Kuna wimbi kubwa sana la Ulimbukeni na ushamba kwa Watanzania hasa Mtu akijua kusoma na kuandika

Kuna wimbi kubwa sana la Ulimbukeni na ushamba kwa Watanzania hasa Mtu akijua kusoma na kuandika

bugzbunny

JF-Expert Member
Joined
Mar 9, 2013
Posts
839
Reaction score
755
Dunia nzima ukisikia jina Ukechukwu, Obina directly linakupeleka kwenye asili yake. Ukisikia Patel, Sanjay, unapata asili yake. Ukisikia Yamamoto, Sadaaki Numata unapata mwanga huyo asili yake wapi. Hali kadhalika kwa Tanzania ukisikia majina kama Kamugisha, Aika, Bhoke unapata picha asili yao.

Nisiandike mengi lakini kuna nguvu katika kuikubali asili yako. Kwanza inaonesha ni jinsi gani kama jamii husika mnajiamini. Pili inapeleka ujumbe kuwa mnauimara na asili yenu na historia yenu.

Sasa tuje kizazi cha sasa, kuna wimbi kubwa sana la 'Ulimbukeni' na ushamba (ndio hivo) miongoni mwetu Watanzania hasa mtu akijua kusoma na kuandika au akiongeza na ka elimu kengine kwa juu. Kidogo utaskia mwanangu anaitwa Jayden, Brighton, Luqman, Norman, Umulkheir, Lincoln, Gianna mara Jadon, haya majina nimeyataja maksudi kwasababu yalikuja juzi juzi tu na upepo wa karate kid 2.

Basi mtanganyika hapo akafanikiwa kumpeleka english medium alafu ukakakuta kwenye watu wengi alafu kakaongea vile vingereza yani watu wanakafanya kavutio cha utalii kabisa kisa kinge. Yani bongo bana. Yani wanaona big deal yani hapo ndio mafanikio yapo kileleni kwa akili za Watanzania. Akili za kitumwa.

Kuna usemi "mkataa kwao mtumwa". Huu usemi una maana kubwa sana. Ukiangalia majina niliyoyataja hapo mwanzo , mataifa yao na yakwetu tunaojidharau asili zetu maendeleo ni tofauti kabisa. Nigeria pamoja na kuwa ni Africa, bado wanafahamika na kuheshimika sana kuanzia kwenye michezo mpaka sayansi. Hali kadhalika Japan , India pia. Ila sisi ambao utakuta mtoto anaitwa Jaden John Emmanuel ndio tupo kama tulivyo.

Wito wangu, ifike mahali tuache ulimbukeni, tujikubali kwanza ndio dunia itatukubali. Nimeamua mimi watoto wangu wote nawapa majina ya kinyumbani yenye maana nzuri ambayo ata padri wakati wa kubatiza hatutasumbuana. Yani ninataka kutengeneza identity. Kataa utumwa wewe chausiku.
 
Umeandika kudhihirisha upumbavu wako. Maana hata ID yako sijaona jina la Kigwangallah au Chogomzinga. Unajiita Bugzbunny. Na unapotaja utumwa huo unaamini ni kwa majina ya kizungu tu. Ila Abdallah, Bin Laden, Al Mudhy, Hussein ni ya kiswahili. Sisi tulio huru hata kelele hatupigi na ndo maana kwa kulitambua hilo hata IDs zetu ni shahidi.
 
Hakuna ulimbukeni kutumia hayo majina ya kizungu, ni mtizamo wako tu,

Nikimuita mtoto Barack, au Baraka maana ni ile ile, tofauti ni kwamba jina moja lipo kiarab lingine kiswahili.

Wakristo na waislam huwapa majina watoto wao kwa heshima ya mitume na manabii waliopo kwenye dini zao

Majina Khadija, Amina, Hashim, Ali Mohamed, Lahman yana maana nzito sana kwa dini ya Kiislam,vile vile jina Immanuel(Yesu), Nehemiah, Saudi, Angel, hakuna ubaya, Wala si utumwa, zamani kwa wakristo ulikuwa huwezi kubatiza jina la lugha ya asili kama Marwa, Mwita, Mkude, Komba, baada ya kuelimika, leo kila kitu poa.

Ushamba, au ujinga ni zaidi ya jina, unaweza ukaitwa bhoke Mwita, Au lutengule Kambona, lakini ukawa Bado na fikra za kuamini wazungu Wana akili kuliko waafrika.

Mi Nina ndugu zangu, Wana majina ya kizungu, wamezaliwa Ulaya, lakini kutokana na malezi waliyopewa, wakifika bongo hapa wanapiga kichaga, kisukuma huwezi amini kama Hawa jamaa wamezaliwa na kukulia Ulaya.

Elimu na uelewa ni zaidi ya jina
 
Dunia nzima ukisikia jina Ukechukwu, Obina directly linakupeleka kwenye asili yake. Ukisikia Patel, Sanjay, unapata asili yake. Ukisikia Yamamoto, Sadaaki Numata unapata mwanga huyo asili yake wapi. Hali kadhalika kwa Tanzania ukisikia majina kama Kamugisha, Aika, Bhoke unapata picha asili yao.
Nisiandike mengi lakini kuna nguvu katika kuikubali asili yako. Kwanza inaonesha ni jinsi gani kama jamii husika mnajiamini. Pili inapeleka ujumbe kuwa mnauimara na asili yenu na historia yenu.
Sasa tuje kizazi cha sasa, kuna wimbi kubwa sana la 'Ulimbukeni' na ushamba (ndio hivo) miongoni mwetu Watanzania hasa mtu akijua kusoma na kuandika au akiongeza na ka elimu kengine kwa juu. Kidogo utaskia mwanangu anaitwa Jayden, Brighton, Luqman, Norman, Umulkheir, Lincoln, Gianna mara Jadon, haya majina nimeyataja maksudi kwasababu yalikuja juzi juzi tu na upepo wa karate kid 2. Basi mtanganyika hapo akafanikiwa kumpeleka english medium alafu ukakakuta kwenye watu wengi alafu kakaongea vile vingereza yani watu wanakafanya kavutio cha utalii kabisa kisa kinge. Yani bongo bana. Yani wanaona big deal yani hapo ndio mafanikio yapo kileleni kwa akili za Watanzania. Akili za kitumwa.
Kuna usemi "mkataa kwao mtumwa". Huu usemi una maana kubwa sana. Ukiangalia majina niliyoyataja hapo mwanzo , mataifa yao na yakwetu tunaojidharau asili zetu maendeleo ni tofauti kabisa. Nigeria pamoja na kuwa ni Africa, bado wanafahamika na kuheshimika sana kuanzia kwenye michezo mpaka sayansi. Hali kadhalika Japan , India pia. Ila sisi ambao utakuta mtoto anaitwa Jaden John Emmanuel ndio tupo kama tulivyo.
Wito wangu, ifike mahali tuache ulimbukeni, tujikubali kwanza ndio dunia itatukubali. Nimeamua mimi watoto wangu wote nawapa majina ya kinyumbani yenye maana nzuri ambayo ata padri wakati wa kubatiza hatutasumbuana. Yani ninataka kutengeneza identity. Kataa utumwa wewe chausiku.
Jina la ID yako asili yake ni mkoa gani??
 
Back
Top Bottom