Shimba ya Buyenze
JF-Expert Member
- Dec 22, 2014
- 182,097
- 1,099,383
Nimekuelewa mkuu wangu, lakini mimi huwa naboreka sana tena sana na mtu anayeingilia uumbaji wa mungu kumuambia mtu kasoro yake ya kimaumbile ni kumkosea mungu kwa mfano mtu akuongelee vibaya ukilema wako,ufupi wako,urefu wako,upofu wako,ubaya wako,mdomo wako kwa ujumla vile vitu vilivyo nje na uwezo wa binadamu kuvilekebisha ni jambo baya mno na lisilo sameheka mbele za mungu. Mimi namuombea aishi maisha marefu sana tena ikiwezekana apate mali nyingi mno,lakini kwenye la mimba aishie kujibebesha mimba feki tu maana anamkosoa sana mungu.Wema ana malipo yake kwenye hilo na atalipwa accordingly lakini sisi kama binadamu tuna jukumu la kuwaombea watu kama hawa kwakuwa nasi tuna mapungufu yetu na tunaombewa na wengine
AOMBAYE NAYE HUPEWA...JE ALIOMBA MSAADA KUHUSU HAYO MAISHA ANAYOISHI?,,....AU WEWE UMEHISI ANAHITAJI KUSAIDIWA?Ameshasemwa sana kwa ubaya ameshaandikwa sana kwa ubaya ameshakuwa na kashfa nyingi...ni wakati sasa wa kumwangalia kwa jicho la tatu.
Hatuwezi kumweka kwenye kundi la malaika wa kifo kwakuwa wapenzi wake wengi bado wako hai. Ni binti mwenye nyota kali ya mafanikio kwake na kwa wapenzi wake pia na nyota yake hii ilichanua mapema kabisa hata akapata mafanikio mengi kwa muda mfupi na akiwa bado mdogo.
Nyota yake bado inawaka lakini imechezewa imefanyiwa kitu kibaya Wema wa bahati sasa ni wema wa mikosi nuksi na balaa.
Habari zake za kuandikwa kila siku kwa mabaya zimemfanya achukiwe na wengi bila kufikiri zaidi..nilikuwa mmojawapo na nikasema ni utoto akikua ataacha...mabinti wengi wamepitia hiki kipindi hata hapa JF tunao.
Wema amejijengea maadui wengi kuliko marafiki, Wema amekuwa centre ya habari kwa lolote afanyalo au linalomtokea iwe kwa ubaya au kwa wema
Lakini hebu tujirudi na kujitafakari upya...
Tabia ya Wema ya sasa ina mahusiano ya karibu na makuzi yake na hasa malezi ya mama! Je tuna la kujifunza hapa?? Tukumbuke na sisi ni wazazi.
Wema wa sasa anaporomoka kuanzia mwili shepu mahusiano nk nk...wengine wengi wamepitia haya lakini yakapita yakaisha, ya Wema hayaishi kila uchao tatizo liko wapi? Je haters wake wamefanya yao kwenye ulimwengu wa giza?
Wema anahitaji faraja ya kila mmoja sasa, kila dakika na kila sekunde pamoja na mapungufu yake yote lakini bado ni binadamu kama sisi mwenye hisia maumivu na roho ya nyama.
ASAIDIWE!
Ana nyota ya mafanikio maana yake ukitembea nae una winAna mafanikio gani huyo binti?
Mbona umefurahi sana mkuu? Au unawaza yale mambo nini? Itabidi ujipange sawasawa kwani binti kama huyu alishaona vingi na ukienda na staili za Kipare aisee waweza adhirika. Good luck sir![emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23]
Ngoja nikuongezee swali la kujiuliza, yeye anawachukia wenzake kwa lipi ???? ( ukisema haujui basi na wewe ni ktk wale waliomjua wema baada ya mimba feki )Hiv umchukie wema kwa lipi!??
Wewe unampenda au unamchukia?Hiv umchukie wema kwa lipi!??
mshana jr, hivi unaupata wapi ujasiri wa kumtetea huyu shori.
Itazame hali yake kwa jicho la kiroho utagundua kituKUNA WAKATI "UNATAKIWA KUWA NA MOYO KAMA WA MWENDA WAZIMU" KUMTETEA WEMA SEPETUNGA....BY THE WAY ANGEKUWA ANAHITAJI MSAADA NAJUA MAGAZETI YOTE YA UDAKU YANGESHAANDIKA NA TAYARI UNGEKUTA MITANDAO YOTE YA KIJAMII NA TEAM ZAO WAMESHAJAZA MITANDAO.
NAPINGA HOJA...KATIKA LIST YA WATU WALIOMGONGA WEMA NINAO USHAHIDI TOSHA KUWA HAWAJAFANIKIWA AU KU-WIN KAMA WATU WA MUJINI MUNAVYOSEMAAna nyota ya mafanikio maana yake ukitembea nae una win