Kuna Sauti inanijia kwamba huenda wabunge 19 wa CHADEMA wana baraka za Mwenyekiti kwa makubaliano maalumu kutotoboa siri

Hilo la kwamba awamu ya tano inaihujumu cdm hilo halina mjadala na ni kupitia madaraka ya rais. Tumeona chaguzi zote toka awamu hii imeingia madarakani, tume ya uchaguzi na vyombo vya dola vikitii amri ya rais bkwa kupitisha wanaccm bila kujali matokeo ya kura. Hayo tumeona kwa macho yetu, na watu kadhaa wameuwawa na wengine kuachwa na vilema.

Tumeona kundi la watu wasiojulikana wakiua, wakiteka na kushambulia wapinzani, na amri inafahamika inatoka wapi. Kwa mara ya kwanza tuliona kwa JWTZ lililotengwa na siasa kikatiba kwenye kamisheni ya jeshi ikitumika kupokea wanaccm! Wote walionunuliwa toka upinzani kwenye operation kuunga juhudi, walipewa ubunge na udiwani kwa chaguzi zilizojaa ukatili, uhayawani na ukatili wa wazi. Haya yote yamefanyika mbele ya macho ya wananchi. Hali hii imepelekea kuwa na wapiga kura wachache sana, huku tume ya uchaguzi ikipika data za idadi ya wapiga kura. Kwasasa wananchi ndio hawatajitokeza tena kupiga kura maana wamepuuza rasmi box la kura, hakuna uwezekano wa wapiga kura kufika tena 5m. Katika mazingira haya unawezaje kusema wananchi wamepuuza upinzani wakati watu wamepuuza siasa za kishenzi za chama dola?
 
Bongo hakuna upinzani...

Rejelea uanzishwaji wa siasa za vyma vingi, haikuwa matakwa ya wananchi bali mabeberu...
Hapa umekosea wananchi walitishwa sana kipindi kile nakumbuka hyo miaka ilipita propaganda kwamba ukichagua upinzani nchi inaingia vitani mara sijui jeshi litapindua kuna watu walifika stage wakasema makanisa yatageuzwa mazizi ya Mbuzi!!

Lakini hawakufanya informed decision lakini ukitaka kuona waliridhia angalia uchaguzi wa 1995!! Mpaka kwa Butiama huko ilikua ni NCCR tu ko unaweza pata picha kwamba walikua tayari ila hawakupata elimu nzuri ya uraia.

Kingine upinzani upo haswaaa na kuhusu wote kuwa wamoja ni vyama kadhaa tu ambavyo vina viongozi moderate ila huwezi niambia mtu kma Mbowe aigize ilihali kafilisiwa mali zote, kalazwa jela, kaporwa jimbo, ssa ina faida kuwa double agent?

Kidogo NCCR au CUF coz wapo moderate ila radicalists kma CHADEMA huwezi sema sio upinzani. Damage waliofanya kwa serikali ndani ya 15 years ni kubwa mnoo kuwa compromised
 
Mimi hadi Leo huwezi niaminisha kwamba Mbowe hakujua chochote kuhusu hao mnaowaita covid kwenda bungeni
 
Mkuu nimeandika tu baada ya kuwaza lakin sikuwa na Maana hiyoo

 
Kwahiyo Mnyika anaifanyia chadema kazi bure [emoji3][emoji3][emoji3][emoji3]

Nimeamini kumbe hiki chama watetezi wake hawajui lolote ndani ya chadema
 
[emoji3][emoji3][emoji3][emoji3]2015 - 2020 sera yao kuu ilikuwa ni kujadili kingereza cha Magu
 
Mimi hadi Leo huwezi niaminisha kwamba Mbowe hakujua chochote kuhusu hao mnaowaita covid kwenda bungeni
Haiingiii akilini hata kidog , piga ua Mbowe amecheza hii movie ..... Mdee hawez alone kuorganize such biggest abusive act dhidi ya chama, haweziiiii
 

..kuna mtu anaitwa Mohamed Said yuko zaidi jukwaa la historia.

..huyu bwana amenifundisha uvumilvu ktk majadiliano.

..@Mohamed Said ukimtukana ndio kama umemchochea awe mstaarabu na muungwana zaidi.
 
Jiwe naye ni tumbo lake!

Lkn akija dictator kama Jiwe, nayo ataivunja. Had it not been for the strong Institutions in the US, Trump would have trodden on their Katiba!
Trump angekuwa afrika angeshinda kwa 99%
 
Haiingiii akilini hata kidog , piga ua Mbowe amecheza hii movie ..... Mdee hawez alone kuorganize such biggest abusive act dhidi ya chama, haweziiiii
Haahaa watu mnachuki na mbowe tu, kisa kakaa kimya.Mgogo ndugai kashapigia mstari....
 
Aliporwa ushindi na wababe, wale waliovamia Capitol hawakuwa vichaa.

..Trump angekuwa Afrika asingeondoka madarakani.

..Na wala wafuasi wake wasingevamia bunge, bali Trump angetoa amri kwa askari kuvamia bunge na kupora matokeo

..Alichofanya VP Mike Pence hakiwezi kufanywa na VP wa nchi za Kiafrika.
 
Chadema ina wenyewe, ndio sababu unaona akina Mdee kwa kupitia viti maalum wako bungeni.Hatuoni Chadema kwenda mahakamani kupinga uwakilishi wa wabunge hao.
Haahaa mahakama ukapinge ili upate nn? Wenzio walishamwandikia spika kwamba wale Sio wanachama wao full stop.Wale wanalindwa na mgogo ndugai
 
..Trump angekuwa Afrika asingeondoka madarakani.

..Na wala wafuasi wake wasingevamia bunge, bali Trump angetoa amri kwa askari kuvamia bunge na kupora matokeo

..Alichofanya VP Mike Pence hakiwezi kufanywa na VP wa nchi za Kiafrika.
Bravo mkuu, kwa ubabe wa trump kwa afrika angetawala mpaka mwisho wa dunia...wenzetu wako mbali
 
Dah... Nyie ndio huwa baadae mnakuja kubaki midomo wazi na kuteseka sana kwa kuwaamini watu.

Imewatokea hivyo kwa Slaa na kwa kina Mdee pia
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…