Kura ya Maoni: Muundo upi wa Muungano unafaa?

Kura ya Maoni: Muundo upi wa Muungano unafaa?

Muundo upi wa Muungano unafaa?

  • Serikali 1

    Votes: 81 23.3%
  • Serikali 2

    Votes: 22 6.3%
  • Serikali 3

    Votes: 241 69.5%
  • Sijui

    Votes: 3 0.9%

  • Total voters
    347
  • Poll closed .
Serikali moja ndo mpango. Huwezi kuunganisha vitu viwili ukapata vitatu.
Ukiunganisha viwili lazima upate kimoja.
Wanaotaka serikali 2 ni waroho wj madaraka wanataka waendelee kuhodhi mfumo mzima wa utawala.
Na wanaotaka serikali 3 ni zaidi ya waroho kwan wana tamaa ya fisi, wanaamini njia hiyo ndo itakayowanusulu kupata nafasi za kutawala ilihali wakiwa njiani kuelekea kuuvunja muungano.

MUUNGANO NI KITU CHA KHERI, LAKINI SIO KITU CHA LAZIMA.
Kosa kubwa walilolifanya waasi ni kuwapeleka watu kwenye muungano pasipo kuwauliza kama wanautaka muungano ama hawautaki.

Na kosa hilohilo wameendelea kulifanya watawala wa sasa kwa kutaka kutengeneza katiba mpya pasipo kuanza kuwauliza wananchi kama wanataka muungano ama hawautaki.

Jibu lingekua ndiyo, hapo moja kwa moja ungeundwa muundo wa serikali moja,taifa moja na nchi moja.

Wala tusingeulizana tunataka serikali ngapi tena. Zaidi hata ubabe ungetumika kuunda muundo serikali moja kwa sababu tiyari wananchi wameshahiyari wanataka MUUNGANO.

Jibu lingekua hapana, tungeachana kila mtu akashka hamsini zake na wale wazanzibar waishio bara na kufanya biashara tungewapa uraia kwa anayetaka na asiyetaka akarudi nchi yake ya asili na akawa anakuja tanganyika kama mwekezaji ama mtalii.
Mwishowe tukabaki kushirikiana na kuishi kama majirani mema huku tukishuhudia wanavyokatana mapanga waunguja na wapemba kama tulivyoshuhudia wauwaji ya kimbari ya 1994 kule kwa majirani zetu ambao ilikua ni sehemu ya tanganyika kabla ya mwaka 1920 Rwanda na Burundi.
Tungepokea wakimbizi na tukaendelea kuzifaidi ajira za UN kupitia UNHCR na kutafuna madolariiiiiii.

Narudia kusema ndg zangu watanyania MUUNGANO NI JAMBO LA KHERI LAKINI SIO LA LAZIMA.
 
Wanajamvi tuweke nyuma hisia zetu na ushabiki wetu kwa vyama na watu mbalimbali nchini, tujadili kwa uelewa,uzoefu na elimu zetu kuhusu mchakato huu wa katiba unaoendelea nchini.Na kwa kuanza tujadili eneo gumu katika rasimu ambalo ni muundo wa serikali.tujadili faida na hasara za serikali moja,mbili na tatu na pia mtu mwenye mawazo tofauti na haya ya serikali moja,mbili na tatu apendekeze aina bora anayodhani inafaaa..
Jamii forum kama inavyojulikana ndani na nje ya nchi tujikite kwenye mjadala huu bila matusi wala hoja dhaifu.maoni yetu yanaweza kua solution kwa bunge maalum la katiba...tuweke uzalendo mbele...karibuni wanajf
 
kama tanganyika na zanzibar waliungana maana yake walikubaliana kuwa kitu kimoja so serikali inabidi iwe moja.
 
Serikali tatu hizi zilizopo ni tata tunaitaka Tanganyika yetu iliyozikwa kwa koti la muungano.
 
Nchi moja, serikali moja, wananchi wamoja. Hiyo ndio suluhu ya kudumu.

Ingependeza hivyo ila kwa mazingira ya sasa unadhani kunahata kanafasi kakuweza kurudi hapo??
 
WanaJF Kwa mda mrefu sasa kuelekea utungaji wa katiba mpya kumekuwa na mjadala mkali kuhusu muungano wetu uwe wa muundo upi sasa ningependekeza tuwe na kura ya maoni hapa JF kuhusu muundo wa muungano, upi ni muundo sahihi?

1.Serikali moja.
2. Serikali mbili.
3.Serikali tatu.


N:B ukiweza kutoa sababu za muundo wa muungano unaoutaka itakuwa vizuri zaidi

===============
Serikali Tatu
 
serikali tatu ndo mpango na maoni ya watanzania wengi wamependekeza tatu kwa maana ya 1 serikali ya muungano, 2 serikali ya tanganyika, na 3 serikali ya mapinduzi ya zanzibar inatosha sana
 
Ama ibaki serikali moja ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania, hizi nyingine ndogo ziondolewe, imeshindikana basi Serikali tatu kama maoni ya wananchi yalivyo kwenye rasmu.
 
Back
Top Bottom