Kuna uwezekano mkubwa kombe la dunia Qatar kuhairishwa

Kuna uwezekano mkubwa kombe la dunia Qatar kuhairishwa

Sababu za Tanganyika kuwepo Znz hadi leo ndio hizo hizo zinazoifanya Russia isioache Ukraine


Sababu zilizofanya Marekani kuigawanya Ujerumani, Korea ndio hizo hizo zinaifanya Russia kuigawa Ukraine
Urusi inatakiwa itambue, Ukraine ni nchi huru na yenye maamuzi yake;kama Urusi itaondoa majeshi, na kutokuingilia Ukraine kwenye maamuzi yao, vita itaisha; na hii itafanikiwa iwapo mpatanishi atatoka G7
 
Mzuka Wanajamvi!

Kutokana na hali ya vita huko Ukraine hali inazidi kuwa tete. Na leo kwenye hotuba yake Putin ameendelea kusisitiza hatanii kutumia mabomu ya nyuklia. Na uwezekano wa kizitumia ni mkubwa kwasababu anapokea mkong'oto wa haja kutoka majeshi ya Yukrein.

Hii itasababisha vita ya tatu ya dunia kwasababu Yukrein naye anatuma maombi NATO.

Kuna uwezekano kombe la dunia Qatar kuhairishwa. Na siyo kombe la dunia ratiba ya vitu vingi vitabadilika dunianina kuvurugika. Mfano Biashara na soko la hisa usafiri na kadhalika.

Inachotupasa tuombeni amani. Huu mzozo au vita ya Ukraine utaisha tu katika meza ya mazungumzo. Kwasababu tunapoelekea Yani hata EPL nayo itasimama.
Wewe tushakwambia bangi hazikufai
 
Sababu za Tanganyika kuwepo Znz hadi leo ndio hizo hizo zinazoifanya Russia isioache Ukraine


Sababu zilizofanya Marekani kuigawanya Ujerumani, Korea ndio hizo hizo zinaifanya Russia kuigawa Ukraine
Kama sababu ni za kiusalama; bado wanaweza kuimarisha ulinzi wa ndani pamoja na kuboresha teknolojia ili kila nchi iwe huru kwenye maamuzi yake
 
Putin anataka kuondoka na watu hatanii kweli kwa jinsi alivyodundwa hata meno anaweza kutumia akiamini yatamsaidia...Putin kashindwa vita ila anaona aibu kure treat..
 
Ukweli sisi raia wa hii sayari tungejifikirisha vizuri ilitakiwa wote tuandamane kulaani kuendelea kwa vita huko ukrein.

Raia wa Marekani hadi Urusi kwenyewe bado wanaona kama nchi zao zina haki ya kufanya wanacho fanya.

Huko nchi za NATO vivyo hivyo, wanaona hayawahusu wanawaachia watawala kufanya wafanyayo.

Huku Afrika raia tunaishia ushabiki mara timu Russia mara timu Marekani.

Lakini hebu tujiulize ukubwa wa gharama iwapo patatokea vita vya nuklia. Nani atasalimika?

Si afadhali tuwapigie kelele watawala waache vita hivyo?
 
Hili movie linalochezwa Kati ya Ukraine na urusi ni marudio tu ambayo yamechezwa Sana na member Hawa wawili yaan USA na Urusi after 2second WW,kwenye Ile issue ya COLD WAR,,tusijisahaulishe kuwa hata USA alishawahi kuivamia CUBA bila urusi kuingilia Kati chini Joseph steering USA alikuwa anaichukua Cuba,,so uhasama unaofanyika hapa ni Kati ya USA na Rusia nyuma ya mgongo wa ukraine
 
Urusi inatakiwa itambue, Ukraine ni nchi huru na yenye maamuzi yake;kama Urusi itaondoa majeshi, na kutokuingilia Ukraine kwenye maamuzi yao, vita itaisha; na hii itafanikiwa iwapo mpatanishi atatoka G7
Huu ufala unaweza kutokea nchi za Dunia ya tatu.
 
Iraq haikua nchi huru? Vipi kuhusu Libya? Vipi kuhusu Afghanistan? Vipi kuhusu Syria na Yemen?

Si ni haohao wanaounda G7 ndio walihusika kuvuruga hizo nchi? Leo Ukraine kuna kipi cha ajabu ambacho hawakukifanya Libya na Syria?
majamaa huwa wananichekesha sana wakizungumzia sovereignty.

Mvamizi namba moja duniani wa mataifa huru kwa kisingizio cha human rights anajulikana.
 
Mzuka Wanajamvi!

Kutokana na hali ya vita huko Ukraine hali inazidi kuwa tete. Na leo kwenye hotuba yake Putin ameendelea kusisitiza hatanii kutumia mabomu ya nyuklia. Na uwezekano wa kizitumia ni mkubwa kwasababu anapokea mkong'oto wa haja kutoka majeshi ya Yukrein.

Hii itasababisha vita ya tatu ya dunia kwasababu Yukrein naye anatuma maombi NATO.

Kuna uwezekano kombe la dunia Qatar kuhairishwa. Na siyo kombe la dunia ratiba ya vitu vingi vitabadilika dunianina kuvurugika. Mfano Biashara na soko la hisa usafiri na kadhalika.

Inachotupasa tuombeni amani. Huu mzozo au vita ya Ukraine utaisha tu katika meza ya mazungumzo. Kwasababu tunapoelekea Yani hata EPL nayo itasimama.
America sio wafanye jitiada kuwapatanisha hizo Nchi mbili vita viishe, yeye anasisitiza tu kutoa msaada wa silaha kwa Ukraine, natamani Russia ilo bomu la nuclear angelipiga america
 
Iraq haikua nchi huru? Vipi kuhusu Libya? Vipi kuhusu Afghanistan? Vipi kuhusu Syria na Yemen?

Si ni haohao wanaounda G7 ndio walihusika kuvuruga hizo nchi? Leo Ukraine kuna kipi cha ajabu ambacho hawakukifanya Libya na Syria?
Utawaweza hao mifugo ya America
 
Vyovyote itakavyokua watakaoumia ni sisi panzi uku tusioweza kujitegemea.Tunakalia ushabiki maandazi wakati hatuna kila kitu.Kuna wajinga hapa naona wanagikiri anayekomolewa ni marekani wakati wamarekani wanakula zao bata uko kwao tunaoteseka ni sisi uku tunaokimbizana na tozo.

Sent from my SM-A107F using JamiiForums mobile app
 
Mfano wako hauna uhalisia. Mfano halisi ni huu:

Kuna wahuni kila siku wanatishia kupiga mawe na kuvunja madirisha ya nyumbani kwako. Alafu jirani yako anawakaribisha, na anakubaliana nao waje kuweka nyumbani kwake mafurushi ya mawe watakayotumia kuvunja madirisha yako.

Utafanyaje? Utamuacha jirani eti kisa anao uhuru wa kuamua mambo ya nyumbani kwake?
Bado hizo sio sababu za maana kwasababu vita zina gharama kubwa kuliko meza ya mazungumzo.Huu ni ujinga wa putin na siku akifa hayo majimbo na hizo nchi lazima zianzishe vuguvugu zakujitenga kwasababu ilishafanyika hivyo uko nyuma.Lakini pia huu ujinga umeathiri ata ambao hawahusiki na unaendelea kuathiri.

Sent from my SM-A107F using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom