Sheillah Sheillah
JF-Expert Member
- Jun 17, 2020
- 653
- 1,698
Habari,
Hivi kwani ni lazima mtu kulia hadi uso uchakae unapofiwa na mtu wako wa karibu (wazazi ,mwenza,mtoto, ndugu)? Au ni lazima kulia mbele za watu wajue umelia?
Kwanini watu wakienda kwenye msiba wanataka wakimuona mfiwa wamuone kachakaa, macho yamevimba uso umeumuka kwa ajili ya kulia? Kwani mtu kuhuzunika ni lazima alie? Au kwani kulia ni lazima? wasipolia ndio inaonekana kifo hakijawaumiza? na hata kama kifo hakijawaumiza nyie mnakasirika nini,?
Kuna watu wakisikia tu mtu kafiwa, halafu waone amependeza zake hajachakaa sura, akiona cha kuchekesha anacheka na simu anatumia anaingia mtandaoni wanakasirika hatari, utasikia "umefiwa mara hii tayari upo sawa na mtandaoni unaingia na kucheka unacheka"..mimi naona ni kama kuwaonea wivu wafiwa.
Kila mtu ana namna yake ya kuomboleza, tuache kuwaletea makasiriko wafiwa wanaoweza kuhandle msiba vizuri.
Hivi kwani ni lazima mtu kulia hadi uso uchakae unapofiwa na mtu wako wa karibu (wazazi ,mwenza,mtoto, ndugu)? Au ni lazima kulia mbele za watu wajue umelia?
Kwanini watu wakienda kwenye msiba wanataka wakimuona mfiwa wamuone kachakaa, macho yamevimba uso umeumuka kwa ajili ya kulia? Kwani mtu kuhuzunika ni lazima alie? Au kwani kulia ni lazima? wasipolia ndio inaonekana kifo hakijawaumiza? na hata kama kifo hakijawaumiza nyie mnakasirika nini,?
Kuna watu wakisikia tu mtu kafiwa, halafu waone amependeza zake hajachakaa sura, akiona cha kuchekesha anacheka na simu anatumia anaingia mtandaoni wanakasirika hatari, utasikia "umefiwa mara hii tayari upo sawa na mtandaoni unaingia na kucheka unacheka"..mimi naona ni kama kuwaonea wivu wafiwa.
Kila mtu ana namna yake ya kuomboleza, tuache kuwaletea makasiriko wafiwa wanaoweza kuhandle msiba vizuri.