Robert S Gulenga
JF-Expert Member
- Jan 3, 2013
- 2,255
- 1,565
Taarifa sahihi ndio msingi wa umoja na mshikamano, kama Taifa tunahitaji kila Mtanzania apate taarifa sahihi kutoka katika vyanzo sahihi. Serikalini katika kila wizara, halmashauri au taasisi kuna kitengo cha habari kwa ajili ya kutoa taarifa ya utekelezaji wa mambo kwenye taasisi hizo au wizara hizo.
Kwa sasa kuna utekelezaji wa miradi mbali mbali unaendelea, kwa mfano Utekelezaji wa ujenzi wa bwawa la kuzalisha umeme(JNHP) unaendelea, ujenzi wa SGR unaendelea vizuri, Ujenzi wa daraja la busisi unaendelea, barabara mbali mbali zinaendelea kujengwa kwa kiwango cha lami. Kuna ujenzi wa shule za masomo ya sayansi kwa wasichana kila mkoa zinaendelea, ujenzi wa hospital, vituo vya afya, zahanati, majengo ya utawala, soko, stendi, miradi ya maji kila kona ya Tanzania. Maafisa habari waliopo kwenye wizara, taasisi na halmashauri wanaelezea hii miradi inayoendelea kutekelezwa kwa kiwango gani? Ni namna gani wanawafikia watanzania?Je, wananchi wanajua hii miradi inayotekelezwa?
Serikali kupitia wizara, taasisi na halmashauri iimarishe vitengo vyote vya habari, wana habari wawezeshwe kuendana na wakati ili waweze kuwapa watanzania taarifa sahihi za utekelezaji wa miradi inayoendelea. Haikwezekani Waziri au Rais ndio anajukumu la kuwaambia watanzania utekelezaji wa miradi ya maendeleo wakati maafisa habari wa serikali wapo.
Mh. Nape Nnauye(Mb) Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari na Mh. Innocent Bashungwa(Mb) Waziri OR - TAMISEMI saidieni kuimarisha vitengo vya habari vilivyopo serikalini hasa halmashauri ili viweze kuonyesha mazuri mengi yanayofanywa na serikali ya awamu ya sita. Leo hii maafisa habari wa zile timu mbili ni maarufu kuliko maafisa habari wengi wa serikali, kuna umuhimu wa kuboresha na kuwezesha vitengo hivi vya habari serikalini.
Haiwezekani iwe Waziri, Katibu Mkuu au Msemaji wa Serikali tu ndio wawe na jukumu la kuelezea utekelezaji wa miradi ya Maendeleo wakati kuna maafisa habari serikalini wenye weledi wa kuweza kuelezea pia. Dunia imehamia kiganjani maafisa habari waje duniani waelezee mazuri yanayofanywa na serikali ya awamu ya sita chini ya Rais Samia Suluhu Hassan.
Wananchi wakipewa taarifa sahihi za utekelezaji wa miradi ya maendeleo, watajua kodi na tozo zinazolipwa kweli zinasimamiwa vizuri katika utekelezaji wa miradi ya maendeleo. Watanania lazima tuelewe kodi na tozo tunazolipa ndizo zinazoenda kutekeleza miradi ya maendeleo ili kuweza kuwahudumia Watanzania.
Maafisa habari wetu wasiogope spana za wakosoaji na wale wenye kazi ya kupinga na kutukana bila hoja, wajitokeze kwenye platform tofauti kuelezea mazuri ya serikali.
Hongereni saaa Mh. Mohamed Mchengerwa(Mb) Waziri wa Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo - Gerson Msigwa -Msemaji Mkuu wa Serikali, DK Hassan Abbas - Katibu Mkuu wa Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mh. Nape Nnauye(Mb) Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Mh. Innocent Bashungwa (Mb) Waziri OR - TAMISEMI, Mh Hussein Mohamed Bashe(Mb) Waziri wa Kilimo, Mh. Juma H. Aweso(Mb) Waziri wa Maji na mawaziri wengine kwa namna mnavyopambana kufikisha taarifa sahihi licha ya wakati mwingine kukutana na sapana kali au kupata kejeli na matusi kutoka kwa watu ambao kazi yao ni kupinga tu. Hamjawahi choka kumsaidia Mh. Rais Samia Suluh Hassan katika kuwahudumia watanzania, mara nyingi mmekuwa mkitolea ufafanuzi wa mambo mbali mbali kwa kuweka ukweli bayana.
Serikali ya awamu ya sita chini ya Mh. Rais Samia Suluhu Hassan kwa mwaka huu wa fedha imetenga jumla ya shilingi bilion 75. 98 kupitia halmashauri zote nchini kwa ajili ya mikopo ya vijana, wanawake na watu wenye ulemavu, vijana tuchangamkie fursa hii adhimu, fedha hizi zimeshaanza kutolewa katika kila halmashauri.
Mungu ibariki Tanzania,
Mungu mbariki Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan
Kwa sasa kuna utekelezaji wa miradi mbali mbali unaendelea, kwa mfano Utekelezaji wa ujenzi wa bwawa la kuzalisha umeme(JNHP) unaendelea, ujenzi wa SGR unaendelea vizuri, Ujenzi wa daraja la busisi unaendelea, barabara mbali mbali zinaendelea kujengwa kwa kiwango cha lami. Kuna ujenzi wa shule za masomo ya sayansi kwa wasichana kila mkoa zinaendelea, ujenzi wa hospital, vituo vya afya, zahanati, majengo ya utawala, soko, stendi, miradi ya maji kila kona ya Tanzania. Maafisa habari waliopo kwenye wizara, taasisi na halmashauri wanaelezea hii miradi inayoendelea kutekelezwa kwa kiwango gani? Ni namna gani wanawafikia watanzania?Je, wananchi wanajua hii miradi inayotekelezwa?
Serikali kupitia wizara, taasisi na halmashauri iimarishe vitengo vyote vya habari, wana habari wawezeshwe kuendana na wakati ili waweze kuwapa watanzania taarifa sahihi za utekelezaji wa miradi inayoendelea. Haikwezekani Waziri au Rais ndio anajukumu la kuwaambia watanzania utekelezaji wa miradi ya maendeleo wakati maafisa habari wa serikali wapo.
Mh. Nape Nnauye(Mb) Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari na Mh. Innocent Bashungwa(Mb) Waziri OR - TAMISEMI saidieni kuimarisha vitengo vya habari vilivyopo serikalini hasa halmashauri ili viweze kuonyesha mazuri mengi yanayofanywa na serikali ya awamu ya sita. Leo hii maafisa habari wa zile timu mbili ni maarufu kuliko maafisa habari wengi wa serikali, kuna umuhimu wa kuboresha na kuwezesha vitengo hivi vya habari serikalini.
Haiwezekani iwe Waziri, Katibu Mkuu au Msemaji wa Serikali tu ndio wawe na jukumu la kuelezea utekelezaji wa miradi ya Maendeleo wakati kuna maafisa habari serikalini wenye weledi wa kuweza kuelezea pia. Dunia imehamia kiganjani maafisa habari waje duniani waelezee mazuri yanayofanywa na serikali ya awamu ya sita chini ya Rais Samia Suluhu Hassan.
Wananchi wakipewa taarifa sahihi za utekelezaji wa miradi ya maendeleo, watajua kodi na tozo zinazolipwa kweli zinasimamiwa vizuri katika utekelezaji wa miradi ya maendeleo. Watanania lazima tuelewe kodi na tozo tunazolipa ndizo zinazoenda kutekeleza miradi ya maendeleo ili kuweza kuwahudumia Watanzania.
Maafisa habari wetu wasiogope spana za wakosoaji na wale wenye kazi ya kupinga na kutukana bila hoja, wajitokeze kwenye platform tofauti kuelezea mazuri ya serikali.
Hongereni saaa Mh. Mohamed Mchengerwa(Mb) Waziri wa Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo - Gerson Msigwa -Msemaji Mkuu wa Serikali, DK Hassan Abbas - Katibu Mkuu wa Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mh. Nape Nnauye(Mb) Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Mh. Innocent Bashungwa (Mb) Waziri OR - TAMISEMI, Mh Hussein Mohamed Bashe(Mb) Waziri wa Kilimo, Mh. Juma H. Aweso(Mb) Waziri wa Maji na mawaziri wengine kwa namna mnavyopambana kufikisha taarifa sahihi licha ya wakati mwingine kukutana na sapana kali au kupata kejeli na matusi kutoka kwa watu ambao kazi yao ni kupinga tu. Hamjawahi choka kumsaidia Mh. Rais Samia Suluh Hassan katika kuwahudumia watanzania, mara nyingi mmekuwa mkitolea ufafanuzi wa mambo mbali mbali kwa kuweka ukweli bayana.
Serikali ya awamu ya sita chini ya Mh. Rais Samia Suluhu Hassan kwa mwaka huu wa fedha imetenga jumla ya shilingi bilion 75. 98 kupitia halmashauri zote nchini kwa ajili ya mikopo ya vijana, wanawake na watu wenye ulemavu, vijana tuchangamkie fursa hii adhimu, fedha hizi zimeshaanza kutolewa katika kila halmashauri.
Mungu ibariki Tanzania,
Mungu mbariki Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan