Kuna ukweli wowote katika aina hii ya utapeli?

Kuna ukweli wowote katika aina hii ya utapeli?

sky soldier

JF-Expert Member
Joined
Mar 30, 2020
Posts
5,407
Reaction score
19,264
Huu utapeli hakufanyika kwa Tamaa kama ilivyozoeleka na ndipo napopata mashaka.


Ni ndugu yangu wa karibu naemwamini sana, nilimtumia pesa laki 6 anunue laptop kwajili ya chuoni. sasa nikawa nafatilia hio laptop naona ananipiga sana chenga, nikafikisha hii kero kwa mama yake ambae ni mamdogo wangu ndio akaelezea kilichomkuta ambacho hadi sasa nahisi ni stori ya uwongo.

Kwamba aliulizwa njia ya kwenda sehem flani, yeye badala ya kuelekeza njia akaanza kumpeleka mtu asiemjua hio sehemu wakati aliulizwa tu njia, njiani wakakutana na mtu mwengine alietoa msaada kumsindikiza huyo alieomba maelezo ya njia.

kufika huko, yule wanaemsindikiza alishukuru sana akawaambia yeye ni mtoto wa chifu na ni mtaalam hivyo atawatolea matatizo yao bure ikiwa kama asante, akaanza na huyu ndugu yangu akamwambia amerogwa, wachawi wameficha nywele kwenye tumbo lake, ndugu yangu akaanza kutema nywele mdomoni, Narudia tena "kutema nywele!"

akaambiwa aende kutoa pesa kibandani, akazitoa zote bila kujielewa, hakuambiwa kwamba hela zitaongezeka au atakuwa tajiri kama ilivyozoeleka, alimwambiwa tu akazitoe, akajikuta anaenda kibandani kutoa zote.

pesa aliondoka nazo akiwa kahakikisha zipo mfukoni, ila anafika kwake anakuta simu imekuwa mbao na hela zote zimekuwa makaratasi ya maboksi.

..............................

Binafsi nimeumia sana, hio pesa inaweza kuwa si chochote kwa mwengine ila kwangu hio laki 6 ni sehem kubwa katika mshahara wangu, Nmeumia mno.

Sasa nmekuja humu kwenye jukwaa la wananchi mnipe ukweli wowote juu ya hii stori maana imekaa kama imetungwa hivi

Pia soma
- Ni namna gani ya kukabiliana na wizi wa kusemeshwa na mtu usiyemjua?
 
Kakutana na wale wataalamu. Kwakweli hayajawahi kunikuta ila sijawahi elewa how do they do it
Hakuna cha kukutana nao wala nini. Wanatumia ujanja wa kuteka watu kwa maneno tu. Huyo jamaa atakuwa kapigwa kweli ila ni yeye aliwapa hiyo simu na hizo fedha kwa tamaa kuwa fedha zinaongezeka, kumbe walibadilisha wakampa maboksi. Hilo la kutema nywele inawezekana kuna ujanja wanatumia na kuziweka kinywani mwake kiaina. Hakuna dawa wala nini.
 
We unaweza cheza na akili ya mtu mpaka aende atm atoe pesa yote akupe pasipo yeye kuwa na ufahamu?
Si kawaida
Huo muda sina ila wale jamaa wanacheza na saikologia tu ya mtu,nimeishi Ubungo zaidi ya miaka 10...... wakati wa stend wengi walikuwa wanaibiwa Kwa kuzuzubaa zubaa tu kushangaa......maana ndiyo mara ya kwanza kuingia dsm.....hapo hapo ndiyo wanapigwa Kwa maneno tu
 
Hakuna cha kukutana nao wala nini. Wanatumia ujanja wa kuteka watu kwa maneno tu. Huyo jamaa atakuwa kapigwa kweli ila ni yeye aliwapa hiyo simu na hizo fedha kwa tamaa kuwa fedha zinaongezeka, kumbe walibadilisha wakampa maboksi. Hilo la kutema nywele inawezekana kuna ujanja wanatumia na kuziweka kinywani mwake kiaina. Hakuna dawa wala nini.
Je wale wanaodai uwa hadi wanaenda atm wanatoa pesa yote wanawapa wengine hadi majumbani kwao halafu wakishaachana nao ufahamu ndo unawarudia.
 
We unaweza cheza na akili ya mtu mpaka aende atm atoe pesa yote akupe pasipo yeye kuwa na ufahamu?
Si kawaida
Hakuna kitu kama hicho. Kuna thread iko hapa juzi tumejadali sana kuhusu hili. Wengine wanadai kuna dawa inafanya mtu anatenda mambo bila free will ila hayo yote ni uvumi. Kungekuwa na dawa za aina hiyo kwanza wangepigwa wenye fedha ndefu tu na wasingehaika na vitu kama simu za techno na fedha za kutoa kwa simu. Na zaidi, wanawake wazuri wangepona? Si wangekuwa wanachukuliwa kama utani tu?
 
Huo muda sina ila wale jamaa wanacheza na saikologia tu ya mtu,nimeishi Ubungo zaidi ya miaka 10...... wakati wa stend wengi walikuwa wanaibiwa Kwa kuzuzubaa zubaa tu kushangaa......maana ndiyo mara ya kwanza kuingia dsm.....hapo hapo ndiyo wanapigwa Kwa maneno tu
Naunga mkono bila ubishi wowote. Mimi watu wa aina hii nimekutana nao mara kadhaa na wakiona wewe ni mjanja wanakimbia haraka sana. Mbona hawajaweza ''kunipumbaza kiakili'' kwa dawa kama watu wanavyodai?
 
Je wale wanaodai uwa hadi wanaenda atm wanatoa pesa yote wanawapa wengine hadi majumbani kwao halafu wakishaachana nao ufahamu ndo unawarudia.
Hii ipo kabisa, una mzee mmoja mstaafu wa mtaani kwetu alipigwa, tena yeye alienda atm mbili tofauti kutoa mpunga.
 
Je wale wanaodai uwa hadi wanaenda atm wanatoa pesa yote wanawapa wengine hadi majumbani kwao halafu wakishaachana nao ufahamu ndo unawarudia.
Wanaenda ATM kutoa kwa sababu wanakuwa wamedangwa kuwa watatengeneza hizo fedha ziongezeke wawe matajiri. Pia wanaambiwa watoe vitu vya thamani kama simu au vitu kutoka majumbani mwao ili dau liwe kubwa na utajiri uongezeke. Sharati kubwa la hao watu huwadanganya kuwa wasimwambie mtu yoyote na wakisema tu dawa haifanyi kazi. Wakishaachana ''ufahamu'' hurudi kwa sababu baada ya kusubiri au kufungua walichoaminishwa ni fedha nyingi na kukuta ni makaratasi ndiyo wanajua ukweli.
 
Back
Top Bottom