Kuna watu wanakera, basi tu! Ungekuwa wewe ungefanyaje?

Kuna watu wanakera, basi tu! Ungekuwa wewe ungefanyaje?

Lanlady

JF-Expert Member
Joined
Feb 27, 2019
Posts
1,836
Reaction score
6,303
Natumaini mu wazima. Binafsi namshukuru Mungu sijambo.

Japo Kuna baadhi ya watu wachache wanaweza kukuharibia siku kwa matendo au hata maneno yao.
Wanakera sana. Utakuta mtu anakulazimisha kukusalimia kwa kukushika mkono wakati amekotoka magali pa 'faragha' ama alikuwa akishika sehemu fulani fulani hivi za mwili wake na hajanawa popote!

Mwingine anakukuta mahali umekaa kwa kutulia anakupulizia hewa ya mdomoni mwake! Sipendi!

Au analazimisha kukukumbatia, ukikataa anakuvuta kwa nguvu.

Kwenye upande wa maneno kuna wale wanaopenda kukuuliza mipango yako kila mara au kama hujaoa/kuolewa basi kila siku lazima wakuzungumzie wewe! Wanatumia muda mwingi kutathimini maisha yako badala ya kutathmini ya kwao! Wananiudhi!

Kumbuka: hao ni watu wazima na familia zao!
 
Mwingine anakukuta mahali umekaa kwa kutulia anakupulizia hewa ya mdomoni mwake! Sipendi

MKUU FAFANUA HAPA UNAPULIZIWAJE HEWA YA MDOMONI?

unamiaka mingapi?
Hii mbona iko wazi kabisa!
Namaanisha kukupumlia hewa yake ya mdomoni kwa kupuliza kuelekea aidha usoni au mgongoni kutegemea na mtu huyo aliposimama
 
Hii mbona iko wazi kabisa!
Namaanisha kukupumlia hewa yake ya mdomoni kwa kupuliza kuelekea aidha usoni au mgongoni kutegemea na mtu huyo aliposimama


😂😂😂😂😂 Mkuu kusema kweli pamoja na ufafanuzi bado sijaelewa. yani mtu anakupuliza tuu kwani wewe ni moshi. au huwa unakuta unavumbi?
 
Natumaini mu wazima. Binafsi namshukuru Mungu sijambo.

Japo Kuna baadhi ya watu wachache wanaweza kukuharibia siku kwa matendo au hata maneno yao.
Wanakera sana. Utakuta mtu anakulazimisha kukusalimia kwa kukushika mkono wakati amekotoka magali pa 'faragha' ama alikuwa akishika sehemu fulani fulani hivi za mwili wake na hajanawa popote!

Mwingine anakukuta mahali umekaa kwa kutulia anakupulizia hewa ya mdomoni mwake! Sipendi!

Au analazimisha kukukumbatia, ukikataa anakuvuta kwa nguvu.

Kwenye upande wa maneno kuna wale wanaopenda kukuuliza mipango yako kila mara au kama hujaoa/kuolewa basi kila siku lazima wakuzungumzie wewe! Wanatumia muda mwingi kutathimini maisha yako badala ya kutathmini ya kwao! Wananiudhi!

Kumbuka: hao ni watu wazima na familia zao!
Kama ulikuwa huujui "muhali" ndio huo basi.
Hapo unatakiwa uongee ili uhukumiwe...
 
Dada ukiona hivyo......ujue washakuona uko muda wa nyongeza........unakaribia matuta kipenga kiite
Japo sijaelewa
ila ukweli ni kwamba sipendi hizo tabia tangu nikiwa shule ya msingi. Na hata nilosoma nao chuo wanajua hilo. Hawa ninafanya nao kazi kuna baadhi wana tabia hizo.

Kwani lazima kushikana mikono wakati wa kusalimiana? Au ni lazima kila mnayefahamiana au unayefanya naye kazi akuzoee??
 
Kwanini usikatae? Ukiandika hapa unadhani ndo wataacha?
Katiba ya Tanzania imempa uhuru wa kutowa maoni yake.

Nimemuelewa sana mleta mada na namuunga mkono 100%. Asikatae nini, na ndiyo anakataa hivi?

Zuwia ujinga kwa mikono yako, ukiwa huwezi, zuwia kwa mdomo wako, ikiwa huwezi, zuwia kwa kuuchukia kwenye nafsi yako.
 
Back
Top Bottom