Kuna Watumishi wasiyo na sifa wanakaimu nafasi ya Wakuu wa Idara kwenye Halmashauri kwa muda mrefu wakati wenye sifa wapo

Kuna Watumishi wasiyo na sifa wanakaimu nafasi ya Wakuu wa Idara kwenye Halmashauri kwa muda mrefu wakati wenye sifa wapo

Ndiyo. Kinacho jaliwa hapo ni service delivery efficiency. Kama huduma za Idara zinaendelea kutolewa kwa ufanisi wa kiwango cha juu, huyo kaimu anatosha au vinginevyo wakiona inafaa wam-confirm au wamthibitishe awe mkuu wa Idara kamili.
Kutangaza kazi au nafasi wazi za Idara ni sawa lakini Mkurugenzi /TAMISEMI anayo kauli kubwa kutoa mapendekezo na maoni yake.
Kumbuka na zingatia kwamba hakuna chuo kinachosomesha Wakuu wa Idara.
Mkuu wa idara ni kiongozi tu au ni sawa tu na Monitor darasani.
Kuwa na Masters au Phd ni added advantage. Mkuu wa Idara, pamoja na Taaluma yake anapewa majukumu ya ziada tu e.g. kusimamia utendaji wa kila siku wa Watumishi/Watendaji walio ndani ya Idara husika na ndiye msemaji mkuu katika Idara hiyo. Anawajibika moja kwa moja kwa Mkurugenzi.
Sasa wapo wakuu wa Idara pamoja na Masters zao hawajui kujenga hoja mbele ya Vikao, hawajui kuandika na kutoa Taarifa sahihi ya kina, sio wabunifu ila kazi yao ni kukimbizana na madokezo/vocha kwa Mkurugenzi na hata wapo wengine ni wababaishaji tuu wanabeba mabegi yenye laptop tu lakini hakuna cha maana. Hao wanakuwa ni kero na wanaifedhehesha sana Idara/Halmashauri na Taasisi kwa ujumla.
Sasa mtu hana sifa watamthibitishaje? Jaman hebu tujenge hoja zenye akili basi, tukizingatia Sheria za nchi yetu
 
Acha kuwasagia kunguni wenzio.
Yeah. Kuna kitu Maslahi amekiona na amekuwa na matamanio nacho kwa siku nyingi. Hao ndo wakipewa Ukuu wa Idara ni hatari na nusu. Atapitia sketi zote Idarani kwake, kila vocha aipitishayo lazima iwe na 10%, atakumbatia mafungu yote ya miradi ya maendeleo, Hatotulia Ofisini kila siku yupo safarini(Semina, warsha, makongamano etc anageuka kuwa Vasco da Gama), anawafokea hovyo subordinates wake n.k.n.k.
 
Nawomba wadau msome uzi muuelewe vizuri ndo mchangie, si lazima uchangie Kama hujaelewa
 
Kuna wajanja huutumia kama mwanya was kupiga madeal na wahusika waliowekwa!!

Nilikuta certificate mmoja ni mwalim mkuu sehem,kumbe anagawana pasu kwa pasu Ile posho na DEO pale halmashauri ,yule DEO alipohamishwa tu Wakateuliwa makundi ya wakuu was shule wapya ili kuwaindoa wale vivuli!!
 
Una hoja ila Qualification ya wasailiwa pamoja na kuwa na Master pia awe na uzoefu kwenye idara hiyo sio chini ya Senior level au 10 years.
Usipofanya hivyo vijana wa Dotcom Hawa miaka 26/27 Wana masters ila hawana uzoefu. Watapasua usaili halafu akifika kule site anakutana na wazoefu miaka 15+ kazini wanaanza kumfundisha kazi. Heshima itapungua
 
Sasa mtu hana sifa watamthibitishaje? Jaman hebu tujenge hoja zenye akili basi, tukizingatia Sheria za nchi yetu
Ndo mana anaishia kwenye Kukaimu tu. Hiyo Nafasi itajazwa na TAMISEMI. TAMISEMI wanaweza kumhamishia mteule wao hapo au kumpromote mwenye sifa aliyeko hapo Halmashauri lakini atabadilishwa kituo cha kazi.
 
Kuna wajanja huutumia kama mwanya was kupiga madeal na wahusika waliowekwa!!

Nilikuta certificate mmoja ni mwalim mkuu sehem,kumbe anagawana pasu kwa pasu Ile posho na DEO pale halmashauri ,yule DEO alipohamishwa tu Wakateuliwa makundi ya wakuu was shule wapya ili kuwaindoa wale vivuli!!
Hahaaaa ni noma
 
Una hoja ila Qualification ya wasailiwa pamoja na kuwa na Master pia awe na uzoefu kwenye idara hiyo sio chini ya Senior level au 10 years.
Usipofanya hivyo vijana wa Dotcom Hawa miaka 26/27 Wana masters ila hawana uzoefu. Watapasua usaili halafu akifika kule site anakutana na wazoefu miaka 15+ kazini wanaanza kumfundisha kazi. Heshima itapungua
Exactly
 
Hadi Kaimu unamsagia kunguni kitu anachofaidi 40k ya Vikao
Sidhani kuwa ni hivyo bali naamini mdau anahoja asikilizwe. Kama hali iko hivyo kweli manake waliochini ya huyo kaimu akiwepo yy mwenyewe wanaona mambo hayaendi na huyo kaimu ana inferiority complex kiasi cha kuwaburuza wale anaowaongoza. Pengine dhana ya ushirikishwaji imemshinda huyo kaimu ila Mkurugenzi ameamua kumpotezea na kuacha mvurugano uendelee ndani ya Idara. Hiyo ni kero.
 
Yeah. Kuna kitu Maslahi amekiona na amekuwa na matamanio nacho kwa siku nyingi. Hao ndo wakipewa Ukuu wa Idara ni hatari na nusu. Atapitia sketi zote Idarani kwake, kila vocha aipitishayo lazima iwe na 10%, atakumbatia mafungu yote ya miradi ya maendeleo, Hatotulia Ofisini kila siku yupo safarini(Semina, warsha, makongamano etc anageuka kuwa Vasco da Gama), anawafokea hovyo subordinates wake n.k.n.k.
Tatizo lako hujaelewa hoja, pole sana
 
Sidhani kuwa ni hivyo bali naamini mdau anahoja asikilizwe. Kama hali iko hivyo kweli manake waliochini ya huyo kaimu akiwepo yy mwenyewe wanaona mambo hayaendi na huyo kaimu ana inferiority complex kiasi cha kuwaburuza wale anaowaongoza. Pengine dhana ya ushirikishwaji imemshinda huyo kaimu ila Mkurugenzi ameamua kumpotezea na kuacha mvurugano uendelee ndani ya Idara. Hiyo ni kero.
Kwanini hamuwezi mkausoma uzi na mkauelewa au jinzi umri unapozidi kwenda na akili zinayumba?
 
Hili siyo jungu ni uhalisia kabisa, huko kwenye Halmashauri zetu ili uwe mkuu wa idara shart moja wapo inatakiwa uwe na Master degree,

Sasa imetokea kuna halmashauri watu wasio na sifa wanakaimu kwa muda mrefu wakati wenye sifa za kushika hizo nafasi wapo labda wangeweza kupatikana kupitia ajira portal au taratibu zingine za uteuzi.

Tunaiomba serikali yetu kuliona hili swala kimapana zaidi ili kuongeza uwajibikaji kwa hawa Watumishi wetu.

Mungu ibariki Tanzania Mungu mubariki Rais wetu 🇹🇿
Upatikanaji wa hizo nafasi, mchoro wake ni 20 millions. Kupitia wizara ya Mkaza Mwana.
 
Hili siyo jungu ni uhalisia kabisa, huko kwenye Halmashauri zetu ili uwe mkuu wa idara shart moja wapo inatakiwa uwe na Master degree,

Sasa imetokea kuna halmashauri watu wasio na sifa wanakaimu kwa muda mrefu wakati wenye sifa za kushika hizo nafasi wapo labda wangeweza kupatikana kupitia ajira portal au taratibu zingine za uteuzi.

Tunaiomba serikali yetu kuliona hili swala kimapana zaidi ili kuongeza uwajibikaji kwa hawa Watumishi wetu.

Mungu ibariki Tanzania Mungu mubariki Rais wetu [emoji1241]
Yawezekana hao wasio na sifa wanasoma ili kufikia hizo masters hapo sawa lakini kama hawasomi na wameweka ndeke hapo kwa muda mrefu njoo inbox taja jina la huyo mtu mm namuanika hapa kama unaogopa kuanika.
 
Back
Top Bottom