Kuna walionufaika kwa kukodisha nyumba zao kwa Bongo Movie Industry kwa kurekodi filamu?

Sky Eclat

JF-Expert Member
Joined
Oct 17, 2012
Posts
57,761
Reaction score
216,011
Ukodishaji wa nyumba kwa filamu una faida kubwa katika nchi ambazo sanaa ya filamu imesimama vizuri. Afrika ya Kusini, Ghana na Nigeria wenye nyumba huwa wana faidika katika biashara hii.

Uzuri wa biashara hii, nyumba hutegemea na hadithi au simulizi la filamu, kuna wanaopenda nyumba za kifahari au hata mbavu za mbwa pia.

Miaka ya 2000, biashara hii ilishamiri na watu waliweza hata kulipa ada za watoto kutokana na kukodisha nyumba zao kwa filamu. Uzuri wa kukodisha huku ni kwa muda mfupi. Manaweza kukubaliana kwa wiki mbili au mwezi mmoja na ukarudishiwa nyumba yako na faida juu.
 
Unaongelea ada gani za watoto kama kipimo cha manufaa.! Sokapohapa.[emoji276]
 

Nihame Kwangu Kisa Bongo Movies Wanataka Wafanyie Sarakasi Zao. Hao Wenye Nyumba Nyingi Ndiyo Wanaweza


Nipo Kyerwa Huku Halafu Nitakaa KWa Nani? Kwa Ambassador Hana Vyumba
 
Duh bonge la bedroom,mbu hawezi kaa hapo.
 
Nadhani wauzaji wa hivo vitu amazing, wachora ramani, desgners, mafundi aina mbalimbali wanafaidi sana
 
Sijajua kwa upande wa movies gharama ni shingapi ila kwa video ya nyimbo gharama haizidi 50k
 
Sijajua kwa upande wa movies gharama ni shingapi ila kwa video ya nyimbo gharama haizidi 50k
Kule Nigeria wanaanza na milioni moja kwa siku kwa majumba yakifahari. Wengine mnakubakiana master bedroom inafungwa kuweka ile heshima tu kitanda cha ndoa.
 
Hii picha lengo lake ni kutufanya tu watu tujisikie wanyonge, hakuna lingine. Ungeweza tu kuandika uzi wako bila hiyo picha na ungeeleweka tu. Sawa bana..πŸ˜’
 
Mtoto anayetungishwa mimba kwenye kitanda hiki lazima awe na akili.
 
Hii picha lengo lake ni kutufanya tu watu tujisikie wanyonge, hakuna lingine. Ungeweza tu kuandika uzi wako bila hiyo picha na ungeeleweka tu. Sawa bana..πŸ˜’
πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚ Sisi tunaoishi kwenye chumba chenye jiko kitanda na sebule hapo hapo.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…