Kuna umuhimu wowote wa mabucha yetu Tanzania kuuza nyama pamoja na mifupa?

Kuna umuhimu wowote wa mabucha yetu Tanzania kuuza nyama pamoja na mifupa?

Sema uvivu TU wa kibiashara mwenye bucha angeweka bei juu ya steki watu wangenunua mbona supermarket unapata steki tupu bila mfupa wowote na watu wananunua

Kenya bucha nyingi huuza steki TU hasa mabucha ya miji mikubwa hukuti huu ujinga wa kutumia gogo na kuuza nyama mchanganyiko utake usitake lazima uondoke na mifupa na mifupa ndio yaweza kuwa mizito na mingi kuliko nyama
Ila nyama bila hata mfupa wa mbavu mi naona hainogi kabisa...
 
Ya jana ndiyo nyama mkuu, hiyo ya leo unakula muscles mkuu! Steak mbona zipo mkuu na bei zake zinajulikana?
Wewe ni kama mimi, hii siri alinipa muuza nyama mmoja Mgogo, yaani kama nyama ni nzuri Sana nainunua kesho yake, ananiwekea...
 
Wewe ni kama mimi, hii siri alinipa muuza nyama mmoja Mgogo, yaani kama nyama ni nzuri Sana nainunua kesho yake, ananiwekea...
Watu wengi hawajui lakini sisi tuliosoma haya mambo ya meat production from rumainants tunajua. Nyama inatakiwa iachwe masaa kadhaa ili kufanya kitu kinaitwa ageing. Ndiyo maana watu huwa wanalalamika nyama ngumu kama mpira, kumbe anatafuna muscles siyo nyama!
 
Mimi siku zote nasemaga kwamba hakuna mfupa mtamu kwa ng'ombe.

Utakuta mtu anasema "napenda nyama mfupa" unapenda wapi bhana huna hela kama mimi tu.

Mimi nikiwa na 10K bora nikanunue steki yote kuliko kutoa 8K kununua mchanganyiko,maana katika hiyo alfu nane kuna mifupa ya nailipia ambayo nakwenda kuitupa tu.
Mimi siku zote nasemaga kwamba hakuna mfupa mtamu kwa ng'ombe.

Utakuta mtu anasema "napenda nyama mfupa" unapenda wapi bhana huna hela kama mimi tu.

Mimi nikiwa na 10K bora nikanunue steki yote kuliko kutoa 8K kununua mchanganyiko,maana katika hiyo alfu nane kuna mifupa ya nailipia ambayo nakwenda kuitupa tu.
Hivi cartilage bones haifai kuliwa?
Vipi makongolo, si ndio wanatengenezea supu ya walevi.
 
Kwa Manundu nyama ya steki inazidi elfu 2 tu kutoka bei ya nyama ya kawaida.

So ukitoa elfu 10 unapata steki.

Halafu kama hautaki mifupa jaribu kununua utumbo tena gharama yake ni nusu ya bei ya nyama.
 
Watanzania tunapenda kulalamika sana aisee,kwa ninavyojua ukitaka steak tupu ina bei yake na mchanganyiko una bei yake sasa unashindwaje kuchagua,na kingne muwe mnaangalia na mabucha ya kununua nyama,bucha ninunualo mm kitoweo jamaa anapanga sana foleni aisee maana kwa nyama nusu anakuwekea vitufupa v2 au v3 basi zingne zote steak
 
Ya jana ndiyo nyama mkuu, hiyo ya leo unakula muscles mkuu! Steak mbona zipo mkuu na bei zake zinajulikana?
Nipe elimu hapa, kumbe nyama inakanuni zake.
Af mie nyama ya jana huwa naiona inepooza na ina kaharufuu fulani
 
Kwa Manundu nyama ya steki inazidi elfu 2 tu kutoka bei ya nyama ya kawaida.

So ukitoa elfu 10 unapata steki.

Halafu kama hautaki mifupa jaribu kununua utumbo tena gharama yake ni nusu ya bei ya nyama.
Kupika utumbo ni bora upike maharage
 
Pamoja na majibu mazuri ya wachangiaji, binafsi naona mleta uzi ana hoja ya kujibiwa.

Tusii-dilute hoja yake kwa kuendekeza mizaha isiyo na tija ilhali kila mmoja wetu anafahamu uhalisia wa mabucha na baadhi yetu mambo haya yamewakuta walipoenda buchani kutafuta kitoweo cha familia.

Ndugu zangu, bucha za Bongo zina udhaifu wa kuzingatia ubora wa kinachouzwa, badala yake inaangaliwa zaidi kurudisha mtaji na faida zao.

Baadhi ya wauza nyama unakuta wanauza nyama yenye ubora wa chini kwa kisingizio cha 'mchanganyiko'. Mteja anawekewa nyama zisizolika kama vile mafuta au 'malapulapu' ambapo ukifikisha nyumbani inakubidi ukate utupe jalalani. Ukijaribu kuwa makini pale buchani lazima ukosane nao, huruhusiwi kuchagua aina ya nyama.

Hebu tafakari, kwa nini ununue nyama kwa fedha, tena kwa kupimiwa uzani, halafu robo hadi nusu ya uzani ni nyama isiyolika kwa raha (Mifupa, sehemu ngumu, mafuta, milenda n.k ) hadi unaamua kuikata na kuitupa.

Hata kama bei haiwalipi wafanyabiashara wa mabucha, tukubali this is primitive!

Kuna pendekezo nahisi nikilitoa hapa nitagombaniwa na wadau kama mpira wa kona.

Lakini tujitafakari upya, kwenye maisha mambo mawili ya msingi - kupata chakula bora na mavazi ndio namna kuu za kutumia pesa zako na ukazifaidi wewe mwenyewe.
Kama bei ya nyama iliyopo haiwalipi watoa huduma, basi mamlaka husika za Serikali ziangalie ni kwa namna gani wananchi wauziwe kilicho bora kwa bei wanayoimudu.

Kwa vile hii 'category' ya mchanganyiko baadhi ya wafanyabiashara wameigeuza kuwa kumbakumba ya kila aina ya nyama za hovyo; Pendekezo mojawapo ni kuweka nyama kwa viwango (lakini ziwe zile tu zenye hadhi ya kuliwa na binadamu ), Kila mtu achague inayoendana na kipato chake, iandaliwe kistaarabu, ikatwe na kupimwa kabla ili kuepusha kuuza kwa kuzingatia sura ya aliyekuja buchani (mtaani kwetu ukituma mtoto mdogo utalia 🙂 ).


Pia, Serikali ifanye uratibu kuhakikisha nyama zilizo duni sana hata buchani zisifike. Zinaweza kuuzwa kwa wanaotengeneza vyakula vya mifugo na matumizi mengine.

Tujenge jamii iliyostaarabika na inayojijali kwa maisha bora.
 
Nipe elimu hapa, kumbe nyama inakanuni zake.
Af mie nyama ya jana huwa naiona inepooza na ina kaharufuu fulani
Ndiyo mkuu, hizi tunazozikuta kwenye mabucha zikidondosha damu siyo nyama hizo mkuu! Nyama inatakiwa iwekwe kwanza kwenye chilling room kwa masaa angalau 12. Baada ya hapo sasa inaweza kuwekwa kwenye cold room. Sasa hiyo ndiyo nyama sasa!
 
Ndiyo mkuu, hizi tunazozikuta kwenye mabucha zikidondosha damu siyo nyama hizo mkuu! Nyama inatakiwa iwekwe kwanza kwenye chilling room kwa masaa angalau 12. Baada ya hapo sasa inaweza kuwekwa kwenye cold room. Sasa hiyo ndiyo nyama sasa!
Kwa nini sio myama, na kwa nini ya kulala imepoa sana unaweza poteza hata hamu ya kuila.
 
Mimi nyama na mifupa..kwangu si nyama...kumbuka nyama iliyolaribu na mfupa ndiyo nyama tamu
 
Ndiyo mkuu, hizi tunazozikuta kwenye mabucha zikidondosha damu siyo nyama hizo mkuu! Nyama inatakiwa iwekwe kwanza kwenye chilling room kwa masaa angalau 12. Baada ya hapo sasa inaweza kuwekwa kwenye cold room. Sasa hiyo ndiyo nyama sasa!
Kitaalamu Zaidi..shida hizi za buchani hawaweki kwenye chilling room zinapigwa na feni siku nzima kama siyo feni basi nzi watatu hapo watazaliana na kuzaliana..sasa ukiinunua kesho unakua ni uchafu
 
Back
Top Bottom