Kuna shida gani kuweka battery kubwa kwenye gari ndogo?

Kuna shida gani kuweka battery kubwa kwenye gari ndogo?

Battery ya babywoka yangu inatabia ya kuweka unga unga mweupe kwenye zile terminals zake. Sijui shida nini.
 
Jamani eh.

Chukulia battery ya gari ni kama storage katika mfumo fulani.

Ukiwa na storage ya 20 litres ukaamua ubadilisha zikawa 40 litres nini kitabadilika kwenye mfumo wako?

The same thing kwenye battery. N50 ina capacity kubwa kuliko N40. Just capacity.

Ndio maana ukiongeza mziki kwenye gari tunashauri pia uongeze ukubwa wa battery.

Ishu tu ni kwamba gari ambayo ilikuwa N40 ukaweka N50 battery itakuwa inachelewa kujaa. Na siyo kwamba utaumiza Alternator sababu hakuna muda alternator haifanyi kazi wakati engine inazunguka.

Shida labda kama utaamua kufunga battery mbili iwe in series au in parallel.
 
Ndio maana nikamuambia gari litaumia sio kumaanisha kwenye engine ni baadhi ya vifaa ya mfumo wa wire/umeme kama fuse taa au sterter winginv yake maana moto unaoenda ni mkubwa watts kuliko kiwango kilichowekwa
Hapana mkuu, toka hapo kwenye moto mwingi kwanza ukitaka kuuelewa huo umeme, uking'ang'ania hapo, wengi watakuwa wanakushangaa.

Betri haisukumi huo umeme mwingi kwenye vifaa, vifaa vinajichotea kwa kadiri ilivyopangwa.
 
Ishu tu ni kwamba gari ambayo ilikuwa N40 ukaweka N50 battery itakuwa inachelewa kujaa. Na siyo kwamba utaumiza Alternator sababu hakuna muda alternator haifanyi kazi wakati engine inazunguka.
Rated output ya alternator wakati huo inasoma ngapi? Tolerance yake ni ipi? Deep cylce?

Nikiunga betri 2, ama mfuatano au sambamba, betri moja ikawa mbovu na moja nzima, nini kinatokea hapo?

Betri kubwa ni load kwa alternator ndogo.
 
Battery ya babywoka yangu inatabia ya kuweka unga unga mweupe kwenye zile terminals zake. Sijui shida nini.
Fungua clamp kwenye terminal husika, safisha hiyo terminal na clamp, funga vizuri clamp kwenye terminal, PAKA GRISI au VASELINE kwenye clamp na terminal.

Hutakaa uuone tena huo unga mweupe.
 
Rated output ya alternator wakati huo inasoma ngapi? Tolerance yake ni ipi? Deep cylce?

Nikiunga betri 2, ama mfuatano au sambamba, betri moja ikawa mbovu na moja nzima, nini kinatokea hapo?

Betri kubwa ni load kwa alternator ndogo.


Mzee kinachomatter ni Cold Cranking Amps

Kama minimum CCA zimekuwa met. Then put any battery. Hakuna shida utapata. Changamoto moja ni kwamba bigger battery haitotosha kwenye space ya kuweka battery hapo kwenye gari yako.
 
Mzee kinachomatter ni Cold Cranking Amps

Kama minimum CCA zimekuwa met. Then put any battery. Hakuna shida utapata. Changamoto moja ni kwamba bigger battery haitotosha kwenye space ya kuweka battery hapo kwenye gari yako.
Unapokuwa unachaji betri ambayo iko exhausted kwa zaidi ya 40%, charging current inakuwa kubwa, tuseme 40A. Kadiri muda unavyokwenda, betri inakunywa chaji na kuanza kujaa. Inapoelekea kujaa, na charging current inapungua mpaka kufika 0A sio? Kisha battery charger inaanza kufanya tricle charging endapo battery iko connected na load.

Sasa kwa kesi ya gari, wakati gari inatembea, vifaa kama sio vyote basi vingi vinapaswa kulishwa umeme na alternator sio? Wakati huo huo alternator inapaswa kuchaji betri na kuhakikisha betri iko full.

Sasa kama vifaa vyote vya kwenye gari, mathalani ni usiku, vimewashwa na vinachukua 40A, battery kwakuwa ni kubwa au bovu, linataka 40A, uwezo wa alternator ni 60A output, kwa safari ya masaa 12, alternator inatoa 60A yote huku deep cycle yake ikisema pengine ni 0.9 max, hakuna lolote litakalotokea kwenye alternator yako?
 
Ndio maana nikamuambia gari litaumia sio kumaanisha kwenye engine ni baadhi ya vifaa ya mfumo wa wire/umeme kama fuse taa au sterter winginv yake maana moto unaoenda ni mkubwa watts kuliko kiwango kilichowekwa
Wewe unaonekana mgeni na mitambo hii. Umeambiwa tatizo pekee litakalokuwepo ni alternator kutochaji betri kwa wakati wa kawaida. Lakini pia Kuna advantage kama gari likifa charging system kwa maana unaweza kuendesha kwa betri na ukafika kwa fundi bila kuzimikiwa. Faida nyingine kwa kuweka betri kubwa ni kuwa unaweza kuongeza vifaa vya umeme kwenye gari kama heavy music system au spot lights. Hakuna kifaa kitakachoharibika.
 
Naomba nikuweke sawa bosi, hata ukiweka N200 kwenye IST, kama ni 12Vdc, basi ni hiyo hiyo. Hakuna moto mwingi utakaoenda kwenye gari yako, ila kama utaziunga betri mbili kwa mtindo utakaokupa 24Vdc, hata kama ni N40, zitauwa vifaa vyako.

Kila kifaa kinapakuwa kwa kadiri ya kinavyohitaji na kilivyopangiwa, kikianza kuzidisha, fuse inaungua na kumkatia huo mgawo.

Kwenye umeme wa majumbani unaweza sema hivyo kwa hali fulani.
Umenena sawasawa na mawazo yangu.

Mimi ninachoelewa N40, N50 au N70 ni size ya battery tu, kikubwa ni kutambua gari yako inatumia v12 au 24.

Kitako cha battery kwenye gari lako ndiyo kitaamua ukaaji wa size ya battery iwe ni N40 au N50.
 
Unapokuwa unachaji betri ambayo iko exhausted kwa zaidi ya 40%, charging current inakuwa kubwa, tuseme 40A. Kadiri muda unavyokwenda, betri inakunywa chaji na kuanza kujaa. Inapoelekea kujaa, na charging current inapungua mpaka kufika 0A sio? Kisha battery charger inaanza kufanya tricle charging endapo battery iko connected na load.

Sasa kwa kesi ya gari, wakati gari inatembea, vifaa kama sio vyote basi vingi vinapaswa kulishwa umeme na alternator sio? Wakati huo huo alternator inapaswa kuchaji betri na kuhakikisha betri iko full.

Sasa kama vifaa vyote vya kwenye gari, mathalani ni usiku, vimewashwa na vinachukua 40A, battery kwakuwa ni kubwa au bovu, linataka 40A, uwezo wa alternator ni 60A output, kwa safari ya masaa 12, alternator inatoa 60A yote huku deep cycle yake ikisema pengine ni 0.9 max, hakuna lolote litakalotokea kwenye alternator yako?

Tusifanye assumptions.

Labda nikuulize wewe swali.

Kwenye full electrical load amps ngapi zinaenda kwenye accessories na ngapi zinaingia kwenye battery?
 
Tusifanye assumptions.

Labda nikuulize wewe swali.

Kwenye full electrical load amps ngapi zinaenda kwenye accessories na ngapi zinaingia kwenye battery?
Sijawahi kuchunguza hili. Na una-refer gari ipi? IST? Naweza kutafuta clamp meter kucheki hili siku moja.

Naanza kukuelewa mkuu, sikuwa na lengo hilo, unisamehe sana!
 
Sijawahi kuchunguza hili. Na una-refer gari ipi? IST? Naweza kutafuta clamp meter kucheki hili siku moja.

Naanza kukuelewa mkuu, sikuwa na lengo hilo, unisamehe sana!

Okay haina shida mkuu.

Kwa gari yoyote lazima huwa kunakuwa na ratio ya current inayokuja kwenye Acc na inayoenda kwenye battery.

Anyway ngoja kukuche me mwenyewe kuna gari kadhaa nitaangalia alternator zake then tunaweza kuwa na mjadala wenye tija.
 
Okay haina shida mkuu.

Kwa gari yoyote lazima huwa kunakuwa na ratio ya current inayokuja kwenye Acc na inayoenda kwenye battery.

Anyway ngoja kukuche me mwenyewe kuna gari kadhaa nitaangalia alternator zake then tunaweza kuwa na mjadala wenye tija.
Hapo sawa, maana nilihofia kuwa naweza kuwa naku-challenge nikaharibu biashara
 
Ndio maana unaambiwa N.40 N70 na N 100 hapo unaumiza gari lako maana moto unalisha ni mkubwa kuliko size yake.
Wa stendi, hapo ni kuangali tu uwqezo wa charging alternator..!! Kama output current ya alternator inaweza kuiendesha hiyo battery wala haina shida
 
Umenena sawasawa na mawazo yangu.

Mimi ninachoelewa N40, N50 au N70 ni size ya battery tu, kikubwa ni kutambua gari yako inatumia v12 au 24.

Kitako cha battery kwenye gari lako ndiyo kitaamua ukaaji wa size ya battery iwe ni N40 au N50.
Yaan wewe ndio kabisa hata maana ya N huijui mkuu, hiyo N siyo size kama unavyo amini N ni Newton ambapo kwa maana nyingine tunaweza sema ni ujazo wa current au kiswahili labda tuseme uzito wa umeme,

Yaan kadri N namba inavyo kuwa kubwa ndivyo battery inaweza kuhimili kuendesha vifaa vingine kwa mda mrefu mfano kama battery ya12VDC N40 inaweza kuwasha mziki kwa volume 70% bila kuzima kwa masaa 6 basi battery ya12VDC N50 itawasha mziki huo huo na kwa volume hiyo hiyo ya 70% ila kwa masaa 8 nadhani hapo utakuwa umeelewa maana ya N.
 
Yaan wewe ndio kabisa hata maana ya N huijui mkuu, hiyo N siyo size kama unavyo amini N ni Newton ambapo kwa maana nyingine tunaweza sema ni ujazo wa current au kiswahili labda tuseme uzito wa umeme,

Yaan kadri N namba inavyo kuwa kubwa ndivyo battery inaweza kuhimili kuendesha vifaa vingine kwa mda mrefu mfano kama battery ya12VDC N40 inaweza kuwasha mziki kwa volume 70% bila kuzima kwa masaa 6 basi battery ya12VDC N50 itawasha mziki huo huo na kwa volume hiyo hiyo ya 70% ila kwa masaa 8 nadhani hapo utakuwa umeelewa maana ya N.
Kweli kabisa inawezekana mimi sijui kitu, lakini naelewa kitu kimoja. Kuna universal language ya size kwenye hii dunia.

Mfano; Size ya battery za remote control zinakuwa determined na letters kuna size za A, AA au AAA. Kwa maana hiyo, kama remote yako ya TV imeandikwa battery size ni AAA, maana yake mimi LAYMAN sio lazima niende na remote dukani ili nitest kama battery zitaenea, bali nahitaji kumwambia mwenye duka anipe battery size ya AAA. Nikichukua size tofauti kwa mfano size AA maana yake hiyo battery haitaenea kwenye remote yangu.

Hii ni universal language ya mtumiaji na ni rahisi kwa watu ambao hawajui kama mimi na kwa maana hiyo sihitaji kupiga hayo mahesabu ya electronics.

Size ya battery ya gari inakuwa determined na hizo N40, N50 na kadhalika. Hii lugha inamsaidia mlaji ambaye hajui kitu kama mimi ili anunue battery sahihi kutokana na specification ya gari. Na mara nyingi, kitako cha battery huwa kinaamua size ipi ununue kwani size ya battery N100 haiwezi ikakaa kwenye kitako cha magari madogo kwa sababu hiyo sio size yake.

Pamoja na elimu yenu ya electronics, viwanda vilirahisisha mlaji ambaye hana elimu anunue size ya ukubwa unaotakiwa badala ya kupiga hesabu zenu za amp na volts.

Kwa maana hiyo, wewe piga hesabu zoote za electronics lakini mimi kama mlaji layman nitaenda kununua battery kutokana na size ya kitako cha gari langu.
 
Kweli kabisa inawezekana mimi sijui kitu, lakini naelewa kitu kimoja. Kuna universal language ya size kwenye hii dunia.

Mfano; Size ya battery za remote control zinakuwa determined na letters kuna size za A, AA au AAA. Kwa maana hiyo, kama remote yako ya TV imeandikwa battery size ni AAA, maana yake mimi LAYMAN sio lazima niende na remote dukani ili nitest kama battery zitaenea, bali nahitaji kumwambia mwenye duka anipe battery size ya AAA. Nikichukua size tofauti kwa mfano size AA maana yake hiyo battery haitaenea kwenye remote yangu.

Hii ni universal language ya mtumiaji na ni rahisi kwa watu ambao hawajui kama mimi na kwa maana hiyo sihitaji kupiga hayo mahesabu ya electronics.

Size ya battery ya gari inakuwa determined na hizo N40, N50 na kadhalika. Hii lugha inamsaidia mlaji ambaye hajui kitu kama mimi ili anunue battery sahihi kutokana na specification ya gari. Na mara nyingi, kitako cha battery huwa kinaamua size ipi ununue kwani size ya battery N100 haiwezi ikakaa kwenye kitako cha magari madogo kwa sababu hiyo sio size yake.

Pamoja na elimu yenu ya electronics, viwanda vilirahisisha mlaji ambaye hana elimu anunue size ya ukubwa unaotakiwa badala ya kupiga hesabu zenu za amp na volts.

Kwa maana hiyo, wewe piga hesabu zoote za electronics lakini mimi kama mlaji layman nitaenda kununua battery kutokana na size ya kitako cha gari langu.
HAPANA mkuu N ya kwenye battery za gari,solar and co. Haimaanishi product size in terms of dimension ila ina maanisha size in terms of voltage currents. Elewa hivyo na usiwe mbishi kwa hilo.

Ndio maana unaweza kukuta battery ndogo hizi N7 na N12 zina fanana kwa umbo.
 
Back
Top Bottom