Kuna siasa ndani yake tukio la wasanii kuhusishwa na matumizi ya dawa za kulevya

Kuna siasa ndani yake tukio la wasanii kuhusishwa na matumizi ya dawa za kulevya

Mimi Nimechoka kusikia Majina ya Polisi yanatajwa kwa jina moja as if Hawajulikani au hawajahakiki TIN zao!
Mlaleo; soma majina ya askari wa Kawe aliyetajwa kama kawaida kwa jina moja la Glory, je, kuna akina Glory wawili Kawe? Kama ni mmoja mchunguzi makini hawezi kutoa jina moja Mara mbili katika list moja. Huu ni ubabaishaji na ukurupukaji kama siku zote. Jina moja linaanza na WP GLORY lingine Glory moja kwa moja, sijui ni kuongeza idadi?
 
Acha mkuu afanye kaz yake hili baaade tueshimiane mambo yakupata pesa kiurahis rahis uku wakiumiza watoto watu na ukaanza kupanda watu vichwan yakome, watu sasa watafute pesa kiualali hili wawe na adabu.Big up sana Makonda.
 
nawe naona kama unatengeneza attention ya kuficha maovu ya hao wasanii,
 
Nenda zako nawewe kwani mtihani huu ndo mtihani wa kwanza watoto kufeli? Kwani ulitaka wataje mapema hayo majina kama walikua hawajakamilisha uchunguzi wa kuwabaini?
Watanzania tunakua na akili za ajabu kila kinacholetwa tunajipanga kukipinga ili mradi tuonekane tuko active, Makonda ameonesha uthubutu hata kama ametaja vidagaa ila Makonda ni mfano wa kuigwa
 
Kiukweli kuna kaka yangu anafanya kazi wizara moja hivi kanipenyezea kuwa hiyo ni fumba macho hilo suala lipite. Lkn mtoa uzi kama nakuelewa hiviii
 
Hivi hawa wasanii si ndo walikuwa wapiga debe no.1 wa chama fulani mwaka juzi? Unamtumia mtu mwovu kupata mkate halafu ukishashiba unakuja kututangazia uchafu wake? Kwani wakati unamtumia hukumuona ana uchafu au ndo ya baniani mbaya? Wamesahau kampeni ya "mama mkanye mwanao vinara walikuwa kina nani? Au tuamini na chama nacho kinachunguzwa kwa kushirikiana na madalali wa unga?
Wale ni wasanii sasa unadhani wangemtumia nani kutumbuiza?
Kua msanii na wakati una jishughulisha na mambo haramu sheria itachukua mkondo wake sio kwamba usanii wako utakufanya upate favour kila sehem hata kama umevunja sheria
 
We skill yako iko sawa kweli hivi ushaona hali ilivyomtaani umeonaa ni jnsi gani wathirikaaa wa madawa walivyongezeekaaa kama hujui ulisemalo kaa kimyaaa....

Ova
Wakuu kwa ninachokiona kwa sasa kwa hili tukio la wasanii kuhusishwa na matumizi ya dawa za kulevya ni kutaka kuondoa attention ya watu kuhusu;

1)matokeo mabovu ya wanafunzi wa kidato cha nne hasa wa dar es salaam
Kwa kuwa si hali ya kawaida kwa kweli

2)kuondoa attention ya watu na kuwasahaulisha kabisa kuhusu sekeseke linaliendelea kwa sasa bungeni

Hii ndio tabia ya viongozi wa nchi wakiona wamebanwa haswaa basi watatengeneza tukio la kisiasa ili kuondoa attention iliyopo katika jamii
Mfano kuhusu ugonjwa wa dengue , kiuhalisia huu ugonjwa haukuwepo ila zimetengenezwa figisu figisu ili kufanya tukio fulani la kisiasa lipite

Hali kadhalika ugonjwa kama ebola haukuwepo nchini ila kwa ajili ya kuondoa attention ya watu waliutangaza kwa nguvu zote ili kupisha upepo wa kisiasa upite

Hivyo basi rai yangu ,
Wananchi msielekeze nguvu zenu kuhusu hawa akina wema na wasanii wengine kesi haitakwenda kokote bali ni kuzubaisha watu wasahau matokeo mabovu ya kidato cha nne na mambo yanayoendelea bungeni

Wewe hujajiuliza kwa nini hili suala limekuja ghafla hivyo? Kwani hapo zamani walikuwa hawajui kuwa wanatumia dawa za kulevya kama vile Chidy benzi kwa nini walikaa kimyaa?

Ukishajiuliza natumai utapata jibu sahihi
Mwenye macho haambiwi tazama wala mwenye maskio haaambiwi sikia



Tchaoooo
 
Hyo petit man kutwa Yuko mtaa wa wibu kino na hao bob crue wanakuwaga na don wao yule nuuzaji nguli wa kino anaekaa tbt..hao ungaa wanauza tu ukweli ndy huo

Ova
Shemeji yenu Petit Man amekamatwa na mzigo kabisa mmeanza kulia-lia,
Pia DJ wenu wa WCB Rommy Jones naye amekamatwa na mzigo ndiyo maana vijana wa WCB mmemchukia Makonda ghafla.
 
Wachangiaji wengi naona kama vile hawataki kushirikisha ubongo wao,yani hili swala liko wazi kweli kabisa afu mtu asema mleta mada naye atakuwa mmoja wao ili hali hata hajatafakari lolote. Watanzania tuko nyuma sana kwenye kupambanua mambo. Asante sana mleta uzi
 
Habar za asubuhi wanachama wote wa jf tujadiliane kwa undani hili swala mhe.paul makonda analo lipigia vita kali lipo kisiasa au ni kututeka kisaikolojia
Karibuni. ........
4eaa5905dceec42920fd7e32590ab24d.jpg
 
Approach ambayo inaonekana kufaulu katika suala hilo ni ile ya Raisi Durtete wa Ufilipino. Yeye anasema, "Tunawaua kwanza ndio uchunguzi baadaye." Kwa kipindi cha mwaka mmoja ameuwa zaidi ya 5000. Aliwaambia Polisi wake kuwa mkishajua kuwa mtu huyu ni muuza unga, piga shaba kwanza, mahakamani baadaye. Miezi iliyopita, Obama alipojaribu kupiga kelele juu ya mauwaji haya, Durtete alimtukana kwa kumwita Mwana wa Malaya aliyezaliwa na malaya Mmarekani aliyefanya umalaya na Mkenya! Obama Kimya. Hata wiki hii kwenye vyombo vya habari aliandikwa akiendelelea na Kampeni yake ya kusafisha wauza unga kwa kuwapiga risasi. Serious!!
Bila hivyo, vita hii hakuna kushinda. Duniani inafanywa na Maraisi na familia zao, Wakuu wa Majeshi, Wakuu wa Polisi, Wakuu wa Usalama, na watu hao ni matajiri kupindukia. Katika nchi za Amerika ya Kati na Kusini watu hawa wana vikundi vyao vya majeshi ya msituni kwa ajili ya kuwalinda. Kazi kwelikweli! Hata hapa nchini huwezi kufanya biashara hii kama huna ulinzi binafsi wa kutosha.
 
Makonda ni mpiga kelele anayechanganya akili za watu wasihoji mambo ya msingi.

Unawezaje kudhibiti madawa haya

-Dsm na kuacha miko mingine ya mpakani kama mbeya, kigoma, Tanga, lindi, mtwara, kagera nk......kote huko ni njia yatapita nakuingia popote nchini

- kupambana na wasanii.....hawa sio wahusika sahihi....alipaswa kuwataja wakuu wao ambao kikwete alipiga kimyaaa...Anapaswa kutafuta shina la mtiwa wa biashara hii na kuling'oa sio kuchuma majani ya mti akitaraji mti kunyauka

-kuacha kushughulika na elimu ambayo ingewapatia vijana ufaham mkubwa wakupata mahitaji muhimu na kujitambuwa kiasi kwamba wasingeshiriki kufanya au kutumia madawa.....Makonda kaifanya elimu kitu kisicho na maana.

Niwazi makonda anapotosha umma na anachofanya ni mzaha katika jambo zito kabisa
 
Kiukweli siasa imeingia ktk suala hili la Makonda kushika wasanii mwaka jana Makonda alikua na operation ya kufanya usafi ktk jiji la Dar es Salaam na akaita wasanii waje wampe support ktk kulisafisha jiji bahati mbaya ama nzuri muitikio ulikua mdogo sana kwa wasanii Makonda akajikuta anang'aa sharubu pale uwanjani na aliahidi kuwashughulikia waliokataa mwito wake na haya ndio matokeo ya kuwabambikia tuhuma za sembe ila Mungu atawasimamia najuta kusoma Finance leo hii ungekuta nimepiga LLB ningekula shavu la kusimamia kesi kwa watakaoamua kumshtaki huyu msela
 
wale dada poa vipi? usafiri wa bure wa walimu je? omba omba dar vipi ?............nk
 
Back
Top Bottom