Kuna wimbi kubwa sana la Ulimbukeni na ushamba kwa Watanzania hasa Mtu akijua kusoma na kuandika

Nimesoma id yako nikaona ninyamaze
 
Bush aliyepata kuwa Rais wa nchi fulani, kiswahili ni Kichaka, sijui hili nalo ni la mitishamba? Au kwa vile liko kwa kinge basi halina shida.
Huyo bwana ni mshamba tuu , anakwambia majina ya kiafrika mabaya[emoji1787][emoji1787][emoji1787] ukimuuliza ubaya wake upi hawezi elezea
 
Hao watu wa utamaduni, maendeleo ya jamii n.k wanalipwa mishahara ya bure. Wanakuza tamaduni za wenzetu badala ya zetu. Maadili yanamomonyoka wao wanakenua meno tu na kula kodi zetu. Tume ya sayansi na technology sijui imepiga hatua gani kwenye kuendeleza mazuri na ya kisayansi ya mira na destuli zetu. Yaani sikuhizi maisha ni ya tamthiria tu. Kizazi hiki kinalelewa na tv.
 
Itakuwa uliishiwa pesa ya sikukuu, Yamoto, Mitimingi, Sato, Masaki, Kumamoto, Kazimoto haya yote majina ambayo wajapani wanayatumia. Mimi Chirwa siyo msomali lakini wasomali wanalitumia jina hilo, Mbowe unajua ni mchaga lakini wanyasa wanalitumia jina hilo, Kabwe ni mtu wa Kigoma, lakini Zambia na Malawi wanalitumia jina hilo, Watonga ni kabila huko Zambia na Malawi lakini huko Mashariki ya Mbali kuna visiwa vya Tonga wanaishi watonga.Nakushauri majina usiyahusishe na kabila au dini.
 
Sawa Nyangema umesikika
 
Umenena vema sana….ubovu wetu mkubwa ni kukumbatia tamaduni za kigeni eti ndio ujanja….na katika kila nyanja ya maisha…
Mobutu Sese Seko Kuku Ngbendu Wa Za Banga ndio aliwakomesha Wacongo Zaire kwa kuwawekea sheria ya kuita majina ya kiasili wote na kuyabadili yale ya kitumwa.



Sent from my SM-G9350 using JamiiForums mobile app
 
Tusipangiane, watoto wangu nawaita majina ninayopenda! Zaa wakwako waite majina ya mitishamba.
hahaha

serikali ibuni sheria ya kuhifadhi majina ya asili kwamba ktk majina matatu ya mtu, surname au jina la mwisho sharti liwe la asili.

mchakato huo kwenye vitambulisho vya taifa
 
Kwahiyo majina ya asili ndio yanafanya uwe mwanasayansi bora au mwanamichezo bora?😁 akili finyu sana hizi👎
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…