#COVID19 Kuna uhalisia kuhusu Corona hatuambiwi?

#COVID19 Kuna uhalisia kuhusu Corona hatuambiwi?

howardlite

JF-Expert Member
Joined
Jul 16, 2016
Posts
242
Reaction score
392
Ndugu Watanzania wenzangu nawasalimu,

Zipo nadharia nyingi kuhusu Ugojwa wa Corona, na kumekuwa na jitihada nyingi za ndani na nje ya nchi yetu za kupambana na virusi hivi vinavyotishia ustawi wa sayari yetu.

Tumekuwa tukisikia tahadhari nyingi kuhusu matumizi ya Chanjo (Vaccines) za Corona, lakini hakuna majibu yanayoondoa mashaka ya tahadhari hizo.

Nani wakuondoa maswali haya tata kuhusu kinachoelezwa juu ya kinachoitwa madhara ya chanjo za Corona? Je, ni serekali? Viongozi wa dini? Wanasiasa? Madaktari? Shirika la Afya (WHO)? Au ni nani?

Nani wa kuaminiwa, nani wa kuondoa mashaka haya?

Maendeleo yoyote katika nyanja yoyote ya maisha yanategemea "watu", Watanzania kwanza maendeleo yanafuata.

Viongozi wetu mliopewa nafasi ya kuiongoza nchi yetu na Watanzania wenzenu, mna dhamana ya uhai wa maisha ya Watanzania na vizazi vijavyo.

Kama kuna mambo mnayajua nyuma ya pazia kuhusu Corona na chanjo zake ambayo yanaweza kuligharimu hili taifa na vizazi kwa vizazi, Mwenyezi Mungu yupo muogopeni yeye, ponyeni nafsi zisizo na hatia. Simameni kwenye kweli ya maisha ya Watanzania wenzenu hata kama kuna gharama, hakuna mbadala wa uhai wa watu.

Jaribuni kuona matamko mnayoyatoa kuhusu Corona na muitikio wa watu wenu, je haitufundishi kitu? Watu hawaelewi? Sio kweli. Kuna mahali labda hatujakuwa wazi kwa sababu tunazozijua Kama Viongozi? Tunaogopa kuusema ukweli? Kuna ulaghai? Ubinafsi? Au matishio?

Heri wenye dhamiri safi za mioyo yao kama viongozi, maana wataliponya taifa letu, maisha yetu, uchumi wetu na vizazi vyetu na majina yao yataandikwa kwa wino usiofutika.
 
Tumeomba kupewa pesa za korona kama Uganda nina subiri tufe kama waganda wanavyo kufa wakati viongozi wao wako vizuri mifukoni nasikia kasauti kwa mbali mtanikumbuka kwa mazurii.
 
Afya na Uhai wako viko mikononi mwako, iwe korona au ugonjwa wowote.
 
Mtoa hoja hii covid 19 ipo na inaua pls pls linda afya yako na familia yako its not a rocket science kupambana na covid 19 do the basic things, vaa mask kila unapotoka nje ya nyumba yako, osha mikono yako kwa sabuni na running water, sanitizing na kila unapoweza stay home, achana na jokes za kwenye social networks.
 
Mama yungali live. Clip yake itapandishwa si muda mrefu. Kasema Corona ipo tuchukue hadhari zote kama tunavyoelekezwa na wataalamu.
 
Wizara ya Afya kupitia kwa waziri wake inapaswa kutujuza mara kwa mara juu ya wimbi hili la tatu la UVIKO 19. Tunategemea taarifa na takwimu mpya na sahihi kutoka kwake kuhusu maambukizi mapya, idadi ya wagonjwa na hata vifo vitokanavyo na gonjwa hili.

Kuzungumzia uhalisia wa tatizo ndiyo kitu pekee kitawafanya watu kujua uzito wa tatizo lililopo hapa nchini. Kama tume ya wataalamu iliundwa na kuleta mapendekezo yake, ni vyema basi tuambiane ukweli kuhusu uhalisia wake pia, ama la kama wananchi wengi wanatilia mashaka mapendekezo ya tume hii, basi jopo lingine la wataalamu wapewe nafasi ya kufanya uchunguzi juu ya mapendekezo yaliyotolewa na kukabidhiwa kwa Rais.
 
Tumeomba kupewa pesa za korona kama Uganda nina subiri tufe kama waganda wanavyo kufa wakati viongozi wao wako vizuri mifukoni nasikia kasauti kwa mbali mtanikumbuka kwa mazurii.
Jinga kabisa! Wakuuwe una nini wewe?
 
Mtoa hoja hii covid 19 ipo na inaua pls pls linda afya yako na familia yako its not a rocket science kupambana na covid 19 do the basic things,vaa mask kila unapotoka nje ya nyumba yako,osha mikono yako kwa sabuni na running water, sanitizing na kila unapoweza stay home ,achana na jokes za kwenye social networks.
Umempa pesa ya kula ili a stay home?
Je wew ume stay home au unazurura?
 
Point ni kuhusu mashaka yaliyopo juu ya madhara ya chanjo yanayosemwa,najaribu tu kufikiri kwa sauti,tahadhari hakuna mtu anapinga,note my words kuna aliyeelewa anaweza kutusaidia.
 
Corona iliondoka na watu wengi akiwemo Magufuli, nyie leteni mizaha tu.
 
Back
Top Bottom