Kuna siri gani ya mafanikio ya ghafla kwa wafanyabiashara ya kuuza smartphones?

Kuna siri gani ya mafanikio ya ghafla kwa wafanyabiashara ya kuuza smartphones?

Naona wauza simu wa makumbusho wamekuja kwenye uzi ngoja tuone kinachoendelea sisi wa tecno za kariakoo
 
Mie naona hizi biashara za simu ni kama kazi ya ziada au kuficha chanzo kikuu cha income yao. Ila ni kweli hawa vijana wanaonekana smart sana na inaonekana wana mkwanja mrefu na usafiri mzuri. ila nakua siamini kama hiyo biashara ya simu pekee ndiyo inawatoa. Kuna kitu nyuma ya pazia
Unakutana na duka Lina cover za simu protector chaji na simu kadhaa lakini muuzaji kapanga nyumba ya 200k ,ana crown na simu Kali .
 
Aiseeh ni kweli kabisa Mimi mwenyewe najjulizaga Sana simu wanazouza Bei yake ni expensive Sana , hafu ni simu ambazo Zina wateja Wachache Sana , unakuta kazipanga dukan Kama 100 ukiuliza Bei ni M1.3+ , hivi wenzetu hizi hela wanapata wapi au Kuna namna?[emoji3]
 
Wengi huwa ni vijana wadogo tu wapo kwenye 20s hasa wahitimu wa degree na diploma.

ni tabaka tofauti na wauza simu wengine, wao hujitofautisha kwa kuuza simu zenye brand zinazotrend ulaya na marekani tu kama iphone, samsung na google pixel... Simu za kichina na vitochi hawauzi.

Simu hizo bei huwa zimechangamka kwahio wengi wapo kwenye majiji yenye watu wenye vipato vya juu wanaoweza zimudu kama Dar (maduka yao yamejaa Makumbusho, Mwenge na kariakoo), Mwanza, Arusha.

kwa macho yangu nimeweza kuwa observe kwa miaka kama miwili hawa vijana na nimeona wengi biashara imebadili maisha yao ghafla.

  • vijana wanaonekana smart sana, wanatupia pamba na hawapo nyuma kwenye fashion.
  • kwenye usafiri nako si haba, kijana mwenye 20s kumiliki crown, subaru, bmw yupo juu huyo.
  • kwakuwa wanazijua simu na wanazifatilia, wengi wanamiliki simu za gharama za kisasa
  • kwenye sekta ya kula bata, hawana shughuli ndogo, uwanja huu wanafanya kweli japo kwa level za kibongo.
  • wanaishi sehemu smart, wapo waliopanga apartment nzuri, wapo waliopanga nyumba nzima, n.k huku wakiendelea na ujenzi
  • ni ngumu sana kugombaniana mwanamke, binti mwenye simu ya kichina ya laki 2 iliyochoka anahongwa hata iphone ya laki 5 yenye wateja wachache, binti kapewa tu hio iphone ashazuzuka bila kujali ya mwaka gani

[emoji23] Make sure ............ ila acha nifute
 
Back
Top Bottom