Uchaguzi 2020 Kupitia miundo mbinu iliyojengwa na Serikali ya Magufuli, CHADEMA wanafanyia kampeni

Uchaguzi 2020 Kupitia miundo mbinu iliyojengwa na Serikali ya Magufuli, CHADEMA wanafanyia kampeni

Tofauti na Nchi nyingine Duniani zenye siasa ya Vyama vingi, Tanzania ndo Nchi pekee ambayo Vyama vikuu vya Upinzani havijui dhana halisi ya Upinzani. Vyama hivi Vikuu Kama CHADEMA, CUF, ACT, na NCCR Mageuzi vimekuwa Vyama vya *"UPINGAJI"* kuliko kuwa Vyama vya Upinzani..
Hapo kwenye serikali ya Magufuli edit isomeke serikali ya Tanzania, ahsante
 
Acha ujinga,karibu kutumia akili hata za Darasa la nne. Miundombinu inajengwa kwa Kodi za watanzania,million 55,hazijengwi kwa michango ya Wana ccm.

Ccm inawanachama 15M,Wananchi tupo million 55!...

Mkuu bila kupinga maelezo yako mazuri, naona umesema ccm ina wanachama 15m. Ccm itoe wapi wanachama 15m? Kama ina wengi sana hawafiki 5m.
 
Tofauti na Nchi nyingine Duniani zenye siasa ya Vyama vingi, Tanzania ndo Nchi pekee ambayo Vyama vikuu vya Upinzani havijui dhana halisi ya Upinzani. Vyama hivi Vikuu Kama CHADEMA, CUF, ACT, na NCCR Mageuzi vimekuwa Vyama vya *"UPINGAJI"* kuliko kuwa Vyama vya Upinzani...
Kuna mambo huwa yananichanga sana yaani sanaa

Kila uchaguzi kuna chama cha Kijani kinadai kinatuletea Tanzania Mpya.

Nafikiri huwa wanamaanisha upya wa matatizo, ujinga na umaskini.

Fikiria kwa miaka 55+ sasa - wanasema tusichague wengine kwa kuwa wataondoa amani lakini wakati chini ya utawala wao wa kiimla tuna WASIOJULIKANA,VIROBA FUKWENI, Disapperance of Azory , kutapeliwa korosho zetu, Kuvunjwa haki za binadamu na sheria mbaya za ovyo ovyo
 
Tatizo la Magufuli ni kuamini kwamba miundombinu ni mali yake yeye na chama chake, na hiyo hupelekea kuchukia anapoona wasiomuunga mkono wanaitumia.

Pia hakuna serikali yoyote ile katika dunia hii ambayo haijengi miundombinu. labda tatizo la kutokusafiri na kutokujifunza toka kwa viongozi wenzake ktk nchi nyingine ndiyo kumepelekea Magufuli kuamini kuwa miundombinu ni mali yake yeye na chama chake.
👊👊
 
..unajua haya maneno muanzilishi wake ni Magufuli mwenyewe.

..fuatilieni hotuba zake tangu akiwa waziri ktk serikali ya awamu ya 4.

Kabisa, hayo maneno kuwa wapinzani wanaandamana kwenye barabara zilizojengwa na ccm, yalikuwa ni maneno ya mara kwa mara ya Magufuli. Hata hili neno kupinga kila kitu ni maneno ya Magufuli, na kwakuwa kawashikia akili wanaccm wote, wanajikuta wanayarudiarudia hayo maneno.
 
Kwani anakusanya kodi kwa wanaCCM peke yao?, kama wanachadema nao wanalipa kodi, basi nao wanahaki ya kutumia miundombinu hiyo. Kwanini uteseke mkuu?.
 
Kabisa, hayo maneno kuwa wapinzani wanaandamana kwenye barabara zilizojengwa na ccm, yalikuwa ni maneno ya mara kwa mara ya Magufuli. Hata hili neno kupinga kila kitu ni maneno ya Magufuli, na kwakuwa kawashikia akili wanaccm wote, wanajikuta wanayarudiarudia hayo maneno.

..inawezekana huo ndio uelewa wa Magufuli kuhusu katiba yetu na demokrasia ya vyama vingi.

..inawezekana kwa dhati ya moyo wake anaamini kwamba hiyo miundombinu ni ya kwake yeye, na wana ccm wenzake.

..na zaidi anaamini kuwa wapinzani wataivunja na kuuza screpa.
 
Ungepewa wewe ungekataaa Acheni Unafki kawapa watanzania wenzenu hajawapa wazungu
Sipokeagi pesa nisiyofanyia kazi. Cha bure ghali sana mkuu. Hasa inapotoka kwa mwanaume mwenzangu
 
..inawezekana huo ndio uelewa wa Magufuli kuhusu katiba yetu na demokrasia ya vyama vingi.

..inawezekana kwa dhati ya moyo wake anaamini kwamba hiyo miundombinu ni ya kwake yeye, na wana ccm wenzake.

..na zaidi anaamini kuwa wapinzani wataivunja na kuuza screpa.
Na inaonekana kuna kina magufuli wengi tu
 
Comments zinaonesha elimu ya uraia iko mahali pake, uzi umefungwa.
 
Tofauti na Nchi nyingine Duniani zenye siasa ya Vyama vingi, Tanzania ndo Nchi pekee ambayo Vyama vikuu vya Upinzani havijui dhana halisi ya Upinzani. Vyama hivi Vikuu Kama CHADEMA, CUF, ACT, na NCCR Mageuzi vimekuwa Vyama vya *"UPINGAJI"* kuliko kuwa Vyama vya Upinzani.

Katika Nchi nyingine Vyama vya Upinzani huja na Sera mbadala kwa lengo la kuongeza ufanisi wa pale Utendaji wa Serikali inayomaliza muda wake ulipofikia. Jambo hili Kwa Tanzania ni tofauti.... Vyama vya Upinzani vimekuwa na tabia ya Kubeza kila Jambo linalofanywa na Serikali ya Chama Cha Mapinduzi bila kuangalia linawanufaisha Watanzania wengi kiasi gani.

Hivi kweli Sera za CHADEMA kuwa Serikali imewekeza kwenye Vitu na sio watu zinatija kwa sisi wananchi wa Hali ya Chini?
Vitu Kama Umeme, Madaraja, Vivuko, Meli, Ndege, Barabara, Treni/Reli, Hospital, Shule, Maji havina uhusiano na Maendeleo ya watu?

Chadema kubeza uwepo wa Miundombinu hii ambayo kwa miaka mitano Dr. John Pombe Magufuli ameweza kufanya vizur katika Ujenzi wake ni kuonyesha Ni kwa namna gani hawana Nia njema na sisi wananchi wanyonge tunaonufaika na Fursa za ajira zinazotokana na Ujenzi wa Miradi hii na hata kuajiriwa kuendesha Miradi hii.

Ni kupitia Miundombinu hiyo hiyo CHADEMA wanaitumia kufanya Kampen zao kwa Uhuru na amani na hakuna anayewabugudhi, Hii ndo CCM, Chama kinachofundisha siasa kwa Vitendo.

Ni muda sasa muafaka kwetu sisi Kama wananchi kuamua kwa kauli moja kuwapuuza wagombea wote wanaotaka kutumia Propaganda kutuaminisha Mambo ya uzushi. Tujipange kuichagua CCM maana ndicho Chama haswa chenye ilani inayotekelezeka kwa manufaa ya Watanzania wote.

CHAGUA JOHN POMBE MAGUFULI KAZI IENDELEE.
Ujenzi wa miundo mbinu Ni wajibu serikali zote duniani, ukiona serikali inayo jisifia ujenzi wa miundo mbinu Ni serikali mufilisi.
 
Mkuu Jitahidi uwe unapata milo yote mitatu na kunywa maji mengi hadi moyo uelee..

May be akili yako itakaa sawa
 
Back
Top Bottom