Uchaguzi 2020 Kundi lipi litawaadhibu/ kuwabeba Magufuli na Lissu katika sanduku la kura?

Uchaguzi 2020 Kundi lipi litawaadhibu/ kuwabeba Magufuli na Lissu katika sanduku la kura?

MOSintel Inc

JF-Expert Member
Joined
Mar 24, 2016
Posts
817
Reaction score
593
Wasalaam wana bodi,
Poleni sana na majukumu ya kulijenga Taifa.

Nchi yetu inaelekea katika uchaguzi mkuu na tayari mbiu imekwisha lia na amsha amsha za hapa na pale zimeanza.

Kuanzia tarehe 27 Agosti, 2020 hadi 28 Oktoba 2020 itakuwa kipindi cha mnyukano majukwaani kwa wagombea kutoka katika vyama vya siasa zaidi ya 10 katika nafasi ya Urais.

Katika kipindi hiki wanasiasa ambao wanaonyesha kuleta ushindani katika uchaguzi wa mwaka huu ni Mwanasheria nguli na mwanasiasa wa muda mrefu Ndugu Tundu Antipas Lissu kupitia CHADEMA na Rais anayemaliza kipindi cha utawala wake wa miaka mitano Ndugu. Dr. John Pombe Magufuli ambaye ameomba tena ridhaa kupitia chama chake cha CCM kuwa Rais kwa kipindi kingine.

Katika uchaguzi kura huwa katika makundi na wanasiasa makini katika kunyakua kura hizi za uchaguzi hurusha sera zao wakijikita katika makundi yafuatayo:

1. Vijana

2. Wakulima

3. Wafanyakazi

4. Wakina mama

5. Wafanyabiashara

Najua kampeni hazijaanza ila wagombea wengi walishaanza kutoa dodoso za nini watafanya. Wanasiasa walioingia ulingoni tumewajua.

Unadhani katika hao wawili niliowataja hapo juu ni mgombea yupi ambaye ana haiba ya kushawishi makundi hayo matano hasa ukizingatia mazingira ya KIUCHUMI(MICRO&MACRO), KISIASA na KIJAMII tuliyonayo kwa Sasa kuelekea uchaguzi?

#UCHAGUZI2020
#VISION2025
#AGENDA2063

images%20(75).jpg
images%20(74).jpg
 
Lissu hana sera wala nini

Yeye anasaka kura za huruma hasa akipoyoka kuwa alipigwa risasi za kutosha lakini akapona.....

Ajiandae kisaikolojia
 
Kwa Hali ya nchi yetu kundi ambalo magu atakuwa na uhakika ni wakulima na wakina mama na wakulima ndo wengi na akina mama ambao ni watu wagumu Sana kubadilika wakisema moja wanashikilia moja lkn kwa vijana, wafanya biashara na watumishi ni ngumu Sana watu wana maumivu na vilio sana Juu ya utawala huu
 
Wakulima Labda wa chato.

Mkulima gani ampigie mtu ambaye alikuta ruzuku ya mbolea na mbegu na kuziondoa?

Mkulima gani wa korosho, Mbaazi atampigia Magu?

Kijana gani timamu atampigia Magu?

Kula za Magu Ni za watu wasio wajibika kama wamama wa nyumbani wasio na kazi na vijana wa uvccm na makada wanufaika wa mfumo wa kishenzi kama wakina Makonda,Gambo na wengine.
 
Kwa Hali ya nchi yetu kundi ambalo magu atakuwa na uhakika ni wakulima na wakina mama na wakulima ndo wengi na akina mama ambao ni watu wagumu Sana kubadilika wakisema moja wanashikilia moja lkn kwa vijana, wafanya biashara na watumishi ni ngumu Sana watu wana maumivu na vilio sana Juu ya utawala huu

Kwani wakulima Magu amewafanyia kitu gani mkuu?
 
Hakuna mgonjwa mpuuzi ambae anaweza kubali kumwachia mwili wake daktari mwanafunzi amfanyie operation ya moyo wakati Dr bingwa yupo
 
Kwa nchi zinazojitambua(ulaya) na zenye watu wanaojitambua kwa makundi hayo hapo juu, karibu yote jiwe ingekuwa ni vigumu sana kupata kura zao, kwani wengi ni wahanga, lakini kwakuwa ndio hivyo tena,
Kwani We unaishi Ulaya au huu uchaguzi ni Wa Ulaya Ongelea Mazingira yanayokuzunguka yaani Mabeberu yameafanya hata kufikiria lazima uwaze Ulaya hahahhaa
 
Lissu sera wala ilani Hana anabwabwaja kinachomjia kichwani chochote hewa ndicho anaongea .Magufuli anaongea kwa Ilani kuwa tuliwaaahidi uchaguzi uliopita tutafanya Moja mbili tatu tumefanya Moja mbili tatu na tunawaahidi.mkituchagua tuna hii ilani mpya kutokana na tuliyofanya ilani iliyopita mtupe ridhaa tutekeleze hii ilani mpya

Lisu anavyongelea abavijua mwenyewe anakoviokota.Akiota usiku kesho ndio ataviongea magroup watakao mpa kurani wavuta bangi Tena wawe wamevuta kabla ya kupiga ila Kama hawajavuta hawatampa

For any serious voter hawezi mpa kura Lisu Ni empty kuanzia kichwani Hana sera wala ilani ya chama Ni kubweka tu kwa mikelele mingi isiyo na mantiki Wala support ya sera au ilani ya chama chake .Ni mpiga miyowe tu kuliko spika yenye volume kubwa ambayo hata Huwezi jua kinaongelewa nini
 
CCM itatangazwa wadhindi hata kura zisipopigwa, iko hivyo.

Mwinyi alipigiwa kura za ndiyo kabla kampeni na alikuwa peke yake.

Sasa kwa Magufuli ndio kitabadirika nini?!
 
Jiwe sijui atapitia wapi? Wakulima, wafanyabiashara, wapiga dili, waliobomolewa nyumba zao , waliofukuzwa kazi kwa maonezi wanaodaiwa kuwa vyeti feki, madereva wa darasa la Saba, walitumbuliwa, walioitwa vilaza wakatimuliwa udom makundi yote haya na familia zao wampigie kura Jiwe wamelogwa? Jiwe hana pa kupitia bila kusahau waliodhumiwa rambirambi za tetemeko la kagera.
 
CCM itatangazwa wadhindi hata kura zisipopigwa, iko hivyo.

Mwinyi alipigiwa kura za ndiyo kabla kampeni na alikuwa peke yake.

Sasa kwa Magufuli ndio kitabadirika nini?!
Mwaka huu 2020 ni wa kipekee sana. Sisi wananchi ndo tutawatoa hawa CCM .

Tumeshaanza kutuma salamu Tunduma na Ukara kule. Sasa mwaka huu ndo ndo watajua kuwa hawajui. Tugawane tu mbao watu wakashtakiwe ICC huko
 
Lisu sera wala ilani Hana anabwabwaja kinachomjia kichwani chochote hewa ndicho anaongea .Magufuli anaongea kwa Ilani kuwa tuliwaaahidi uchaguzi uliopita tutafanya Moja mbili tatu tumefanya Moja mbili tatu na tunawaahidi.mkituchagua tuna hii ilani mpya kutokana na tuliyofanya ilani iliyopita mtupe ridhaa tutekeleze hii ilani mpya...
Mbona Mimi sina sifa hizo ulizotaja ; Maana Nina elimu tena inaweza kuwa hata zaidi yako, sivuti bhangi, Nina upeo mzuri kichwani (Mungu ni mwema) ,sina lugha chafu za kejeli au zilizokosa staha unlike you...lakini nitampigia Tundu Lisu kura.
 
Lisu sera wala ilani Hana anabwabwaja kinachomjia kichwani chochote hewa ndicho anaongea .Magufuli anaongea kwa Ilani kuwa tuliwaaahidi uchaguzi uliopita tutafanya Moja mbili tatu tumefanya Moja mbili tatu na tunawaahidi.mkituchagua tuna hii ilani mpya kutokana na tuliyofanya ilani iliyopita mtupe ridhaa tutekeleze hii ilani mpya....
Mjomba kampeni hazijaanza. Ccm wao sera yao ni Magufuli, basi.
 
Mwaka huu 2020 ni wa kipekee sana. Sisi wananchi ndo tutawatoa hawa CCM .

Tumeshaanza kutuma salamu Tunduma na Ukara kule. Sasa mwaka huu ndo ndo watajua kuwa hawajui. Tugawane tu mbao watu wakashtakiwe ICC huko
Hahaha mpaka sasa majimbo wameshachukua robo ya idadi ya bunge,mpaka kampeni zianxe watakuwa wameshajaza bunge kwanini tuendelee na uchaguzikwa rough hizi.

Magufuli aliahidi uchaguzi huru na haki, ndio hii haki na uhuru alioahidi?!
 
Back
Top Bottom