Kuna madhara yoyote ukiachana na mtu ambaye ushamlipia mahari na kumvisha pete ya uchumba?

Kuna madhara yoyote ukiachana na mtu ambaye ushamlipia mahari na kumvisha pete ya uchumba?

Wana JamiiForums hope mko poa kabisa

Naomba kuuliza hili maana linanitesa sana. Mimi nilikuwa na mpenzi wangu ambaye nimemlipia mahari na nikamvalisha pete.

Ila mimi baada ya kuona aeleweki nikampotezea Swali ni kuna madhara yoyote ukiachana na mtu ambaye ushamlipia mahari na kumvisha pete ya uchumba.
Hata mimi nafikiria kufanya maamuzi hayo lakini sijatoa mahali wala sijamvalisha pete ya uchumba
 
Mjínga nn.

Hiyo Pesa ya Mahari, ungempa Mama yako ,siangekuombea Baraka.


Kama wanakuzengua, Komaa wakurudishie Mahali.
 
Kiroho hapo ulishaungana naye kimahusiano. Makabila mengine ukishatoa mahari tayari huyo ni mkeo.

Kumvisha pete huwa ni utambulisho kuwa huyu mwanamke ameshakuwa -booked hivyo unaiambia familia yake wasipokee mwanaume mwingine.

So nashauri mchukue mshenga mkavunje huo muunganiko ili mwanamke awe huru na wewe uwe huru.

Na huwa si ngumu, ni mazungumzo tu halafu wao wanarejesha kiasi kidogo na ile pete kama ishara ya kuvunja kilichofanyika awali.

Na hapo mahusiano yanakuwa yamekufa baina yenu.

Ustaarabu ndio huo, dunia inazunguka na sisis ni Pipo.
 
toasababumalay wewe
Unajiita una hela na umeajiri watu hata kuandika hujui... Huna ustaarabu kabisa mdogo wangu, kila sehemu michango yako huwa ni ya kipuuzi tu! Matusi, kuandika visivyoeleweka na kujiona we ndio wewe

JF ni sehemu nzuri sana ya kutengeneza mahusiano mazuri na watu, kuna watu wengi wa aina mbalimbali ambao watakutoa hapo ulipo kwenye maisha magumu ya ugali na kumbikumbi, angalau na wewe sehemu ukivaa suruali ikukae. Endelea ku-portray upumbavu ulionao hivyohivyo kwenye public alafu utakuja kuona matokeo yake mwisho wa siku.

Kuna mwenzako hivyohivyo alikuwaga anajifanyaga ana hela, yeye tajiri, yeye ndio yeye... Yalimshinda, akafungua nyuzi ya kuomba msamaha na akaweka wazi maisha yake magumu asaidiwe kazi. Endelea kuleta ukatuni kwenye mambo ya maana. 😊
 
Chochote unachokifanya kama kitamuumiza mtu hisia zake kuna madhara.

Mfano, umelipa mahari, na umemvisha pete ya uchumba. Hayo yote umewashirikisha ndugu zake na ndugu zako bila kusahau marafiki na majirani zenu. Lengo likiwa ni kufunga ndoa.

Sasa usipomuoa huyo mchumba wako utawaumiza zaidi kihisia wazazi wake na ndugu zake. Pia yeye mwenyewe utamuumiza kihisia sababu wapo watakao mdhihaki kwa kutolewa mahari na kuachwa kabla hata ya ndoa.

Machozi na manung'uniko ya watu unaowaumiza kwa namna moja ama nyingine huwa hayakuachi salama.

Kuna kitu wazungu wanaita "divine retribution", lazima itakupata kama wewe ndiye mwenye hatia hata kama sio leo, ipo siku yatakupata.

Amini nakwambia kuna Wanawake machozi yao yana mikosi sana.

Na ndiyo maana mnaambiwa kabla ya kufanya maamuzi yoyote yale, tafakari kwa kina. Ulipaswa kutafakari kabla ya kutoa mahari na kumvisha pete ya uchumba.
Nimekushangaaa zaidi ya mara7000!!!

Yaani umegundua haeleweki kisa machozi uingie naye kwenye ndoa?

Aisee heri nusu Shari kuliko Shari kamili mkuu. Mwache alie ajutie ujinge wake na aambiwe nimeamua kukuacha Kwa sababu ABC sitaweza.

Wanawake wanatuacha hata kama kesho ni harusi yenu anatoroshwa na mwingine!!
 
Wana JamiiForums hope mko poa kabisa

Naomba kuuliza hili maana linanitesa sana. Mimi nilikuwa na mpenzi wangu ambaye nimemlipia mahari na nikamvalisha pete.

Ila mimi baada ya kuona aeleweki nikampotezea Swali ni kuna madhara yoyote ukiachana na mtu ambaye ushamlipia mahari na kumvisha pete ya uchumba.
Madhara yaliyopo ni kwamba UTAROGWAAAA
 
Back
Top Bottom