Kuna kitu hakipo sawa makanisani, ni muda wa wakristo kuamka na kuhoji

Kuna kitu hakipo sawa makanisani, ni muda wa wakristo kuamka na kuhoji

Wakati unatusifia Waislamu, sisi huku wenyewe tunatamani tungekuwa na moyo wa kutoa sadaka kama wenu.

Sisi ni changamoto watu wazito kutoa sadaka, madrasa na misikiti mingi inahitaji ukarabati na shule pia. Ila watu wetu wazito mno wa kutoa sadaka. Sadaka mpaka zitokee kwa waarabu ndio madrasa zijengwe
Haha!kuna jamaa angu ana kisehem kutea copy na ku print...bac kuna jamaa kila baada ya mwez anakuja na kubadilisha tu figure na kuhamishia nyingine..kumbe jamaa anaombea msaada wa kujenga msikit huko singida ....huwa anazunguka sana Tz hii hadi viziwani huko...ila hakuna mchango anaopeleka zaid ya kufanya mahemezi ya familia yake tu....naona kwa ss iv kafanya kama ndo kaz yake
 
Nakuunga mkono asilimia mia moja braza. Mimi hapa nina deni la 500,000(Laki tano) nilipledge kwenye harambee. Nashauri utaratibu wa win win situation utafutwe ili waumini wasipungue kanisani kwa ajili ya michango. Ukienda kwenye Makanisa ya walokole ndo balaa.
 
Leo ni Jumapili ya matawi Yesu anaingia Jerusalem, lakini nikitafakari imani yangu ya ufuasi wa kristu napata mashaka makubwa sana.

To declare interest mimi nimezaliwa nimejikuta tu ni mkatoliki kwahiyo nipo hivyo mpaka leo, mahusiano yangu na Mungu naamini ni mazuri kiroho lakini mahudhurio yangu kanisani kwa miaka ya karibuni si mazuri huwa nakwenda na kuacha kwenda.

Basi mambo yasiwe mengi last Sunday nikatimba church kwenye parokia yetu mambo niliyokutana nayo huko ni ya kusikitisha na nathubutu kuita kile alichokikemea mwokozi wetu Yesu kristu kwamba wasigeuze nyumba ya baba yake kuwa pango la walanguzi, kwa hakika hicho ndicho kinachoendelea parokiani kwetu si kanisa tena bali ni pango la walanguzi.

Sisi Wakatoliki huko nyuma tulikuwa tukiwacheka Lutheran kwa utaratibu wa sadaka nyingi na bahasha nyingi kumbe sasa utaratibu huo umeingia kwa speed kubwa kwenye kanisa katoliki ibada ya misa moja sadaka mnatowa mara saba, sina hakika na parokia zingine hali ikoje.

Sasa kila mwanaparokia unapewa kadi ya kuchanga pesa ya kuwa mkatoliki mume na mke 10,000)= kwa mwezi na watoto buku mbilimbili kila mwezi hii ni nje ya sadaka harambee na michango mingine, tunakwenda wapi?

Najuwa wapo watetezi waliolewa mvinyo wa dini watatetea uharamia huu kwa utetezi ni lazima tuchangie ujenzi wa kanisa, hakuna anayekataa hilo na tumekuwa tukijitolea miaka yote kwa kiasi, lakini naamini mtu ambaye yuko free minded hawezi kutetea uharamia huu kugeuza kanisa kuwa pango la walanguzi, na wasiokuwa na pesa za kuamka kwenye mabenchi mara saba kutowa hizo sadaka hawatojisikia vizuri na wataacha kuja kanisani kwa kuteswa kihisa kila watu wakiinuliwa kwenye mabenchi wao hawana kitu.

Hiyo sasa tisa kumi ni hawa jamaa zetu born again, nipo hapa nyumbani namsikiliza mtumishi wa Mungu akitangaza viwango vya sadaka ya kugombowa uzao wa kwanza ni laki mbili, uzao wa pili laki na na nusu, uzao wa tatu laki.

Kutokana na uharamia huu na unyang'anyi unaoendelea kupitia mwamvuli wa dini serikali haiwezi kusaidia lolote katika hili kwa sababu ni partners muhimu in crime.

Kwakuwa waislamu wanajitambuwa sana katika hili ni wakati sasa kwa wakristu wote kuamka na kupinga dhulma hii ambayo cha kusikitisha sasa imeingia radmi kanisa katoliki na hakuna hata mkatoliki mmoja aliwahi kuhoji miradi yote ya kanisa hadi mkombozi bank ipo kwa faida ya nani na inalisaidia vipi kanisa?

Tumsifu Yesu kristu.
Na Yale Maelfu kumi kumi unayoyaacha pale kaunta ya baa Kila wiki,mbona huyalalamikii.
 
Sema tunaweza kuchukia kutoa kanisani ila kwenye mambo mengine ya kawaida tunatoa bila kujiuliza
1.betting
2.kuhonga
3.bia,soda ,vilevi mbali mbali
4.kulipia kuangalia mipira
5.kwenda beach na kuspend hela
Mungu anatuhurumia sana kwa rehema zake ila binadamu sisi ni wabinafsi sana
 
Naupongeza Uongozi mzima wa Kanisa kubwa Bora ambalo mwanzilishi wake ni Kristo mwenyewe. Kanisa Katoliki Jimbo la Dsm kwa Kuwa nimeshuhudia mchango wenu pale mlipotuchangia parokia yetu kununua mali ilokuwa ikiuzwa kwa zaidi ya milioni 200.
Ahsante.
 
Wewe hama kanisa, dini au achana na dini kabisa. Haya ni malalamiko yasiyokuwa na msingi
 
Wangekuwa wanajenga hata hospital watu watibiwe bure ili kurudisha shukran wao kila siku michango na haiishi jamani
 
Kuna ile ya kuwataka waumini waliofiwa na wapendwa wao eti watoe sadaka kubwa kubwa kadri wawezavyo kama kikokotoo cha kuwawezesha hao wapendwa wao waliotangulia mbele ya haki kupata ahueni ya maisha huko kaburini. Yaani mimi hii haijawahi kuniingia akilini kabisa.

Hehehehe wizi kabisa
 
Mkuu, hata ukitoa unaweza usipewe huduma vilevile!

Mimi mama yangu mzazi alikua kiongozi wa jumuia huko kijijini na alikua mtoa sadaka asie na kifani, shughuli zote za ujenzi wa kanisa alishiriki kikamilifu kwa maisha yake yote mpaka amezeeka.

Bahati mbaya akaja kupata tatizo la kiafya ambalo limemuweka kitandani zaidi ya miaka 10 sasa. Cha ajabu eti kila mwaka analetewa bahasha ya zaka na kanisa linatishia kwamba akifa halitamzika kama sisi watoto hatutakua tunatoa hela za kwetu na zake!

Sasa mimi najiuliza, mtu ambae amelala kitandani hilo fungu la 10 analitoa wapi? Tangu amelala kitandani, kanisa limemsaidia vipi? Michango yote aliyochanga tangu akiwa binti mdogo mpaka sasa ni mzee, haijatosha tu? Ni mpaka tone la mwisho??

Ni wezi kabisa yaan kanisa halimisaidii muumini
 
Mkuu, hata ukitoa unaweza usipewe huduma vilevile!

Mimi mama yangu mzazi alikua kiongozi wa jumuia huko kijijini na alikua mtoa sadaka asie na kifani, shughuli zote za ujenzi wa kanisa alishiriki kikamilifu kwa maisha yake yote mpaka amezeeka.

Bahati mbaya akaja kupata tatizo la kiafya ambalo limemuweka kitandani zaidi ya miaka 10 sasa. Cha ajabu eti kila mwaka analetewa bahasha ya zaka na kanisa linatishia kwamba akifa halitamzika kama sisi watoto hatutakua tunatoa hela za kwetu na zake!

Sasa mimi najiuliza, mtu ambae amelala kitandani hilo fungu la 10 analitoa wapi? Tangu amelala kitandani, kanisa limemsaidia vipi? Michango yote aliyochanga tangu akiwa binti mdogo mpaka sasa ni mzee, haijatosha tu? Ni mpaka tone la mwisho??
Ndio Mjue Mnapigwa
 
Sisi parokia yetu imezaa parokia tatu, unaweza kuelewa machozi na damu tuliyopitia.

Tuna nyumba ya masista, tuna nyumba ya mapadri ya zamani, ikajengwa ghorofa likaja hilo ghorofa likaonekana dogo utadhani mapadre wetu ni matembo tukajenga ghorofa nyingine mpya kubwa.

Tumemnunulia paroko Prado, tuna dispensary tuna maternity tuna Ambulance tuna nursery school, kama hiyo haitoshi kuna nyumba nne jirani tumezinunuwa tumevunja ndio umeanza upuuzi eti tujenge nyumba ya mama bikira Maria.

Yani the way nilichojifunza hakuna kipindi mtaachwa mpumuwe ni kutwishana mizigo mwaka mzima.

Ehee na wenyewe wanawafaidisha nin?
 
Ukishaingia mfumo wa jumuia lazima utowe pesa ya kuwa mkatoliki kila mwezi.

Pili harambee za kipuuzi na sadaka nyingi kwenye ibada inaondoa system ya kikatoliki ambayo tulizoea ibada ya misa ya jumapili ni lisaa limoja na nusu tu na ikizidi kwa special case ni masaa mawili tu, sasa kwa huu upumbavu ulioanza ibada inakwenda mpaka masaa matatu, misa ya kwanza mnaingia saa 12 asubuhi mnatoka saa mb

Daaah! Nilifikiri Ni Mimi tu inafikia hatua siendi kanisani Kama ninasadaka haifiki 5000 maana utapata psychological torture but,si kweli kwamba sipendi kusali ila Kuna aibu wenzio wanaponyanyuka wote unabaki wewe tu kwenye benchi halafu unayo afya tele !kazi hasa sijui tunafanyaje wakati mwingine njia nzuri ya kusali naikosa sijui Ni ipi michango Ni kikwazo sana
Huendi kanisan kisa sadaka? Unahofia macho ya watu? Sio nzuri, Mungu akijua huna sadaka inatosha, lakin usiache enda Ibadan kisa sadaka, Hapo unakuwa hutoi sadaka cz utakuwa unafuata taratibu za ibada. Sadaka inatolewa kwasbb unampenda Mungu, (Moyo wa kupenda) lakin ukitoa kama taratibu za Ibada utalalamika Kila siku. Nenda Kaabudu usibaki nyumbani
 
Kama hujui mimi nilikuwq mnistrant mpiga chetezo ila hawa RC wamekuwa wazinguzi sana wahitaji unachanga tena na wakati sadaka ya pili ilikuwa ni kwenda kuwaona wahitaji in short hawa ma padre nao wamestuka wana familia tunalisha familia zao
Kuwa ministrant sio hoja.Kama wewe hutaki kutoa sisi wengine tutamtolea MUNGU maana kuna baraka nyingi ktk kutoa.
 
Sema tunaweza kuchukia kutoa kanisani ila kwenye mambo mengine ya kawaida tunatoa bila kujiuliza
1.betting
2.kuhonga
3.bia,soda ,vilevi mbali mbali
4.kulipia kuangalia mipira
5.kwenda beach na kuspend hela
Mungu anatuhurumia sana kwa rehema zake ila binadamu sisi ni wabinafsi sana
Kila mtu anataka atoe ili apate makanisa wao wanapokea na kujinemeesha wao Tu ingekuwa waumini wao wanalipa Ada pungufu kwenye mashule Yao au vyuoni au kwenye mahosspitali Yao wala wasingekuwa wanaumia ivi shule tunajenga pamoja na bado tunazidi kuiudumia Ila Ada kubwa kuliko kawaida gharama za hospital ndyo usiseme kwann watu wasilalamike
 
Siku moja nimemtembelea mzee wangu nilipofika akaniambia anadaiwa elfu hamsini kanisani kwa ajili ya harambee.Akanieleza kuwa kila jumuiya imepangiwa kiasi flani cha fedha ambazo zimegawanywa kwa kila nyumba.Mzee wang anakaribia miaka 80..Na alinieleza kuwa siku ya harambee kila familia wanakuwa wanasomwa kanisani mnapita mbele kwenda kukabidhi hicho kiasi cha fedha na kama huna lazima utoe sababu za maana hapo na linakuwa deni mpaka ulilipe. Mambo yamekuwa magumu mno siku hizi.
Pole sana.
Mimi nakuwa mkali sana kwa hawa viongozi wa dini wakina na haya mambo.
Kuna siku wale vijana wanajifanya wajuaji wameitisha kikao eti tutengeneze mfuko wa kusaidia maisha ya Mchungaji, hapo kumbuka ana fungu la kumi na mengineyo...niliwatolea uvivu, nikawaambia Yesu mwenyewe alikua seremala ili aishi,mchungaji atafute chanzo cha mapato.nadhani walimwambia maana upendo ulikata.
 
kweli dunia imekwisha!!
yaani muumini wa kanisa unalalamika kutoa sadaka?!
hujui umuhimu wa sadaka kwako binafsi na kwa familia yako?!

Elimu inahitajika juu ya Kutoa Sadaka ktk nyumba za ibada.
Hatulalamiki sadaka,Bali michango.

Watumishi wanaishi maisha ya anasa na pesa zetu.

Bora turudi old school, tunapeleka mazao na mifugo tunachinja na kuchoma moshi upande mbinguni. Sasa mapesa yote wanayaita sadaka wanaweka kwenye acc zao .
 
Mh ingekuwa hivyo basi pia wachamungu wa kweli wangekuwa wengi lakini tunaona watu wanadini ila bado wanafanya na mambo yenye kusababisha kwenda motoni.

Hilo unalizungumziaje?
dini imekuwa ni ya kutakatishia pesa,kujikomba na kujitafutia sifa mbele za watu
 
Ukiona huko Katoliki na Lutheran sadaka zinakutisha na kukuchosha basi jaribu makanisa ya Pentekoste ndio utakiona cha mtema kuni.

Huko Pentekoste utatakiwa kutoa
1. 10% ya kipato chako chochote (kama una mshahara wa 1m kwa mwezi, basi kila mwezi laki moja lazima pastor aikunje mfukoni, na pastor atataka kuona mpaka salary slip)

2. Kuna sadaka za shukrani kila unapofanikiwa jambo lolote (na hii inapaswa kuwa sadaka nono fulani)

3. Kuna sadaka ya kusindikizia maombi yako kila unaposaka kuombewa mambo yako. (Hapo utapigwa mikwara kibao)

4. Kuna sadaka ya kuchangia shughuli mbali za kanisa (kuanzia ujenzi, vyombo vya muziki, uinjilisti, suti ya mchungaji, gauni la mama mchungaji nk)
5. Washirika kwenda kusaidia kazi za mchungaji, iwe kilimo,ujenzi n.k

6. Nowadays, michango ya kuwanunulia wachungaji magari...ila sisi wanatuwekea mikono wakituombea tupate magari wakat wao wanachangisha
 
Back
Top Bottom