Kuna watu wanalia wengine kufurahi lakini ujue Mungu ndie mpangaji wa yote haya

Kuna watu wanalia wengine kufurahi lakini ujue Mungu ndie mpangaji wa yote haya

Mmmmmh. Kwanza , simjui sasa naanzaje kuamini hivyo kuwa kaniumba!?

Pia, najua uumbaji ni Baba na Mama ndiyo waumbaji.

Mfano, kwa nini baadhi ya watu wakose uzazi kama Mungu anaumba!?
Utamjua tu hata mwaka haupiti

Unajua binadamu wa kwanza duniani alitokea wapi?
 
Bila dini hizo sheria za Mungu ungezipata wapi? Mungu unayemjua wewe ndo huyo uliyefundishwa kanisani.
Mtoa mada unajichanganya, hueleweki hata chembe.
Dini haijaleta sheria za Mungu
Sheria za Mungu zipo tangu Mungu alipomwumba binadamu wa kwanza so ukisema bila dini ningezijua wapi hata zisingekuepo ningezijua tu cha msingi ni nia yako uliyonayo
 
Kila kitu huwa kina majira yake, kila jambo duniani lina wakati wake :

Kuna wakati wa kuzaliwa na wakati wa kufa,
Wakati wa kupanda na wakati wa kuvuna kilichopandwa,

Wakati wa kuua na wakati wa kuponya

Wakati wa kubomoa na wakati wa kujenga

Wakati wa kulia na wakati wa kucheka

Wakati wa kuomboleza na wakati wa kucheza

Wakati wa kutupa mawe na wakati wa kuyakusanya

Wakati wa kukumbatia na wakati wa kuacha kukumbatia

Wakati wa kutafuta na wakati wa kupoteza

Wakati wa kuhifadhi na wakati wa kutupa

Wakati wa kurarua na wakati wa kushona

Wakati wa kukaa kimya na wakati wa kuongea

Wakati wa kupenda na wakati wa kuchukia

Wakati wa vita na wakati wa amani

Usije ukafikiri kinachokutokea ni kwa bahati mbaya iwe furaha iwe huzuni yote ni mipango ya Mungu

Furaha yako inaweza kugeuka kuwa huzuni na huzuni yako kuwa furaha

Yote ni Mungu anakupangia

Muhimu ni kuendelea kuomba kwa alie juu juu kabisa

Hakuna anayepangia wanadamu desteny zao na maisha yao bali ni wanadamu wenyewe katika matendo yao na minds zao.

Idea ya kusema "Mungu ni mpangaji" haina logical explanation.
 
Hakuna anayepangia wanadamu desteny zao na maisha yao bali ni wanadamu wenyewe katika matendo yao na minds zao.

Idea ya kusema "Mungu ni mpangaji" haina logical explanation.
Na Mungu akubariki eti mtu anajipangia tu aandike jf kua Mungu ndio mpangaji wa yote anashindwa kutofautisha kati ya mweza wa yote na mpangaji wa yote
 
Na Mungu akubariki eti mtu anajipangia tu aandike jf kua Mungu ndio mpangaji wa yote anashindwa kutofautisha kati ya mweza wa yote na mpangaji wa yote
Unabisha wakati hujui nimenukuu wapi

Kubali kataa Mungu ndiye mpangaji wa kila jambo

Sasa sijui kuna tofauti gani kati ya Mungu ni muweza wa yote na Mungu ndie mpangaji wa yote
 
Hakuna anayepangia wanadamu desteny zao na maisha yao bali ni wanadamu wenyewe katika matendo yao na minds zao.

Idea ya kusema "Mungu ni mpangaji" haina logical explanation.
Hivi unajua kazi kubwa ya Mungu aliyompa binadamu baada ya kumuumba

Sishangai unavyobisha Mungu sio mpangaji wa kila jambo

Ukweli ni kuwa Mungu ndie kila kitu hakuna asichohusika nacho
 
Hivi unajua kazi kubwa ya Mungu aliyompa binadamu baada ya kumuumba

Sishangai unavyobisha Mungu sio mpangaji wa kila jambo

Ukweli ni kuwa Mungu ndie kila kitu hakuna asichohusika nacho
Ndugu icho ni kitabu cha kwako kielezacho hivyo bali Mungu ni mweza wa yote na ni muumba Mungu kaumba akili ila hakupangii cha kuwaza wala sio ndo anae tengeneza mabomu tuuwane bali ni mpango wa mwanadam hajapanga kutengeneza gest house au bar ili kumchukiza yeye
 
Yesu gani we unaempenda hata hujui Mungu ndie mpangaji wa kila kitu alichokiumba
Imani yangu kwake ni kua yeye ni mweza wa yooooote yaani anaweza kunilinda na kunibariki sio mpanga watu wanywe pombe sio ndie aliepanga watu wazini hapana wala sio mpangaji wa watu wawe mashoga wala sio mpaji wa watu kukaa uchi wala sio ndie aliepanga mmomonyoko wa maadili
 
Ndugu icho ni kitabu cha kwako kielezacho hivyo bali Mungu ni mweza wa yote na ni muumba Mungu kaumba akili ila hakupangii cha kuwaza wala sio ndo anae tengeneza mabomu tuuwane bali ni mpango wa mwanadam hajapanga kutengeneza gest house au bar ili kumchukiza yeye
Kweli Mungu anavyosema watu wangu wanakosa maarifa kwa kijifanya wajuaji hakukosea kabisa
 
Imani yangu kwake ni kua yeye ni mweza wa yooooote yaani anaweza kunilinda na kunibariki sio mpanga watu wanywe pombe sio ndie aliepanga watu wazini hapana wala sio mpangaji wa watu wawe mashoga wala sio mpaji wa watu kukaa uchi wala sio ndie aliepanga mmomonyoko wa maadili
Hakuna ambacho Mungu hajakiumba so kila kitu anakiamulia atakavyo
 
Back
Top Bottom