Kuna shida Gani kwenye Operation za Uzazi? Hivi vifo ni mimi tu naona?

Kuna shida Gani kwenye Operation za Uzazi? Hivi vifo ni mimi tu naona?

Hii kitu ni nyeti sana, bahati mbaya sana wengi tunaandika tu hapa, lakini hatujui kitu, tunasukumwa na hisia tu, ukweli hatuufahamu.

Imebidi niingie chimbo kuuliza wataalamu wa afya kuhusiana na hii, na nilichoelezwa kimeniacha mdomo wazi, nimeshangaa mnoo.
Labda niweke facts chache katika hili baada ya kuhoji sana wataalamu kadhaa.

1. Operation yoyote ile ni risk ya mgonjwa kupoteza maisha, na kadri operation itahusisha dawa za nusu kaputi au kupoteza damu nyingu basi risk huwa zaidi ya maradufu. Na operation ya kujifungua ni very risk kwa sababu uhusisha hayo. Ni kufa au kupona.

2. Matokeo ya operation yoyote ile hutegemea maandalizi, vifaa, wataalamu, madawa na uangalizi (monitoring). Kupelea kwa chochote kile katika hivyo kunaweza kupelekea lolote lile kutokea.

3. Kwa mujibu ya wataalamu wa kidunia (WHO?) ili ufanisi wa operation ya kujifungua uwe mzuri, inabidi at least kuwe na timu ya wataalamu wasiopungua 12 standby! Ambao ni:
(i)Daktari mkunga (Obstetrician)
(ii)Daktari msaidizi (medical Doctor)
(iii)Daktari wa dawa za usingizi.(Anasthesiology)
(iv)Daktari msaidizi wa dawa za usingizi. (Anasthestist)
(v)Muuguzi mtaalamu wa operation (theatre nurse)
(vi) Muuguzi mtaalamu msaidizi
(vii) Muuguzi mkunga (Nurse widwifery)
(viii) Daktari wa vichanga (Neonatologist)
(ix)Mtaalamu wa vifaa (Medical equipment technician)
(x) Mfamasia
(xi)Mtaalamu wa maabara.
(xii)Daktari muokozi (Resuscitation Doctor).

4. Kifalsafa katika fani ya utabibu, kila Daktari ni mwanafunzi, tofauti ni ngazi za uanafunzi. Kadri Daktari anavyofanya kazi ya kutibu kwa mtizamo wa kiuanafunzi ndivyo anavyoweza kutengeneza matokeo bora na chanya yakuponyesha and vice versa is true.

5. Kwa kadri operation za kujifungua watoto zinapokuwa nyingi pasipo sababu ya msingi ya ulazima wa moja kwa moja (absolute indication) ndivyo na idadi ya vifo vya wakina mama wanaojifungua kwa operation itazidi kuongezeka.

Mwisho ni scenario ambayo ilinishtua zaidi. Kuna kituo kimoja duni cha afya cha serikali, kipo maeneo ya vijijini, ambacho hakikuwahi kuwa na wataalamu mbali mbali muhimu, hakina Daktari bingwa wa wanawake, wala daktari bingwa wa dawa za usingizi na wataalamu wengine mahususi, wala vifaa vya kisasa sana vya upasuaji, katika mazingira hayo hayo kikafanikiwa bure kuwasaidia wakina mama kujifungua kwa njia ya operation (wastani wa operation moja kwa siku) kwa kipindi cha miaka mitano mfululizo pasipo kuwepo rekodi ya kifo hata kimoja cha mama.
 
Pole mkuu !

Naomba unisaidie maswali haya

1.Vifo vya wapendwa wako vilitokea baada ya upasuaji au wakati wa upasuaji?

2.Mmoja umegusia Pamba (Gauze) iliyoachwa tumbuni kule Dodoma.Hii pamba iligundulika baada ya muda gani kuwa imeachwa tumboni ?Ndiyo iliyosabisha kifo?
Sorry sikuingia humu tangu niandike huu uzi,
1. Vyote vilitokea baada ya Upasuaji,
Mtu ashashonwa Baadae akaanza kuumwa, karibuni wote Waliporudishwa hospital walifanyiwa operation tena ndio makosa yakaonekana yakarekebishwa...

2. Baada ya kua anasumbuliwa na Tumbo karibuni week, maumivu makali mno, ikabidi arudi hospital, kufika wakamfanyia operation tena, ndio wakakuta Pamba imeoza, usaha n.k
Wakamsafisha, Akapata ahueni siku mbili,
Ya tatu akafariki.
 
Je Kwa mwanamke anaeanza kuzaa na umri wa miaka 30 bado Kuna complications
Hapana, kuanzia 35 mara nyingi kama hujazaa hata.ila bado sio general rule.

Ila kutokana na lifestyle, vyakula magonjwa etc kuna complications nyingi nowdays. Hivyo tunashauri ukichelewa kuzaa unapopata ujauzito anza clinic mapema na kama hali inaruhusu tafuta specialist wa wamama (gyno) akufanyie vipimo vyote ktk kila hatua ya ujaz uzito.

Kupima na kujua mapema inakuasaidia kujiandaa.

Mfano.. kwa maisha yetu ya kiswahili almost kila mwanamke anajua ukifika wakati wa kujifungua atajifungua kawaida tu kumbe hali haiko hivyo..

kuna wengine wameumbwa njia ndogo wengine wanaishiwa nguvu ya kusukuma mtoto au hata kwa sababu tu za kisayansi mtoto anakosa nguvu ya kutoka mwenyewe hivyo hawa wote wanahitaji msaada wa kitaalamu inapofika muda wa kujifungua.

Unapochukua hatua mapema inasaida sana kuokoa maisha ya mama na mtoto..otherwise tunaweza kupoteza mama, mtoto au wote.
 
Inaumiza sana ndugu zangu.
Watu wa 3 ninaowafahamu, wengine wa 3 ni watu wa karibu wa marafiki zangu..
Katika miezi 4 wamepoteza maisha Wote kwa operation ya uzazi, achilia mbali wale ninaosikia mtu pembeni akiongea.

Inauma Sana ndugu zangu,
Mnampeleka mpendwa wenu hospital akiwa mzimaa mpate malaika, mnaambulia Miili miwili isiyotikisikaa... Mbaya zaidi uone kuna hali ya uzembe ilifanyika.
Isikie tuu hii kwa mtu ndugu yangu..

Hiki ni nini? Au ni coincidence tuu kwa bahati mbaya imetokea zaidi kwa watu ninaowafahamu?
Hivi hua hospital wana keep Data? If yes Are they real? Data zinasemaje? Zinafanyiwa kazi? Maana sidhani kama ni kawaida..

Kwa Moyo wa dhati NIIOMBE Serikali kupitia wizara ya Afya Fuatilieni hili Zaidi, kuna uzembe,
Mmoja kati ya hao Pamba ilisahaulika Tumboni Dodoma hapo, mwingine naye mistake katika kutenganisha Kitovu, Mwingine naye kuna sehemu ilikawa vibaya...
Haya ni makosa ya kibinadamu..
Hatuna chance ya makosa ya kibinadamu katika Afya ya mtu jamani..

Wahusika Niwaombe ndugu zetu, nyie ni professional, mmekula viapo, Mnalipwa, Jitoeni katika kazi zenu, Fanya Ukijua uhai wa viumbe hao upo mikononi mwako,
Kueni makini na Afya za Mama zetu, Dada zetu na wote kwa ujumla, mmeaminiwa sanaa..
Itokee kwa mipango ya Mungu ila sio kwa uzembe..

Serikali nawaomba Sana viongozi wangu, Chukueni hili katika positive way ya kuokoa mama na mtoto..
Siandiki hapa kama Niliyepoteza Mke au Ndugu, naandika kama binadamu niliyeumia SANAA kuona ndugu zetu hawa Wanatutoka katika picha kama hizo...

Nawaomba Tena Chukueni hili katiaka Positive way,
Mpo hapo kuokoa jamii kubwa nyuma yenu, Jivunie Kuo mmoja wa waliokoa mamia ya mama zetu na taifa la kesho, Siku Moja utalipwa, this is real sio siasa.
Ni suala la kitaalamu, litatuliwe kitaalamu.

Rai kwa Mama na dada zangu, Mnaopokua wajawazito, Punguzeni Utandawazi, epukeni Uzazi wa operation usio wa lazima kwa kisingizio hutaki uchungu, Jipe mazoezi.

Poleni Sana Wote mlitokwa na Wapendwa Wenu katika picha kama hii..

AMEN.
Inaumiza sana.
 
Hii kitu ni nyeti sana, bahati mbaya sana wengi tunaandika tu hapa, lakini hatujui kitu, tunasukumwa na hisia tu, ukweli hatuufahamu.

Imebidi niingie chimbo kuuliza wataalamu wa afya kuhusiana na hii, na nilichoelezwa kimeniacha mdomo wazi, nimeshangaa mnoo.
Labda niweke facts chache katika hili baada ya kuhoji sana wataalamu kadhaa.

1. Operation yoyote ile ni risk ya mgonjwa kupoteza maisha, na kadri operation itahusisha dawa za nusu kaputi au kupoteza damu nyingu basi risk huwa zaidi ya maradufu. Na operation ya kujifungua ni very risk kwa sababu uhusisha hayo. Ni kufa au kupona.

2. Matokeo ya operation yoyote ile hutegemea maandalizi, vifaa, wataalamu, madawa na uangalizi (monitoring). Kupelea kwa chochote kile katika hivyo kunaweza kupelekea lolote lile kutokea.

3. Kwa mujibu ya wataalamu wa kidunia (WHO?) ili ufanisi wa operation ya kujifungua uwe mzuri, inabidi at least kuwe na timu ya wataalamu wasiopungua 12 standby! Ambao ni:
(i)Daktari mkunga (Obstetrician)
(ii)Daktari msaidizi (medical Doctor)
(iii)Daktari wa dawa za usingizi.(Anasthesiology)
(iv)Daktari msaidizi wa dawa za usingizi. (Anasthestist)
(v)Muuguzi mtaalamu wa operation (theatre nurse)
(vi) Muuguzi mtaalamu msaidizi
(vii) Muuguzi mkunga (Nurse widwifery)
(viii) Daktari wa vichanga (Neonatologist)
(ix)Mtaalamu wa vifaa (Medical equipment technician)
(x) Mfamasia
(xi)Mtaalamu wa maabara.
(xii)Daktari muokozi (Resuscitation Doctor).

4. Kifalsafa katika fani ya utabibu, kila Daktari ni mwanafunzi, tofauti ni ngazi za uanafunzi. Kadri Daktari anavyofanya kazi ya kutibu kwa mtizamo wa kiuanafunzi ndivyo anavyoweza kutengeneza matokeo bora na chanya yakuponyesha and vice versa is true.

5. Kwa kadri operation za kujifungua watoto zinapokuwa nyingi pasipo sababu ya msingi ya ulazima wa moja kwa moja (absolute indication) ndivyo na idadi ya vifo vya wakina mama wanaojifungua kwa operation itazidi kuongezeka.

Mwisho ni scenario ambayo ilinishtua zaidi. Kuna kituo kimoja duni cha afya cha serikali, kipo maeneo ya vijijini, ambacho hakikuwahi kuwa na wataalamu mbali mbali muhimu, hakina Daktari bingwa wa wanawake, wala daktari bingwa wa dawa za usingizi na wataalamu wengine mahususi, wala vifaa vya kisasa sana vya upasuaji, katika mazingira hayo hayo kikafanikiwa bure kuwasaidia wakina mama kujifungua kwa njia ya operation (wastani wa operation moja kwa siku) kwa kipindi cha miaka mitano mfululizo pasipo kuwepo rekodi ya kifo hata kimoja cha mama.
Sawa
Umeeleza vizuri nadharia, fanya link up na mifumo yetu kama nchi ili tujibu swali la mtoa hoja.
 
Wewe usifananishe kila kitu na marehemu.

Unakuwa Kama kipofu aliyeona punda.


Majanga ya madeni ya kijinga aliyotuingiza yule bwana saa hizi pesa tunazolipia nadeni yake ya kijinga zingesaidia sehemu kubwa sana ya Watanzania.

Tukubali tu, alikuwa na nazuri yake machache na alikuwa na makosa yake mengi tu.
hakuwa mwema hapa ila ukiangalia kipindi cha jiwe kuna woga ulikuwepo kidogo wa kufanya mambo ya kipuuzi
 
Back
Top Bottom