Ali Nassor Px
JF-Expert Member
- May 6, 2022
- 2,384
- 3,926
UTANGULIZI
Msanii ni mtu anayetumia lugha kufikisha ujumbe( kazi zake za sanaa) kwa jamii. kwa lengo la kuburudisha na elimisha.
Katika kutoa maana halisi ya fasihi simulizi kwenye kipengele cha msanii (mwanafasihi) kuna mtazamo unasema 'Msanii ni kioo cha jamii'. Kioo kazi yake kubwa ni kutuonesha kasoro zilizopo mwili huenda tunaziona tukapuuzia au hatukuziona kabisa hivyo kupitia kioo tutaziona hizo kasoro.
Msanii ni kioo cha jamii kupitia maudhui (contents )ya kazi zake kama nyimbo, maigizo, uchoraji, uchongaji nk.
Tunaweza kujiangalia kupitia hizo kazi na kujirekebisha ili kuendana na utaratibu rasmi wa jamii yetu.
Lakini pia kioo kinaweza kuvunjika hivyo kushindwa kutoa taarifa kamili au kwa usahihi kwa mtazamaji husika hivyohivyo msanii anaweza kuwa na tabia mbovu ambazo zinaweza kutoa taarifa chafu na zisizofaa kabisa kwa jamii yake.
Ni vema wasanii wakatambua kuwa wana jukumu kubwa katika jamii kuelimisha na si kupotosha.
Sanaa katika jamii zetu imeendelea kutumika kama dhana ya kusaidia jamii kujikosoa na kupata burudani.
Ajabu siku hizi wasanii badala ya kuwa kioo cha jamii wamegeuka kuwa giza, ambalo halionyeshi na hugubikwa na mambo ya ajabu.
CHANGAMOTO
Sanaa katika Jamii au taifa lolote lile ni sawa na kiumbe hai, ambacho kinaendelea kukua na kujifunza kulingana na wakati na kufanyia mabadiliko sanaa yake ambayo ni kielelezo cha utamaduni wa taifa hilo. Sanaa pamoja na wasanii ni nguzo muhimu katika kuelimisha jamii hasa pale jamii inapojitahidi kunakiri mambo bila kujua uzuri au ubaya wa jambo husika, hivyo sanaa ikitumika vizuri inaweza kusaidia kuondoa tatizo hili kwa jamii ambayo pengine imekosa elimu, au teknolojia mpya, na hata kushindwa kujifunza kwa sababu ya utofauti mkubwa wa mazingira na maendeleo.
Mmoja; Katika kufaninikisha malengo ya kuelimisha jamii, serikali huunda chombo cha kusimamia, kukuza na kuongeza maendeleo ya utengenezaji wa kazi za sanaa kulingana na maadili ya taifa.
Ndani ya Tanzania tunachombo ambacho kinaitwa Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA).
Chombo hiki kinatakiwa kiwe ndio kiranja mkuu kwa kusimamia kazi za wasanii ili ziweze kuchezwa au kuonyeshwa kulingana na maadili ya taifa letu.
ukweli ni kuwa chombo hiki kinayumba na katika kujiendesha chenyewe na pia kwenye kusimamia maadili ya kazi za wasanii kwani wasanii sasa wamekuwa na nguvu ya kuleta mmomonyoko wa maadili katika ndani ya taifa letu.
Siku hizi kuna kazi za sanaa zenye maudhui machafu zinapigwa redioni na katika runinga. na mamlaka inashindwa kuzizuia mapema, huku BASATA inaonesha wameshindwa kuwawajibisha wale wasanii wachache wanaoharibu sifa nzuri ya kazi ya sanaa.
Taifa letu lina wananchi wa rika mbali mbali lazima kuwe na utaratibu kama ilivyo katika nchi za wenzetu onesho lolote lilizozalishwa ndani au nje ya nchi linaonyeshwa katika vyombo vyetu vya habari linatakiwa lioneshe ni rika gani wanatakiwa kulitazama.
Kwa mfano; ikionyesha kuwa Onesho hili ni “ Parental Guidance (PG) 13” hii inamaanisha kuwa wenye ruksa ya kutazama onesho hilo ni wale wote wenye rika ya miaka 13 na kwenda kuendelea ,wale ambao hawajafika umri huu sio busara kuona onesho hilo.
hivyo sheria au utaratibu ukieleweka, jamii nayo sasa inaanza kuwajibika kwa kuwaelimisha na kuwakemea kwamba hawastahili kuangalia onesho hilo.
Pili; kuwa tatizo la mmomonyoko wa maadili ni la muda mrefu. Mmomonyoko huu umekuwa ukiendelea na kukua labda kutokana na ukimya wa mamlaka husika (BASATA), kwa kuwa upande wa msanii au kumuonea muhali msanii fulani.
imefikia hatua hivi karibuni baadhi ya kazi za sanaa zisizo na maadili zinaifikia jamii. na jamii hususani watoto wanaipokea hiyo kazi na kuiona kama kazi ya kawaida tu kumbe ndo maadili yanamong'onyoka.
Kazi inaingia kwa jamii (wasikilizaji/ watazamaji) na haina maadili. inaenda kuathiri jamii. baada ya athari BASATA ndo inatoa tamko la kukemea. mda wote huu BASATA ilikuwa wapi mpaka kazi inawafikia jamii kazi ya kuratibu kazi za sanaa inafanywa na nani sasa.
aiishi hapo BASATA wanakemea kuwa kazi ya sanaa hiyo haina maadili lakini kwenye tuzo kazi hiyo hiyo wanaiteua tena ishindanie na inashinda na kupewa tuzo juu.
BASATA linakemea jamii lakini inatakiwa kujua makosa ni yule aliye upitisha huo wimbo ufike Kwa walaji wa mwisho (jamii).
SULUHISHO
Baraza letu la sanaa (BASATA) linatakiwa kuanza kuchukua hatua kwa ajili ya kudhibiti mmomonyoko wa maadili kupitia sanaa.
i. Baraza linatakiwa kuendelea kuwaelimisha wasanii; kufanya kazi za sanaa na kuishi ndani ya maadili wakiwa nje na ndani ya kazi zao na sio kusingizia Pombe kuwa ndio iliyofanya mambo haya yote. kumekuwa na video nyingi chafu za wasanii zikisambaa mitandao kila siku.
ii. Udhibiti wa mamlaka na usimamizi wa wazazi ; Uwepo utaratibu wa kudhibiti kazi za sanaa ambazo husababisha mmommonyoko wa maadili kwa kwa vijana wetu. kazi za wasanii wetu kwa ujumla hazioneshi umri wa kuzitazama Parental Guidance (PG) na baadhi ya nyimbo zinatumia maneno mazito ambayo yamekuwa yakiimbwa na watoto.
mamlaka ipambanie kutimiza jukumu lake lakini pia jamii itimize jukumu lake la kusimamia maadili yake.
iii. Utekelezaji wa sheria bila kuoneana muhari;
sheria zitekelezwe pale msanii anapovunja sheria za baraza bila kutazama ukubwa wake.
Utekelezaji wa sheria utapendeza kama pia kutakuwa na ushirikishwaji wa wasanii kabla ya kutunga sheria na kanuni zitakazotoa muongozo wa maadili wa kazi zao za sanaa kiujumla.
Hii itasaidia kupunguza lawama na uvunjwaji wa sheria na kanuni baina ya wasanii na baraza lakini pia kwa jamii kiujumla.
iv. Elimu kwa wasanii; wasanii wetu wanahitaji elimu ya kuijua sanaa kuundani na busara ya kumchanganua nini waonyeshe, nini wavae, nini waimbena namna gani wacheze na pombe kama ni lazima itumike, itumike wapi na kwa kiasi gani.
kwani jukumu la wasanii ni kuelimisha na kuburudisha na sio kuburudisha tu. burudani bila mipaka inapeleka kupotosha jamii.
Itabidi BASATA wakae pamoja na wasanii kuwapa elimu kuhusu swala la maadili kiundani zaidi.
USHAURI KWA BASATA
Iwapo BASATA wameshindwa Kuwajibika ipasavyo kwa kusimamia na kutekeleza majukumu yao. kazi zisizo na maadili zitaendelea kuzalishwa kila siku.
Tunahitaji sanaa ambazo zitatuburudisha na kutuelimisha pia.
kinyume na hapo dhana ya sanaa na msanii ni kioo cha jamii itakuwa haina maana ya kuendelea kutumika tena.
Ukienda kuoga, kisha ukamaliza kuoga na ukatoka bafuni, ghafla ukagundua kuna povu halijatoka unaweza akaamua mmoja katika mawili.
ama UKAJISUUZE au UJIFUTE na taulo. Ingawa maamuzi yote yanaweza kuwa sawa lakini moja litakugharimu bila wewe kujua.
Nawasilisha.
Msanii ni mtu anayetumia lugha kufikisha ujumbe( kazi zake za sanaa) kwa jamii. kwa lengo la kuburudisha na elimisha.
Katika kutoa maana halisi ya fasihi simulizi kwenye kipengele cha msanii (mwanafasihi) kuna mtazamo unasema 'Msanii ni kioo cha jamii'. Kioo kazi yake kubwa ni kutuonesha kasoro zilizopo mwili huenda tunaziona tukapuuzia au hatukuziona kabisa hivyo kupitia kioo tutaziona hizo kasoro.
Msanii ni kioo cha jamii kupitia maudhui (contents )ya kazi zake kama nyimbo, maigizo, uchoraji, uchongaji nk.
Tunaweza kujiangalia kupitia hizo kazi na kujirekebisha ili kuendana na utaratibu rasmi wa jamii yetu.
Lakini pia kioo kinaweza kuvunjika hivyo kushindwa kutoa taarifa kamili au kwa usahihi kwa mtazamaji husika hivyohivyo msanii anaweza kuwa na tabia mbovu ambazo zinaweza kutoa taarifa chafu na zisizofaa kabisa kwa jamii yake.
Ni vema wasanii wakatambua kuwa wana jukumu kubwa katika jamii kuelimisha na si kupotosha.
Sanaa katika jamii zetu imeendelea kutumika kama dhana ya kusaidia jamii kujikosoa na kupata burudani.
Ajabu siku hizi wasanii badala ya kuwa kioo cha jamii wamegeuka kuwa giza, ambalo halionyeshi na hugubikwa na mambo ya ajabu.
CHANGAMOTO
Sanaa katika Jamii au taifa lolote lile ni sawa na kiumbe hai, ambacho kinaendelea kukua na kujifunza kulingana na wakati na kufanyia mabadiliko sanaa yake ambayo ni kielelezo cha utamaduni wa taifa hilo. Sanaa pamoja na wasanii ni nguzo muhimu katika kuelimisha jamii hasa pale jamii inapojitahidi kunakiri mambo bila kujua uzuri au ubaya wa jambo husika, hivyo sanaa ikitumika vizuri inaweza kusaidia kuondoa tatizo hili kwa jamii ambayo pengine imekosa elimu, au teknolojia mpya, na hata kushindwa kujifunza kwa sababu ya utofauti mkubwa wa mazingira na maendeleo.
Mmoja; Katika kufaninikisha malengo ya kuelimisha jamii, serikali huunda chombo cha kusimamia, kukuza na kuongeza maendeleo ya utengenezaji wa kazi za sanaa kulingana na maadili ya taifa.
Ndani ya Tanzania tunachombo ambacho kinaitwa Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA).
Chombo hiki kinatakiwa kiwe ndio kiranja mkuu kwa kusimamia kazi za wasanii ili ziweze kuchezwa au kuonyeshwa kulingana na maadili ya taifa letu.
ukweli ni kuwa chombo hiki kinayumba na katika kujiendesha chenyewe na pia kwenye kusimamia maadili ya kazi za wasanii kwani wasanii sasa wamekuwa na nguvu ya kuleta mmomonyoko wa maadili katika ndani ya taifa letu.
Siku hizi kuna kazi za sanaa zenye maudhui machafu zinapigwa redioni na katika runinga. na mamlaka inashindwa kuzizuia mapema, huku BASATA inaonesha wameshindwa kuwawajibisha wale wasanii wachache wanaoharibu sifa nzuri ya kazi ya sanaa.
Taifa letu lina wananchi wa rika mbali mbali lazima kuwe na utaratibu kama ilivyo katika nchi za wenzetu onesho lolote lilizozalishwa ndani au nje ya nchi linaonyeshwa katika vyombo vyetu vya habari linatakiwa lioneshe ni rika gani wanatakiwa kulitazama.
Kwa mfano; ikionyesha kuwa Onesho hili ni “ Parental Guidance (PG) 13” hii inamaanisha kuwa wenye ruksa ya kutazama onesho hilo ni wale wote wenye rika ya miaka 13 na kwenda kuendelea ,wale ambao hawajafika umri huu sio busara kuona onesho hilo.
hivyo sheria au utaratibu ukieleweka, jamii nayo sasa inaanza kuwajibika kwa kuwaelimisha na kuwakemea kwamba hawastahili kuangalia onesho hilo.
Pili; kuwa tatizo la mmomonyoko wa maadili ni la muda mrefu. Mmomonyoko huu umekuwa ukiendelea na kukua labda kutokana na ukimya wa mamlaka husika (BASATA), kwa kuwa upande wa msanii au kumuonea muhali msanii fulani.
imefikia hatua hivi karibuni baadhi ya kazi za sanaa zisizo na maadili zinaifikia jamii. na jamii hususani watoto wanaipokea hiyo kazi na kuiona kama kazi ya kawaida tu kumbe ndo maadili yanamong'onyoka.
Kazi inaingia kwa jamii (wasikilizaji/ watazamaji) na haina maadili. inaenda kuathiri jamii. baada ya athari BASATA ndo inatoa tamko la kukemea. mda wote huu BASATA ilikuwa wapi mpaka kazi inawafikia jamii kazi ya kuratibu kazi za sanaa inafanywa na nani sasa.
aiishi hapo BASATA wanakemea kuwa kazi ya sanaa hiyo haina maadili lakini kwenye tuzo kazi hiyo hiyo wanaiteua tena ishindanie na inashinda na kupewa tuzo juu.
BASATA linakemea jamii lakini inatakiwa kujua makosa ni yule aliye upitisha huo wimbo ufike Kwa walaji wa mwisho (jamii).
SULUHISHO
Baraza letu la sanaa (BASATA) linatakiwa kuanza kuchukua hatua kwa ajili ya kudhibiti mmomonyoko wa maadili kupitia sanaa.
i. Baraza linatakiwa kuendelea kuwaelimisha wasanii; kufanya kazi za sanaa na kuishi ndani ya maadili wakiwa nje na ndani ya kazi zao na sio kusingizia Pombe kuwa ndio iliyofanya mambo haya yote. kumekuwa na video nyingi chafu za wasanii zikisambaa mitandao kila siku.
ii. Udhibiti wa mamlaka na usimamizi wa wazazi ; Uwepo utaratibu wa kudhibiti kazi za sanaa ambazo husababisha mmommonyoko wa maadili kwa kwa vijana wetu. kazi za wasanii wetu kwa ujumla hazioneshi umri wa kuzitazama Parental Guidance (PG) na baadhi ya nyimbo zinatumia maneno mazito ambayo yamekuwa yakiimbwa na watoto.
mamlaka ipambanie kutimiza jukumu lake lakini pia jamii itimize jukumu lake la kusimamia maadili yake.
iii. Utekelezaji wa sheria bila kuoneana muhari;
sheria zitekelezwe pale msanii anapovunja sheria za baraza bila kutazama ukubwa wake.
Utekelezaji wa sheria utapendeza kama pia kutakuwa na ushirikishwaji wa wasanii kabla ya kutunga sheria na kanuni zitakazotoa muongozo wa maadili wa kazi zao za sanaa kiujumla.
Hii itasaidia kupunguza lawama na uvunjwaji wa sheria na kanuni baina ya wasanii na baraza lakini pia kwa jamii kiujumla.
iv. Elimu kwa wasanii; wasanii wetu wanahitaji elimu ya kuijua sanaa kuundani na busara ya kumchanganua nini waonyeshe, nini wavae, nini waimbena namna gani wacheze na pombe kama ni lazima itumike, itumike wapi na kwa kiasi gani.
kwani jukumu la wasanii ni kuelimisha na kuburudisha na sio kuburudisha tu. burudani bila mipaka inapeleka kupotosha jamii.
Itabidi BASATA wakae pamoja na wasanii kuwapa elimu kuhusu swala la maadili kiundani zaidi.
USHAURI KWA BASATA
Iwapo BASATA wameshindwa Kuwajibika ipasavyo kwa kusimamia na kutekeleza majukumu yao. kazi zisizo na maadili zitaendelea kuzalishwa kila siku.
Tunahitaji sanaa ambazo zitatuburudisha na kutuelimisha pia.
kinyume na hapo dhana ya sanaa na msanii ni kioo cha jamii itakuwa haina maana ya kuendelea kutumika tena.
Ukienda kuoga, kisha ukamaliza kuoga na ukatoka bafuni, ghafla ukagundua kuna povu halijatoka unaweza akaamua mmoja katika mawili.
ama UKAJISUUZE au UJIFUTE na taulo. Ingawa maamuzi yote yanaweza kuwa sawa lakini moja litakugharimu bila wewe kujua.
Nawasilisha.
Upvote
11