Kuna watu wanakula utadhani wanahamisha upande wa pili.

Kuna watu wanakula utadhani wanahamisha upande wa pili.

Gatabhanya

JF-Expert Member
Joined
Nov 16, 2024
Posts
2,644
Reaction score
5,178
Habari.
Juzi nilikuwa kwenye harusi ya ndugu. Wakati wa kupata chakula kuna jamaa alikuwa anakula hatarii alikula sahani saba hadi kamati ya chakula wakakataa kumpa chakula kingine alikuwa bado anadai. Nini kinasababisha mtu kula sana wataalam??
 
Inasababishwa na nini kitaalam?

Kisaikolojia
•Msongo wa Mawazo au Hisia Mbaya: Watu wengi hutumia chakula kama njia ya kukabiliana na hisia kama huzuni, wasiwasi, au upweke.

•Tabia za Kulewa Chakula: Chakula chenye sukari nyingi, mafuta, au chumvi kinaweza kuchochea mfumo wa ubongo unaohusiana na raha, na kusababisha hamu ya kula kupita kiasi.

•Kukosa Udhibiti wa Kibinafsi: Baadhi ya watu hupata changamoto kudhibiti matamanio yao ya chakula, hasa mbele ya vyakula wanavyovipenda sana.


Kimazingira
•Upatikanaji wa Chakula Kingi: Katika mazingira ambapo chakula kinapatikana kwa urahisi na kwa wingi, watu huwa na uwezekano mkubwa wa kula kupita kiasi.

•Utamaduni wa Kula Kupita Kiasi: Katika baadhi ya jamii, kula kwa wingi huonekana kama ishara ya ustawi au furaha, na hilo linaweza kuchochea uroho.

•Matangazo na Ushawishi wa Kibiashara: Biashara nyingi za vyakula hutengeneza hali ya kishawishi kwa kutumia matangazo yanayolenga hisia, ambayo yanaweza kuwafanya watu washindwe kujizuia.


Kiafya
•Hitilafu za Homoni: Homoni kama leptin (inayodhibiti shibe) na ghrelin (inayodhibiti njaa) zikiwa hazifanyi kazi vizuri, zinaweza kusababisha mtu kuwa na njaa mara kwa mara na kula kupita kiasi.

•Magonjwa ya Kisaikolojia: Baadhi ya magonjwa kama vile binge eating disorder (BED) husababisha mtu kula kwa wingi bila kujizuia.

•Mfiduo wa Kemikali Fulani: Baadhi ya vyakula vya viwandani vina kemikali zinazoongeza hamu ya kula hata mtu akiwa tayari ameshiba
 
sahani 7 itategemea zina ujazo gani sio mnapimia watu ujazo wa kikombe kimoja cha chai na wakisema hawajashiba mnawaona walafi.! na hii inachangiwa na tabia ya wenye sherehe kuwachangisha watu pesa ndefu utasikia single 50,000 alafu akifika kwenye hiyo sherehe mnataka alambelambe tu sio kushiba wakati 50 yake inamuuma lazima afukie kisawa sawa
 
sahani 7 itategemea zina ujazo gani sio mnapimia watu ujazo wa kikombe kimoja cha chai na wakisema hawajashiba mnawaona walafi.! na hii inachangiwa na tabia ya wenye sherehe kuwachangisha watu pesa ndefu utasikia single 50,000 alafu akifika kwenye hiyo sherehe mnataka alambelambe tu sio kushiba wakati 50 yake inamuuma lazima afukie kisawa sawa
Ilikuwa kilo kwa watu wa nne
 
Habari.
Juzi nilikuwa kwenye harusi ya ndugu. Wakati wa kupata chakula kuna jamaa alikuwa anakula hatarii alikula sahani saba hadi kamati ya chakula wakakataa kumpa chakula kingine alikuwa bado anadai. Nini kinasababisha mtu kula sana wataalam??
Ulienda kwenye sherehe kuhesabia watu wanakula sahani ngapi?
 
sahani 7 itategemea zina ujazo gani sio mnapimia watu ujazo wa kikombe kimoja cha chai na wakisema hawajashiba mnawaona walafi.! na hii inachangiwa na tabia ya wenye sherehe kuwachangisha watu pesa ndefu utasikia single 50,000 alafu akifika kwenye hiyo sherehe mnataka alambelambe tu sio kushiba wakati 50 yake inamuuma lazima afukie kisawa sawa
kuna harusi nilichangia 70 kabisa ikifika kwenye msosi tuliokuwa nyuma tutakosa tukaishia kula vitunguu na soda aisee njaa iliniuma hiyo siku
 
Back
Top Bottom