Kuna watu Duniani ni zaidi ya Gaidi wa kawaida pale unapoishi nao, sitosahau hii

Kuna watu Duniani ni zaidi ya Gaidi wa kawaida pale unapoishi nao, sitosahau hii

The Eric

JF-Expert Member
Joined
Feb 23, 2019
Posts
6,446
Reaction score
10,976
Wakuu habari za wakati na poleni kwa majukumu kwa ujumla.

Nina stori naleta kwenu na hichi ni Kisa cha kweli kuwahi kunitokea mimi katika maisha yangu, basi niaze nakusema maisha yana mengi sana wakuu.

Miaka ile ya 2000's nikiwa bado shule nilifika mahali nikawa nimekwama mahitaji ya kujikimu kama daftari, kalamu, kujinunulia msosi kutokana na niliishi na babu tu maana wazazi walishatangulia mbele ya haki na babu hakuwa na uelewa wakunikazania nikaona bora nijichanganye kitaa na kushindwa kuendelea na shule hivyo kuna hali ilinipelekea nikawa na makuzi ya kitaa kama mtoto wa mtaani (hawa wanao itwa chokoraa) miaka hii nilikuwa Arusha japo mimi ni mzaliwa wa mkoa wa Kilimanjaro na shule nilianzia moshi.

Kwanza kabla sijaenda Arusha kuna mwalimu wangu wa shule alinipa mchongo wa kazi huko kenya hapo la saba nilishamaliza ndio niko form one sasa, Mwl. fulani alitokea kunikubali akaona dogo anajipambania afu anafight japo shule kiukweli ilikuwa haipandi kiivo kutokana na mawazo mengi, kula yangu tu ni mpaka nioshe magari siku nyingine lazima niwe mtoro siku 3 au week nifanye vikazi vya saidia fundi na vikazi vya hapa na pale ili niishi.

Ticha alinipa mchongo pale shule ilipofungwa kipindi cha mwezi wa sita ilikuwa na akanielekeza namna nitavyo pokelewa huko Kenya na mwenyeji wangu.

Kuvuka KENYA nilivushwa pori na Rasi mmoja niliyemfahamu kwa sasa ni marehemu aliitwa Rasta P. Apumzike kwa amani Rasi ni broh alikuwa piece kitaani pale, alikuwa kaenda hewani na mbavu anazo alikuwa na piki piki baja XR lile la machalii wa chuga, maana alikuwaga ni apolo yaani wale wachimba ulanga kule mererani wanaotafuta madini ya Tanzanite. so aliwahi kaa mererani sana miaka kadhaa way back to 2000's nakuotea Tanzanite kiaina.

To make story short Tulifanikiwa kuvuka pori na kufika kenya pale mitaa ya chumvini pale yaani ukivuka tu boda ya Tanzania nikakabidhiwa kwa jamaa mmoja pale ni mtanzania ila yupo Kenya.

Kisha Rasi akarudi zake Tanzania.

baada ya maongezi kadhaa tulifikia nyumbani kwa huyo jamaa alikuwa naye ni mchagga tu kama sisi maana rasi naye alikuwa mchagga so tulibonga kinyumbani fresh na jamaa alitoa maelekezo ya kazi pale.

Nitakuja kuendelea kuwajuza zaidi wakuu hii bado stori mbichi kabisa ni kisehemu cha kwanza.

Sehemu ya kwanza.....01. itaendelea
 
Naweka kambi hapa, Usituache njia panda kama yule jamaa wa Safari ya Kitchanga....
 
Wakuu habari za wakati na poleni kwa majukumu kwa ujumla.

nina stori naleta kwenu na hichi ni Kisa cha kweli kuwahi kunitokea mimi katika maisha yangu, basi niaze nakusema maisha yana mengi sana wakuu...
Aisee

Itakuwa na sehemu ngapi hii series?
 
Sahv ikija story nikusoma kwanza chini sitaki alosto.
 
Inaendelea sehemu ya .........01.

Baada ya yule Rasta P kuondoka na kutuacha mimi na mwenyeji, alinipa maelekezo ya mimi kulala kwenye nyumba fulani ni karibu na kwake hapo hapo pale naweza sema ni servant quarter ina two bedroom......

Ticha wangu aliyenipaga mchongo wa kazi niseme kweli aliwahi nipaga vikazi vyake vya shambani na kuniagiza hapa na pale hivyo kuondoka kwangu hakakubali moja kwa moja ila alikuja baadae kukubali kishingo upande kwani alihisi kunikosa kwenye vikazi vyake.

Basi ilipotimia saa 12:00pm jioni siku ya jumamosi ndiyo siku niliyoweza kufika pale Chumvini Kenya nakuambiwa kijana karibu Kenya, kazi yako itakuwa ni uangalizi wa shambani na sisi tuna mashamba ya nyanya, Boss au mwenyeji wangu alisema hivo huku akiwa amechangamka na bia mbili tatu wakati huu alikuwa na glass anakunywa guiness huku kwa mbali anamoka cigarettes.....nami nikajibu kwa kilugha asante na tupo pamoja.....

Aliendelea kunieleza kesho kutwa tutaanza kazi nanitakupa muongozo pamoja na vijana wenzako, wakati anasema hivo ghafla walitokea watu na kugonga geti kisha kufunguliwa na aliye kuwa dada wa kazi anayeitwa Recho (nilimsikia boss akiita Recho) walijitokeza vijana wawili pale home na boss kwa haraka haraka kabla ya kuwasalimu aliita kwa nguvu Mark huyu ni kijana mwenzenu mtakaa naye kazini huyu chali kuanzia Jumatatu, sawa Obed, huyo Obed ni kijana mwingine.....
Boss alifahamika kwa jina la Kipara almaarufu yake mtaani....

Basi bhna ikawa usiku nikapata sapa chakula kilicho andaliwa pale nyumbani kwa boss na mpishi Recho, ilipotimia majira ya saa nne usiku nilienda kulala kwenye nyumba ya servant kisha pakakucha jumapili na ile siku kufupisha stori hakukuwa na pilika pilika au heka heka palipoa sana huku nikiona masaa hayaendi .

Vile vile Boss kipara alinieleza yupo kaka yake anaitwa Frank anaishi hapo nyumbani ila kwa siku ile alikuwa Tanzania.

Baadae nitaendelea wakuu......itaendelea
 
Back
Top Bottom