Uchaguzi 2020 Kuna umuhimu wa kupiga kura 2020 wakati tume iko mfukoni kwa Rais?

Tume ilikuwa hivyo tangu Tanzania Bara ipate uhuru, Enzi za Mwl ilikuwa hivo, za Ruksa ilikuwa hivo, wakati wa Rais Mkapa na Kikwete ilikuwa hivyo!! Sasa kelele za nini? Awamu ya tano inaendeleza yale mazuri yaliyokuwepo. Period.
Kwa hiyo hata kama haifanyi kazi kwa uweledi iachwe tu kwakua historia ndivyo ilivyo?
 
Mizengwe itawafanya wengi wapite bila kupingwa! Tutafanyaje bora wanaopita bila kupingwa wapigiwe kura za ndio au hapana.
Ni vema tujiandae kupigara na tuandae basi mazingira...

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Binafsi sioni umuhimu. It is just a waste of time and tax payer's money. Magufuli and CCM should just carry on maana kupigwe kura kusipigwe kura the end result is the same.
 
2020 naona umiamua kuja kivingine.. hongera mwanangu
 







Miaka yote mlikuwa mnapiga kura time ilikuwa kwenye mfuko wa nani?
 
Bila tume huru ya uchaguzi hakuna kushiriki ,Kama ilivyokuwa uchaguzi wa serikali za mitaa.
 
Binafsi sioni haja ya kuwa na uchaguzi ambao ni kiini macho. Anaeteua wasimamizi wa uchaguzi alishawahi kuwaambia (tena hadharani) kuwa: "mshahara nikulipe mimi, gari nikupe mimi halafu wewe umtangaze mpinzani kuwa ndie mshindi?
 
Kiinimamacho kivipi fafanua.
Tusiwadanganye wananchi wakakosa kutumia haki yao kikatiba kushiriki kupiga Kura 2020
 
Mbowe kushiriki au kutoshiriki huo ni uamuzi wake na chama chake, ila sisi wapiga kura tunaojitambua tumeshafanya maamuzi, kama hakuna tume huru ya uchaguzi, hatushiriki uchaguzi wa kishenzi fullstop.

Wewe ndio msemaji wa Wapiga Kura nchini?
 
Utajuaje wingi wa kura za upinzani ndani ya sanduku ambavyo kura ni siri ys mtu?

Muhimu ni mawakara kutorubunika kwa vipesa na kila chama cha ipinzani kiwe na kamati ya kila kijiji ya kupita katika vituo vya kupigia kura ili wajumlishe matokeo. Kamati hizo za kiiji zitime mayokeo katika ngazi ya kata hadi taifa. Hiyo ifanyike mara tu. baada ya matokeo kubandikwa.

Lakini bila ya mawakala waaminifu hata ikiundwa tume huru ya uchaguzi hakuna matokeo chanya. Kumbuka vijjn na hata mijini kwa kila mtaa wanafahamiana sana. Hivyo ni rahisi chama tawala kula njama na kumshawishi wakala mrafi wa upinzani akaomba nafasi ya uakala na akawa msimamizi wa uchaguzi.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…