Kuna shida gani Tanzania ikitangaza rasmi kuisaidia Congo kupambana na M23? Tuna Viongozi wa namna gani?


..tunatakiwa tupeleke askari wengi, angalau BRIGEDI, vifaa vyepesi na vizito vya kutosha, kuweza kudhibiti hali ya kiusalama mashariki ya DRC.

..Mzee Robert Mugabe ali-commit askari wengi wa Zimbabwe mwaka 1999 ambao waliweza kuzuia majeshi ya Rwanda, na Uganda, yasiigawane DRC.

..utaratibu wa kupeleka vikosi vidogovidogo ambavyo vinakuwa chini ya mifumo, na maelekezo, ya UN, hauna msaada wowote kwa wananchi wa DRC.
 
Uko sahihi! Jeshi linatakiwa litumike kwa faida za kiuchumi yale mambo ya kukaa kusubiri vita ni upotevu wa hela! Pasipo kupigania fursa hatuwez tobacco! Kenya kapeleka polisi haiti
 
Hakuna vita Goma wala Mashariki ya DRC. Ilikuwa ni march au parade ya wanajeshi wa M23 kuingia mji wa Goma huku wakishangiliwa na wakazi wa Goma. Fuatilia haya mambo vizuri na uache kukulupuka maana huelewi chochote kuhusu chimbuko la mgogoro wa mashariki ya DRC. Hakuna namna TZ inaweza kufanya maana hakuna vita mashariki mwa DRC, leo ilikua hitimisho la march au parade ya muda mrefu ya wanajeshi wa M23 kuingia mji mkuu wa Goma wa majimbo wa KIVU mashariki mwa Congo. Hakuna bomu wala risasi ata moja iliyorushwa na wamepokelewa na wananchi kama liberators. Fuatilita yanayoendelea kwa umakini pia take your time kustudy mgogoro huo toka enzi za colonial partition of Africa during berlin concefernce ya mwaka 1885 ambapo Kindgom ya Rwanda iligawanywa mara mbili upande wa kushoto ilichukuliwa na Ubelgiji ( side hii ilikuja kufall under Zaire/ Congo DRC) na kulia ilienda German East Africa.( Side hii ndo present day Rwanda)
Mambo ni mengi muda ni mchache hatuwezi andika kila kitu hapa. Soma au uliza wenye ufaham wa hii historia au waliowahi ishi au kukaa ukanda huo

Adios
 
Mmeshindwa ku maximaze soko la ndani ndo mtegemee kutajirika Congo? Hiyo akili au matope?

Hao Congo wamekwambia wapo tayari kujenga SGR au mtawajengea?

Yani sahizi nchi ianze kuzingatia Congo wakati kuna miradi kibao yenye potential kubwa, less risky bila kuhitaji association na mtu yeyote yule. Umevuta bangi ya wapi? Matter of fact, nchi za hovyo kama Congo na S. Sudan hazikupaswa kuwa hata in the EA community just yet. Hazina hata hela ya kulipa fees zao.

Itakua hujui historia ya Congo kama unadhani M23 ndo tatizo pekee la Congo.

Hata wewe ni think tank sio kila kitu serikali ifanye. Kama unaona Congo kuna faida nenda wewe, hizo nchi ulizotaja serikali ni mratibu tu watendaji ni private sector ndo maana inaitwa capitalism.
 


..anachosema mtoa mada ni kwamba Tanzania haipaswi kuwa VUGUVUGU katika masuala ya kisiasa, na kiusalama, ktk nchi zinazotuzunguka. Tuamue kuwa upande wa M23, au upande wa serikali, bila kificho wala kuona haya.
 
Kila nchi inabid ikae pembeni. Huu mgogoro ni wa Congo wenyewe kwa wenyewe. Ndo maana M23 wanaitwa rebels. M23 ni raia wa Congo DRC wanaoipinga serikali ya Tshekedi yenye makao makuu yake mgharibi ya nchi Kinshasa, sasa mnataka Tanzania au Rwanda waingilie huo mgogoro kwa manufaa ya nani??? M23 ni wacongo wanaongea kinyarwanda. Haya yote yana mzizi kwenye mipaka ya wakoloni. Hiyo vita au mgogoro wa mashariki ya DRC haina uhusiano wowote na Tanzania au Rwanda, utamalizwa na wacongoman wenyewe wenye nchi yao ya DRC
 
Taarifa Rasmi kutoka serikali ya Rwanda, Kigali kuhusu kinachoendelea huko mashariki ya DRC
 
Gharama ya vita unaijua lakini? Heri hiyo reli iishie Kigoma watafuata mizigo huku kwanza itawafikia mapema tofauti na sasa. Vita itafanya tuchukue sides na ukimsaidia Congo ina maana Rwanda unampoteza na sioni sababu ya sisi kujiingiza huko mradi tuna Rwanda, Burundi na Uganda hao Congo wamalize tofauti zao.
 
Vita vya Congo ni gorriller war. Uwezi kumaliza kwa kupeleka jeshi bali kwa meza ya Mazungumzo..... maana Congo pia wanasupport waasi kihutu kupindua serekali ya RPF . Ndio maana Kikwete alimshauri kagame ukweli , akanunua...kukomesh ni meza ya Mazungumzo kati ya Rwanda na waasi wa kihutu, na Congo na m23.
 

..unapozungumzia mipaka ya wakoloni unatutisha Watanzania.

..Waafrika tulikubaliana tutaiheshimu mipaka ya iliyoachwa na wakoloni ili nchi za Kiafrika ziishi kwa amani bila vita.

..Nchi za Kiafrika zikianza kuchora mipaka yake upya bara zima linaweza kuingia katika migogoro isiyokuwa na mwisho.
 
Umemaliza !🙏
 
Drc ambaye ni mwanachama wa EAC imevamiwa na nchi jirani ambayo pia ni mwanachama wa EAC.

Ila hii jumuiya imeshindwa kutatua huu mzozo baina ya nchi wanachama.
 
Ukichukua into consideration ya mipaka ya wakoloni, M23 Banyamulenge ni wacongo wanafall kwenye mipaka ya DRC. Kwa mantiki hiyo huo mgogoro ni purely wa DRC mataifa mwngine yote yakae pembeni umalizwe na wenyewe kwa wenyewe au waombe masaada AU, SADC, UN kama walivyokuwa wakifanya awali. Sion mantiki ya mtoa mada kuomba Tanzania tuingilie kati au Kenya au Uganda maana huo mgogoro hauwahusu. Ni sawa sawa kusema twende Mali kukabiliana na waasi wa huko au Sierra Lion au nchi yoyote ile ambayo ina migogoro nje ya mipaka ya Tanzania
 
Nani kakwambia Congo haina Pesa?

Congo wanaajiri hadi mercenaries kutoka Urusi kwa pesa zao za madini ndo washindwe kununua izo silaha kwa maelekezo ya Jeshi letu?
Kwanini sasa Drc wasitumie vizuri hizo pesa walizonazo kulijenga vizuri jeshi lake Ili liweze kuilinda nchi yao ?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…