Labda ni style yake..wengine wanaiita tolerance wewe unasemaje?, wanafiki wanaomsifia ni kina nani? wakati tunaongelea vitu vinavyonekana kwa macho yenu kila siku...kila mahali unaweza kuficha barabara? unaweza kuficha watuhumiwa wanaohaha mahakamani na kesi?..Kikwete ni tumaini lililopotea. Wasaidizi wake ni ushahidi tosha na kigezo kizuri cha kupimia uwezo wake kwani udhaifu unapogeuka na kuwa sifa kuu ya kiongozi, ujue utawala wake uko rehani. Kiongozi dhaifu hukwepa majukumu na si ajabu wanafiki wakamsifia huku wakitoa lawama lukuki kwa wapambe - hapana tatizo ni Kiongozi mwenyewe, period.
Mkuu wangu mifano kama hii ndio huniacha hoi kabisa! Lakini yanibidi kukubali kwamba sikutegemea kabisaaa na bado siamini..Ama kweli kila kitu kina sura mbili,Rais anasifiwa matokeo yakionekana, hauwezi kulazimisha sifa zisipostahili.
- Rais amefanya ziara bandarini, kuna uozo wa hali ya juu pale, akaishia zake. hamna maagizo wala nini. Watu bado wanapitisha mizigo Mombasa kusiko na rushwa.Sasa alienda bandarini kufanya nini?
- Alifanya ziara Magereza, hamna mabadiliko yoyote.
- Alifanya ziara moja USA akapata msaada wa $ 2 million akaitisha press conference na kutaja hiyo kama mafanikio ya ziara, wakati EPA zimeibiwa hela mara 70 ya hizo alizoopewa.
- Ardhi takribani ya ukubwa wa kisiwa cha Unguja amepewa mwekezaji na kufukuza wazawa Loliondo, hii ni mwaka huu.
- Alitembelea TRA akasema "nina majina ya wala rushwa wote hapa", sasa alifanyia nini majina yale?
- Amechagua baraza la mawaziri limejaa vihiyo na "wezi" haya ni maneno ya naibu waziri wa fedha juzijuzi , siyo yangu.
Rais wetu siyo decisive.
Mkuu mchango mzuri ila majibu yake kwa ufupiKwa maoni yangu Kikwete uongozi umemshinda na mimi sioni chochote cha kumpongeza. Alipata ushindi wa kishindo kwa kuahidi kuipitia mikataba upya ya uchimbaji madini yetu ambayo ilisainiwa na Mkapa hadi hii leo pamoja na kuunda kamati ya madini bado mapendekezo yaliyotolewa na kamati hiyo hadi hii leo bado tunaendelea kupata 3% ya mapato yote ya dhahabu na kuwaachia wageni 97% ya mapato. Pamoja na bei ya dhahabu kuongezeka kwa kiasi kikubwa sana (Wakati Mkapa anasaini Bei ya dhahabu ilikuwa ni dola 233 na sasa ni zaidi ya dola 1,100. Kwa kifupi bado tunaliwa kwenye rasilimali zetu.
Aliahidi Maisha bora kwa kila Mtanzania, sijui kama alikuwa na mikakati ya kuhakikisha hili analifanikisha vipi kama kiongozi au ilikuwa na kauli tu ambayo haikuwa na mikakati yoyote bali ni katika kupata kura nyingi toka kwa Watanzania.
Kwenye swaala la ufisadi mpaka sasa hivi ameshindwa katika kila ufisadi uliofanywa dhidi ya nchi yetu. Tukianzia Kiwira ambayo Mkapa alijiuzia kiwiziwizi mgodi ule wenye thamani ya shilingi bilioni 7 kwa shilingi milioni 700 tu na kulipa shilingi 70 millioni. Hadi leo Mkapa hajachunguzwa iliWatanzania tufahamu ni nani aliyeidhinisha uuzwaji wa mgodi ule. Mkapa pia alichukua mkopo wa shilingi bilioni 7 toka NSSF na hadi hii leo hakuna anayefuatilia mkopo huo ili Mkapa na Yona waanze kuurudisha. Pia si ajabu Mkapa na Yona wanaweza kulipwa mabilioni ya shilingi na Serikali eti kuwafidia katika gharama walizoingia kuhusiana na Kiwira.
Tukija EPA kitendo cha kutwambia kwamba wahusika wa EPA wamerudisha shilingi bilioni 70 na wakati huo huo kushindwa kuyaweka majina ya watuhumiwa hao hadharani na kiasi kilichorudishwa na kila mmoja kwa maoni yangu ni usanii wa hali ya juu. Na mimi siamini kama watuhumiwa wa EPA wamerudisha hata senti tano vinginevyo sioni ugumu wowote wa majina yao na kiasi walichorudisha kuwekwa hadharani. Kesi za EPA nazo zimejaa usanii mtupu hili siyo siri kabisa wote tunalijua. Balozi wa Marekani nchini wakati ule aliahidi nchi yake kuisaidia Tanzania kumrudisha nchini mhusika mkuu Balalli kama Serikali ingewaomba msaada huo, lakini Kikwete akaamua kukaa kimya bila ya kuchangamkia msaada ule mpaka Balalli akafa
Tukija kwenye ufisadi wa Kagoda wa $40 millioni tunajua fika kwamba muhusika na ufisadi wa Kagoda papa fisadi Rostam hawezi kabisa kuguswa hivyo hadi hii leo hakuna uchunguzi wowote unaofanywa ili Watanzania tuweze kufahamu nini kilichojiri katika ufisadi wa Kagoda ambapo zilichotwa
Tukija kwenye Rada yule mtuhumiwa Vithlani alikuwa nchini anahojiwa na vyombo vya dola, lakini kwa kuwa ufisadi ule unawagusa vingune wengi katika awamu ya tatu na ya nne basi wakampa upenyo akimbie nchi ili kuwasitiri wahusika wa ufisadi ule wa $12 millioni
Kwenye Richmond/Dowans nako mapendekezo ya kamati iliyoundwa na Bunge mpaka leo Kikwete na Serikali yake imeshindwa kuyafanyia kazi bila kuwa na sababu zozote zile za msingi na wahusika waliochota $172 millioni bila kuzifanyia kazi bado wanapeta mtaani na huku mjadala wake ukiendelea kwa mwaka wanne sasa
Meremeta ambapo $155 millioni zilichotwa, hii tumeambiwa kwamba inahusiana na usalama wa Taifa na wizi wowote unaohusiana na usalama wa taifa haustahili kujadiliwa popote pale!!! Mhhh!
Rukia Mipasho Simba anasema hawezi kujiuzulu hadharani. Mzee wa Vijisenti Chenge Mnyunyizaji anatamka hadharani kwamba hakuna anayemchunguza kama yupo amfuate jimboni kwake. Papa fisadi Rostam kwa mara ya pili anaomba uchunguzi wa Richmond ufanyike tena kwa sababu hakubaliani na ripoti ya kamati ya Bunge mara ya kwanza alitaka uchunguzi mpya ufanywe na majaji. Haya yote yanaonyesha kwamba hawa wameshafahamu fika kiongozi wa nchi ambaye ana madaraka makubwa aliyokabidhiwa na Watanzania baada ya kumchagua kwa kishindo hana kabisa ubavu wa kuyatumia madaraka aliyokabidhiwa. Hawa kila mtu anaropoka kivyake vyake tu maana wanajua hakuna athari yoyote itakayowapata kutokana na kuropoka huko.
Mashule yetu bado mengi majengo yake hayana hata hadhi ya kuitwa ****** wachilia mbali madarasa, asilimia kubwa ya Wanafunzi bado wanakaa chini walimu ndiyo wa kubahatisha na wakti mwingine hawako kabisa, huko CCM kutokana na uongozi wake dhaifu migongano chungu nzima isiyokwisha na kuonyeshana ubabe hadharani, na mipasho ya hali ya juu na wengine hata kutishiwa maisha yao!!
Mimi kwa maoni yangu ukitilia maanani ufisadi wa Richmond, $172, EPA $133 millioni, Rada $12 millioni, Meremeta $155 millioni Kagoda millioni $40 basi ni haki kabisa kutumia ufisadi kama kigezo cha kumpima Kikwete na hata tukitumia vigezo vingine vyovyote vile hakuna hata kigezo kimoja ambacho anastahili kupewa pongezi.
Sasa tukitilia maanani hayo yote niliyoyaandika hapo juu tutaona kwamba Kikwete siyo tu hastahili pongezi zozote bali pia hastahili kugombea tena 2010. . Tumeshaona Kikwete kama kiongozi alivyo dhaifu katika mambo mbali mbali na hii kwa maoni yangu ni sababu tosha kabisa ya kuhakikisha tunapata kiongozi mpya 2010 ambaye atakuwa tayari kuyatumia madaraka aliyonayo bila kumuogopa yeyote yule.
Kama kiongozi mwenye mediocre perfomance kiasi hiki anashindwa kuambiwa kwamba kazi tuliyokupa imekushinda hivyo kaa pembeni ili tumtafute kiongozi mpya basi Tanzania tuna matatizo makubwa sana
Mchango wangu wa thumni huo
..............
Tuangalie mambo mengine mengi anayoyafanya na kufanikiwa mfano:
a) Kuongezeka kwa enrollment kuanzia primary mpaka university kwa miaka ya ke minne --kielimu siyo mafanikio hayo??
b) Kuna program za kujenga zahanati kila kata..kusogeza huduma za afya karibu na wananchi---siyo mafanikio??
c) Kuongezeka kwa utalii na watalii tangu ashike nchi..siyo mafanikio hayo???
d) Barabara za lami mpaka kigoma.rukwa nasikia dodoma-arusha 😕is on track..siyo mafanikio hayo?? kwa miaka minne
e) Uhuru wa habari and tolerance of our president to the freedom of expression..zitto ameliona hili naye..
Bana ye mnyonge mnyogeni haki yake mpeni...mlitaka awafanyeje? wana JF mbona hamna shukrani hasa wewe mwanakijiji.
Na kweli hivi kwa nini Makao makuu hadi leo hayajahamia Dodoma?
Statistics zipo kaka..hivi vyote ni vitu unaona kwa macho yako yote mfano:-
1. Watu wanaotuhumiwa wako mahakamani (baadhi) hilo nalo huoni?? rais gani amewahi kufanya acha tanzania hata hapo karibu kenya...ambayo ni 20 most corrupt country in the world
2. Barabara zote nilizosema nimeziona na kupita kwasababu ya kazi zangu..Rukwa-mbeya, rukwa-kigoma, dodoma-singida, Aursha-Dodoma (inaendelea), Arusha- singida (inaendelea) jamani kwa miaka minne ..he has done something worth ...
3. Shule na Zahanati zimeanza kujengwa kila kata..shule ofcourse imeanza wakati wa mkapa..lakini zahanati ni Kikwete iniative, vyuo vikuu vimejengwa (state university of dodoma for example)..enrollment kuanzia primamry mpaka chuo kikuu ni kubwa kupita wakati wowote nchini..need more..ni mafanikio hayo???
Mkuu mambo ya kuangalia na kuona hayapo tena mkuu. Kiongozi yoyote mafanikio yake hupiwa na facts siyo kwa kuangalia tu. Hao wanao tuhumiwa kwenda mahakamani kesi zote ni kiini macho tu. Wangapi umeona wame hukumiwa kwa makosa yao? Ditopile kaua wakaifanya manslaughter. Zombe yuko wapi?
Hizo barabara mkuu pia lete data. Kama kweli zime fanyika haku kosekani data. kajenga barabara ngapi? Ngapi zilikua initiatives zake? Haya mambo ya kuona tu yana danganya sana. barabara zinaweza hata kujengwa bila initiative ya raisi.
Mkuu UDom siyo Kikwete kabisa. That was all Mkapa. Ime kuja kumalizika tu wakati Kikwete ni raisi. Na kuhusu hizo enrollment mtu utaonaje kwa kuangalia tu mkuu? kama kweli zimeongezeka una shindwake kuweka data kwamba kabla ya Kikwete ilikua hivi na baada ya Kikwete imekua hivi? Unataka kuniambia enrollment unaweza kuona imeongezeka kwa kuangalia tu bila data?
....... Let's look the "history from below" and see who was a better leader between Kikwete, Mkapa, Mwinyi and Nyerere.
Crystal and clear good onePole sana kaka na wewe nadhani unatoa hizi habari kwa wototo wa miaka 10.
Mie ni mtu wa miaka 50's sidanganyiki.
Mwinyi aliacha nchi haina kabisa pesa kwenye consolidated fund hizo pesa aliziomba wapi? Nchi ilikuwa na hali mbaya sana.
Tupe data ku Substantiate hoja yako hizo pesa alizipata wapi Mwinyi bwana.
Tunajua mpango mahususi wa mkapa wa kujenga barabara zetu kutokea katika internal funds alianzisha yeye na utekelezaji ulifanyika, na Mwinyi hastahili sifa yoyote kwa hili.
Narudia sisi ni watu wazima hatudanganyiki kwa kitu mkuu tumeshuhudia mengi ya uongo yakitolewa na watu kama nyinyi.
MF
Pole kaka, na pia asilimia kubwa ya barabara za Mkapa, zilikuwazishapangwa na kutafutiwa wafadhili na Mwinyi.
So kuna issue ya kupokezana vijiti mzee, ukiona mkandarasi yuko site, ujue kazi ya ujenzi na uchoraji ilianza miaka mitatu nyuma... okay!!!
So do not expect... unasanifu mwaka huu, unatoa tenda mwaka huu, ujenzi unaanza mwaka huu na unaisha mwaka huu... tulia kidogo ufikiri kaka... kujenga barabara sio sawa na kununua ndizi sokoni tandale.
Nimechoka na vigezo vinavyotumika kupima uwezo na mafanikio ya rais wetu kwa muda wote katika JF forums je
1. Si halali kupima uwezo wa rais kwa kigezo kimoja tu cha kuzibiti ufisadi ..yaani EPA, Richmond..etc after all watuhumiwa wako mahakamani wengi tu..ala..
Tuangalie mambo mengine mengi anayoyafanya na kufanikiwa mfano:-
a) Kuongezeka kwa enrollment kuanzia primary mpaka university kwa miaka ya ke minne --kielimu siyo mafanikio hayo??
b) Kuna program za kujenga zahanati kila kata..kusogeza huduma za afya karibu na wananchi---siyo mafanikio??
c) Kuongezeka kwa utalii na watalii tangu ashike nchi..siyo mafanikio hayo???
d) Barabara za lami mpaka kigoma.rukwa nasikia dodoma-arusha is on track..siyo mafanikio hayo?? kwa miaka minne
e) Uhuru wa habari and tolerance of our president to the freedom of expression..zitto ameliona hili naye..
Bana ye mnyonge mnyogeni haki yake mpeni...mlitaka awafanyeje? wana JF mbona hamna shukrani hasa wewe mwanakijiji.
1. Ndugu, hakuna shida yeyote wananchi wa bagamoyo kupata barabara..ni maendeleo hayo?
2. Kuna barabara ya kwenda Handeni kutokea mkata inajengwa kiwango cha lami na kutokea korogwe kwenda handeni kiwango cha lami..ni maendeleo hayo...???
3. Kuna barabara ya Arusha -Dodoma, Arusha -singida kiwango cha lami..maendeleo hayo??
4. Barabara ya Rukwa-Kigoma, Rukwa -Mbeya kiwango cha lami..maendeleo hayo??
Hizi zote ni project za awamu ya nne?? miaka minne kafanya kazi bana ..acheni hizoo??
Kuna ndugu anasema mipango ya awamu ya tatu NO NO, Kuna mambo vile awamu ya tatu iliyakuta kutoka awamu ya pili..mfano barabara ya kusini (rufiji) ilishasainiwa na mwinyi na wafadhili kutoka kuwait lakini baadaye ilionekana kama ya Mkapa vile...tuwe wakweli bana!
Tumaini, Institution zote hizo PCB (now PCCB), CAG office, Banking systems, investment climate, Macro ecomomic stability etc za utawala wa Ben, to this he deserve his credit. The incurmbent kakuta structures na istutirions ziko in place so much was expected.
Ndio maana ya vijiti kupokezana ndugu..Mkapa kakuta mambo kibao kwa mwinyi..na yeye JK ataacha vitu kibao ...kwa rais wa awamu ya tano...ndio tunaijenga nchi hivyo..Tumaini, Institution zote hizo PCB (now PCCB), CAG office, Banking systems, investment climate, Macro ecomomic stability etc za utawala wa Ben, to this he deserve his credit. The incurmbent kakuta structures na istutirions ziko in place so much was expected.
Prior Master, umezungumzia point muhimu sana... rais wa sasa amekuta everything on track including structures, institutions with surplus.. hivi leo nchi tena ina madeni na haina surplus... huyu hafai kusifiwa .... mi nasema both in macro and micro economics JK has failed, ila his loyal followers wako busy doctoring the figures lakini sasa imefika mahali ukweli haufichiki tena.
Umeshasahau kwamba Wanazuoni wa TZ bado wanatumia vigezo hivyo hivyo (bila ya facts) kumsifia Nyerere? Let's look the "history from below" and see who was a better leader between Kikwete, Mkapa, Mwinyi and Nyerere.