Kura ya Maoni: Muundo upi wa Muungano unafaa?

Kura ya Maoni: Muundo upi wa Muungano unafaa?

Muundo upi wa Muungano unafaa?

  • Serikali 1

    Votes: 81 23.3%
  • Serikali 2

    Votes: 22 6.3%
  • Serikali 3

    Votes: 241 69.5%
  • Sijui

    Votes: 3 0.9%

  • Total voters
    347
  • Poll closed .
Hakuna kura ya maoni zaidi za kuipigia kura rasimu itakayopendekezwa na Bunge la Katiba! Wewe baada ya miaka 50 unaanza kujiuliza kuwa baba uliye naye ni baba yako au la, ya nini kujipa pressure ya bure? Huu Muungano ukivunjika Western Powers hazitakubali "another Somalia!" Waarabu na Al Shabaab/Al Qaeda nao hawatakubali kuona "Makafiri" wakikalia hivyo Visiwa! Don't think kwamba Tanganyika itakuwa salama eti kwa kuwa itakuwa si sehemu ya Zanzibar!
Think BIG brother/sister!

Tanganyika itakuwa salama tu kama ilivyokuwa kabla ya Muungano, na vitendo vyovyote vya kuihujumu Tanganyika vitakabiliwa with maximum force, Tanganyika hatuwezi kutawaliwa na na mawazo ya kisiwa.
 
WanaJF Kwa mda mrefu sasa kuelekea utungaji wa katiba mpya kumekuwa na mjadala mkali kuhusu muungano wetu uwe wa muundo upi sasa ningependekeza tuwe na kura ya maoni hapa JF kuhusu muundo wa muungano, upi ni muundo sahihi?

1.Serikali moja.
2. Serikali mbili.
3.Serikali tatu.


N:B ukiweza kutoa sababu za muundo wa muungano unaoutaka itakuwa vizuri zaidi
Serikari Moja tu inatosha Kumbuka Nyerere na Karume waliasisi Muungano wakitarajia Muungano utakuwa ukiboreshwa kulingana na wakati lengo ikiwa ni Kuja Kuwa na Serikari moja tu ambayo ingepunguza wingi wa Marais na makamu wa Marais na Kuwa na Rais Mmoja tu ambaye angehamia Dodoma na kuliepusha jiji na foleni zinazozidi kuongezeka kila kukicha baada ya Serikari kuacha kuhamia Dodoma na kutumia Pesa nyingi kulea na kubembeleza Muungano huku Zanzibar wakitumia Fursa hiyo kujineemesha kirahisi kwa kuzidisha Malalamiko juu ya Kero za muungano zisizokwisha Tambua Zanzibar wapo 1.5 million tu lakini wana idadi kubwa Ya wabunge na viongozi wengi sana wanaofaidi Mavuno ya rasilimali za Tanganyika kisha wanapaza Sauti za kuwapumbaza Watanganyika wasijitambue Kuwa wanachunwa kijanja . Serikari Moja tu Ndio Tiba pekee ya kumaliza mzizi wa Fitna yaani Zanzibar atawale Gavana na huku Bara atawale Gavana kisha Rais awe mmoja tu
 
seikali 3 but rais mmoja tu wa muungano na n mawaziri wakuu wawili kila nchi waziri mkuu mmoja.
 
Serikali moja ya Tanganyika. Sitaki muungano,kwa nini tunatumia rasilimali nyingi kwa kuungana na kanchi kenye uchumi mdogo kuliko Arusha na ardhi ndogo kuliko Serengeti. Tanganyika hatufaidiki kitu ni bora tuishi kwa ujirani mwema kuliko gharama zisizo na lazma. Yaani hapa tu ndo cmwelewagi Nyerere alikua anawaza nini na huu muungano.
 
mojaa hasa, mbili na tatu ni siasa

Serikari Moja pekee ndiyo itakayomaliza Vuvuzela za wazanzibar na itawasaidia Siku Visiwa Vikimezwa na maji ya Bahari waweze kuhamia Tanganyika bila Swali la Uhamiaji
 
Kama wajumbe wa bunge la katiba wana akili timamu basi na wazingatie maoni ya wananchi Serikali tatu ndio mpango mzima kulingana na maoni yaliyotoka mashinani vinginevyo tutakutana ktk kura ya maoni!
 
Serikali moja ya Tanganyika. Sitaki muungano,kwa nini tunatumia rasilimali nyingi kwa kuungana na kanchi kenye uchumi mdogo kuliko Arusha na ardhi ndogo kuliko Serengeti. Tanganyika hatufaidiki kitu ni bora tuishi kwa ujirani mwema kuliko gharama zisizo na lazma. Yaani hapa tu ndo cmwelewagi Nyerere alikua anawaza nini na huu muungano.

Nyerere aliunganisha Nchi kubwa na Visiwa Akiwa na nia Bora kabsa lakini baada ya kuungana Wazanzibar wamekuwa wajanja zaidi sasa wanajilia kiulaini pesa za Tanganyika kisha wanalalamika sana yaani Sera Yao ni kura ukishiba lalamika
 
Tuwe na federal 2 zanzimbar na tanganyika.naktk hzo federal kuwe na rais wa fedaral.gavana ndye awe mku wa federal
 
Serikali tatu.

Sababu-maana halisi ya "muungano" itakuwa sahihi kwani nchi mbili zitakuwa zimeungana, na si kwamba moja kuwa imemezeshwa kwa nyingine kihuni.

Kwa wanaotetea muungano-bora wangesimamia kwenye serikali moja na Zanzibar iwe wilaya/mkoa tu.

NB: Muungano ni jambo la kihistoria tu,zaidi unatuletea kelele kila siku na baadhi kujiona bora zaidi ya wengine.
 
Mimi sijui msimamo wangu na wala sihitaji kuujua ila nataka kama zanzibar wana rais basi na bara tuwe naye, kama zanzibar wana katiba basi na bara tuwe nayo, kama zanzibar bendera basi na mimi naitaka bendera yetu, kama wao wana wimbo basi nataka nami niimbe wimbo wa taifa langu, walioko bungeni tumewaamini mtuletee katiba tafadhari naomba muache unafiki wa kutumiana sms kuwa "bila 500,000 mnapitisha serikali tatu" naanza kushawishika kuwa kumbe kuna kitu mmeahidiwa ili mtimize azma ya watu fulani au kikundi fulani.....
 
Tanganyika should be restored,nimemsoma Mwl Nyerere kwenye Tanzania na hatima ya uongozi sikukubaliana nae. Ninampenda na kumheshimu JK Nyerere lkn serikali tatu ni must.
 
Serikali 2 ndo mpango mzima! Tukiendekeza 3 Serikali ya Muungano itakuwa haina hata ardhi (ardhi si suala la Muungano) na itakuwa ombaomba kwa nchi washirika kwa kuwa haina vyanzo vya mapato vya kwake!


Hata ardhi yenyewe tuliyonayo mbona tayari ishanunuliwa hasa hiyo ya huko kwake Katavi utasikia ana hisa katika hiyo ardhi aliyowapa hao WAMAREKANI wazalishe sana. Tanzania kwa uwongoo bora tupate Tangannyika yetu ya mababu zetu sie.3 ndio sahivi ati
 
Back
Top Bottom