Tulikuwa naye 'power Mwamgiga', anakula ndoo ya wali ya lt10, galoni la maziwa, mkungu wa ndizi na creti la soda ndiyo anashiba.
Soda anafungulia ukucha.
Akitaka kubeba maji, ni pipa mbili zinajazwa halafu mzega wa kubebea ni mwamba wa nguzo za simu za Ttcl, mwanaume anaondoka nazo.
Gari mbili anazizuia kwa mkono mkavu.
Chai yake ni chai ya maziwa birika zima na mkate unakatwa kati kati kwa mkono unafinywa na kusokomezwa mdomoni, hataki silesi!
Mgekutana na mtu wa hivyo, mgelimwandika kwa kulalamika na kujaza server.