Kuna wengine wana ifahamu hii theory?

1. Kufagia usiku mwiko

2. Kukata kucha usiku mwiko

3. Kuhesabu nyota mwiko

4. Kunyoa usiku hapana

5. Mwanaume kutumia kipekecho kupika ugali mwiko. Hata haipendezei.

na nyingine nyingi.
Na hizo ndizo sayansi kabambe zetu tulizo nazo sisi waafrika![emoji4][emoji4][emoji4]
 

asubuhi unasafisha mabaya na kukaribisha malaika
 
Faida ya hii theory ikoje
 
Ipo hiyo, kwetu hata kufagia usiku hairuhusiwi.

Kukata kucha usiku hairuhusiwi.

Ukiwa kwenye hedhi huendi kumwaga taka jalalani.
mna mambo mengi na je kununua chumvi dukani usiku
 
We ni msukuma, hiyo ipo sana usukumani!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kukatazwa kutoka nje usiku inatokana na maisha ya enzi hizo. Enzi hizo kulikua na wanyama pori wengi wanazurura zurura na kuzunguka zunguka kwenye miji ya watu kuanzia jioni saa 12 kunapokuchwa hadi kunapokucha mida ya saa 12 asubuhi. Wanyama hao ni pamoja na wanyama wakali kama simba, chui, fisi, mbwa mwitu na hata majoka.

Kwa vile wazee walikuwa wanatumia vitisho kutoa makatazo au walikuwa wakikopi jamii nyingine pasipo kujua chanzo cha makatazo, au kutotaka kuwaelezea vijana kwani wangekaidi na kupata madhara, ilibidi watumie sababu za kiimani kama kufukuza malaika, baraka na hata wageni.

Kwa zama hizi unaweza kufanya chochote hata kama ni kuomba moto au chumvi kwa jirani wakati wa usiku na hakuna dhara litalotokea.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…