Kuna mbinu za makusudi za kuiua Serengeti ya Tanzania na Masai Mara ya Kenya ili kukuza Dubai Safari Park kwa ajili ya utalii wa wanyama wa porini?

Kuna mbinu za makusudi za kuiua Serengeti ya Tanzania na Masai Mara ya Kenya ili kukuza Dubai Safari Park kwa ajili ya utalii wa wanyama wa porini?

Synthesizer

Platinum Member
Joined
Feb 15, 2010
Posts
12,699
Reaction score
22,598
Nadhani hivi karibuni kila Mtanzania na ulimwengu mzima kwa ujumla, wameshangazwa na kufadhaishwa na kauli ya Raisi Samia kutoa agizo kwamba madini yaliyoko Serengeti yachimbwe, kwa sababu simba na tembo hawali madini.

Tangazo la raisi Samia
1721636978610.png

Sasa labda watu wengi wasichoelewa ni kwamba, kwa miaka kadhaa, UAE wamefanya jitihada kubwa ya kutengeneza mazingira ya "Serengeti" huko Dubai, kwa lengo la kukuza utalii wa wanyama pori huko Dubai. Na kila mtu anajua kwamba wengi wa wanyama waliopelekwa Dubai Safari Park wametoka Tanzania, na bado hadi leo wanapelekwa. Hii ni kutia ndani na tembo, simba, viboko, vifaru, nyoka, vinyonga, fisi, ndege, swala, duma, nyani, twiga, kenge, mamba, sokwe, chui, nk. Dubai walichofanya ni kutengeneza kwa gharama kubwa mazingira kama ya Serengeti huko Dubai, kutia ndani na mito, misitu, miamba nk, na kuingiza wanyama kwenye mbuga hii "artificial savanna".

Baadhi ya picha katika Dubai Safari Park ni hizi
1721636908591.png


Lengo la UAE ni kuteka biashara ya utalii wa wanyama pori, hasa kutoka Afrika, ambayo ndio mshindani mkubwa wa Dubai Safari Park. Hivyo, kwa namna moja au nyingine, Serengeti ikifa, basi Dubai Safari Park itakuwa mdadala mkubwa wa Serengeti.

Athari ya kuchimba madini ndani ya Serengeti ni kuiua Serengeti, na siyo Serengeti tu, bali pia Masai Mara ya Kenya, kwa sababu Masai Mara ni sehemu ya Serengeti. Hivyo hili ni jambo ambalo litaathiri sana utalii wa wanyama pori Tanzania na Kenya, na atakaefaidika ni UAE na Dubai. Kwa hiyo basi, ni jukumu la Watanzania na ndugu zetu Wakenya kuungana na kukosoa na kupinga kwa nguvu zote uamuzi huu wa raisi Samia, kwamba hauna manufaa ya muda mrefu ya nchi zetu, bali manufaa ya muda mrefu ya Dubai. Madini yeyote katika Serengeti yakichimbwa, sana sana yatadumu kwa mika 20-30, na yatakapoisha hakutakuwa tena na Serengeti wala Masai Mara.

Kumbuka, mazingira ya utalii katika Dubai Safari Park ni ya kisasa sana, luxury, lakini bado hawajaweza kutoa ushindani mkubwa kwa Serengeti na Masai Mara. Sasa je, kuna mbinu za makusudi za kuziua Serengeti na Masai mara ili kusiwe na ushindani mkubwa kwa Dubai Safari Park?

Sasa ndio maana tunajiuliza, hili wazo la kuchimba madini katika mbuga ya Serengeti, ambalo kwa muda mrefu TANAPA wamelipinga kwa nguvu zote, ni la raisi Samia mwenyewe, au ushauri kutoka Dubai? Na mnafikiri nani atapewa mikataba ya kuchimba madini ndani ya Serengeti, kampuni toka Dubai? Je atachimba madini hayo kwa lengo la kutoathiri wanyama wa Serengeti?

Jambo hili kwa sasa linahusishwa pia na mabadiliko ya baraza la mawaziri la hivi karibuni, hususa kumuondoa Jerry Slaa katika wizara ya ardhi ambako ameonekana kama kero kwa baadhi ya watu kutia ndani "wawekezaji" toka nchi fulani fulani ambazo sitaki kuzitaja. Pia limemgusa Makamba wizara ya mambo ya nje. Je, wamekuwa kikwazo katika mipango kama hii ambayo inahusishwa na kuiua Serengeti na Masai Mara kwa manufaa ya Dubai?

Tukumbuke documentary ya TANAPA - Serengeti Shall Never Die, chini ya raisi yeyote wa Tanzania.

Kwa wale msioijua Dubai Safari Park bofya hapa

View: https://www.youtube.com/watch?v=us8Sl-w9n20
 

Attachments

  • 1721636733690.png
    1721636733690.png
    768.5 KB · Views: 8
  • 1721636776466.png
    1721636776466.png
    797.7 KB · Views: 6
Kwa ukubwa wa Serengeti kama 10% tu ya eneo lake litakuwa na madini either dhahabu au madini ya Vito kama safire n.k basi ni heri yachimbwe tu. Mapori yako mengi. Artificial safari ya Dubai haitaweza kushindana na Tanzania yenye hifafhi kama utitiri.
 
Kwa ukubwa wa Serengeti kama 10% tu ya eneo lake litakuwa na madini either dhahabu au madini ya Vito kama safire n.k basi ni heri yachimbwe tu. Mapori yako mengi. Artificial safari ya Dubai haitaweza kushindana na Tanzania yenye hifafhi kama utitiri.
Nakubali, lakini mtu mwenye mbinu ya kuua Serengeti atatumia hoja kama hizo, kwamba mbona ni kidogo tu? Na unajuaje hayo madini yapo sehemu ndogo tu ya Serengeti? Na ni wakati gani kadiri unavyochimba madini na kukuta yapo mengi, utasema aaah, sasa basi tuishie hapa kwenye kuchimba 50% ya Serengeti?

Point yako ni sawa na kusema nitamchukua dada poa lakini nitagusa tu, kwa hiyo sio tatizo!
 
Kwa ukubwa wa Serengeti kama 10% tu ya eneo lake litakuwa na madini either dhahabu au madini ya Vito kama safire n.k basi ni heri yachimbwe tu. Mapori yako mengi. Artificial safari ya Dubai haitaweza kushindana na Tanzania yenye hifafhi kama utitiri.
Samia ataharibu nchi yetu baada ya miaka 5 atarudi kwao Zanzibar huku Watanganyika tukimuangalia tu.

Yeye ndani ya miaka 5 anataka afanye kila kitu, auze bandari, auze mbuga za wanyama, akope mikopo isiyo ya kawaida, abinafsishe kila kitu kwa miaka 5 tu.

Angalia, ndani ya miaka 3 amekopa Trilioni 35, ndani ya miaka 3 ameuza bandarini xote, ndani ya miaka 3 anataka abinafsishe mbuga zote za wanyama, LNG, karibu kila kitu. Baada ya hapo atarudi kwao Zanzibar watanganyika tukibakia na madeni na mikataba ya kimangungo.
 
Nakubali, lakini mtu mwenye mbinu ya kuua Serengeti atatumia hoja kama hizo, kwamba mbona ni kidogo tu? Na unajuaje hayo madini yapo sehemu ndogo tu ya Serengeti? Na ni wakati gani kadiri unavyochimba madini na kukuta yapo mengi, utasema aaah, sasa basi tuishie hapa kwenye kuchimba 5o% ya Serengeti?

Point yako ni sawa na kusema nitamchukua dada poa lakini nitagusa tu, kwa hiyo sio tatizo!
Nakwenda mbali zaidi ni kwamba kama 10% ya eneo la Serengeti litachimbwa madini basi itapatikana pesa nyingi sana itakayoweza kuendesha nchi bila kuyumba kwa miaka kadhaa, na kama asilimia zitazidi na pesa itaongezeka hivyo ustawi katika jamii utaongezeka.
Tuna hifadhi nyingi sana. Tuna mapori tengefu mengi , Dubai mwenye kieneo kidogo tena artificial hataweza kukompiti na Tanzania kwenye wild tourism labda tu kwasababu ya ujinga wa watu wachache watakaosomamia hizo hifadhi zetu
 
Nakwenda mbali zaidi ni kwamba kama 10% ya eneo la Serengeti litachimbwa madini basi itapatikana pesa nyingi sana itakayoweza kuendesha nchi bila kuyumba kwa miaka kadhaa, na kama asilimia zitazidi na pesa itaongezeka hivyo ustawi katika jamii utaongezeka.
Tuna hifadhi nyingi sana. Tuna mapori tengefu mengi , Dubai mwenye kieneo kidogo tena artificial hataweza kukompiti na Tanzania kwenye wild tourism labda tu kwasababu ya ujinga wa watu wachache watakaosomamia hizo hifadhi zetu
Na hiyo asilimia 10% ya Serengeti ni kakipande kadogo pembeni mwa Serengeti tutakapochimba, kwa hiyo hakuna tatizo? Ndani ya mbuga ya Serengeti, hata kama ni eneo la 2% ya mbuga, haifai kabisa kuchimba. Suala sio kuchimba tu, ni pamoja na logistics za kuendesha mradi wa uchimbaji kutia ndani wafanya kazi, nyumba za kuishi, magari, mitambo, uwanja wa ndege, umeme, maji, vumbi, sumu za ku process madini, nk! Kuna sababu za msingi kwa nini TANAPA walisema ni marufuku! Na kumbuka, Serengeti ya wanyama itaishi muda gani, na madini ndani ya Serengeti yatachimbwa kwa muda gani? Is it worth it kuharibu kitu cha kudumu kwa ajili ya kitu cha faida ya muda mfupi?

Waulize wachumi wakufanyie hesabu net present value ya Serengeti kama mbuga ya Wanyama, na Serengeti kama mradi wa madini!

Lakini swali la msingi, ni kwa kiwango gani Tanzania inafaidika na madini tuliyonayo ambayo inabidi yachimbwe na kampuni za kigeni? Dhahabu, almasi, Tanzanite, gesi nk, ni kwa kiasi gani vimetunyanyua sana kiasi kwamba leo tukivikuta ndani ya Ngorongoro ni afadhali tuharibu Ngorongoro ili kuvipata?
 
Serengeti si ya Samia. Si ya kujiamulia tu kufanya unachotaka. Ile ni urithi wa dunia.

Ikolojia yake tu haipaswi kuwa disturbed kwa kuweka lami. Lazima UNESCO wakupe ruhusa ya kufanya hivyo. Ije kuwa shughuli za uchimbaji? Kuna idadi kubwa sana ya dollars zinamwaga kuitunza Serengeti. Watu wanatoa pesa zao za misaada kuendeleza hifadhi hiyo.

Wakati fulani Kikwete alitaka kushinikiza tuchimbe chumvi pale ziwa Natron. Makazi ya zaidi asilimia 75 ya Flamengo dunia nzima. Alichoambiwa, akafunga mdomo na dili lote likayeyuka.

Kuna upuuzi mwingi unashinikizwa kwa manufaa ya watu fulani fulani. Na Rais pasipo kufanya utafiti vema akayavaa mazima mazima. Tukemee.

Hakuna cha maana tunachofaidika haswa na madini yetu. Mapapa wa madini wananeemeka, sisi tunaachiwa mashimo na kemikali hatari kwa wananchi wetu..

Sasa tunaamua kujaribu kuiua Serengeti kwa manufaa ya wajomba. Tukemee.
 
Daah sijui nani kamdanganya Mama hayo madini mengine yaliyo nje ya mapori Watanzania wanafaidika na nini aisee yaani wanataka kuharibu mazingira kwa hela ambazo mikataba yake ni ya kihuni tu huku Wananchi ndio wakitwikwa zigo la Tozo kwenye magari na mambo mengine hao wahunj wanakuja na Exemption mpaka wanatoka Mama nakuomba achana na kuwapeleka hao wahuni kwenye Mbuga ambayo imetunzwa miaka nenda rudi kwa Viongozi wote waliopita..
 
Serengeti si ya Samia. Si ya kujiamulia tu kufanya unachotaka. Ile ni urithi wa dunia.

Ikolojia yake tu haipaswi kuwa disturbed kwa kuweka lami. Lazima UNESCO wakupe ruhusa ya kufanya hivyo. Ije kuwa shughuli za uchimbaji? Kuna idadi kubwa sana ya dollars zinamwaga kuitunza Serengeti. Watu wanatoa pesa zao za misaada kuendeleza hifadhi hiyo.

Wakati fulani Kikwete alitaka kushinikiza tuchimbe chumvi pale ziwa Natron. Makazi ya zaidi asilimia 75 ya Flamengo dunia nzima. Alichoambiwa, akafunga mdomo na dili lote likayeyuka.

Kuna upuuzi mwingi unashinikizwa kwa manufaa ya watu fulani fulani. Na Rais pasipo kufanya utafiti vema akayavaa mazima mazima. Tukemee.

Hakuna cha maana tunachofaidika haswa na madini yetu. Mapapa wa madini wananeemeka, sisi tunaachiwa mashimo na kemikali hatari kwa wananchi wetu..

Sasa tunaamua kujaribu kuiua Serengeti kwa manufaa ya wajomba. Tukemee.
Jana Stroke kanistua kuhusu hili jambo nilishangaa sana yaani tumefikia kutaka kugawa kila kitu kwa wahuni ambao hatupati kitu hivyo vitu vingine walivyogawa tunafaidika nini wakati huduma za jamii kupata bado mtihani kila kitu unanunua kina 18% VAT mpaka nguo za watoto chini ya miaka 4 wanazipiga kodi harafu madini,bandari,gesi na sasa Mbuga wanataka kuwapa wahuni tena..
 
Jana Stroke kanistua kuhusu hili jambo nilishangaa sana yaani tumefikia kutaka kugawa kila kitu kwa wahuni ambao hatupati kitu hivyo vitu vingine walivyogawa tunafaidika nini wakati huduma za jamii kupata bado mtihani kila kitu unanunua kina 18% VAT mpaka nguo za watoto chini ya miaka 4 wanazipiga kodi harafu madini,bandari,gesi na sasa Mbuga wanataka kuwapa wahuni tena..
Ndipo tulipofikia. Tulianza na wanyama, kisha misitu, tukaja bandari, bado tunasonga...
 
Ndipo tulipofikia. Tulianza na bandari, bado tunasonga...
Nachoona hata maeneo ya mashamba watachukua tutabaki tupu wakimaliza kugawa hizo mbuga..sasa makampuni ya Utalii ya nini kama huko huko tena anavuruga ina maana hayo madini yapo mbuga za Tanzania tu haoni Nchi zingine wapo makini kwenye hili swala..
 
Nakwenda mbali zaidi ni kwamba kama 10% ya eneo la Serengeti litachimbwa madini basi itapatikana pesa nyingi sana itakayoweza kuendesha nchi bila kuyumba kwa miaka kadhaa, na kama asilimia zitazidi na pesa itaongezeka hivyo ustawi katika jamii utaongezeka.
Tuna hifadhi nyingi sana. Tuna mapori tengefu mengi , Dubai mwenye kieneo kidogo tena artificial hataweza kukompiti na Tanzania kwenye wild tourism labda tu kwasababu ya ujinga wa watu wachache watakaosomamia hizo hifadhi zetu
we jamaa kama mpumbavu hivi?
 
Nakwenda mbali zaidi ni kwamba kama 10% ya eneo la Serengeti litachimbwa madini basi itapatikana pesa nyingi sana itakayoweza kuendesha nchi bila kuyumba kwa miaka kadhaa, na kama asilimia zitazidi na pesa itaongezeka hivyo ustawi katika jamii utaongezeka.
Tuna hifadhi nyingi sana. Tuna mapori tengefu mengi , Dubai mwenye kieneo kidogo tena artificial hataweza kukompiti na Tanzania kwenye wild tourism labda tu kwasababu ya ujinga wa watu wachache watakaosomamia hizo hifadhi zetu
Kwa nini unasema 10%
 
Kwa ukubwa wa Serengeti kama 10% tu ya eneo lake litakuwa na madini either dhahabu au madini ya Vito kama safire n.k basi ni heri yachimbwe tu. Mapori yako mengi. Artificial safari ya Dubai haitaweza kushindana na Tanzania yenye hifafhi kama utitiri.
Yale yote mliokwishachimba yamewanufaisha nini kama nchi na wananchi wake?
 
Kwa ukubwa wa Serengeti kama 10% tu ya eneo lake litakuwa na madini either dhahabu au madini ya Vito kama safire n.k basi ni heri yachimbwe tu. Mapori yako mengi. Artificial safari ya Dubai haitaweza kushindana na Tanzania yenye hifafhi kama utitiri.
Kwenye madini mlisema hivi hivi, mwisho wa siku tunaachiwa tu mashimo! Kwenye gesi nako mlisema hivi hivi wakati mnawakabidhi Mabeberu! Mwisho wa siku hakuna kitu! Na kwenye bandari nako wakati mnammilikisha Mwarabu, porojo ni zile zile! Hakuna kitu!! Na hata sasa mnahamia kwenye mbuga!! Nako mambo yatakuwa tu ni yale yale!!

Kiufupi Afrika imejaliwa tu raslimali. Ila haina viongozi wa kuzisimamia na na kuzilinda hizo raslimali kwa manufaa ya wananchi walio wengi. Isipokuwa hao viongozi wamegeuka kuwa makuwadi wakuu wa kufanikisha wajanja wachache kujimilikisha hizo raslimali. So sad! ☹️
 
Back
Top Bottom