Tetesi: Kuna mgawanyiko mkubwa ndani ya CHADEMA kuhusu kuacha kuhudhuria vikao vya Bunge. Kuna fukuto la chini kwa chini


Mimi nahisi Chadema wameteleza pakubwa kipindi hichi, ccm walikuwa hoi kipindi hiki bungeni kwa nondo kutoka upinzani na kuna wakati mtazamo wangu ulikuwa unaonyesha ccm wanapoteana na nilifikiri chadema wangetumia hili gape la corona kumtoa jamaa magogoni, hoja za upinzani pale bungeni zilikuwa zina hit sana kwenye hisia za watu juu ya weakness kubwa sana kwa serikali kwenye hili gonjwa lakini kama wameamua kutoka bungeni hawa ccm watarudi kivyao na kuonyesha kama nchini hakuna tatizo kubwa, Chadema walipaswa kuutumia huu mwanya hata kama bunge sio live lakini kinachotoka watu wanakithamini kwa asilimia 100%. Chadema wamekosea
 
Ni aibu Chadema kukimbia mapambano, wametusaliti Watanzania
 
Sasa Kwanini umehamia kwenye Sacos ya dj?
Uko sahihi na ni kweli kwamba CCM ya Magufuli si tu siijui bali siielewi ila nashukuru CCM ya Hayati Mwalimu naijua na ilinilea!!!
 
Kichwani ana shida,pili bundle za Polepole zinawasumbua, kwasasa taifa linahitaji brain lkn yenyewe yanawaza utumbo yaliyoambiwa na Polepole,yanashindwa kutofautisha wakati

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wanatumia Nguvu kubwa Kwasababu hawakubiliki na Wananchi hao Chadema

Kama hawakubali why kila siku mnapanga watu wa kutoa taarifa wakati mbunge wa chadema anaongea?

Linganisha hotuba ya sugu juzi na ya mbunge wenu yoyote,

Kwanza wabunge wenu wanaisemea serikali na sio wananchi
 
Hill huwezi kulipinga, kuacha vikao kwa Siku 14, Ni Sawa Na kuacha posho ya 3,420,000/= kwa300,000/= kwa Siku.Hapo wabunge wanaotamani mahela lazima kinuke.Ndo maana wabunge Wa ccm wanaendelea Na vikao.
 
Sasa Kwanini umehamia kwenye Sacos ya dj?

Aliyekudanganya kuwa kila Mtu anayempinga Mwenyekiti wako Taifa ( CCM ) au Chama chake Tawala basi automatically huyo anakuwa ni Mpinzani tena wa kutokea CHADEMA ni nani? Nilishawahi kuweka Msimamo wa hii ID yangu ya Mzukulu a.k.a Mzukulu ya Bazukulu kuwa sina Urafki wala Uadui na Chama chochote kile cha Kisiasa hapa nchini na Siku CCM ikipatia nitaipongeza ( nitaikongole ) ila Siku ikikosea tu pia nitaisiliba ( nitaisema ) na hivyo hivyo kwa Chama cha CHADEMA na vinginevyo vya Upinzani. Kwa Kukuthibitishia hili rejea posts zangu za nyuma zipo ambazo nimempongeza mno Rais Magufuli na hata CCM yake / yako na pia zipo posts zingine nimewasema sana CHADEMA na hata Wapinzani wengine. Mbona huko sikukuona ukijitokeza Kuniunga mkono? Kwahiyo leo kwakuwa nakugusa Wewe na Chama chako cha CCM hadi Mwenyekiti wako Taifa ( Rais JPM ) ndiyo naonekana Adui na Mpinzani? Na ndiyo maana Kutwa huwa nakuambia huna Akili unabaki Kunikasirikia tu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…