Kupinga serikali tatu kwa kisingizio cha gharama ni upuuzi

Kupinga serikali tatu kwa kisingizio cha gharama ni upuuzi

mleta thread naona hata hajitambui.wizara hazijapunguzwa,hizo zilizosemwa ni za muungano tu.hapo bado za tanganyika,hao wazenji wakafie mbali na wizara zao hazituhusu.huku bara utakutana na mafisadi watataka kula so watajitengenezea nafasi nyingi tu.bado mabunge matatu,wabunge watatu kila jimbo,wakuu wa mikoa/wilaya,makatibu,manaibu waziri na wapambe wao.ukisikiliza madai ya wazenji ndio utachoka so kwa nini tusivunje tu muungano kama watu wanataka mamlaka kamili?
 
Naunga mkono. Ni upuuzi kwa kudhani kuwa mfumo wa uendeshaji wa nchi utakuwa huu uliopo, hivyo kuwa mzigo. Hautakuwa huu kabisa. Taasisi ya Uraisi wa Muungano itakuwa ndogo kwani mambo ya utawala yatakuwa yanafanywa na serikali za washirika ambazo pia zinaweza kubanwa kuondoa mambo mengi yasiyo ya lazima katika mfumo wa utawala uliopo sasa. Fikiria kuwa Tanzania bara nayo iwe na serikali yenye wizara zisizozidi 15. Fikiria kuwa labda ngazi ya ukuu wa wilaya iondolewe na majukumu yake yafanywe na Kurugenzi ya halmashauri za Wilaya. Nina maana kuwa kutakuwa na mabadiliko makubwa na wala haitakuwa mzigo. Ikumbukwe kuwa hata rasimu ya Katiba ya Tanzania bara haipo. Tusiogope mabadiliko kwani hayana budi kutokea kwa sasa. Tukikataa mabadiliko tunayoyaratibu wenyewe, yatakuja kwa njia ambayo hatutairatibu na ita kuwa mbaya yenye gharama ya kutisha. Kumbukeni mabadiko yaliyotokea katika nchi za Afrika ya Kaskazini. Waliogopa mabadiliko wakati upepo wa demokrasia ya vyama vingi ulipokuwa unavuma lakini kwa kuwa mabadiliko hayanabudi kutokea yakatokea kwa njia ambayo iligharimu umwagikaji wa damu na uharibifu mkubwa wa nchi. Cha kuangalia kwa sasa ni juu ya Katiba mpya, ya kidemokrasia, nzuri, makini, ya Tanzania bara.

Well Said Mkuu, ila Hapo kwenye "Tanzania bara", Unge substitute na "Tanganyika" Ningekupa Tano Nyingine
 
serikali ya zanzibar
serikali ya Tanganyika
serikali ya Shirikisho
Hata kwa hoja ya gharama huoni kuwa ni ukweli wa wazi.
Kila serikali itakuwa na baraza la mawaziri, rais, na bunge lake.
Ukizingatia iyo katiba yenu mnayoishadadia inatupa wabunge wawili kila jimbo... mtu na demu wake!
Hivi tuna majimbo mangapi?
Na mangapi yataongezwa kwa kuvunja majimbo yanayoongozwa na Chadema?
Ila hii naipendea kitu kimoja... ambacho watanganyika tunakitamani na wazenji wanajidanganya eti wanaitaka...
...uyo kiongozi wa shirikisho ataachwa solemba akiwa yuko hewani... rejea USSR

Problem ni Kwamba una Speculate tu, Hujaiona hata Rasimu ya Katiba ya Tanganyika.
Unaweza uka estmate roughly Ukubwa Cabinet ya Tanganyika???, Je Muundo wa Serikali nzima utakuweje???
Then compare na Current cabinet including Zanzibar then from there ndo unaweza ukaja na Kigezo cha Gharama.
Otherwise, hiyo ni Justification ya Baadhi ya Wana Siasa wa CCM amabao wanaona kabisa kwa Rasimu hii ya Katiba ,hawana chao 2015.
 
Wakuu JF, Amani iwe Nanyi
Kuna watu wameshaanza tayari ,nina uhakika watu hawa wanatumiwa.
Wanapinga Rasimu ya Serikali tatu kwa kigezo cha Gharama.
Eti Nchi itakuwa na Gharama Kubwa ku Run na Marais wa Tatu.
Watu kama hawa wanastahili Kukumbushwa kuwa kwa Sasa Nchi ina Ma Rais wa Tano na Wa Tatu wanatokea zanzibar.
Watu hawa wamekuwa wapofu kuona kuwa Tume ya Warioba imependekeza Baraza lenye Ma Waziri wasiozid 15.
Kwa Sasa Baraza lina Zaid ya Mawaziri 45, Mbona hawasemiGharama kubwa za ku Run the Current Baraza la Mawaziri?????
Hawaoni kuwa kwa Kupunguza Baraza la Mawaziri Mpaka 15 tUtakuwa tumeokoa Kiasi kikubwa sana Cha Fedha.
Watu wanaopinga Serikali 3 Hawastahili kuishi Tanzania,
TUSIMAME KUWAPINGA HAWA WACHUMIA TUMBO

Mbona na we kama hujasoma Rasimu! Baraza la mawaziri la Muungano litakuwa na mawaziri 15 jumlisha na manaibu sijui wangapi watakao shughulikia mambo yote ya muungano. Tanzania bara nayo itakuwa na mawaziri watakaoshughulikia mambo yasiyo ya mungano. unajua yapo mangapi? Pia ukubwa wa serikali tunaousema ni kwamba itafika mahala 80% ya bajet itaendesha serikali na 20% maendeleo unategemea nini! hata hzi mbili ni gharama ni kubwa mno.
 
Mambo ya serikali tatu hayana maana,maana ni kama vile hakuna muungano.Tumeungana basi tunataka serikali moja.

Mimi nasimama na wewe. Maana ya kuungana ni kuwa mwili mmoja, sasa vichwa vitatu kila kimoja na maamuzi yake ili iwe nini. Hawa wanaotaka serikali 3 ni wale wenye uchu wa madaraka. Wanataka kuwe na post nyingi za ulaji.

Aidha serikali moja, au muungano na ufe. Binafsi sijajua mimi niliyetoka Mara huu muungano una manufaa gani kwangu. Nijuavyo watu huungana ili wawe Taifa kubwa lenye nguvu. Kama tunaungana kwa bendera huku nguvu tunatawanya, hii faida ya nani kama sio kujidanganya?
 
Kuwa na serikali tatu nadhani tunajaribu kubembeleza2 Muungano usivunjike lakin ki-uhalisia umesha vunjika, Hii selikali ya tatu kazi yake nn? ikiwa haitakuwa na uwakilishi wowote kimataifa like UN coz Tanganyika na Zanzibar ndizo zitakazo wakilkisha UN na km serikali ya muungano itawakilisha UN hiz za Tanganyika na zanzibar kazi yake itakuwa nn?, Kazi za raisi wa Muungano, Bunge na Mahakama kubwa na ya maana ni ipi? au ndo kuhakikisha hatuvunji muungano? Tujiulize kwani ni lazima sana kuwa na Muungano wa Tanganyika na zanzibar kwa nini tucwe2 kwenye muungano wa East Africa! Serikali tatu inaacha maswali mengi kuliko majibu!!!! lets talk seriously on this.....!!!!!!!
 
nitapinga serikali tatu nimechoka kuongezewa kodi kwa mambo yasiyo ya msingi na kuongezea ulaji watu wengi hawajui kodi zao ndio zinaendesha serikali lakini watu hao hao ndio wa kwanza kulalamika jibu ni wazi kama tunatoka serikali mbili tunatakiwa tuelekee serikali moja zaidi ya hapo tuvunje muungano ili atakayeona adha ya kuwa nje ya muungano amwombe na kukubali masharti atakayopewa na mwenzake ili kuungana tena na muungano kutetereka inatokana na viongozi na wanachama wengi wa ccm kutoujua vizuri na unafiki waliouonyesha kwa baba wa taifa
 
Wasaka Urais ndani ya CCM wamepagaishwa na na pendekezo la Serikali tatu! Mimi bila kujali wakuu wa serikali za Znz na Tanganyika wataitwaje naunga mkono uwepo wa serikali tatu muhimu Katiba iweke majukumu ya serikali zote na kusiwepo migongano.

Nahisi inaweza ikawa moja ya tiba ya mtu mmoja kurundikiwa madaraka na kuchezea kodi za Watanzania. Haitawezekana tena pesa za wananchi kuibiwa na wahusika wakauchuna. Hii ndiyo njia pekee ya kuokoa Muungano. Serikali moja Wazanzibari hawaitaki,serikali mbili wanasema wananyonywa.
 
kama kweli tunaitaji muungano uendelee kuwepo, hatuitaji kuwa na marais watatu katika hizi serikali 3. tanganyika na zanzibar ziongozwe na waziri wakuu or gavana, tuwe na rais mmoja tu anayetambuliwa kimataifa kama kweli tumekubali kuungana lazima tukubali kupoteza baadhi ya title la sivyo tutachanganyana tu
 
jamani uwepo wa serikali 3 utaongeza Ajira why? mnakwepa gharama wakati mnataka kitu kizuri?
mleta thread naona hata
hajitambui.wizara hazijapunguzwa,hizo zilizosemwa ni za muungano tu.hapo
bado za tanganyika,hao wazenji wakafie mbali na wizara zao
hazituhusu.huku bara utakutana na mafisadi watataka kula so
watajitengenezea nafasi nyingi tu.bado mabunge matatu,wabunge watatu
kila jimbo,wakuu wa mikoa/wilaya,makatibu,manaibu waziri na wapambe
wao.ukisikiliza madai ya wazenji ndio utachoka so kwa nini tusivunje tu
muungano kama watu wanataka mamlaka kamili?
 
Mimi kwa mtazamo wangu serikali moja au mbili ndio suluhisho!kama serikali 3 ya bara na zbar ziwe na PM tu sio rais na PM apatikane kwa kuteuliwa na Rais wa Muungano .....nguvu zote awe nazo rais wa JMT!hiyo rasimu imepita kuwakomoa watu fulani ili wabadilishe mtazamo wao walionao sasa maana gharama za kuendesha serikali na kuchangia JMT sio mchezo!
 
Mtu kama Kadinali Pengo huwa na mheshimu sana na naogopa kumvunjia heshima lakini jana alinishangaza sana na hii "Iresponsible Statement" eti serikali tatu ni gharama kubwa sana kuziendesha. Hivi ameshafanya upembuzi yakinifu kujua hii serikali ya sasa inatumia kiasi gani. Jamani tuaje milopoko tufanye upembuzi yakinifu ndipo tutoe maoni hadharani. Kwa sasa tunamaraisi zaidi ya watano; kuna Kikwete, Bilali, Sheni, Pinda, sefu, na yule mwingine wa zanzibar sijui anaitwa nani. Wote hawa wanaitwa viongozi wakuu wa serikali, huyu anaekuja na hoja dhaifu ya gharama ameshatathimini gharama za hawa.
 
Serikali tatu zitapunguza gharama kwani ukiisoma rasimu yote utagundua kuwa kutakuwa na uwajibikaji zaidi, ni huu uwajibikaji utakaoondoa kulindana na hivyo kupunguza gharama. Mfumo wa serikali 2 ambao inaonekana wazi zanzibar inataka kuimeza Tanganyika ikijidai kuwa yenyewe ndiyo itamezwa na Tanganyika, umeshapitwa na wakati.
Upuuzi mwingine ukiowekwa kwenye rasimu eti ni kukwepa gharama, nimeujadili katika thread yangu inayoitwa rasimu ina mapungufu mengi - yarekebishwe haraka.
Hapa mawamegea kukwepa gharama kwa kuondoa chaguzi ndogo:
A) KUJAZA NAFASI WAZI ZA WABUNGE

Katika utangulizi wa Katiba ambao unaonyesha misingi ya Katiba ambayo imekubaliwa na wananchi, kuna kipengele kinasema:
"NA KWA KUWA, tunaamini kuwa misingi hiyo inaweza tu kutekelezwa katika jamii yenye mfumo wa demokrasia na utawala bora ambayo Serikali yake inasimamiwa na Bunge lenye Wabunge waliochaguliwa na wanaowawakilisha wananchi na Mahakama huru zinazotekeleza wajibu wa kutoa haki bila woga wala upendeleo wowote, na
kuhakikisha kuwa haki za binadamu zinalindwa na kudumishwa na kwamba wajibu wa
kila mtu unatekelezwa kwa uaminifu";
Hii inaonnyesha kuwa wananchi wanaamini katika bunge lenye wabunge wa kuchaguliwa na wanaowakilisha wananchi (yaani wananchi wote bila kujali itikadi za vyama vya siasa au dini nk)

Pia kifungu cha 105 kinasaema :
105.-(1) Kutakuwa na Bunge la Jamhuri ya Muungano.
(2) Wajumbe wa Bunge watakuwa wa aina zifuatazo:
(a) Wabunge waliochaguliwa kuwakilisha majimbo ya
uchaguzi;
(b) Wabunge watano watakaoteuliwa na Rais kutoka miongoni
mwa watu wenye sifa za kuchaguliwa kuwa wabunge
kuwakilisha watu wenye ulemavu kwa kuzingatia uwiano wa
Washirika wa Muungano.

Yaani kifungu hiki kinasisitiza kuwepo kwa wabunge waliochaguliwa na wananchi kuwakilisha majimbo (na hao watano tu walemavu wa kuteuliwa)

Pia kifungu cha 119 kinasisitiza wabunge wa majimbo wawe wa kuchaguliwa na wananchi:
"119.-(1) Wabunge wanaowakilisha majimbo ya uchaguzi
watachaguliwa na wananchi kwa kufuata masharti ya Katiba hii na vile vile
masharti ya sheria iliyotungwa na Bunge kwa mujibu wa Katiba hii,
inayoweka masharti kuhusu uchaguzi wa Wabunge.


SASA Kifungu cha 106 kinaua kabisa msingi ambao wananchi wanauamini
"116 (4) Endapo Mbunge anayetokana na chama cha siasa atapoteza sifa

za kuwa mbunge kwa sababu yoyote isiyokuwa ya Bunge kumaliza muda
wake, Tume Huru ya Uchaguzi ya Jamhuri, kwa mujibu wa masharti
yatakayowekwa na sheria itakayotungwa na Bunge kwa ajili hiyo, itamteua
na kumtangaza kuwa mbunge mtumwingine kutoka kwenye orodha ya
majina ya wagombea iliyowasilishwa na chama hicho kwa mujibu wa Ibara
ndogo ya (5)

Kwa maana ya kifungu hiki wananchi watawekewa mtu ambaye hawakumchagua kuwa mbunge wao. Suala kuwa chama husika kilimuweka katika orodha ya wagombea wake haina maana kuwa orodha hiyo ya chama ilichaguliwa na wananchi wote. Orodha hiyo inaandaliwa na chama husika kwa utaratibu wanaoujua wao ambao hauko kwenye katiba.
Je hii si kuvunja msingi iliotajwa kwenye utangulizi na kuwekewa msisitizo katika kifungu cha 105 na 119?
NAPENDEKEZA UWEPO UCHAGUZI MDOGO KUJAZA NAFASI WAZI. Tusikwepe gharama kwani hakika hiyo ni gharama ya demokrasia.

Suala hili likiachwa kama lilivyo kutajitokeza matatizo mengi kwenye uchaguzi mkuu kuzidi ilivyokuwa huko nyuma. Yaani chama kitaamua kutumia nguvu nyingi na mbinu zisizohalali ili kihakikishe kinapata kiti cha ubunge kikijua kuwa hata kama itathibitika kuwa mbinu mbaya zilitumika, chama kama chama hakitakuwa na cha kupoteza kwani kitaendelea kushikilia kiti chake.
Ni afadhali basi katiba ingesema kuwa aliyekuwa mshindi wa pili ndiye apewe hiyo nafasi hiyo kwani ana kura za wananchi, na pia itazuia nguvu na mbinu haramu kutumika wakati wa uchaguzi.
 
Mkuu hao ni WAVIVU wa kufikiri, achilia mbali mzigo wa watawala waliopo sasa hivi, baraza la mawaziri (mpaka waziri asiyekuwa na wizara maalum) pia idadi ya miko/wilayaa inayoota kama UYOGA siku hizi ni gharama mno. Haya kwao wanaona sawa tuu maadamu walikuwepo/wapo madarakani vyoo vyao vinafurika kila mwezi!!!!!!!!!!
 
Kabla ya kuunga mkono hoja naomba nitoe ufafanuzi mfupi ufuatao:

1. Nchi ya Tanganyika ilipata uhuru wake kutoka kwa Waingereza chini ya Gavana Sir Richard Turnbull mnamo tarehe
9.12.1961 na Mh.Mwal.Julius Kambarage Nyerere akawa ni ndiye
Rais wa kwanza wa Tanganyika hasa ilipokuwa Jamhuri mnamo tarehe 9.12.1961 mwaka mmoja baadaaya uhuru.
2.Nchi ya Zanzibar ilifanya mapinduzi ya amani mnamo tarehe 12.01.1964 kutoka kwa Waarabu na Mh.Sheick Abeid
Amani Karume akawa ndiye Rais wa kwanza wa serikali ya mapinduzi ya Zanzibar.
3. Mwalimu Nyerere na Mh.Karume walikubaliana kuunganisha nchi zao ili kuwa na nguvu wasiweze kuvamiwa na Wakoloni
pamoja na walowezi wa Kiarabu kwa wakati ule na ndipo mnamo tarehe 26.04.1964 ILOZALIWA JAMHURI YA
MUUNGANO WA TANZANIA LAKINI kutokana na umaskini na uhaba wa watumishi wa kuongoza serikali zetu wazee wetu walikubaliana zibaki serikali mbili yaani ya Muungano na Zanzibar licha ya kwamba mkanganyiko huu wa serikali hizi ulionekana tangu zamani.

4. Baada ya muungano hitilafu zilianza kujitokeza na walikuwepo watu ambao hawakutaka muungano huo na ndio maana tarehe 17 Aprili 1972 walimuua Mh.Karume.

MATATIZO NA DOSARI ZILIZOPO ZA MUUNGANO.

1. Baada ya muungano Zanzibar ilibaki kama nchi inayojitawala kwa kuwa na Rais wake na mamlaka mengine ya kiutawala.

2. Zanzibar wana wimbo wao wa Taifa, TANGANYIKA wanatumia wimbo wa muungano.
3. Zanzibar wana RAIS WAO wakati Tannganyika wanatumia Rais wa muungano.
4. Zanzibar wana bendera yao ya TAIFA wakati Tanganyika wanatumia bendera ya Muungano.
5. Wakati wa uchaguzi mkuu Zanzibar wanapiga kura mara mbili, yaani kura kwa Rais wa Zanzibar na Kura kwa Rais wa muungano.
6.Zanzibar wana mamlaka yote kama nchi na Rais wao anayo mamlaka ya kiutendaji huko Zanzibar yaani wana baraza la mawaziri la serikali ya mapinduzi ya Zanzibar, Baraza la wawakilishi na mamlaka nyingine zote za utawala WAKATI ZANZIBAR IKIWA VILE KWA UPANDE WA TANZANIA BARA MAMLAKA NYINGI ZINATUMIKA ZA MUUNGANO.

HIVYO basi kutokana na mkanganyiko huu ninaunga mkono hoja na kukubali rasmu ya katiba mpya kuwa na serikali TATU yaani ya Zanzibar, Tanganyika na ya MUUNGANO.CCM eti ni gharama kuendesha serikali hizo? Gharama kitu gani tusikubali akili ndogo itawale akili kubwa kwani kwa sasa tunaweza kuona eti ni gharama kubwa lakini matatizo yatakapojitokeza tutajutia gharama hizo.
Muungano kwa hivi una chokochoko nyingi kutokana na mkanganyiko huu hapo juu, serikali tatu ni suluhisho.
 
Kweli hizo ni SABABU zenye Mantiki?

Mangi Marealle sehemu aliyokuwa anaitawala ILIkUWA na WIMBO wake wa TAIFA
Mangi alikuwa kiongozi wao na Serikali ya Queen ilikuwa ni representative wa UN
Mangi walikuwa na Bendera yao
Wananchi chini ya Mangi walikuwa na Uwezo wa kulichagua Baraza la Mangi
Mangi alikuwa na Banki
Mangi alikuwa na SHULE hadi VYUO

* Sasa kama sababu zako ni finyu kama unavyozijadili; Kuna Makabila Mengi yaliyokuwa yanajitegemea yenyewe nimekupa mfano wa Wachagga hao wa Marangu; kuna Mwamachame; Wahaya; Wasukuma; Wanyakyusa; Wahehe etc
 
Serikali tatu ni jibu la muungano wetu kwa sasa hakuna mbadala, wako watu wanafikiri kinyume cha serikali tatu ,watu hawani wanafiki wasiopenda ukweli ufanyekazi ,tumepata matatizo mengi ya serikali mbili maneno yasiyoisha kilasiku wazanzibar wanalalamika wanataka watambuliwe kimataifa sasa tufike mahali tumeze sindano inayo choma lakini ituponye wote. Tanganyika irudi tusije tatiza vizazi kwa unafiki na uroho wa madaraka
 
Nafikiri suluhu ya kudumu ni turudi kwenye uhalisia wa nchi zetu,Tanganyika Tanganyika na Zanzibar Zanzibar!
 
Muungano wa serikali mbili yapasa tupate serikali moja. mengine yote ni kuogopana na unafiki tu!
 
Back
Top Bottom