Kuongea mwenyewe ni tatizo au ni kawaida?

Kuongea mwenyewe ni tatizo au ni kawaida?

Wazaramo wanaiita "Self Explaining" ni kitu cha kawaida na ni kizuri pale ambapo una mawazo fulani badala ya kuyaweka ndani unayatoa nje ndio hiyo "kuongea peke yako"

The smartest people on Earth, talk to themselves
 
Habari wana Jamvi, Poleni na baridi.

Nilikuwa nauliza Wataalam je Kuwaza hadi kujikuta unaongea mwenyewe kwa sauti ni tatizo au kawaida tu?
Mwanzoni nilikuwa nikimuona mtu anaongea mwenyewe nilizani ni ugonjwa. Lakini sasa hivi nimejilizisha kabisa ni hali ya kawaida maana imenitokea mara kadhaa na sijakoma.
 
Kuna watu wamenifanyia vitu wiki hii wamenitafakarisha sana.
Aisee hali ya shida ya akili ni kubwa sana,sijui miaka kadhaa mbele itakuwaje?
 
Kuna watu wana stigma katika hili. Huwa naongea mwenyewe, na niko kwenye mid 20s wala sio uzee sijui kuchoka maisha. Sababu muda mwingi siongei na watu endapo hatuendani vitu tunapendelea. Sipendi mpira, mieleka, matamasha, mazishi au sehemu yoyote yenye watu wengi naona kama kuna gaidi atalipua bomu hapo au mtakanyagana mfano kama ni uwanjani. Hata sehemu zangu za kutulia ni kwenye watu wachache sana.

Wasio na akili kabisa wala kuelewa mambo kidogo wanaishi kwa raha maana hawaumizi vichwa. Ila wenye akili kiasi inabidi wajadili, sasa kama huongei na mtu unaongelea ndani kwako ni hatari. Bora ujadili mwenyewe kwa sauti, ujiulize na kujijibu, ujihoji na kutengeneza debate mwenyewe. Tofauti na hapo kuna kitu unakifungia ndani na kitakupa matokeo kwenye magonjwa ya moyo.

Unahisi Isaac Newton alivyogundua gravity aliongea na nani? Alijiuliza mwenyewe alipoangukiwa na tufaa.
Au Archimedes mpaka anagundua Archimedes' Principle akiwa anaoga kwamba alikuwa na mtu wanaulizana. Hadi alikosa wa kuongea nae akakimbia uchi anashangilia amegundua kitu.

Watu wanaoongea peke yao naturally kwa kiasi na kwa mpangilio (sio wenye stress) huwa wana IQ kubwa kidogo.
 
Mpo wengi sana sikuhizi... Halafu mkigundua mtu anakun'gaza mnashtuka flani hvi.
 
Wazaramo wanaiita "Self Explaining" ni kitu cha kawaida na ni kizuri pale ambapo una mawazo fulani badala ya kuyaweka ndani unayatoa nje ndio hiyo "kuongea peke yako"

The smartest people on Earth, talk to themselves
self explaining.

The smartest people on earth, talk to themselves.
 
Kuna siku nilikuwa naongea pekeaku wakati natembea barabarani kuna jamaa ambae yeye mwenyewe inaonyesha alikuwa na matatizo ya akili aliniambia tunaanzaga hivyohivyo karibu chama la machizi mixture vichaa

Ila wanasema kuongea mwenyewe ni ishara ya kuwa na akili nyingi na maranyingi watu wanaoongea peke yao akiwa anahutubia hatumii kalasi ya kusoma hotuba anafloor bila kusoma
 
Wazaramo wanaiita "Self Explaining" ni kitu cha kawaida na ni kizuri pale ambapo una mawazo fulani badala ya kuyaweka ndani unayatoa nje ndio hiyo "kuongea peke yako"

The smartest people on Earth, talk to themselves
Jibu ni hili kitaalamu
 
Back
Top Bottom