Kuna shida gani Tanzania ikitangaza rasmi kuisaidia Congo kupambana na M23? Tuna Viongozi wa namna gani?

Vita ya m23 na serikali ya congo ni ya kimkakati. Unaweza ambiwa leo kuwa, waasi wa m23 wamesalimisha silaha na makumi ya waasi wamejisalimisha,lakini kesho ukaambiwa tena goma na kivu yote zipo mikono mwa waasi wa m23.
Ni ujinga tu unafanyika.


Tunaweza ingia makubaliano tukaikomboa ile Goma na Kivu na tukaweka military Base pale.

Tunaweza kuwa nchi ya kwanza ya Afrika kuwa na military Base nje ya mipaka yake alafu tukafanya uchumi.
 
Mkuu,
Ni recklessness kufananisha nchi yenye uchumi mkubwa miaka zaidi ya 200 na wewe mwenye miaka 60 ya kua huru.

Huku ujinga ,umaskini, maradhi umeshindwa ku deal navyo alaf ujipeleke kwenye vita vya jirani yako yaan unaenda kuzima moto kwa jirani huku Kwako panaungua.
 
Tumeshindwa kushughulika na ujinga maradhi na umaskini kwa ujinga wa CCM tu sio kwamba hatuna uwezo!
 
Mkakati wowote utakaohusisha jeshi kuwaondoa tu hao M23 huko Mashariki mwa Congo hauwezi kuwa suluhu ya amani ya kudumu ya hilo eneo. Lazima kuwe na mkakati wa utawala na siasa katika hilo eneo baada ya vita. Vingineyo itakubidi uweke hapo maelfu ya wanajeshi wa kudumu, wakae tu hapo miaka yote, jambo ambalo haliwezekani.
 
Sisi tunaweza kutoa mkopo in terms of man power.

Silaha tunanunua kwa fedha zao na kuwasaidia kukomboa eneo lao.
Kabla ya kuwaza Tz tukasaidie pale, jiulize kwanini ile vita haishi? M23 wanatoa wapi fedha, silaha, na chakula, nguvu ya kushindana na serikali wanaitoa wapi?
Kuna askari wa umoja wa mataifa wapo pale na askari wetu pia wakiwemo kwahyo wanajua kinachoendelea pale.

M23 ni mtoto ambae ametangulizwa mbele.
 
Kivipi isiwe suluhu? Kwa hiyo kuwaacha waue watu ndo suluhu?

Au we mnyarwanda nini? Declare interest kwanza!
 
Nadhani tungekuwa tumepakana na DRC kupitia nchi kavu, tungelazimika kuingia msituni hata kimya kimya. Bahati tunapakana na DRC kupitia Ziwa Tanganyika. Ili kuingia DRC kwa nchi kavu kutokea TZ lazima upite ama Zambia (kwa mpaka wa kusini) au upite Burundi, Rwanda na Uganda (kwa mpaka wa kaskazini). Kwa hiyo vita yoyote ya msituni inapaswa kushirikisha nchi hizo; ambazo baadhi zinanufaika na mgogoro huo.
 
Suluhisho, hizi nchi za kusini mwa bara la Africa waungane kuiwekea vikwazo Rwanda, pia litengenezwe kundi lingine la kijeshi kuififisha Rwanda kiuchumi na kijeshi.

Bandari zetu, Kenya n.k waache kuruhusu bidhaa kwenda na kutoka Rwanda, gari zao zinazochukua chakula Tanzania , Kenya, Uganda n.k zizuiliwe, Rwanda watengwe katika kila nyanja, halafu tuone hao M23 hiko kiburi wanakipata wapi... wakati huo huo M23 wapelekewe moto vilivyo na kuzuia logistics zao kupata silaha na chakula.

Ndani ya mwaka mmoja tu M23 inapotea.

M23 ndio Rwanda, hivyo tunashirikiana na M23 wakati huo huo tunapambana nao, hakuna vita hapo ni ujinga...
 
Wako bussy na uchaguzi mkuu namna ya kuiba kura!!!
 
Wako bussy na uchaguzi mkuu namna ya kuiba kura!!!
 
Hatuuelewi mgogoro kivipi?

Kwa hiyo wakimbizi waliopewa uraia wa Tanzania waliopo kule Tabora na Katavi wakisema Tabora na Katavi ni mali yao tuwaache tu?

Unafikiri kwa kutumia nini?
Lakini wale pale congo walikuja na ardhi Yao..kuwafukuza ni waondoke na ardhi Yao...nafkiri mgogoro upo hapo
 
kagame, uganda,m23, jeshi la congo, raisi wa congo, kiongozi wenu, SADC, UN, JWTZ...hivyo vyote ni kama KETE ZA DRAFTI ambazo kuna watu wanazichezesha kwa kutaka hii ikae pale na kete hii ifike pale....so wewe kama KETE huna uwezo wa kujipeleka popote pale,bali utasubiri mchezaji akupeleke anapotaka yeye...VITA YA CONGO NI MCHEZO...✍️✍️
 
Kama naanza kukuelewa vile
 
Utazishawishije Kenya na Uganda ziiwekee Rwanda vikwazo? Wao huo mgogoro wa M23 unawapunguzia fursa gani?
 
Kila siku wanaambiwa waboreshe Navy kwenye bahari na maziwa yetu wanaishia kununua Mabus ya mchina na kuwapa wanajeshi.

Ile Congo endapo tukiweza kuisaidia itatufaidisha kweli kiuchumi
 
Ni ujinga tu unafanyika.


Tunaweza ingia makubaliano tukaikomboa ile Goma na Kivu na tukaweka military Base pale.

Tunaweza kuwa nchi ya kwanza ya Afrika kuwa na military Base nje ya mipaka yake alafu tukafanya uchumi.
kwanza kuomba tu kuisaidia CONGO tayr unatangaza vita na uchina,marekani,ubelgiji na ufaransa.
 
Tumeshindwa kushughulika na ujinga maradhi na umaskini kwa ujinga wa CCM tu sio kwamba hatuna uwezo!
😅😊☺️ Mkuu kwaio tungekua ni ulaya ndogo

War siku zote ni easy to start Ila difficulty to end.

Tukiingia kwenye hii vita itasababisha hasara kubwa kuliko faida yaan ni Bora kusaidia ki jumuia Ila kichwa kichwa hata maadui zetu wata side na m23 then tukajikuta tunapoteza hata hicho kidogo tulicho nachoo
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…