Kupangiwa kazi vijijini tayari unakuwa umeuliwa kifikra na kitaaluma

Kupangiwa kazi vijijini tayari unakuwa umeuliwa kifikra na kitaaluma

Mtumishi aliyeko vijijini huko kujiendeleza labda kulima na kufuga huko ila kwenye mambo ya kitaaluma inakua ndio mwisho wako.

Huwezi hata kujiendeleza kitaaluma kupitia evening classes maana hakuna vyuo, colleges wala VETA, vyote hivyo asilimia kubwa vipo vijijini.

Kupata ruhusa kwenda kusoma ni kwa mizengwe mingi maana unakuta watumishi wapo wachache.

Wale madaktari wanaotegemea vijiwe baada ya kazi, ukiwa vijijini kwishaaa.

Wewe ndio Daktari pekee zahanati ya kijijini huko, nani atakupa ruhusa ukasome?

NB: mjini patabaki kuwa mjini tu.
Naunga mkono hoja mkuu.
 
Huwa nawaonea huruma sana hasa waalimu wa kike yaani unakuta binti kakulia Dar halafu anakuja kupangiwa kazi kijijini ndani kabisa tena mkoa tofauti unakuta wakazi wa huko hawajui hata kiswahili wanaongea kirugha chao tu, kijiji kizima hakuna hata duka na internet haikamati hata simu yenyewe mtandao unasoma kwa taabu!
Mbaya zaidi hakuna umeme wala maji
Ni mwendo wa kibatari na maji ya kisima tena ya kufuata kijiji cha tatu
Hapo ni mwaka mmoja tu binti wa watu keshazeeka kachooka kama kikongwe wa miaka 90
Unakuta ameshakuwa chakula cha wafugaji[emoji1787][emoji1787][emoji1787]
Hivi Kuna maeneo bado wanatumia mafuta taa?
Kwamba hata solar hamna?

Umaskini upo lakini sio kama ulivo-potray hapa
 
Kijijini fursa nyingi sana, hasa kwenye sekta ya ardhi, kilimo, ufugaji (ng'ombe wa maziwa, mbuzi...), usafirishaji, uvuvi (kwa baadhi ya maeneo), maji, na viwanda vidogo (kama kufyatua tofali, kutengeneza makochi, kushona nguo...).

Pia kijijini wana jamii wanakuwa na ushirikiano mkubwa sana kwa wataalamu wa afya, jambo linalokupatia faraja kubwa ambayo ina thamani kubwa isiyoweza kupimwa kwa kipato cha pesa.

Kijijini pia unapata muda wa kuwa karibu na familia yako kama unayo.

Kijijini unaweza kupata nyumba ya serikali bure, au ukapata nyumba nzuri kwa gharama nafuu, hivyo kusave something.

In short kijijini fursa ni nyingi kuliko mjini kwa watu wenye mshahara unaolingana, na kwa mwenye akili inachangamka zaidi nje ya your comfort zone kuliko kudumaa mjini na vijiwe (kufanya fani moja pekee).
Katika dunia ya utandawazi kuishi mahali pasipo na umeme wala mtandao kisa kilimo na nyumba za bure zisizo na umeme ni ufala.

Sitakaa eneo la namna hii tena bora kufa masikini.

Wanasiasa wanakula bata kwenye ma-V8 hawakumbuki wenzao wa vijijini eti kisa hata mbuyu ulianza kama mchicha.

Unaweza kuishia kuwa mchicha kiboya
 
Huwa nawaonea huruma sana hasa waalimu wa kike yaani unakuta binti kakulia Dar halafu anakuja kupangiwa kazi kijijini ndani kabisa tena mkoa tofauti unakuta wakazi wa huko hawajui hata kiswahili wanaongea kirugha chao tu, kijiji kizima hakuna hata duka na internet haikamati hata simu yenyewe mtandao unasoma kwa taabu!
Mbaya zaidi hakuna umeme wala maji
Ni mwendo wa kibatari na maji ya kisima tena ya kufuata kijiji cha tatu
Hapo ni mwaka mmoja tu binti wa watu keshazeeka kachooka kama kikongwe wa miaka 90
Unakuta ameshakuwa chakula cha wafugaji[emoji1787][emoji1787][emoji1787]
Nikipata ajira huko ni mwaka tu au miwili nawabwagia kazi yao.

Serikali inachezea sana hatima za watu
 
Katika dunia ya utandawazi kuishi mahali pasipo na umeme wala mtandao kisa kilimo na nyumba za bure zisizo na umeme ni ufala.

Sitakaa eneo la namna hii tena bora kufa masikini.

Wanasiasa wanakula bata kwenye ma-V8 hawakumbuki wenzao wa vijijini eti kisa hata mbuyu ulianza kama mchicha.

Unaweza kuishia kuwa mchicha kiboya
Hayo sawa, shida ni kukosekana fursa za kujiendeleza kitaaluma huku ukiwa kazini
 
Kijijini fursa nyingi sana, hasa kwenye sekta ya ardhi, kilimo, ufugaji (ng'ombe wa maziwa, mbuzi...), usafirishaji, uvuvi (kwa baadhi ya maeneo), maji, na viwanda vidogo (kama kufyatua tofali, kutengeneza makochi, kushona nguo...).

Pia kijijini wana jamii wanakuwa na ushirikiano mkubwa sana kwa wataalamu wa afya, jambo linalokupatia faraja kubwa ambayo ina thamani kubwa isiyoweza kupimwa kwa kipato cha pesa.

Kijijini pia unapata muda wa kuwa karibu na familia yako kama unayo.

Kijijini unaweza kupata nyumba ya serikali bure, au ukapata nyumba nzuri kwa gharama nafuu, hivyo kusave something.

In short kijijini fursa ni nyingi kuliko mjini kwa watu wenye mshahara unaolingana, na kwa mwenye akili inachangamka zaidi nje ya your comfort zone kuliko kudumaa mjini na vijiwe (kufanya fani moja pekee).
Hivi wewe umewahi Fanya kazi kijijini? Unavifahamu vijiji vya mkoa wa Simiyu au shinyanga? Huku wenyeji hawataki muona mgeni akifanikiwa uchawi Kila Kona tena hadi watumishi wanatumia ndumba hasa wenyeji wa huko unakuta Kijiji kina kaya 400 katika hizi kaya 97 ni za waganga wa kienyeji kaya 250 ni wachawi kaya zilizobaki ndo Zina ahueni umasikini ni WA kutupa halafu kuna mtu anasema vijijini kuna fursa ninawasi wasi utakuwa umetembelea vijiji vya DSM pekee! Kuna vijiji huku greda halijawahi fika kuna Barbara za ng'ombe tu usiombe upate dharula wakati wa masika utajuta.
 
Eeh kwa kuzungumza tu fursa huwa nyingi sana fika kijijini sasa
Mm ninazungumza kwa experience.
Hivi wewe umewahi Fanya kazi kijijini? Unavifahamu vijiji vya mkoa wa Simiyu au shinyanga? Huku wenyeji hawataki muona mgeni akifanikiwa uchawi Kila Kona tena hadi watumishi wanatumia ndumba hasa wenyeji wa huko unakuta Kijiji kina kaya 400 katika hizi kaya 97 ni za waganga wa kienyeji kaya 250 ni wachawi kaya zilizobaki ndo Zina ahueni umasikini ni WA kutupa halafu kuna mtu anasema vijijini kuna fursa ninawasi wasi utakuwa umetembelea vijiji vya DSM pekee! Kuna vijiji huku greda halijawahi fika kuna Barbara za ng'ombe tu usiombe upate dharula wakati wa masika utajuta.
Nimewahi kufanya kijijini, mpakani na Malawi, nilihudumia vijiji viwili kwa wakati mmoja, Katumbasongwe na Mpunguti.

Uchawi hata mjini upo. Kama huwezi kupambana sio kosa lao wao.

Umesema hata watumishi ni wachawi, kwa issue sio kijijini ni imani yako binafsi.

Changamoto za masika nimeziishi na mafuriko pia. Lakini nilipambana, baada ya miaka mitatu nikapata fursa kurudi masomoni ndio namna nilivyochomoka.
 
Kijijini fursa nyingi sana, hasa kwenye sekta ya ardhi, kilimo, ufugaji (ng'ombe wa maziwa, mbuzi...), usafirishaji, uvuvi (kwa baadhi ya maeneo), maji, na viwanda vidogo (kama kufyatua tofali, kutengeneza makochi, kushona nguo...).

Pia kijijini wana jamii wanakuwa na ushirikiano mkubwa sana kwa wataalamu wa afya, jambo linalokupatia faraja kubwa ambayo ina thamani kubwa isiyoweza kupimwa kwa kipato cha pesa.

Kijijini pia unapata muda wa kuwa karibu na familia yako kama unayo.

Kijijini unaweza kupata nyumba ya serikali bure, au ukapata nyumba nzuri kwa gharama nafuu, hivyo kusave something.

In short kijijini fursa ni nyingi kuliko mjini kwa watu wenye mshahara unaolingana, na kwa mwenye akili inachangamka zaidi nje ya your comfort zone kuliko kudumaa mjini na vijiwe (kufanya fani moja pekee).
Niko halmashauri ya vijijini kwa miaka 13 sasa ila nachowaza ni kuhama tu.

Watu wengi wanaoniambiaga "usihame kijijini Kuna fursa" huwa nawajibu "Njoo wewe huku mi nije mjini" naonaga hukaa kimyaa na hawanijibu.

#YNWA
 
Back
Top Bottom