Kuomba sana, kuwa mwema sana sio sababu ya Mungu kukubariki

Mpigania uhuru wa pili

JF-Expert Member
Joined
Apr 12, 2023
Posts
3,380
Reaction score
6,376
Ukiangalia kwenye maisha kuna watu hawana habari na Mungu hata kidogo na wanamaisha mazuri biashara zao zinazidi kukua kila uchwao mfano mzuri ni wana-science wako mstari wa mbele kumpinga Mungu ila kila siku wanazidi kuvumbua vitu

Njoo kwa sisi ambao tunaomba kila siku wengi wetu maisha yetu ni ya kawaida sana tunajizuia kwenye kutenda dhambi ila maisha bado ni magumu tunaombea sana biashara zetu, kazi zetu ila hata promotion kupata ni kwa mbinde

Ukweli ni kwamba Mungu anabariki mtu yeyote bila kujali matendo yake ya mwilini kwa hiyo usijidanye kwamba kusali sana ndo kutakupa maisha mazuri unatakiwa uondoe hiyo dhana

Unapataje baraka za Mungu kwa wewe ambaye umeamua kumtumikia Mungu, kumbuka wapo wengi wanaomtumikia Mungu ila hawazioni baraka kwenye kumtumikia Mungu

UPENDO
Mtumikie Mungu kwa sababu tu unampenda hiyo ndo iwe motives yako ya kwanza

UNYEYEKEVU
Baraka za Mungu unazipata kwenye maisha yako kupitia unyenyekevu, unaweza ukawa unasali sana, unafunga sana, wewe ni mwema lakin kama huna unyenyekevu kwa Mungu ni kazi bure
Mfano;- unapokutana na changamoto kwenye maisha yako kupitia unyenyekevu hakikisha unamshukuru Mungu na hakikisha au-mdharau Mungu na Mungu atakuonyesha njia au suluhisho la changamoto unayoyopitia

Mfano 2: kuna watu wengi wanataka kuujua utukufu wa Mungu lakin ghafla wanaamua kuwa wapagani atheist na wanakua mstari wa mbele kupinga uwepo wa Mungu nakuhakikishia Mungu ataondoa amani ndani yako na kila mda ukisikia habari zake utakua unajisikia vibaya sana hio ni laana
 
Thank you Jesus, Hakuna utajiri na mbaraka mkubwa maishani kama amani ya moyo,

hakika kumtegemea Mungu kuna faida sana tatizo wengi wamekariri kuwa na mihela mingi ndio kipimo cha kubarikiwa ilhali hawajui kuna baraka nyingi ambazo zimetugusa kwenye maisha yetu ambazo hata mimi binafsi huwa inapita miaka mingi lakini nikikumbuka ya nyuma nasema hakika Mungu hukuniacha ulinitendea mema pale ni muujiza wako tu ndio ulinivusha hivyo shukrani na sifa zirejee kwako🙏🏿

Nitanukuu kifungu toka kwenye Biblia

Mhubiri 9:11
[11]Nikarudi, na kuona chini ya jua, ya kwamba si wenye mbio washindao katika michezo, wala si walio hodari washindao vitani, wala si wenye hekima wapatao chakula, wala si watu wa ufahamu wapatao mali, wala wenye ustadi wapatao upendeleo; lakini wakati na bahati huwapata wote.
 
Umeandika pumba
Ukishashiba mawazo ya kipumbavu kama haya yanakuja
 
Umenikumbusha Kuna mama mmoja alikutwa na mafuriko kwa mvua ilonyesha Dar usiku wa kuamkia jmosi

Akaanza kuomba kwamba Mungu atuokoe watu atuepushe na mvua hyo yenye maafa,

Cha ajabu na kesho yake ikanyesha tena.


#Maombi hayafanyi kazi tuishi uhalisia
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…