Kuna Mgongano wa Katiba ya Zanzibar na ya Muungano, ufumbuzi wake tutake tusitake ni katiba mpya!

Kuna Mgongano wa Katiba ya Zanzibar na ya Muungano, ufumbuzi wake tutake tusitake ni katiba mpya!

Problem kubwa, ni kuwa Rais wa Zanzibar akiamua kuisimamia kikamilifu katiba ya Zanzibar aliyoapa kuilinda lazima atakwaruzana tu na rais wa JMT, kwa sababu katiba hizi mbili kuna vitu vya msingi sana zinapingana

Sasa huwezi kumtikisa rais wa Zanzibar kisha Muungano usipitie hali ya kuchafuka kwa hali ya hewa. Lazima Nguvu za Kijeshi zitatumika kurudisha hali sawa ikitokea situation kama hiyo na hilo halitaleta picha nzuri, na muungano wenyewe utageuka defacto occupation ambayo nayo haitodumu kwa sababu Wazanzibar wataikataa!

Ikitokea kwa mfano rais wa JMT akaamuru Majeshi ya Muungano kuingia Zanzibar Kutuliza hali, halafu rais wa Zanzibar naye akaamuru Vikosi Maalum vya SMZ viilinde Zanzibar unadhani nini kitatokea?, Kumbuka rais wa Zanzibar kwa mujibu wa katiba ya Zanzibar ana mamlaka za kuamuru vikosi vya SMZ kufanya LOLOTE kwa ajili ya Maslahi ya Zanzibar.
Vikosi vyote vya SMZ havina nguvu nje ya visiwa na hata hivyo huko Zanzibar kuna kikosi kamili cha jeshi la wananchi ambalo liko chini ya mabrigedia kutoka bara. Wewe unafikiri kwa hicho unachokiandika kama sio jeshi kuwepo huko pangetulia? Thubutu, haiwezekani.
 
Vikosi vyote vya SMZ havina nguvu nje ya visiwa na hata hivyo huko Zanzibar kuna kikosi kamili cha jeshi la wananchi ambalo liko chini ya mabrigedia kutoka bara. Wewe unafikiri kwa hicho unachokiandika kama sio jeshi kuwepo huko pangetulia? Thubutu, haiwezekani.
Brother bado huelewi vitu, una think anticlockwise

Sent from my 5023F using JamiiForums mobile app
 
Brother bado huelewi vitu, una think anticlockwise

Sent from my 5023F using JamiiForums mobile app
Wewe ndio huelewi chochote kabisa na utaendelea kubaki na kilema hicho cha kukuelewa lolote asilani.

Kaamurishe basi hivyo vikosi vyako viende kinyume uone watafaywa nini na jeshi; hao ni sawa na Suma JKT au Mgambo, Katiba ya Zanzibar kutamka kwamba ni nchi haiwezi kusababisha wawe 'Soverign State'.

Hebu panuka ubongo
 
Wewe ndio huelewi chochote kabisa na utaendelea kubaki na kilema hicho cha kukuelewa lolote asilani.

Kaamurishe basi hivyo vikosi vyako viende kinyume uone watafaywa nini na jeshi; hao ni sawa na Suma JKT au Mgambo, Katiba ya Zanzibar kutamka kwamba ni nchi haiwezi kusababisha wawe 'Soverign State'.

Hebu panuka ubongo
Wewe unazungumzia kwamba maadamu JWTZ ipo basi scenario ya Rais wa Zanzibar siku moja kuleta ukorofi kwa kutumia vikosi maalum vya SMZ (ambavyo katiba ya Zenji imempa power ya kuvitumia atakavyo) basi haitokuwepo!

Ukweli ni kwamba usidharau kikundi chenye muundo wa kijeshi, kina silaha za kijeshi, kina komandi za kijeshi na ukiachilia mbali hilo KINA wajibu wa KUFANYA LOLOTE Kitakachitumwa kufanya (Kwa mujibu wa Katiba ya Zanzibar).
Sasa tusingoje siku tuone JWTZ na Vikosi Maalum vya SMZ vinazichapa mchana kweupee kisa tu kuna Mkanganyiko katika katiba hizi mbili ambapo upande Mmoja kuna Mtu ni Amiri jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama kwa mujibu wa Katiba ya JMT na Upande wa Pili kuna Mtu kapewa powers na katiba ya Zanzibar Kuunda vikosi maalum kadri anavyooba inafaa na pia ana Powers za Kuviamrisha vikosi hivyo vifanye lolote!

Ndugu,, Jaribu kufikiria scenario tofauti tofauti ya haya nambo. Hiyo scenario unayoisema wewe ni BEST case Scenario ambapo tuna viongozi wenye busara kutoka pande mbili, na pia wanatoka chama kimoja, wanasikilizana na hivyo kila kitu kiko Shwari.

Sasa hebu fikiria WORST CASE Scenario, ambapo una rais wa Zanzibar aliyeamua kwenda na Katiba ya nchi yake, Akaamua kuunda vikosi maalum vyenye nguvu (katiba ya nchi yake ya Zanzibar inamruhusu), kwa hoja ya kulinda maslahi ya Zanzibar akaanza kupatrol mipaka ya bahari ya Zanzibar, kwa kufanya hivyo akahatarisha Maslahi ya JMT, Akaanza kugoma Mashauriano na Mwenzie wa JMT, Ikaamuliwa Ashughulikiwe Kijeshi na Yeye akaamua kuamuru vikosi vya SMZ vijibu Mapigo, Wakati huohuo kama alivyosema Mchangiaji mmoja huko Juu Wananchi wa Zanzibar wakaamua kusimama na Rais wao, Huoni hapo tayari hii itakuwa Vita ya wenyewe kwa wenyewe?
 
Hatuhitaji katiba mpya kwa sasa iliyopo inatosha,period. Nguvu zetu wote tuzielekeze kwenye kuwa-letea wananchi maendeleo.Tuungane wote katika hili.
After all mwananchi wa kawaida hana habari na katiba mpya,what he/she wants is a better life.
Maneno ya wanafiki.
 
IMG_7026.png

Tujadili huku tuliko toka, ndio msingi wa Muungano wetu. Kumefanyika hadaa nyingi kuidhoofisha Zanzibar nje ya Muungano na Ndani ya muungano huu, huu muungano hakuna alie mkubwa wala mdogo, nchi zote ni Equal, hamtaki basi sisi tutaendelea kuhoji uhalali wake na kumetumika sheria zipi za kimataifa mpaka kubadili jina la Muungano wetu , mpaka kumuondoa Rais wa Zanzibar umakamo wa Rais, mpaka kuifuta Tanganyika.
 
Maneno ya wanafiki.
Wanafiki ni wale wanaotumia siasa ili waonekane wanawajali wananchi,kumbe ni wachumia tumbo fulani tu.

Kwanza Waafrika hatuna asili ya written constitutions,mta-copy na ku-paste mpaka lini? Kama written constitutions zingekuwa muhimu, kwa kiwango
mnnacho-aminishwa na mabeberu,si Britain
wangekuwa na a written constitution, mbona hawana na wao ni mabeberu!Don't you find this queer?Amkeni jamani,mbona mnaingizwa mkenge kirahisi hivyo?

Other countries with unwritten constitutions
are Canada, Israel, Libya, New Zealand, Oman and Saudi Arabia.
 
Wanafiki ni wale wanaotumia siasa ili waonekane wanawajali wananchi,kumbe ni wachumia tumbo fulani tu.

Kwanza Waafrika hatuna asili ya written constitutions,mta-copy na ku-paste mpaka lini? Kama written constitutions zingekuwa muhimu, kwa kiwango
mnnacho-aminishwa na mabeberu,si Britain
wangekuwa na a written constitution, mbona hawana na wao ni mabeberu!Don't you find this queer?Wake up men.

Other countries with unwritten constitutions
are Canada, Israel, Libya, New Zealand, Oman and Saudi Arabia.
Hao unaowataja walishakuwa wastaarabu katika mifumo yao ya utawala na uongozi . WaAfrica na especially Tanganyika ustaarabu bado zero. Bila kuwa na muongozo imara tutakuwa na kina Trump wa kiAfrika wa kutaka kufia madarakani.

Tumeona Mugabe akitaka afie madarakani , Ccm wakijinasibu kuongeza muda hata kama kiongozi hataki !!. So Africa na especially Tanganyika inahitaji katiba ya wananchi dhidi ya watawala
 
Tumeanza kuamka baada ya kuona Marais wote ni wazanzibar, Na kutokana na katiba ya 2010 kwamba Zanzibar ni nchi hapa panaleta ukakasi ,
 
Kwa sasa inaonekana kama kila kitu kiko shwari katika muungano wetu lakini Ukweli ni kuwa kuna ufa mkubwa sana ambao ni hatari kwa muungano na nchi kiujumla.

Ukweli wenyewe ni kwamba Katiba mbili, yaani ya Muungano na ya Zanzibar (toleo la mwaka 2010)vinakinzana na hivyo kupelekea mkanganyiko ambao hauna afya kwa nchi na hivyo ili kuondoa jambo hili ambalo ni serious lazima mabadiriko katika Katiba ya Zanzibar au ya Muungano lazima yafanywe ili kurekebisha hili tatizo

Vifuatavyo ni vifungu katika katiba ya Zanzibar ambavyo vinapingana waziwazi na katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

1. Kipengele cha kwanza ni kuhusu Zanzibar kuwa ni nchi

Katiba ya Zanzibar ibara ya 1 imetamka kwa sauti kubwa kuwa ni NCHI na Imeainisha mipaka yake waziwazi

Ibara hiyo inasema hivi:

"1. Zanzibar ni Nchi ambayo eneo la mipaka yake ni eneo lote la
Visiwa vya Unguja na Pemba pamoja na Visiwa vidogo vilivyoizunguka
na bahari yake ambayo kabla ya Muungano wa Tanganyika na
Zanzibar ikiitwa Jamhuri ya Watu wa Zanzibar."

Kujitangaza huku kwa Zanzibar kuwa ni nchi haukuwemo kwenye toleo la kwanza la katiba ya mwaka 1984, Je ni kwa nini basi katika mabadiriko ya katiba hiyo toleo la 2010 Wazanzibar wakaamua kuiita Zanzibar kuwa ni nchi?

Wakati wazanzibar wakiutangaza Unchi wao na mipaka yao waziwazi kwenye katiba yao bado Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inaendelea kutambua uwepo wa nchi moja tu iitwayo Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na mipaka ya hiyo Tanzania.

2. Ibara ya pili nayo ina contradiction, Katiba ya Zanzibar toleo la mwaka 2010 imetwaa Madaraka ambayo awali yalikuwa ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Kumpa rais wa Zanzibar. Awali kabisa, katiba ya JMT ilikuwa ikimpa rais wa JMT uwezo wa kuigawa Zanzibar katika mikoa na Wilaya kwa "kushauriana" na Rais wa Zanzibar lakini kwenye katiba ya Zanzibar, nguvu hizo kapewa rais wa Zanzibar kwa kufuata sheria zitakazotungwa na baraza la wawakilishi.

Ibara ya 2A ya Katiba ya Zanzibar toleo la 2010 inasema:

"2A. Kwa ajili ya utekelezaji bora wa shughuli za Serikali, Rais
aweza kuigawa Zanzibar katika Mikoa, Wilaya na maeneo mengineyo
kwa kufuata utaratibu uliowekwa na sheria iliyotungwa na Baraza la
Wawakilishi"

3. Katiba ya Sasa ya Muungano ibara ya 105(1)(b), Inatambua Muundo wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar wa Zamani, ambapo kuna cheo cha Waziri kiongozi na siyo muundo wa sasa wenye vyeo vya Makamu wa Kwanza na wa pili wa rais.

Hili siyo jambo dogo, maana ni ajabu uwe na kifungu cha katiba chenye kuelezea cheo ambacho hakipo!!. Kuacha ibara hii iendelee hivihivi kuwemo ndani ya katiba ja JMT wakati tayari Wazanzibar walisharekebisha muundo wa serikali yao maana yake inaweka hata question mark kwenye uhalali wa muundo mpya. Kunahitajika mabadiliko ya katiba ili kuweka jambo hili sawa!

4. Katiba ya Zanzibar ya toleo la 2010 inataka baraza la wawakilishi litunge sheria ya namna Wazanzibar watakavyoshiriki katika majeshi kwa ajili ya ulinzi wa Taifa

Kwanza tunajua kuwa kwa mujibu wa Katiba ya JMT, Suala la Majeshi ya Ulinzi wa Taifa ni suala la Muungano, Kwa muktadha huo, Sheria za Ulinzi wa JMT ni suala la Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Ninatambua wazi kuwa katiba ya Zanzibar haitumii neno Majeshi kuhusu vikosi vya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, bali inatumia neno "Idara Maalumu". Wakati huohuo Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania haitambui Mahali popote kuwa hizo Idara maalumu ni Majeshi ya Ulinzi wa Taifa!
Na Katiba ya nchi, yaani ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imepiga Marufuku kuanzisha Jeshi la Ulinzi kinyume cha Sheria ya bunge

Sasa swali la Msingi ni je?
(a). Hiyo katiba ya Zanzibar ilipotamka neno Majeshi ilimaanisha Majeshi gani?, kwa nguvu gani ambazo baraza la wawakilishi linazo juu ya majeshi hayo?

(b). Kama Kwa kutamka hilo neno "Majeshi" ilimaanisha idara Maalumu au vikosi Maalumu vya SMZ, Je Kamanda mkuu wa Vikosi hivyo ambaye kwa mujibu wa Katiba ya Zanzibar ni rais wa Zanzibar sasa anaweza kuamuru vikosi hivyo kuingia vitani kuilinda Zanzibar?
Maana kwa mujibu wa katiba ya Zanzibar toleo la 2010 rais wa Zanzibar ana mamlaka ya kuviagiza vikosi ya SMZ (idara maalum) kufanya shughuli(mission) yoyote atakayoona inafaa kwa ajili ya Maslahi ya Taifa (Zanzibar), pigia Msitari maneno SHUGHULI YOYOTE ATAKAYOONA INAFAA!

5. Katiba ya Zanzibar Imepoka Mamlaka ya Amiri Jeshi Mkuu.

Katiba Ya Zanzibar toleo la mwaka 2010 inatamka Vikosi Maalum ya SMZ kwa kutumia jina (Idara Maalum) na Imetaja Idara hizo kuwa Ni Jeshi la Kujenga Uchumi (JKU) na Jeshi la KMKM (Jeshi la Kuzuia Magendo) ba Idara ya Chuo cha Mafunzo(Magereza).
Na imetamka kwenye Ibara ya 123(1)Kuwa Rais wa Zanzibar atakuwa KAMANDA MKUU WA IDARA HIZO na Anaweza KUFANYA CHOCHOTE, pigia Msitari naneno KUFANYA CHOCHOTE kwa Ajili ya Maslahi ya Zanzibar, Sasa kama huu Siyo Uamiri jeshi mkuu ni nini?

Katiba hiyohiyo ibara ya 123(2) inasema kuwa Rais wa Zanzibar anaweza kuunda Idara nyingine yoyote atakayoona Inafaa na ANAWEZA KUIPA SHUGHULI YOYOTE ATAKAYOONA INAFAA KWA MANUFAA YA TAIFA. Pigia Msitari maneno "Shuguli yoyote", What if shughuli hiyo ikawa ni kupigana vita?
Sasa kama huu siyo uwezo wa Kuunda Majeshi kwa mgongo wa jina "Idara Maalum ni nini?"


6. Rais Wa Zanzibar akila Kiapo cha Kulinda Katiba ya Muungano (wakati wa kuapa kuwa mjumbe wa baraza la Mawaziri) na Akila Kiapo cha Kulinda Katiba ya Zanzibar anakuwa anaapa kufanya vitu vyenye contradiction

Tumeshaona, mahali ambapo katiba hizi mbili, Ya Zanzibar na ya Muungano zinapingana. Sasa ukiwa Rais wa Zanzibar ukaapa kulinda na kutetea vyote viwili, unakuwa unaapa viapo vyenye utata. Je utatekeleza kiapo gani kwanza maslahi ya pande mbili yakikwaruzana?


7. Katiba ya Zanzibar toleo la mwaka 2010 Imepoka mamlaka ya Mahakama ya Rufaa ya Tanzania kuhusu uwezo wa Mzanzibari kukata rufaa katika mahakama ya Rufaa ya Tanzania kwa makosa yanayohusu uhuru na Haki za binadamu baada ya hukumu kuwa imetolewa na mahakama kuu ya Zanzibar.

Sote tunajua kuwa miongoni mwa mambo ya Muungano ni Mahakama ya Rufaa, hata hivyo katiba ya Zanzibar imemega mamlaka haya ya Mahakama ya Rufaa ya Tanzania kinyume cha Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Katiba ya Zanzibar inasema kwenye Ibara ya 24(3) kuwa:

"Rufaa dhidi ya uamuzi wa Mahkama Kuu katika Shauri lililofunguliwa dhidi ya Masharti ya sura hii ya Katiba yatasikilizwa na Mahkama Kuu mbele ya Majaji watatu bila ya kujumuisha Jaji aliyeamua shauri hilo mara ya kwanza. Majaji hao watatu watateuliwa na Jaji Mkuu na uamuzi wao utakuwa ni wa mwisho na hautokatiwa rufaa kwenye Mahkama ya Rufaa ya Tanzania"


Mwisho Kabisa
Wazanzibar Katika katiba yao toleo la 2010 kuna Mambo wameyawekea Kinga yasibadiishwe kirahisi, Mojawapo ni ZANZIBAR KUWA NCHI, Ukitaka Kubadilisha hili ni lazima Uitishe kura ya Maoni ya Wazanzibar, Sasa Jiulize kama hili itawezekana?
Kwanza Kipengele hiki peke yake Kinaua Ndoto hata ya CCM ya Serikali mbili kuelekea kwenye Serikali Moja

Kwa hiyo Ndugu Zangu, ni lazima tukubaliane, Hatuwezi kuwa na katiba mbili nchini zinazokinzana, Hatuwezi kuwa na Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inayotambua vyeo ambavyo Havipo, Hatuwezi kuwa na Katiba ya Zanzibar inayompa rais wa Sehemu moja ya Muungano uwezo wa Kuunda Vikosi na Akavipa "MISSION YOYOTE" atakayoona Inafaa kwa Masilihi ya Sehemu ya Nchi hiyo halafu tusiogope What If Mission hiyo ni Kutangaza Vita!

Kutokana na Hilo, TUNAHITAJI KATIBA MPYA itakayoondoa Mkanganyiko huu!

Hatuwezi kuendelea Kutegemea GOODWILL YA VIONGOZI kwenye kuudumisha huu Muungano,, Bali tunahitaji Mfumo wa Kikatiba na Kisheria Uliokaa sawa ili hsya mambo yaende vizuri, ili kesho na keshokutwa hata Marais wa Pande hizi mbili wasipotoka Chama Kimoja, Kila Rais ajue mipaka ya Majukumu yake Kikatiba.

KATIBA MPYA HAIEPUKIKI, TUNAWEZA KUJIFICHA KWENYE MCHANGA KAMA MBUNI TUKAJIAMINISHA KUWA KILA KITU KIKO SHWARI LAKINI SIYO KWELI.

TAIFA LINAHITAJI KATIBA MPYA!

Link ya Kupata katiba ya Zanzibar toleo la 2010 ni hii hapa chini:


Nyerere alikuwa smart sana lakini viongozi waliofuata baada ya Nyerere walikuwa wajinga sana.

Mpaka sasa tungekuwa tumeshafikia serikali moja na hizi chokochoko za uzanzibar na tanganyika zisingekuwepo.

Leo hii mambo vururuvururu tu.

Cha kukurekebisha tu suala la tawala za mikoa na serikali siyo suala la Muungano hivyo ni sahihi katiba ya Zanzibar kumpa mamlaka rais wa Zanzibar kufanya hivyo.
 
Hao unaowataja walishakuwa wastaarabu katika mifumo yao ya utawala na uongozi . WaAfrica na especially Tanganyika ustaarabu bado zero. Bila kuwa na muongozo imara tutakuwa na kina Trump wa kiAfrika wa kutaka kufia madarakani.

Tumeona Mugabe akitaka afie madarakani , Ccm wakijinasibu kuongeza muda hata kama kiongozi hataki !!. So Africa na especially Tanganyika inahitaji katiba ya wananchi dhidi ya watawala
Sijui kwa nini mnapenda kunyooshea vidole nchi zenu na ninyi mnakaa humo humo.Kilichotokea Marekani November 2020 katika uchaguzi wa kishenzi kabisa kuwahi kutokea katika historia ya Marekani ulikiona,au kwa kuwa kilitokea Marekani sio shida.

Na yanatokea Canada na Australia unayajua?Na Malkia wa Uingereza je,ana-chaguliwa na nani,si amejipachika tu.Na hapa nimetaja nchi moja tu ya Ulaya yenye Kingship na Queenship,ziko nyingi.Unajua kwa nini system hiyo ipo?Acheni kushabikia vitu ambavyo hata hamvielewi.
 
Ikishindikana hiyo Katiba Mpya, basi wajitenge tu na hivyo kujitegemea kwa kila kitu! Natamani pia kuona siku moja na sisi tukijivunia Utanganyika wetu.
Ni hatari mno kwa Zanzibar kujitenga sana sana urithi pekee tutakaowaachia wajukuu zetu ni kuhakikisha Zanzibar inakaliwa na watanganyika tu.
 
Hao ni wehu wa ccm achana nao sisi tunaitaka Tanganyika na Zanzibar zenye usawa hatutaki Tanganyika ipotee halafu zanzibar iwepo huo sio Muungano
Kinachotakiwa ni kupigania Tanzania moja na siyo kuwa na kakipande sehemu.
 
Nyerere alikuwa smart sana lakini viongozi waliofuata baada ya Nyerere walikuwa wajinga sana.

Mpaka sasa tungekuwa tumeshafikia serikali moja na hizi chokochoko za uzanzibar na tanganyika zisingekuwepo.

Leo hii mambo vururuvururu tu.

Cha kukurekebisha tu suala la tawala za mikoa na serikali siyo suala la Muungano hivyo ni sahihi katiba ya Zanzibar kumpa mamlaka rais wa Zanzibar kufanya hivyo.

Nyerere alikuwa Smart lakini Maalim Seif naye alikuwa Smart sana.
Maalim pamoja na kuwekewa Figisu na CCM nyiiiingi na kwa miaka mingi lakini kwa kushirikiana na Karume Jr alifanikiwa kuwabeat CCM at their own game kwa kuja na katiba ya Zanzibar toleo la 2010.

Hii katiba ya Zenji ya 2010 ni bonge la ushindi kwa Wazanzibar katika jitihsda zao za kufungua vifungo vya koti la muungano.

Naamin, CCM walijaribu kumfrustrate Maalim kwenye uchaguzi wa 2020 lengo lao likiwa asuse ili waende wakaibadili hii katiba ya Zanzibar, maana walihakikisha wanajipa Wajumbe wa baraza la wawakilishi wa kutosha kwelikweli, Maalim akaona isiwe tabu ngoja awe sehemu ya serikali!. Siamini kama ni kwa Interest ya Hussein Mwinyi kuitisha mabadiliko ya Katiba ya Zanzibar na kubadili vipengele vya katiba hiyo kwa sasa.

Tukubali tu, The only way ya kucounter move ya Wazanzibar ya mwaka 2010 ni kutengeneza Katiba mpya ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kinyume cha hapo mgongano wa katiba hizi mbili zilizopo sasa ni time bomb kwa mustakbali wa muungano
 
Hatuhitaji katiba mpya kwa sasa iliyopo inatosha,period. Nguvu zetu wote tuzielekeze kwenye kuwa-letea wananchi maendeleo.Tuungane wote katika hili.
After all mwananchi wa kawaida hana habari na katiba mpya,what he/she wants is a better life.
Unaletaje maendeleo wakati nikiwa na Bidhaa zangu kutoka zanzibar zikija Bara zinatozwa kodi mara ya pili?
Sukari kutoka Zanzibar kuja bara ni marufuku?

-Eti muungano na maendeleo , Serikali ya Zanzibar hairuhusiwi kuomba misaada ya nje kuijenga Zanzibar, na ikimpata mfadhili ,ni mpaka Muungano waridhie ndio apewe msada huo tena kwa mashartiya Kuigawabara % ya huo msaada,?

-Unasemaje Katiba iliyopo inatosha huku wazanzibari waliokimbizwa na mapinduzi wakitaka kurudi nyumbani hawakubaliwi na Tanganyika hata zanzibar yenyewe inawatamani warejee?

-Suala la Uraia kuwa Moja ni Msiba mkubwa Kwa Znzibar, kwani raia wa Zanzibar si Raia wa Tanganyika, kwa hiyo Tanganyika ndiye anaamua yupi awe raia na yupi asiwe?

TUNAHITAJI KATIBA MPYA ILI TUWE A MUUNDOMPYA WA MUUNGANO.
 
Wewe unazungumzia kwamba maadamu JWTZ ipo basi scenario ya Rais wa Zanzibar siku moja kuleta ukorofi kwa kutumia vikosi maalum vya SMZ (ambavyo katiba ya Zenji imempa power ya kuvitumia atakavyo) basi haitokuwepo!

Ukweli ni kwamba usidharau kikundi chenye muundo wa kijeshi, kina silaha za kijeshi, kina komandi za kijeshi na ukiachilia mbali hilo KINA wajibu wa KUFANYA LOLOTE Kitakachitumwa kufanya (Kwa mujibu wa Katiba ya Zanzibar).
Sasa tusingoje siku tuone JWTZ na Vikosi Maalum vya SMZ vinazichapa mchana kweupee kisa tu kuna Mkanganyiko katika katiba hizi mbili ambapo upande Mmoja kuna Mtu ni Amiri jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama kwa mujibu wa Katiba ya JMT na Upande wa Pili kuna Mtu kapewa powers na katiba ya Zanzibar Kuunda vikosi maalum kadri anavyooba inafaa na pia ana Powers za Kuviamrisha vikosi hivyo vifanye lolote!

Ndugu,, Jaribu kufikiria scenario tofauti tofauti ya haya nambo. Hiyo scenario unayoisema wewe ni BEST case Scenario ambapo tuna viongozi wenye busara kutoka pande mbili, na pia wanatoka chama kimoja, wanasikilizana na hivyo kila kitu kiko Shwari.

Sasa hebu fikiria WORST CASE Scenario, ambapo una rais wa Zanzibar aliyeamua kwenda na Katiba ya nchi yake, Akaamua kuunda vikosi maalum vyenye nguvu (katiba ya nchi yake ya Zanzibar inamruhusu), kwa hoja ya kulinda maslahi ya Zanzibar akaanza kupatrol mipaka ya bahari ya Zanzibar, kwa kufanya hivyo akahatarisha Maslahi ya JMT, Akaanza kugoma Mashauriano na Mwenzie wa JMT, Ikaamuliwa Ashughulikiwe Kijeshi na Yeye akaamua kuamuru vikosi vya SMZ vijibu Mapigo, Wakati huohuo kama alivyosema Mchangiaji mmoja huko Juu Wananchi wa Zanzibar wakaamua kusimama na Rais wao, Huoni hapo tayari hii itakuwa Vita ya wenyewe kwa wenyewe?

Na chengine anachoshindwa kufahamu, ndani ya hilo jeshi la JWTZ muna wazanzibari wengi tu, kwa Scenario kama hiyo ni wazi kuwa most of them wataliasi JWTZ na kuungana na Raisi wa Zanzibar.
 
Nyerere alikuwa Smart lakini Maalim Seif naye alikuwa Smart sana.
Maalim pamoja na kuwekewa Figisu na CCM nyiiiingi na kwa miaka mingi lakini kwa kushirikiana na Karume Jr alifanikiwa kuwabeat CCM at their own game kwa kuja na katiba ya Zanzibar toleo la 2010.

Hii katiba ya Zenji ya 2010 ni bonge la ushindi kwa Wazanzibar katika jitihsda zao za kufungua vifungo vya koti la muungano.

Naamin, CCM walijaribu kumfrustrate Maalim kwenye uchaguzi wa 2020 lengo lao likiwa asuse ili waende wakaibadili hii katiba ya Zanzibar, maana walihakikisha wanajipa Wajumbe wa baraza la wawakilishi wa kutosha kwelikweli, Maalim akaona isiwe tabu ngoja awe sehemu ya serikali!. Siamini kama ni kwa Interest ya Hussein Mwinyi kuitisha mabadiliko ya Katiba ya Zanzibar na kubadili vipengele vya katiba hiyo kwa sasa.

Tukubali tu, The only way ya kucounter move ya Wazanzibar ya mwaka 2010 ni kutengeneza Katiba mpya ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kinyume cha hapo mgongano wa katiba hizi mbili zilizopo sasa ni time bomb kwa mustakbali wa muungano
Suluhisho la kudumu ni kuanzisha effective assimilation policy ambayo within 50 years itakuwa imeshafuta uzanzibar na kubaki na Tanzania tu.
 
Unaletaje maendeleo wakati nikiwa na Bidhaa zangu kutoka zanzibar zikija Bara zinatozwa kodi mara ya pili?
Sukari kutoka Zanzibar kuja bara ni marufuku?

-Eti muungano na maendeleo , Serikali ya Zanzibar hairuhusiwi kuomba misaada ya nje kuijenga Zanzibar, na ikimpata mfadhili ,ni mpaka Muungano waridhie ndio apewe msada huo tena kwa mashartiya Kuigawabara % ya huo msaada,?

-Unasemaje Katiba iliyopo inatosha huku wazanzibari waliokimbizwa na mapinduzi wakitaka kurudi nyumbani hawakubaliwi na Tanganyika hata zanzibar yenyewe inawatamani warejee?

-Suala la Uraia kuwa Moja ni Msiba mkubwa Kwa Znzibar, kwani raia wa Zanzibar si Raia wa Tanganyika, kwa hiyo Tanganyika ndiye anaamua yupi awe raia na yupi asiwe?

TUNAHITAJI KATIBA MPYA ILI TUWE A MUUNDOMPYA WA MUUNGANO.
Huyo anavuta bangi
 
Back
Top Bottom