikia, umempata nduguyo.
Mathayo 18:16 La, kama hasikii, chukua pamoja nawe tena mtu mmoja au wawili, ili kwa vinywa vya mashahidi wawili au watatu kila neno lithibitike.
Mathayo 18:17 Na asipowasikiliza wao, liambie kanisa; na asipolisikiliza kanisa pia, na awe kwako kama mtu wa mataifa na mtoza ushuru.


Kwa hiyo,usiache kwenda kusali jumuiya au Kanisani kwa visingizio vya kitoto vya eti fulani amenikwaza au fulani na fulani hatuelewani.Huu ni ushauri tu.
Sawa. Nimekuelewa. Uko sahihi sana. Najipa nafasi kwanza. Nitakwenda pasi na shaka

Sent from my SM-G960U using JamiiForums mobile app
 
Sawa,baki hivyo hivyo,na uwaambie na ndugu zako wote kuwa siku ukifariki wasiwasumbue Watumishi wa MUNGU kuja kukufanyia ibada ya mazishi.Maana watu km nyie huwa mnakuja kuleta shida mkiwa mmefariki na Ndugu zenu wanaanza kulilaumu Kanisa kuwa halipo fair Kumbe ninyi wenyewe mlijichagulia kuishi pasipo kuwa na mahusiano mema na MUNGU,kwa kujitenga na Kanisa (Excommunication).
Nakazia hoja
 
Back
Top Bottom