Kupanda na kuanguka kwa utawala wa tatu Ujerumani - The rise and fall of the third Reich

Kupanda na kuanguka kwa utawala wa tatu Ujerumani - The rise and fall of the third Reich

Tuendelee...

Hitler alijaribu tena mwaka uliofuata na wakati huu michoro yake ilikuwa ya kiwango duni kiasi kwamba hakuandikishwa kwenye majaribio. Kwa kijana mwenye malengo makubwa Kama Hitler, Kama alivyokuja kuandika baadae, hili lilikuwa pigo ambalo hakutegemea. Alikwisha jiaminisha pasipokuwa na shaka kwamba angefanikiwa, kutoka kwenye maandiko yake mwenyewe ndani ya 'Mein Kampf', Hitler akaomba ufafanuzi kutoka kwa mlezi wa ile academy.

"Yule mtu muungwana alinihakikishia Mimi kwamba michoro niliyowasilisha ilionyesha kuwa sina nafasi kwenye sanaa ya uchoraji wa rangi, na kwamba ni wazi uwezo wangu upo zaidi kwenye eneo la uhandisi; kwa upande wangu, alisema, shule ya academy ya uchoraji sio mahali pangu, mahali pangu ni kwenye shule ya uhandisi."

Kijana Adolf alilazimika kukubali ila haraka, kwa masikitiko, alitambua kuwa kufeli kwake kuhitimu 'high school' kunaweza pia kumzuia kujiunga na shule ya uhandisi.
Wakati huohuo mama yake alikua akikisogelea kifo kwa ugonjwa wa kansa ya titi hivyo akarudi Linz. Toka Adolf aache shule, Klara Hitler na ndugu zake walimsaidia huyu kijana kwa miaka mitatu, na hawakuona matunda yoyote ya huo msaada.
December 21, 1908 wakati mji ukianza kuikaribisha Krismasi, mama wa Adolf Hitler alifariki, na siku mbili baadae alizikwa huko Leonding pembeni ya mumewe.

Kwa huyu kijana wa miaka 19, lilikuwa pigo kubwa mno. ".... Nilimheshimu baba yangu, ila mama yangu nilimpenda... Kifo chake kimeweka mwisho wa ghafla kwenye mipango yangu yote mikubwa... Umasikini na ukweli mchungu ulinilazimisha kuchukua maamuzi ya haraka... Nilikumbana na tatizo la kuendesha maisha yangu mwenyewe."

Kwa namna fulani! Hakuwa na fani yoyote. Hakuwahi kupenda kazi za mikono. Hakuwahi kujaribu kuingiza senti moja yeye mwenyewe. Ila hakuwa na shaka. Akiwaaga ndugu zake, aliazimia kuto kurudi mpaka mambo yatakapokuwa mazuri.
" Nikiwa na begi lililojaa nguo mkononi mwangu na moyo mkuu, nilianza safari kwenda Vienna. Mimi pia nilikuwa na matumaini ya kufanya mambo makubwa kuliko aliyofanya baba yangu miaka 50 iliyopita; Mimi pia nilikuwa na matumaini ya kuwa "mtu kati ya watu". Ila kwa namna yeyote sio mtumishi wa umma.


Inaendelea....
 
Tuendelee...

"KIPINDI CHA HUZUNI ZAIDI KATIKA MAISHA YANGU"

Miaka minne iliyofuata, kati ya mwaka 1909 na mwaka 1913, iligeuka kuwa miaka ya mateso makali na unyonge kwa huyu kijana mpambanaji kutoka Linz. Katika miaka hii ya mwisho kabla ya kuanguka kwa Hapsburgs na ukomo wa hili jiji kama makao makuu ya himaya ya watu millioni 52 katikati ya Ulaya, Vienna ilikuwa na muonekano na uchangamfu uliokuwa tofauti sana na miji mikuu mingine ulimwenguni.
Sio tu uhandisi wake, ila sanamu zake, muziki wake, ila katika mioyo mikunjufu na inayopenda starehe ya watu wake ambayo ilotoa muonekano ambao hakuna jiji lingine la magharibi lilitambua.

Ikiwa kandokando ya Danube ya blue na chini ya vilima vyenye misitu vya Wienerwald, vilivyopendezeshwa na miti ya matunda ya njano na kijani, Ilikuwa sehemu ya uzuri wa asili uliowavutia wageni na kufanya watu wa Vienna waamini kwamba uumbaji umewapendelea kwa namna ya kipekee sana. Muziki ulitanda kwenye hewa, muziki mkubwa wa nyimbo za asili za vipaji, wanamuziki wakubwa kuwahi kutokea Ulaya, Haydn, Mozart, Beethoven na Schubert, na, katika miaka ya mwisho ya majira ya joto ya India, mwanamziki shoga kipenzi cha Vienna, Johann Strauss.

Kwa watu waliobarikiwa hivi, na ambao walikuwa na chapa ya maisha ya starehe, maisha yenyewe yalikuwa Kama ndoto na watu wazuri wa jiji hili walimaliza siku zao nzuri mchana na usiku wakifurahia muziki na mvinyo, au katika mazungumzo ya hapa na pale katika migahawa ya kahawa, wakisikiliza miziki na kutazama sinema na maigizo, au katika kutomasana na kufanya mapenzi, wakitumia muda mwingi katika maisha yao kwenye starehe na ndoto.

Ili kuwa na hakika, hii himaya ilipaswa kuongozwa, jeshi la ardhi na jeshi la maji walisimamia, mawasiliano yalitunzwa, biashara ziliendelea na kazi zilifanyika. Ila ni wachache tu ndani ya Vienna waliofanya kazi masaa ya ziada - au hata masaa kamili yanayohitajika kazini - katika mambo hayo.
Kulikuwa na upande mwingine wa shilingi bila shaka. Hili jiji, Kama tu majiji mengine yote, lilikuwa na masikini wake : waliokosa mlo kamili, waliokuwa na mavazi makuukuu na walioishi sehemu za hovyo. Ila Kama mji mkubwa wa viwanda katika ulaya ya kati na pia Kama makao makuu ya himaya, Vienna ilikuwa na maendeleo, na haya maendeleo yalisambaa katikati ya watu na kuteremka chini. Wengi kati ya wale wa daraja la chini la kati walishikilia jiji katika siasa; wafanyakazi waliendesha sio tu vyama vya wafanyakazi ila pia chama chenye nguvu cha siasa cha aina yake, "The Social Democrats".

Kulikuwa na mabadiliko katika maisha ya jiji, ambalo Sasa wakazi wake walifikia watu milioni mbili. Demokrasia ilikuwa ikiondoa utawala wa kizamani wa kiimla wa Hapsburgs, elimu na utamaduni vikifunguka kwa kwa walio wengi hivyo kwamba wakati Hitler alipokuja Vienna mwaka 1909 kulikuwa na fursa kwa kijana huyu asiyekuwa na shilingi kupata elimu ya juu au kupata maisha mazuri tu ya kawaida, kama moja kati ya millioni wanaoingiza mshahara, kuishi katika maisha ya kiungwana ambayo makao haya makuu yaliwapatia watu wake.

Si hata rafiki yake wa pekee, Kubizek, masikini na aliyekosa fursa Kama yeye, tayari alikuwa akijijengea jina katika Academy ya muziki! Ila kijana Adolf hukufuatilia matamaanio yake ya kujiunga na shule ya uhandisi. Ilikuwa iko wazi kwake pamoja na kukosa diploma ya elimu ya juu. Vijana walioonyesha kipaji cha tofauti waliandikishwa bila hicho cheti - ila kwa jinsi inavyofahamika mpaka sasa hakufanya maombi hayo. Wala hakuhamasika kujifunza fani au kuomba ajira yoyote ya kudumu. Ila alipendelea kufanya kazi ngumu Kama: Kupiga chepe kuondoa barafu, kuosha makapeti, kubeba mabege nje ya kituo cha reli cha magharibi, mara kadhaa kwa siku chache akifanya kazi kama 'saidia fundi' kwenye ujenzi.

Inaendelea....
 
Tuendelee...

Mwaka 1909, karibu kufika mwaka baada ya kuwasili Vienna "kupangilia maisha yake ya baadae", alilazimika kuacha chumba chake chenye vitu vyote vya msingi huko Simon Denk Gasse, na kwa miaka minne iliyofuata aliishi katika nyumba za hovyo au kwenye "kotaz" mbovu sana za wafanyakazi huko 27 Meldemannstrasse kwenye wilaya ya ishirini ya Vienna, karibu na Danube, akitafunwa na njaa hivyo kwenda mara kwa mara kwenye majiko ya supu ya hisani ya jiji.

Sio ajabu kwamba karibu miongo miwili baadae, aliweza kuandika : Kwangu mimi, Vienna, jiji ambalo kwa walio wengi lilikuwa kitovu cha starehe zisizo na hatia, uwanja wa mapumziko kwa wapenda starehe, kwangu liliwakilisha, samahani kwa kusema, kumbukumbu za maisha katika kipindi cha huzuni zaidi katika maisha yangu.

Hata leo jiji hili linaweza kuamsha ndani yangu, si chochote ila mawazo hasi. Kwangu mimi, jina la jiji hili linawakilisha miaka mitano ya magumu na mateso. Miaka mitano ambayo nililazimishwa kupambania maisha, kwanza Kama mfanyakazi wa kutwa, baadae kama mchoraji mdogo; kiwango kidogo mno cha mapato ambacho kamwe hakikuweza kutosheleza njaa yangu ya siku.

Wakati wote anapoongelea nyakati hizi, huongelea njaa.
"Njaa wakati ule alikuwa mlinzi wangu mwaminifu; hakuwahi kuniacha hata wakati mmoja na alichukua chochote nilichokuwa nacho...maisha yangu yalikuwa mapambano endelevu dhidi ya huyu rafiki asiye na hiyana.

Ila kamwe, haidhuru, haikuwahi kumsukuma upenuni mwa kutafuta ajira ya kudumu. Kama anavyoweka wazi katika Mein Kampf, alikuwa na hofu wanayokuwa nayo matajiri ya kuangukia kwenye makundi ya wafanyakazi, ya kazi za kutwa - hofu ambayo baadae aliweza kuifanyia kazi katika kujenga chama cha kijamaa cha Taifa (National socialist party) katika uwanda mpana wa kazi isiyo na uongozi, isiyolipa vizuri, na iliyosahaulika, kazi ya daraja la kola nyeupe, ambayo mamilioni yake yalipendezesha fikra kwamba angalau wao ni bora zaidi katika jamii kuliko wafanyakazi!

Pamoja na kwamba Hitler anasema kwamba alijopatia sehemu ya mapato Kama 'mchoraji mdogo', hatoi taarifa zozote za kazi hii kwenye andiko la maisha yake isipokuwa kusema kwamba miaka ya 1909 na 1910 alikuwa ameimarisha kipato chake kiasi kwamba hakuhitaji tena kufanya kazi kama mfanyakazi wa kawaida. "Katika wakati huu", anasema, " nilifanya kazi binafsi kama mchoraji wa rangi za maji".
Hi kwa namna inapotosha, Kama yaliyo maelezo mengine ya maisha yake ndani ya Mein Kampf.

Pamoja na kuwa ushuhuda wa wale waliomfahamu kwa wakati ule ulionekana kuwa adimu ila wenye ushahidi wa kuaminika zaidi. Ushuhuda mwingi umekusanywa pamoja kutoa picha ambayo angalau ni sahihi zaidi na timilifu zaidi. Kwamba Adolf Hitler hakuwahi kuwa fundi rangi kwenye nyumba kama ambavyo mahasimu wake kisiasa walikuwa wakimnanga, hii ni hakika.
Angalau hakuna ushahidi kwamba aliwahi kufuata fani hiyo. Ambacho alifanya ni kuchora kwa kalamu au kwa rangi michoro isiyokuwa na viwango sana ya Vienna. Mara nyingi ya sehemu zilizofahamika sana Kama St. Stephen's Cathedral, nyumba za maigizo, 'the Burgtheatcr', ikulu ya Schoenbrunn au mabaki ya utawala wa Roma huko Schoenbrunn Park.

Watu waliokua karibu wanasema alinakili kutoka kwenye michoro iliyokwisha kuchorwa awali; kwamba hakuweza tu kuchora kitu kwa kukitazama kwenye uhalisia wake. Michoro haikuonyesha uhalisia wala uhai, kama michoro ya mhandisi anayechipukoa isiyokuwa na umakini mkubwa na maumbo ya binadamu ambayo wakati fulani aliyaongeza yalikuwa mabaya kiasi cha kumkumbusha mtu Visa vya katuni.

Inaendelea...
 
Hitler ni noma. Nimependa Sana pale anaposema rafiki yake mwaminifu asiye na hiyana wala huruma kamwe hakumwacha awe Mpweke.
 
Back
Top Bottom