Kuna uhusiano kati ya umasikini, ujinga na kelele?

Kuna uhusiano kati ya umasikini, ujinga na kelele?

1. Kwanini kwenye usafiri wa ndege huwa hawapigi mziki mkubwa kama alivyo kwenye basi?, halafu angalia aina ya watu wanaopanda basi na wale wanaopanda ndege.

2. Kwa nini maeneo kama Masaki, upanga na Osterbay hayana kelele , ukilinganisha na Bugurini, Mwananyamala n.k, halafu angalia aina ya watu wanoishi katika naeneo hayo.

3. Kwa nini sehemu za starehe za watu ambao ni high profile huwa hazina mziki mkubwa ukilinganisha na zile za makabwela?

Kwa nini vyumba za kupanga huwa zina kelele ya mziki mkubwa, tofauti na nyumba ambazo wanaishi wamiliki wa hizo nyumba.

Swala hili limenisumbua sana naomba maoni na mtazamo wenu.
Masikini na utulivu wa akili au ustaarabu wapi na wapi ?
 
Watu wanaomiriki IST,Forester,ndio wanaoweka exhaust ipige makelele,umeishawahi kuona V8,au bmw imewekwa exhaust pipe linalopiga kelele?
Maskini,kinachowapa aueni ni makelele,akili inakuwa imeathirika,haoni tabu kupayuka!!matajiri ni wasomi,wanataka utulivu watafakari mambo ya Dunia,na jinsi ya kuitawala na kupata ukwasi,,maskini anawaza ngono,kula,umbea,anakua na hasira,
Panda shabiby kutoka Dom kuja dar,kwa 35K,au 28K,harafu siku nyingine panda mkweche wa 18K,au 22K,uone tofauti,
Uhusiano wa Exhaust na umaskini sijauona.

Umewahi iskia Brabus G_ Wagon ikipita? Au wrangler jeep..? Hapa tunazungumzia quality ya sauti.. kuna sound ukiiskia ww mwenyew unaangaza kuitafuta gari inatokea wapi.
 
Hata utajiri una sphere zake unaweza kuwa Tajiri wa mali na Umaskini wa roho nzuri.
Na kila mtu Ni mjinga bila kujali una intelijensia kubwa kiasi gani ila utahitajika kujielimisha muda wote kila unapofikia hatua ya kukutana na ombwe kutoka unachokijua na usichokijua.
 
Kuna jamaa yangu anaishi Tandika amepdnga chumba kwenye nyumba yenye vyumba kama 12 hivi.

Nilienda kumtembelea J2 moja. Kuingia tu kwenye corridor ya ile nyumba ni kama umeingia club. Kila chumba wamefungulia muziki full blast tena nyimbo tofauti tofauti. Mwenye mchiriku, mnanda, taarab, bongo fleva.
Jamaa anakwambia hiyo ni kawaida siku za weekend.
Nyumba ikishakuwa na wapangaji zaidi ya 4 inakuwa ni shida.
 
Kuna jamaa yangu anaishi Tandika amepdnga chumba kwenye nyumba yenye vyumba kama 12 hivi.

Nilienda kumtembelea J2 moja. Kuingia tu kwenye corridor ya ile nyumba ni kama umeingia club. Kila chumba wamefungulia muziki full blast tena nyimbo tofauti tofauti. Mwenye mchiriku, mnanda, taarab, bongo fleva.
Jamaa anakwambia hiyo ni kawaida siku za weekend.
hiyo nyumba itakuwa na UNYAMA mwing sana,
 
Hata wachawi na waganga wa kienyeji wanapenda utulivu,na hufanya kazi utulivuni🤣🤣 shetani anaijua siri ya utulivu,ndomana ametupiga bao kwenye mambo mengi🙏hata matajiri nao hawapendi kelele,shida ya masikini tunapenda kelele🎵wakati wa kuumbwa ulimwengu,roho wa Mungu,alitulia juu ya maji,kimya,kimya,alifanya kazi yake katika utulivu🙏
Hii ni nyimbo by annoint amani inaitwa utulivu🙏jaribu kuipakua utainjoi na ujumbe murua.
 
Umewaza mbali mkuu
Matajiri huwakuti kwenye makelele
 
Watu wanaomiriki IST,Forester,ndio wanaoweka exhaust ipige makelele,umeishawahi kuona V8,au bmw imewekwa exhaust pipe linalopiga kelele?
Maskini,kinachowapa aueni ni makelele,akili inakuwa imeathirika,haoni tabu kupayuka!!matajiri ni wasomi,wanataka utulivu watafakari mambo ya Dunia,na jinsi ya kuitawala na kupata ukwasi,,maskini anawaza ngono,kula,umbea,anakua na hasira,
Panda shabiby kutoka Dom kuja dar,kwa 35K,au 28K,harafu siku nyingine panda mkweche wa 18K,au 22K,uone tofauti,
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Ngoja tumuulize Chalamila.

NB: mwisho wa siku hakuna kitakachosalia
 
Back
Top Bottom