Kuna uwezekano mkubwa miradi ya SGR na Stieglers' Gorge isikamilike

Kuna uwezekano mkubwa miradi ya SGR na Stieglers' Gorge isikamilike

Mukulu wa Bakulu

JF-Expert Member
Joined
Aug 12, 2014
Posts
4,051
Reaction score
12,954
Hizi nchi zetu masikini ikitokea changamoto kidogo ni shida kubwa sana.

Tanzania inategemea mapato ya utalii kwa zaidi ya 25%. Utalii mwaka huu ni kama umekufa kabisa kama sio uko chini ya 2%. Hasa kipindi hiki cha March hadi June hua kuna watalii wengi sana nchi hii, ila sababu ya corona kila mtu anajua kinachoendelea.

Maana yake ni kua mapato ya utalii tumeyakosa na hata mwaka wa 2020/2021 ni vigumu kuyapata kwa sababu nchi karibu zote Duniani zimeathirika na chumi nyingi Duniani zitaporomoka. Kama kutakua na watalii ni wachache sana.

Kwa miezi 9 ya mwaa huu wa fedha TRA wamekusanya 10.9 Trillion ila tegemea robo ya mwaka huu, yaani March-June makusanyo kua madogo sana kwa sababu hakuna biashara, wafanyabiashara wengi wanaomba kufunga na mambo yameharibika. Hivyo mwaka huu tu ni changamoto kubwa. Kitakachopatikana chote kitaishia kwenye matumizi.

Kutokana na uchumi kuvurugika serikali italazimika kukopa zaidi na hiyo mikopo haitakua ya maendeleo, itakua ya matumizi kwa sababu hata makusanyo ya matumizi itakua ni changamoto. Serikali italazimika kuachana na miradi yake mikubwa ili kugharimia matumizi ya kawaida na ya lazima.

Kws mtazamo wangu, serikali italazimika kukopa ma moja ya masharti ili ipewe mkopo ni kuachana na miradi kama SGR na Stieglers. Ikitokea hivyo ujue mradi ndio utakufa au utachukua mida mrefu kukamilika. Naona yunaelekea huko.

Binafsi naunga mkono miradi kama Stieglers na SGR ila naona kuna uwezekano mkubwa sana corona kutia mchanga kitumbua chetu na kuturudisha nyuma kama sio kutumaliza kabisa.

Itakapotokea tukaweka nchi kwenye lock down ndio itakua mwisho ya hiyo miradi na mbaya zaidi uchumi hautakuja kuka vizuri hivi karibuni. Madhara ya corona kiuchumi yanaweza kuja kukaa vizuri baada ya miaka kadhaa mbele.

Hata wahisani wetu wa maendeleo sina hakika kama watatoa hela maana wao ndio wameathirika zaidi. Njia pekee itakua ni mikopo na mikopo hiyo itakua ni eitha WB au IMF, tegemea masharti ya kuachana na miradi kama hii.

Tusubiri tuone itakuaje.

Screenshot_20200420-190533_Twitter.jpg
 
Hiyo miradi iliishaonekana White Elephants toka mwanzo na hii hali itakuwa imekuwa tu ni a blessing in disguise.

Huwezi ukaanzisha miradi ya nchi kwa mapenzi yako mwenyewe bila kuzingatia the economic viability zake ili tu kujitafutia cheap popularity.

Mdololo ujao unaweza kuwa another opportunity kwa wafadhili kuibada hii serikali iweze kuheshimu haki za binadamu na kuanzisha mchakato wa katiba mpya.
 
When one door is closed the other is opened.

Miradi itaendelea labda litokee lingine.

Historia inaonesha hakuna calamity ya endemic/pandemic iliyomaliza mwaka mmoja bila kutulia.

Umeandika kiushabiki kama vile unafurahi hiyo miradi isipokamilika.

Miradi itakamilika na utaendelea kuuguza majeraha ya moyo huku upo ndani ya SGR.

Umeniaminisha wachawi wengi Tanzania.
 
When one door is closed the other is opened.

Miradi utaendelea labda litokee lingine.

Historia inaonesha hakina calamity ya endemic iliyomaliza mwaka mmoja bila kutulia.

Umeandika kiushabiki kama vile unafurahi hiyo miradi isipokamilika.

Miradi itakamilika na utaendelea kuuguza majeraha ya moyo huku upo ndani ya SGR.

Umeniaminisha wachawi wengi Tanzania.
Kweli, mkiamua kwa lazima itakamilika, kama kawaida yenu mtatoa huku mpeleke kule, na atakaeuliza sijui kiasi fulani kimepotelea wapi hana kazi!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
SGR na Umeme wa bonde la nyerere ni uwekezaji mkubwa kimkakati kwa maendeleo ya taifa! Hiyo miradi lazima ikamilike kwa gharama yoyote! Hii miradi piga ua lazima ikamilike hata kwa watumishi kupunguzwa au kulipwa nusu mishahara! Bado bandari hipo inapitisha mizigo kwa nchi zaidi ya 8 hela itapatikana!
 
Hiyo miradi iliishaonekana White Elephants toka mwanzo na hii hali itakuwa imekuwa tu ni a blessing in disguise.

Huwezi ukaanzisha miradi ya nchi kwa mapenzi yako mwenyewe bila kuzingatia the economic viability zake ili tu kujitafutia cheap popularity.

Mdodolo ujao unaweza kuwa another opportunity kwa wafadhili kuibada hii serikali iweze kuheshimu haki za binadamu na kuanzisha mchakato wa katiba mpya.
Nadhani wengi mmesahau kuhusu utakatifu na vigezo vya kuupata.

Kama havipo inabidi vilazimishwe.
 
Tusitafute excuses, tatazo la Tz ni kuwapa madaraka watu wasio na weledi wala huruma kwa wananchi.
We jiulize tumepoteza kiasi gani cha pesa sababu ya UPUMBAVU na UJINGA wa kurudia uchaguzi kisa watu wanaunga juhudi, TATIZO LA TANZANIA NI CCM hakuna kingine

Sent using Jamii Forums mobile app
CCM ipo mpaka Tanzania itowe watakatifu.
 
Unazingua endemic au pandemic
When one door is closed the other is opened.

Miradi itaendelea labda litokee lingine.

Historia inaonesha hakuna calamity ya endemic iliyomaliza mwaka mmoja bila kutulia.

Umeandika kiushabiki kama vile unafurahi hiyo miradi isipokamilika.

Miradi itakamilika na utaendelea kuuguza majeraha ya moyo huku upo ndani ya SGR.

Umeniaminisha wachawi wengi Tanzania.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Corona hapa inasingiziwa tu. Hata kusingekuwa na corona, hiyo miradi isingekamilika hata ndani ya miaka 20. Mtu kwa kutumia ubabe ame-dismantle business sector, atapata wapi mapato ya ku-finance hiyo miradi? Aishukuru corona maana imempa kisingizio.

Na si ajabu amewatuma nyie wapambe wake ili hiki kisingizio kianze kutangazwa kwa nguvu ili wadanganyika wadanganyike na kuamini hizo propaganda.
 
Hizi nchi zetu masikini ikitokea changamoto kidogo ni shida kubwa sana.

Kws mtazamo wangu, miradi kama SGR na Stieglers ujue mradi ndio utakufa au utachukua mida mrefu kukamilika.
Mkuu Gambino, tumeishajiandaa kwa yote, hili likitokea miradi hiyo kusimama kutokana na Corona, hiyo hali kisheria inaitwa force majeure, hivyo kitakacho fuata, ni kumuongezea muda wa kutosha rais Magufuli aendelee kusalia madarakani hadi akamilishe miradi mikubwa yote ndipo tumruhusu.

P
 
Back
Top Bottom