Lt Col,
Kama unafahamu historia na siasa za Zanzibar, serikali moja Tanzania kamwe haitawezekana kwa sababu wenzetu huko wataona ni kama tunaimeza Zanzibar na kuifanya mkoa wakati kihistoria Zanzibar na Tanganyika zimeingia katika muungano kama nchi sawa.
Wanaweza kukuambia ukitaka serikali moja basi iwe "Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar" na Tanganyika nzima iwe mikoa ya Zanzibar kimsingi. Kama watu wa bara wasivyoweza kukubali hilo ndivyo watu wa Zanzibar wasivyoweza kukubali serikali moja itakayovunja waliyo nayo sasa.
Suala hili, from a practical point of view, ndilo lililomfanya Mwalimu Nyerere akubali kuwa na serikali mbili Tanzania.
Ndiyo maana husikii watu kuzungumzia sana serikali moja, si kitu chenye a realistic chance of happenning, even as we can debate the theoretical side of it.