Kuna wengine hatujui tulipokosea

Kuna wengine hatujui tulipokosea

Ep 21

Siku zilienda Dav hakuamini kama ningesema basi. Nilirudisha pete kwa mhuisika Dav hakuamini kama ningemwacha nilimwambia kuwa siku ukiona umebadilika na unaweza kuniheshimu japo kidogo na kutulia utanitafuta ila sio kwa sasa Dav nahitaji kupumzisha akili yangu sasa. Nikikaa sawa nitakwambia ila sidhani kama naweza kukusamehe. Hivi hatujaoana Dav huko hivi ukiniweka ndani ukajua tayari nipo chini ya himaya yako itakuwaje. Kinachoniuma mwanamke yuleyule toka umepanga mpaka umejenga kwako bado tunakosana kwa sababu yake. Kitanda kilekile ninachokilalaiaga mimi bora mgeenda sehemu nyingine si hapa. Au ningewakuta sehemu nyingine sio hapa kwako ningekusamehe kabisa. Au angekuwa mwanamke mwingine siku ile si ulikana ukasema ulikuwa unampa hela ili akupikie na hapa alikuja kukupikia tena sababu unampa hela? Dav alilia sana, alinipigia magoti lakini sikujali kilio chake wala magoti yake niliondoka zangu nikawaacha kwenye kikao na nikaazimia kumuondoa Dav kabisa Dav kweye Maisha yangu na nilifanikiwa kumuondoa mazima.

Mahusiano yangu na Dav yalidumu kwa miaka mitatu na miezi minne na kipindi chote hicho japo ilikuwa long distance relationship sikuwahi kumsaliti wala kuwaza kufanya hivyo mpaka tunaachana. Nikawa bize na Maisha yangu japo ilikuwa ngumu lakini mwisho wa siku niliamua kukubali matokeo.

Maisha yana pilika pilika nyingi sana. Kwenye heka heka za hapa na pale nikakutana na kijana mwingine mtanashati ni daktari katika hospitali kubwa hapa dar alinisumbua kwa kipindi cha mwaka na zaidi. Nilishamtoa Dav kwenye akili yangu nikaamua kuwa naye ila kumbe yule jamaa alikuwa ameoa na ana Watoto watatu familia yake inaishi mkoani lindi.

Nilivyogundua tu sikutaka kuangalia nyuma wala sina cha kupoteza kwake nikakimbia futi mia. Hakuna mtu namwogopa kama mume wa mtu. Maisha yalisonga nilikaa single miaka miwili yaani mtu akiniambia habari za mapenzi simwelewi kabisa hata kidogo. Nikaamua kujikita kwenye kazi zangu.

Nikaja nikakutana na huyu mpendwa namaanisha mlokele ni mtu maarufu kidogo nikaanza nae mahusiano nikiamini huyu ni mtumishi wa Mungu hawezi kunitenda. Msinilaaumu jamani Lisa nakula nashiba kuna siku tulijikuta tumevunja amri ya sita hata sielewi ilikuwaje. Mungu naye hakuwa mbali jamani mimba hiyo. Nikalea mimba yangu mpendwa yule naye kumbe ni silent killer ana matukio yake pia. nikaamua sasa kuwa bize na mimba yangu.

Namshukuru sana Mungu alinijalia handsome boy mwanangu ana miaka miwili sasa ananipa kila sababu ya kupambana. Sasa hivi nina amani na katoto kangu nikiwa single mother.

Kuhusu nyumba ya antie aliyokuwa anajenga niliimalizia na document zake ninazo mimi siku yoyote akitokea nipo tayari kumpa pasipo kudai chochote kile.

Dav alikuja kuoa mwanamke mwingine lakini walishindwana. Walikatana mpaka mapanga wakapelekana mpaka mahakamani. Dav siku hizi ni chapombe ana midevu kama osama yaani usmat ule hana tena nilikutana mwaka juzi nilivyooenda kumsalimia baba tulikutana mjini bahati mbaya nikiwa na kichanga aliumia sana. Kuna siku huwa anamfuata baba yangu na kuanza kumsumbua baba kuwa mimi nimke wake anamtaka mke wake nilimwambia baba ampeleke polisi. Ila baba hataki anampenda Dav ila mimi nilishakula viapo na viapo siwezi kurudi tena kwa Dav. Simchukii nilishamsamehe kabisa ila pia simpendi namchukulia kama mtu wa kawaida tu.

Mama naye yupo south Africa kuna kipindi aliumwa sana alipata ajali akateguka mguu akawa anahitaji msaada wetu ndugu zake wakatwambia kuwa twende kumuuguza tukagoma sio mimi sio Joy alikubali kwenda south Africa kumuuguza ilibidi aende mdogo wake. Alivyopona tu alikuja Tanzania akatuomba msamaha, tulimsamehe hivyo alirudi south kuendelea na Maisha yake ila tuko poa kabisa. Joy naye anaendelea vizuri mwezi wa 7 tunatarijia kula ubwabwa mdogo wangu antarajia kufunga ndoa. Hatuna ukaribu wa kivile ila tunawasiliana japo kidogo kidogo.

Baba naye ndoa yake inapumulia gas walitengana chumba na mama yetu wa kambo na mdogo wetu ni mdangaji maarufu Morogoro mjini. Yaani ni ameshindikana. Kwa baba mimi na Joy tuliacha kwenda kabisa nina miaka mitatu toka nilivyoenda mwaka 2021 sijawahi kukanyaga tena. Nikimmisi baba yangu huwa najitahidi kwenda na mabus ya kufika mapema moro na mtoto wangu tunafikia ofisini kwa baba jioni tunaru zetu Dar naondoka juu kwa juu.

Katika hekaheka zote hizo nimefanikiwa kujenga kakibanda kangu kadogo kazuri japo si kivile lakini kanaridhisha kapo Mbezi Msumi. Nitaarajia kuhamia kabla ya pasaka mwaka huu. Nina amani furaha na afya njema mimi na mtoto wangu tuko poa kabisa.

Sijutii kuwa single mother sababu mtoto wangu ananipa kila namna ya kupambana na ndiye mtu pekee niliye naye katika Maisha yangu japokuwa ni mdogo lakini ananipa furaha. Nina amani na sasa hivi naufanyia kazi msemo wa Joy naishi ulimwengu wangu kabisa. Mwanangu ndiye dunia yangu.

Asanteni kwa kuwa na mimi, niliyemkosea au kumkwaza kwa namna moja ama nyingine naomba anisamehe. Na samahani kwa kuwachosha ila nina Imani kuna mtu japo mmoja amejifunza kitu kutokana na historia ya Maisha yangu.

NAWAPENDA!

Mwishooooo.
Ei nafikiri pole haikufai asee, unafaa hongera... Hongera sana.
Kuna Mdau alisema mara nyingi watu wanaonapitia kashkash nzito hua na kitu cha kipekee ndani. Nafikiri wewe ni miongoni. Wishing you Great Future.
 
Wakuu huo uzi ulioandikwa na patrickk naupataje? Mtu anipe link tafadhali
 
Dav ananitamani leo kesho. mimi nimepita matatizo mengi hvyo hata wazo la kuolewa sina kabisa akilini mwangu.
Pole sana dada kwa uliyopitia, maisha ni 10% ya Yale tunapitia na 99% ya vile tunaamua kurespond Yale tuliyopitia, sis tumesoma story tumeumia lakin wew uli experience hayo yote Tena ukiwa peke Yako. Hatuna nafasi sana ya kuweza kukushaur nin Cha kufanya sababu mwitikio wako kwa Yale uliyopitia yalikua ndyo yamekuweka hai na Hadi Sasa umekua na confidence ya kuweza kutusimulia.

Pamoja na kua hatuna nafasi kubwa ya kushauri lakin kwa Ile nafasi ndg tuliyonayo mim nami naunga mkono wa kuangalia kua na mahusiano Tena, naweza mpendekeza Dav lakin kama ukipinga basi mwingine yeyote ambae moyo wako utaridhia, hii ni kwa afya ya akili Yako na itapendeza mkiwa rasmi mbele za Mungu Ili iwe ni sehemu ya ibada pia🙏
 
  • Thanks
Reactions: rr4
Epi 3

Mwaka umepinduka bibi mzaa mama na babu na bibi wanapambana kuhakikisha naendelea na masomo wananitafutia chuo wanakuta nafasi zimeisha naambiwa kuwa tusubiri mpaka mwakani.

Si baba wala mama anayetoa ushirikiano wao wako bize na Maisha yao wanaoangaika ni babu na bibi tu pande zote mbili.

Wakati chuo ambacho walikuwa wameki- target wamesema tusubiri hivyo nikawa nipo tu kijijini.

Sina hili wala lile nipo na bibi tunapiga stori anapokea simu na kunipa simu na kunambia Lisa simu yako. Napokea simu kumbe ni dada yangu mtoto wa baba yangu mkubwa anayeishi mjini ananiambia kuna kazi kwenye kampuni yao anakofanya kazi wakati naendelea kusubiri kwenda shule ningeenda kujishisha pale ili nisikae bila kazi. Basi dada yangu akanitumia nauli kesho yake asubuhi nikaenda mjini na keso yake naanza kazi pale kama kibarua. Tunalipwa sh 4,000 kwa siku ila wanalipa kila mwisho wa wiki nakakubali make kwa kipindi hicho ilikuwa kubwa kumbuka sina majukuma nakula bure nalala bure kwa dada yangu.

Nimezoea kazi sasa na haikuwa kazi ngumu Lisa nimenenepa ghafla kama nimelkula hamira nimependeza yaani Lisa, Lisa kweli nina rangi ya choklate si mfupi si mrefu, nina jicho la kusinzia, vidimpo vya uchokozi na kidoti changu kwenye paji la uso. Lisa si haba wanaume wanaanza kujipendekeza kuanzia kazini kwetu mpaka mtaani. Naletewa zawadi kila iitwapo leo kidogo mji umenchangamsha nimekuwa muongeja japo dada yangu ni mpole.

Dada ananipa somo.

Sikia mdogo wangu Lisa usije ukajiloga ukaanzisha mahusiano na wanaume wa pale kazini. Utafukuzwa kazi na ukifukuzwa kazi hupo tayari kurudi kijijini?

Dada Hapana sitaki kurudi kijijini nakuahidi sitakuwa na mahusiano yoyote pale kazini nataka nitafute hela niwe kama wewe dada yangu.

Dada yangu ni fundi cherehani akitoka kazini huwa anashona nguo hiyo ni kazi yake ya ziada. Sasa dada oda ni nyingi kutoka kazini kwetu na wateja wengi ni wanaume. Jumamosi na jumapili watu hawakatiki nyumbani kwa dada. Wanalete nguo awashonee lakini wengi wao ni kuniwinda Lisa. Maneno ya dada yanatembea kwenye akili yangu sitaki kuwa na mahusiano na wanaume wa kazini. Hivyo nikawa nawatolea nje.

Wengine wakawa wanazusha wenyewe kuwa wana mahusiano na mimi wakati sio kweli. Kumbe hata supervisor wetu alikuwa ananitaka ila hajaniambia tukiwa kazini ananiuliza kama natoka soda nikikubali tunanunuliwa staff nzima. Nikikataa watu hawanywi soda. Baadhi ya watu wakadhani natoka nae maneno mpaka yakamfikia dada yangu ambaye tulikuwa vitengo tofauti. Na kila kitengo walikuwa na ofisi yao. Kwa hiyo mimi na dada tulikuwa tunaachana getini tu.

Dada akaniuliza nikamwambia kuwa siwezi kuvunja ahadi yangu kwakohata siku moja.

Kuna dada mmoja kumbe anatoka na supervior staff mwenzangu mtu mzima kidogo, nikimwamkia haitikiii, kumbe kadaivet simu yangu ili ajue huwa tunaongea nini mimi na supervisor.

Weekend dada hayupo ananipigia kunipa maagizo ya nyumbani simu yangu haipo hewani anapokea Ana (aliyedaivet simu yangu) dada anagundua kuwa simu yangu imedaivetiwa. Jumatatu tunaenda kazini dada yangu aliikuwa anafanya kazi upande wa utawala Ana anaitwa na kupewa onyo kali na uongozi. Tukio hilo likanifanya niendelee kuwa maarufu pale kazini.

Kuna rafiki yangu huyu kipenzi tumwite Hawa si jina halisi tunafanya wote kazi na umri wetu hatujatofautiana sana tunaambiza visiri vyetu vya kitoto.

Kuna jamaa tumwite Omary si jina lake sasa huyu jamaa tumemkuta pale kazini ni handsome anajua kuvaa akipita ananukia ana bezi kama ya Jaiva nae alikuwa kati ya wale wanaoniwinda. Kimoyomoyo nikasema potelea mbali maneno ya dada nitamkubali Omary nampenda sana.

Nikaona nimshirikishe shoga yangu Hawa. Kumbe Hawa ni mjanja keshapiga hatua moja mbele zaidi yangu kumbuka yeye amekulia mjini mimi ni wakuja tu.

Natarudi. mimi ni mvivu sana kesho nitajitahidi kumalizia jamani
niliemkwaza anisamehe
Ok
 
Ei nafikiri pole haikufai asee, unafaa hongera... Hongera sana.
Kuna Mdau alisema mara nyingi watu wanaonapitia kashkash nzito hua na kitu cha kipekee ndani. Nafikiri wewe ni miongoni. Wishing you Great Future.
asante sasa na mimi naamini hivyo lazima kuna sababu ya mimi kuyapitia hayo.
 
Pole sana dada kwa uliyopitia, maisha ni 10% ya Yale tunapitia na 99% ya vile tunaamua kurespond Yale tuliyopitia, sis tumesoma story tumeumia lakin wew uli experience hayo yote Tena ukiwa peke Yako. Hatuna nafasi sana ya kuweza kukushaur nin Cha kufanya sababu mwitikio wako kwa Yale uliyopitia yalikua ndyo yamekuweka hai na Hadi Sasa umekua na confidence ya kuweza kutusimulia.

Pamoja na kua hatuna nafasi kubwa ya kushauri lakin kwa Ile nafasi ndg tuliyonayo mim nami naunga mkono wa kuangalia kua na mahusiano Tena, naweza mpendekeza Dav lakin kama ukipinga basi mwingine yeyote ambae moyo wako utaridhia, hii ni kwa afya ya akili Yako na itapendeza mkiwa rasmi mbele za Mungu Ili iwe ni sehemu ya ibada pia🙏
asante. nahitaji kutulia kwanza
 
nilikuwa napitia commet leo kuanzia page ya kwanza. walio upande wa Dav mnazidi kuwa wengi... basi niungeni na mimi mkono jmn. ujue wewe mimi ni mwanamke mwenzako wewe
Msimamo wangu ni uleule naomba nikuone na Dav mmalizie vizuri uzee wenu
 
Nimesoma kisa cha patrickk na bado nafuatilia wakati tukiendelea kumsubiria naomba nami nishare na nyinyi historia ya maisha yangu kwa ufupi. nia visa humu ni kujifunza, kushauriana na kutiana moyo. Karibu.

Kwa jina naitwa Lisa (sio jina halisi) natokea katika mmoja wa mikoa ya kanda ya ziwa.

Nilipoanza kujitambua kuwa mimi ni nani nilikuwa nikiishi kijijini kwa babu na bibi wazaa baba. Wazazi wangu hawakuwa pale walikuwa mjini. Jinsi navyoeendelea kukua ndo nagundua kuwa hawapo pamoja wametalikiana. Mama yupo na Maisha yake na baba pia yupo na mke mwingine na wana Watoto.

Niliendelea kukua nikapelekwa shule ya msingi huko kijijini. Nikaendelea na masomo yangu kama kawaida darasani nilikuwa na akili sana hali iliyonipelekea kuwa kipenzi cha walimu. Mpaka nafika darasa la nne nilikuwa sijawahi kuziona sura za wazazi wangu wala wadogo zangu ambao nawasikia kwa majina tu.

Nakumbuka nilikuwa nje tupo likizo tunajiaanda kuingia darasa la tano nilikuwa nje naosha vyombo mara wakaja watu wa baiskeli ndo tuseme walikuwa ndo bodaboda wa kipindi kile. Na mizigo mabegi ya kutosha na mmababa mmoja hivi nikamwamkia akaniangalia sana akaanza kulia sasa mimi nashangaa huyu mbaba analia nini sasa wakati naendelea na kazi yangu ya kuosha vyombo mara bibi akatokea akamkumbatia huku akitaja jina lake mwanangu umekuja nae akaanza kulia. Ndo nikagundua kuwa kumbe huyu ndo baba yangu.

Bibi akanigeukia Lisa mwamkie baba yako aisee nilisikia kitu kama kinanikaba nikatengeneza chuki kubwa kati yangu na baba yangu najiuliza siku zote hizi alikuwa wapi. Nikamjibu bibi nimeshamwamkia ilikuwa mchaba kama saa sita hivi. Basi bibi na baba wakaingia ndani na mizigo ikaingizwa ndani mimi hata sikuwashobokea nikaendelea na kazi zangu bibi akaniita nami niingie ndani nikamgomea. Nilikasirika sana. Muda wa chakula ukafika bibi akaanda chakula huku anaimba nyimbo kuonyesha alivyofurahi kumwona mwanae. Wakapakua chakula nikagoma kula na baba nikamwambia bibi siwezi kukaa sehemu moja na huyu mbaba wao wanalia mimi nina hasira tu.

Babu wakati huo hakuwepo alikuwa amesafiri kikazi ameenda mjini make alikuwa na wadhifa kidogo serikalini. Jioni babu anarudi make babu alikuwa ananidekeza sana nilivyomuuona tu nikamkibilia na kumkumbatia namwambia kuwa kuna mbaba yupo ndani yupo na bibi wanajiliza wanadai ni baba yangu. Babu nakumbuka alinituliza na vijizawadi vya mjini. Ndo nikakubali kuingia ndani.

Baba alikaa kijijini kama wiki mbili hivi na alikuja na zawadi kibao kwa ajili yangu. Na kila akitaka kwenda sehemu ananibembeleza tunaenda wote. Hali hiyo ilipelekea kuanza kidogo kidogo kumzoea na kuamini kuwa ni baba yangu. Wakati wa kurudi kwenye kutafuta nakumbuka nilimsindikiza na mpaka mjini nililia sana kuona anaondoka na kuniacha alimbembeleza sana akiahidi kurudi kunichukua. Nikamkubalia akaondoka huku mapenzi ya mtoto yakazaliwa mpaka leo nampenda sana baba yangu hunambii kitu kwake.

Maisha yakaendelea kama kawaida kwa babu, tulikuwa tunaishi Maisha mazuri tu ya kawaida ila sio magumu sababu babu yangu kidogo alikuwa anajiweza yaani kwa ufupi pale kijijini tulikuwa wakishua.

Upande wa mama kwao napo sio mbali na pale kijijini kwetu nikijiji cha Jirani tu hivyo nilikuwa nikienda mara kwa mara kuwasalimia babu na bibi pia japo pia mama yangu nilikuwa simfahamu.

Nilikuwa darasa la sita sasa ukatokea msiba upande wa mama, mama mkubwa dada yake na mama alifariki alikuwa akiishi Dar es Salaam lakini nilikuwa namfahamu make akija Kijiji ilikuwa lazima aje nyumbani kwa babu mzaa mama kunisalimia na kuniletea zawadi za hapa na pale. Huyu nilikuwa namchukulia kama mama yangu. Mama alikuwa anaweza kuja kwao kutoka Dar na asije kwetu kuniona nitasikia tu mama yako alikuja na kuondoka hivyo moyoni mwangu hata hakuwepo. Ndugu upande wa mama niliwaona ni bibi, babu, mamamkubwa (aliyekufa) na mjomba make hao ndo walikuwa wakinijali na kuja kuniona mara kwa mara hivyo upendo wa mama sijawahi kuupata mpaka leo.

Endelea kuwa na mimi nitarudi.

Naweka kambi hapa
 
Back
Top Bottom