KERO Kuna maafisa Manispaa ya Iringa, Mtaa wa Kajificheni wamechimba mashimo barabarani na kuyatelekeza

KERO Kuna maafisa Manispaa ya Iringa, Mtaa wa Kajificheni wamechimba mashimo barabarani na kuyatelekeza

Hii ni kero ambayo mwananchi ameiwasilisha JF akitaka wahusika kuchukua hatua
Joined
Sep 23, 2024
Posts
64
Reaction score
43
WhatsApp Image 2024-12-04 at 12.54.19_d9f651fe.jpg

WhatsApp Image 2024-12-04 at 12.54.19_fbc6e2fa.jpg
Mimi ni Mkazi wa Manispaa ya Iringa, Kata ya Ilala, Mtaa wa Kajificheni kwa niaba ya wenzangu tunaomba msaada wa kusemewa kuhusu shimo lililotelekeza kwa dhumuni la kutengeneza ‘kalavati.

Kuna Maafisa ambao walikuwa wakishirikiana na Uongozi wa Serikali za Mtaa kuchimba mashimbo hayo kwa ajili ya kile walichoeleza kuwa wanaweka Kalavati, lakini sasa ni zaidi ya mwezi hakuna kinachoendelea.

Wamechimba wametuachia mashimo ambayo ni hatarishi kwetu, watumiaji wengine wanaopita hapo na hasa Watoto, kwani jirani nae neo hilo kuna Shule.

Hivyo, Wanafunzi wengi wamekuwa wakipita hapo, na sasa hivi ambapo kuna mvua zinanyesha, mashimo yanakuwa hatari zaidi.

Tunaomba wanaohusika waje wamalizie kazi waliyoianza, wamesababisha limekuwa eneo hatarishi.
WhatsApp Image 2024-12-04 at 12.54.17_d9fa99a8.jpg

WhatsApp Image 2024-12-04 at 12.54.16_c8d39953.jpg
 
Back
Top Bottom